My Web

Emmanuel

CONTACT

Thursday, June 7, 2012

MADA

DAWA YA MBU ALIYEKUAMBUKIZA MALARIA SIO KUMPIGA BUNDUKI,NI EXPEL TU..
HASIRA HASARA
Idadi ya chuki na hasira unazobeba moyoni mwako kutokana na vile wapenzi wako wa zamani walivyokufanyia vitu ambavyo unadhani hukustahili kufanyiwa,aidha kwa kupigwa kibuti bila kutegemea,au mpenzi kuchukua kipusa kipya na kukutosa kwa kashfa,au kuwa cheated pale ulipopenda sana,kutakufanya uwe kilema wa kupenda siku za usoni.

Kamwe usipende kuingia mahusiano mapya bila kusamehe kile kilichotokea ...kwenye past relationship,ukifanya hivyo,utakuwa kama mtu aliyegongwa na nyoka,hata akiona mkanda mweusi anashtuka.

Utajikuta unaishi kwa dalili,ukiona wingu kidogo unahisi kuna el nino inakuja kumbe ni watu tu wamechoma takataka nyumba ya Jirani....

Jifunze kusamehe waliokutekenya moyo na kuuacha unacheka wenyewe,lasivyo utajikuta unalalamika kwamba huwezi kupenda tena kumbe kosa ni la kwako umeshindwa kuachilia visasi vya Past.Dawa ya mbu aliyekusababishia Malaria kamwe sio kumpiga na bunduki kwa hasira,nunua Expel tu kwa Mangi unampulizia kidogo tu.

Tuesday, June 5, 2012

Rais wa Somalia amaliza ziara yake nchini Tanzania



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Rais wa Somalia, Mheshimiwa Sheikh Shariff Sheikh Ahmed jana Juni 4, 2012 kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro, baada ya mgeni huyo kuhitimisha ziara yake ya siku mbili nchini. Rais huyo wa Somalia alikuja nchini kwa mazungumzo na Mheshimiwa Rais Kikwete ambapo alitoa shukrani zake kwa Tanzania kutokana na misaada mbalimbali ya kibinadamu iliyopata na inayoendelea kupata pamoja na kuisemea vyema Somalia katika medani za Kimataifa na za Kikanda kila alipopata nafasi hiyo. (PICHA NA IKULU)

Monday, June 4, 2012

Uzinduzi wa tawi la Chadema Washington DC


CHANGAMOTO ZA HUIFADHI WA MISITU

The film is produced by TFCG/MJUMITA through their partnership project "Forest Justice in Tanzania" for the purpose of raising local community and general public awareness on REDD standards



Changamoto za uhifadhi wa misitu Pwani, Part 2 This film was taken between November 2011 - January 2012 in Ruvu south forest reserve. The forest is about 30 km from the doorstep of the Forest and Beekeeping Division. For more details visit: http://www.tfcg.org/pdf/Arc%20Journal%2026%20FINAL.pd



Changamoto za uhifadhi wa misitu ya pwani Part 1
This film was taken between November 2011 - January 2012 in Ruvu south forest reserve. The forest is about 30 km from the doorstep of the Forest and Beekeeping Division. For more details visit: http://www.tfcg.org/pdf/Arc%20Journal%2026%20FINAL.pdf




MAKAMUZI YA SUGU

Saturday, June 2, 2012

matukio ya rahisi Jijini Arusha


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na ujumbe wa Zanzibar katika Mkutano Mkuu wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika wakati wa hafla ya chakula cha usiku baada ya ufunguzi wa mkutano huo Mei 31, 2012 usiku katika hoteli ya Ngurdoto Mountain jijini Arusha.

Friday, June 1, 2012

usiku wa Dar Live jumapili hii na Mh. SUGU

UONGOZI WA CHAMA CHA CHADEMA WAKUTANA NA MH. BALOZI WASHINGTON DC

Wabunge Pamoja na Viongozi wa tawi la chadema Washington DC Watembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani
Baada ya kazi pevu ya uzinduzi wa tawi la Chadema jijini Washington Dc wabunge wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamtembelea rasmi Balozi wa Tanzania nchini Marekani.

New