My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, February 16, 2016

BUSARA KWA WANAWAKE. YAFUATE HAYA MAHUSIANO YAKO YADUMU


1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubutu wako.

2. Mwanamke anaemuheshimu mumewe ni mwanamke bora ambae kila mwanaume angetamani kuwa nae.

3. Tabia yako na misimamo yako ndio itakayomfanya mumeo ajute au afurahie kukuoa wewe.

4. Kuwa mke bora inakubidi uwe vizuri katika maarifa ya kutawala hasira zako na sio kuwa mtu wa kulipiza visasi.

5. Kuwa kiongozi huko kazini kwako lakini kuwa mtu wa kunyenyekea nyumbani kwako kwa mumeo. Hiyo ni busara.

6. Usiweke mashindano na mumeo, mpe hongea na mtie moyo kwa kila hatua anayopiga katika maisha.

7. Kuwa na ubinadamu, sio kosa dogo tu mumeo amefanya ukatamani kulipiza kisasi. It won't help u!

8. Kuwa mkarimu, kila mwanaume anamuheshimu mwanamke mkarimu na mwenye msimamo.

9. Usijaribu kumpa adhabu mumeo ya kumnyima chakula cha usiku kitandani, hii itamlazimu kutafuta chakula nje ya ndoa.

10. Hakuna kitu kibaya kama utakubali kuwa ulikosea kama kweli ulikosea. Kuwa mrahisi kukubali kama kweli ulikosea. Na omba radhi pale inapobidi.

11. Jiandae kumsamehe  mumeo pale anapokosea kwa maana mke atoae msamaha kwa mumewe ni mke mwema tofauti na yule aliejaa visasi.
 
12. Tengeneza maamuzi ya kuwa mke mwema, pasina kuwa na hofu yoyote na Mungu atakubariki.

13. La mwisho na la muhimu tambua kwamba mwanamke aliejaliwa umbo zuri na sura nzuri pasina maarifa kichwani anafaa kwa usiku mmoja, lakin yule mwenye maarifa na ufahamu yeya afaa kwa maisha yote!

MUNGU AWABARIKI WANAWAKE!

DONDOO KUMI KWA WANAUME ILI KUTENGENEZA MAHUSIANO YENYE AFYA.

 1. Usijisahau katika mahusiano ukawa comfortable kiasi kwamba zile mbwembwe zote za kipindi unamtongoza ukazipotezea. Mwanaume smart haachi kumfanya mwanamke wake ampende zaidi. Mwanaume anaemfanya mwanamke wake ampende zaidi mahusiano yao hudumu mpaka uchweo.

 2. Usisahau kufanya tabasamu kuwa kipaumbele cha mwanamke wako. Ole wao wanaume wanaowanyima tabasamu wapenzi wao wakaacha wanaume wengine ndio wawape tabasamu wanawake zao. Nawaambien mpo kwenye matatizo makubwa.

 3. Yatunze maneno yako kwa uaminifu mkubwa. Uaminifu ni msingi imara wa mahusiano yenye afya. Mwanaume wa kweli hakimbii majukumu.

 4. Usiwe mkoloni katika mahusiano. Kuna haki ya kusikiliza na kusikilizwa (natural justice). Kuwa mwanaume, admit kama umekosea. Kuwa na ujasiri wa kurekebisha pale ulipokosea

 5. Usimfanye mwanamke wako aone kama anashindana na muda wako, mfanye ajisikie na yeye anathamani katika muda wako. Sio sababu ya kuwa na muda au laa bali ni jitihada ya wewe kutengeneza muda wa pamoja.

 6. Usiwe mvivu. Kuna mtu mwingine pembeni ambaye anatamani kuwa na huyo mwanamke. Linda tunu yako kwa upendo, furaha na amani nae. Usiwe mvivu kumfurahisha, kumlinda, kumridhisha na kumsifia. Pombe na nyama choma zisije zikakuponza.

 7. Usihukumu. Kila mmoja anafanya makosa na anajifunza kwayo. Usihukumu makosa yake wala past yake. Na kitu cha muhimu usimhukumu kwa vile unafikiri tofauti na yeye. Binadamu tunatofautiana sana. Enjoy kuwa nae kwa jinsi alivyo. Usilazimishe awe kama wewe.

 8. Usi assume kwamba anajua kama unamjali, mwonyeshe kweli unajali. Mpe support katika shughuli zake i.e masomo, biashara, kilimo, etc. Mtumie sms, msikilize, msifie, muonyeshe mapenzi kwa maneno na vitendo na uwe mbunifu.

 9. Usiwe mwanaume jina, acha tabia ya kuzila na kususa ,onyesha kuwa wewe ni mtu wa majukumu na ni kichwa katika mahusiano, jenga mahusiano kwa busara zaidi na sio kwa ki imla (dictatorship). Maumuzi yako ya kijinga kijinga yatakutokea puani.

 10. Usikate tamaa kirahisi, najua maisha ni magumu ila mwanaume wa kweli anapotaka kitu, atafanya kila awezalo kukipata, unasubiri nini? fanya hivyo sasa.

Nawatakia week njema. 

Wewe ni nani? Karoti, yai au Mbegu ya kahawa



Binti alienda kwa bibi yake na kumuelezea jinsi anavyoishi na ugumu wa maisha katika ndoa yake. Mume wake amekua hamuheshimu ni ugomvi na malumbano kila siku iitwayo leo. Hakujua afanye nini na aliazimia kukata tamaa. Alichoka na ugomvi na manyanyaso. Ilionekana kila akitatua jambo hili linaibuka jambo jingine fasta.

Bibi yake alimchukua binti na kumpeleka jikoni. Bibi akajaza maji sufuria tatu na zote akaziweka katika moto. Punde maji ya kila sufuria yakachemka. Katika sufuria ya kwanza bibi akaweka karoti, sufuria ya pili akaweka yai, na la  tatu akaweka mbegu ya kahawa. Akaacha vichemke bila kusema neno.

Baada ya kama dakika ishirini akazima moto na kuepua sufuria zote tatu. Akatoa karoti na kuiweka katika bakuli, akatoa yai na kuweka kwenye bakuli pia na akamimina kahawa katika kikombe.

Baada ya hapo akamgeukia mjukuu wake na kumwambia "niambie sasa unaona nini?"

Binti akajibu "karoti, yai na kahawa"

Bibi akamsogezea vile vitu kwa karibu zaidi na akamwambia aiguse karoti na kuibinya. Akafanya hivyo na kugundua kuwa ilikuwa imelainika sana. Bibi akamwambia mjukuu wake alichukue lile yai na kujaribu kulivunja. Akagundua kuwa lilikuwa gumu mno.

Mwishoe bibi akamwambia ajaribu kuonja kahawa. Binti akatabasamu baada ya kujaribu ladha nzuri ya kahawa. Baada ya hivyo binti akamuuliza bibi "vitu hivi vinamaaninsha nini?"

Bibi akamfafanulia kwa kumuambia kwamba kila kitu yani kahawa, yai na karoti vimekabiliwa na tabu moja ya kuunguzwa na maji. Na kila kimoja kime react tofauti. Karoti kabla ya kuwekwa ktk maji ilikuwa ngumu kweli lakini baada ya kuunguzwa ikawa laini laini na kusinyaa.

Yai kabla ya kukutana na dhahama ya maji ya moto lilikuwa fragile kiasi kwamba ni rahisi kupasuka na ganda la nje lilikuwa likilinda kimiminika cha ndani ya yai. Lakini baada ya kuunguzwa na maji ya moto kimiminika cha ndani kikawa kigumu na si kimiminika tena.

Mbegu ya kahawa ilikuwa ya kipekee, lakini baada ya kuunguzwa na maji ya moto imeyabadilisha rangi maji yote.

Wewe upo wapi kati ya hivyo vitu vitatu? Bibi akamuuliza mjukuu wake. "pale unapokabiliana na matatizo ambayo kwa muktadha huu nimeyafananisha na maji ya moto huwa unareact vipi? Je wewe ni karoti, yai au mbegu ya kahawa?

Fikiria hivi: mimi ni nani? Je mimi ni karoti ambayo huwa ngumu, lakini pale ambapo ninakabiliana na maumivu na mateso makali nakuwa laini na kupoteza nguvu zangu?

Je mimi ni yai ambae nina moyo wa kimiminika lakini nabadilishwa na joto kali la maji. Nina moyo wa kimiminika ambapo baada ya kifo, kuachana, matatizo ya kiuchumi au majaribu mengine nakuwa mgumu na imara? Je ganda la nje linaonekana vile vile lakini ndani ni moyo jasiri, enye nguvu usioteteleka?

Au mimi ni kama mbegu ya kahawa? Ambayo kimsingi inayabadilisha maji ya moto rangi, je mimi ni jasiri kiasi kwamba ingawa nakabiliana na matatizo mengi lakini nakuwa jasiri kukabiliana nayo na kuyabadili? 

Mjukuu wangu ni vema ukawa kama kahawa au yai. Kamwe usiwe kama karoti, ukiwa hivyo utawanufaisha wale wakuumizao! Maana kwao watafurahi kukuona ukizidi kuwa mnyonge na mwenye kunyong'onyea pale wakuumizapo. Lakini kama utakuwa mgumu kama yai utawaacha wakijiuliza maswali mengi pasina majibu.

Hakuna tunu kubwa duniani kama furaha mjukuu wangu, wewe hata wakuumize kiasi gani! Usioneshe huzuni mbele yao! Wewe tabasamu tu. Kufanya hivyo utawaacha wakiwa na maswali yasiyo na majibu!

Unakabiliana vipi na majaribu yako? Je wewe ni karoti, yai au kahawa!! 

Jibu unalo wewe mwenyewe.

Monday, February 15, 2016

KOSA MOJA TENA DOGO LINAWEZA LIKAKUFANYA UWE MTUMWA WA KUDUMU.


Vijana wawili waliokuwa na hali ngumu ya maisha waliamua kwenda kuomba kazi kwa tajili mmoja aliyekuwa amejenga pembeni kidogo mwa mjii wenye watu masikini. Vijana hao mara baada ya kufika na kuonana na huyo tajili walijieleza namna maisha yao yalivyo magumu huku wakimuomba tajili huyo awape kazi yoyote, kwa kipato chochote, nao watafanya kwa moyo wote.

Yule tajili baada ya kuwasikiliza kwa umakini alijisikia kuwapa wale vijana kazi na akawaomba wafanye kazi kwa moyowote kama walivyojieleza huku akiwasisitiza wawe makini pindi wanapofanya kazi kwani alikuwa hapendi kuona kitu chochote kikihalibiwa kwa uzembe. Basi akatoa kazi mbili na kumsihii kila mmoja achague kazi anayoipenda.Kazi ya kwanza ilikuwa ni kazi ya jikoni yanii Kupika, pamoja na kufanya usafi wa ndani kama vile kudeki, kusafisha vyombo pamoja na kufua nguo na kazi ya pili ilikuwa inahusu shughuri zote za nje yani kufyeka majani, kupalilia bustani pamoja na kulisha mifugo.

Vijana walichagua kazi na kila mmoja aliipenda kazi yake, Hao vijana walijitaidi kufanya kazi vizuri ili wapendwe zaidi na boss wao. baada ya kumaliza kufanya kazi ya siku vijana walikuwa huru kucheza au kukaa tuu huku wakisubiri siku ipite. Kijana aliyekuwaanafanya kazi za nje alikuwa anamaliza kazi zake mapema kwani baadhi ya kazi zilikuwa sii za kufanya kila siku kwa mfano kupalilia bustani na kufyeka majani, kazi iliyokuwa kubwa kakwe ilikuwa ni kulisha mifugo asubhi, mchana na jioni.

Basi sikumoja kijana anayefanya kazi za nje baada ya kumaliza kazi zake alitengeneza manati na kuanza kulenga vindege vilivyokuwa vinatua kwenye mabanda ya mifupo, kwa bahati mbaya alikosea shabahaa na kupiga kuku aliyekufa papohapo. kijana yule alimkimbilia yule kuku na kumtia kwenye mfuko kisha alimzika haraka kabla boss wake hajaona, kwa bahati mbaya yule rafiki yake anayefanya kazi za jikoni alimuona akifanya kosa hilo. Basi yule Kijana anayefanya kazi za nje alimuomba kijana anayefanya kazi za ndani asiseme kwa boss kwani alikuwa anaogopa sana kufukuzwa kazi endapo boss angejua, yule kijana anayefanya kazi za ndani alikubaliana na ombi la rafiki yake kwa mashariti ya kusaidiwa kazi za ndani kwa siku hiyo. Hiyo siku kijana anayefanya kazi za nje aliambiwa aoshe vyombo, basi yule kijana anayefanya kazi za nje akaona siyo mbaya mara mia aoshe vyombo kuliko kufukuzwa kazi. Bahati mbaya ule utumwa uliendelea siku hadi sikuu na alipojalibu kukataa kufanya kazi za ndani basi yule mfanyakazi wa ndani alikuwa anamtishia na kusema kama unakataa naenda kwa boss na kumwambia habari za KUKU.

Basi zikapita siku, wiki, hatimaye miezi kadhaa, kijana anayefanya kazi za nje akajikuta amekuwa mtumwa wa kazi za ndani na nje, akakonda kwa kazi nzito huku jamaa yake akiendelea kunenepa maana ulifika wakati yule anayehusika na kazi za ndani hakuwa anafanya kazi yoyote. Siku moja yule kijana aliyekuwa anahusika na kazi za nje baada ya kupata taabu nyingi akakata shauri na akaamua kwenda kuonana na boss ili aombe msamaha kwa kosa alilofanya. Boss alimkalibisha yule kijana ili aweze kusikiliza mahitaji yake. Yule kijana alianza kulia kabla ya kujieleza hatimaye boss alijitaidi kumnyamazisha kisha alimsihii aelezee yanayomsibu. Kijana alipiga magoti na kuelezea kosa alilotenda ikiwa ni pamoja na taabu (utumwa) alizopata baada ya kufanya kosa lile la kuua kuku. Boss alishanga kuona lile jambo limemkondesha yule kijana kiasi kile na alisema mimi siku ile ile ya kwanza unamuua yule kuku nilikuona na nilisha kusamehe siku ile ile maana nilijua wazi kuwa hukukusudia kufanya hivyo lakini kwa bahati mbaya nilikuwa sijui kama lile jambo liliendelea kukutesa na kukufanya uwe mtumwa hadi ukakonda kiasi hiki. Basi yule kijana baada ya kusamehewa alishukuru ndipo boss akamwambia kila siku hakikisha unapikiwa mayai manne na rafiki yako ili mwili wako ujirudi haraka.

Kijana alimshukuru sana boss kwa msamaha aliopewa kisha akaondoka akiwa na furaha, bahati mbaya sana yule kijana aliyekuwa anahusika na kazi za jikoni alikuwa amelala akitegemea yule anayefanya kazi za nje atafanya kazi za ndani siku hiyo asijue kuwa kijana anayefanya kazi za nje ataenda kuomba msamahaa kwa boss. Basi aliamka na kukuta hamna kazi ya ndani iliyofanywa, Alimsihii kijana anayefanya kazi za nje aanze mara moja kufanya hizo kazi laa sivyo ataenda kusemelea habari za kuku kwa Boss. Kijana anayefanya kazi za nje akamjibu hunitishii kama vipi nenda ukaseme ndo kwanza kabisa nakusindikiza, basi yule kijana aliekuwa anahusika na kazi za ndani kwa hasira alitoka na kwenda kusemelea kwa boss habari za mauaji ya kuku. Boss alishangaa kuona jambo la zamani anaambiwa siku ile, akamuhoji yule mfanyakazi kwanini hukusema siku ile unaamua kusema leo? yule mfanyakazi alikosa maelezo ya kutosheleza kwani alisingizia kuwa alikuwa anaogopa kumbe boss ameshapata stori yote hata jinsi alivyomtumikisha mwenzake.

Ikabidi boss aelezee namna alivyofanya kosa la kuka na udhaifu wa mtu kwa mda mrefu huku akisikitishwa sana na jinsii alivyoutumia udhaifu huo kumtesa mwenzeke hadi kufikia hali ya kukonda kiasi kile, kisha akamwambia hawezi kukaa na mtu anayeficha maovu kwa mda mrefu na anaamua kuyaweka peupe hadi siku anayoona hanufaiki na uovu huo. Basi siku hiyohiyo yule kijana anayefanya kazi za ndani alisimamishwa kazi kisha yule boss akatafuta mfanyakazi mwingine.

USHAURI WANGU, CHINI YA JUA HAYUPO ALIYEKAMILIKA NA MUNGU ANAYETUJUA VEMA MDA  MWINGINE ANATUSAMEHE HATA KABRA YA KWENDA KUOMBA MSAMAHAA,JITAIDI KUSAMEHE BURE NAWE UTASAMEHEWA BURE.

MGOMBEA URAIS WA MAREKANI ..DONALD TRUMP ASEMA AFRIKA NI LAZIMA ITAWALIWE TENA KIKOLONI



Donald Trump: “There Is No Shortcut To Maturity, Africa Should Be Recolonized”
American business mogul Donald Trump has said that Africa needs to be recolonized. This time around he has directed his anger to African leaders who according to Trump, have failed to exercise leadership and are keeping their people in worse conditions.
Speaking yesterday in Nebraska, Trump said that Africans are slaves living like slaves in their own land yet they claim they are independent.
Trump was responding to a question by a South African journalist on whether he thinks African leaders were right to seek mass withdrawal from the Hague based International Criminal Court.
“It is shameful for African leaders to seek exit from ICC. In my view, these leaders want to have all the freedom to oppress their poor people without anyone asking them a question. I think there is no shortcut to maturity and in my view, Africa should be recolonized because Africans are still under slavery. Look at how those African leaders change constitutions in their favour so that they can be live presidents. They are all greedy and do not care about the common people” Said Trump
“When I saw them gang up against ICC yet they can’t even find an amicable solution for the ongoing quandary in Burundi, I thought to myself these people lack discipline and humane heart. They can’t lead by example. The only thing they are interested in is accumulating wealth from poor tax payers. Before they think of exiting from ICC, they should first restore peace in Burundi and other war-tone countries rather than gathering like hyenas with the aim of finishing the poor people” Added Trump.

Wednesday, January 13, 2016

Samatta afanyiwa party iliyopewa jina la Samatta Party

IMG_20160112_232125

Zawadi ya Samatta kwa Waziri mkuu ikipokelewa na waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi

Headlines za Mbwana Samatta kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wa ndani ya Afrika, bado inazidi kuleta furaha kwa wapenzi, mashabiki, watanzania na viongozi wa serikali kwa ujumla. Usiku wa January 12 Mbwana Samatta alifanyiwa party iliyopewa jina la Samatta Party. Party ilifanyika na serikali kutangaza kumpatia zawadi ya kiwanja Kigamboni na siku kadhaa mbele atakabidhiwa hati.

IMG_20160112_232228

Mkuu wa idara ya Vodacom kanda ya Pwani Harrieth Koka akiwa katika picha ya pamoja na Samatta

IMG_20160112_232252

Mshindi wa Big Brother Afrika Idris Sultan akiwa na Samatta

IMG_20160112_231625

IMG_20160112_231648

Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba Zacharia Hans Pope kushoto na mwandishi wa habari za michezo Saleh Ally

IMG_20160112_231728

IMG_20160112_231754

Samatta katikati, kushoto waziri wa michezo Nape Nnauye na waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi

IMG_20160112_231815

IMG_20160112_232012

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akithibitisha serikali kumzawadia fedha na kiwanja maeneo ya Kigamboni.

IMG_20160112_231838

IMG_20160112_231857

IMG_20160112_231916

IMG_20160112_231936

Thomas Ulimwengu alikuwepo pia kumsapoti Samatta

Monday, January 11, 2016

Technology


Toto toiletImage copyrightToto
Image captionThe prototype toilet is designed to kill bacteria and stay stain-free

An "intelligent" toilet that opens when you approach it and self-cleans with every flush is on display at the Consumer Electronics Show in Las Vegas.

It also cleans the user with an aerated wand, which delivers warm water and warm air "from a seated position", a spokeswoman said.

Despite a $9,800 (£6,704) price tag, more than 40 million earlier versions of the Neorest toilets have been sold.

Bathroom firm Toto said the new prototype was still in development.

Its self-cleaning process uses a combination of a disinfectant and a glaze - made out of zirconium and titanium dioxide - which coats the bowl.

Toto toiletImage copyrightToto
Image captionThe toilet cleans its user with a "wand" and uses an ultraviolet lamp to keep itself hygienic

"Once it flushes it sprays the interior of the bowl with electrolysed water," explained Toto spokeswoman Lenora Campos.

She said the "proprietary process" essentially turns the water into a weak bleach.

"This bleaches the interior, killing anything in the bowl," said Ms Campos.

Meanwhile an ultraviolet light in the lid charges the surface.

That makes it super-hydrophilic - or water-loving, so nothing can stick to it - and also photocatalytic, enabling oxygen ions to break down bacteria and viruses.

Toto toiletImage copyrightToto
Image captionThe device uses oxygen ions to speed up the decomposition of fecal matter stuck to its sides

"You don't have to clean the toilet bowl for over a year," said Ms Campos.

The BBC asked several of Las Vegas' hotels if they might be interested in such a product, but all declined to comment.

However, one smart home expert said the device proved there was still space for innovation beyond hooking things up to the internet.

"It illustrates the notion that tech breakthroughs involve rethinking things," said Frank Gillett from the tech consultancy Forrester Research.

"It's not necessarily about adding anything new."

Potential purchasers should be warned, however, that the device does not totally absolve them of toilet cleaning duties since its cleansing techniques do not extend to spills outside of the bowl.


Thursday, December 17, 2015

Wananchi wa Kenya watamani kuwa na Rais kama Magufuli


Akamatwa Akitorosha Madini Ya Tanzaninte


Hela za Elimu Bure zapatikana Bilioni 131/- zatengwa elimu bure




RAIS John Magufuli amewahakikishia Watanzania kuwa fedha kwa ajili ya kutimiza ahadi ya kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari, zimetengwa Sh bilioni 131 mwezi huu na kupelekwa moja kwa moja katika shule husika.

Amesema Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa, watapatiwa nakala za taarifa za ugawaji wa fedha hizo na kuonya kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayethubutu kuzitumia vibaya.

Rais Magufuli alisema hayo Ikulu Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe aliyemtumia salamu za pongezi kwa kuchaguliwa kuiongoza Tanzania.

Dk Magufuli aliongeza kuwa fedha hizo ambazo ni pamoja na fedha za maendeleo, fedha za mitihani na fedha vifaa vya ku fundishia zitaanza kutumwa kila mwezi kuanzia mwezi huu.

Katika kipindi cha kampeni, Rais Magufuli aliahidi kutoa elimu bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari kidato cha nne na hivi karibuni kupitia Wizara ya Elimu ilitoa waraka maalumu wa kusisitiza agizo hilo la elimu bure.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amempongeza Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk Philip Mpango kwa kazi nzuri ya ukusanyaji wa mapato inayofanywa na mamlaka hiyo.

“Kwa mara ya kwanza mwezi huu ukusanyaji wa mapato hayo unatarajiwa kuwa zaidi ya shilingi trilioni moja na bilioni mia tatu,” alisema Rais Magufuli katika taarifa hiyo iliyotolewa jana na Ikulu.

Rais Magufuli pamoja na mambo mengine, jana alipokea ujumbe maalumu wa maandishi kutoka kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe uliowasilishwa na Waziri wa Nchi anayeshughu likia Mambo ya Nje ya Japan, Seiji Kihara.

Ujumbe huo umemueleza Rais Magufuli kuwa Japan imeridhishwa na hatua ambazo Serikali ya Tanzania inazichukua katika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuahidi kuongeza msukumo kwa upande wa Japan katika kuharakisha utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Japan nchini.

Mjumbe huyo juzi alishuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ujenzi wa njia ya umeme yenye urefu wa kilometa 441.5 kutoka Singida - Manyara - Namanga na kuunganisha hadi Kenya, ambapo Japan imetoa mkopo wa Dola za Marekani milioni 96 ili kufanikisha mradi huo.

WALIOJENGA PEMBEZONI YA BONDE LA MTO MSIMBAZI WAPITIWA NA BOMOA BOMOA

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Manispaa za jiji la Dar es salaam zitafanya zoezi la kuondoa wavamizi maeneo yote ya Mabondeni, kingo za mito  na za Bahari, maeneo ya wazi, maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi zaidi ya 150 katika  jiji la Dar es salaam. Bomoa bomoa ya leo inaendelea katika Bonde la mto msimbazi.Mkuu wa Kitengo cha Sheria Balaza la Taifa la usimamizi wa mazingira Tanzania (NEMC), Manchale Heche akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Bomoabomoa maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi nakuwataka wananchi waliojenga katika fukwe za bahari Kingo za mito na mikondo ya bahari kuhamisha mali zao mapema.
Wananchi wakitoa samani pamoja na vitu mbalimbali ndani ya nyumba zao ili kupisha ubomoaji wa nyumba zilizo maeneo hatarishi. 

WAZIRI KITWANGA AWAPA POLISI SIKU MOJA YA KUJIELEZA NI KWA NINI HAWALINDI BANDARI YA DAR ES SALAAM


Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga ametoa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza ni kwa nini askari hawalindi Bandari ya Dar es Salaam badala yake kazi hiyo inafanywa na kampuni binafsi za ulinzi.
Kitwanga amepanga kukutana na viongozi waandamizi wa Polisi kesho ili kujadili mipango na mikakati mbalimbali ya kuongeza ufanisi wa kazi ya kuwahudumia wananchi.
Akizungumza na maofisa waandamizi wa polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam baada ya kufanya ziara katika Chuo cha Taaluma ya Polisi na kuangalia makazi ya askari, Kurasini, Kitwanga alieleza kusikitishwa na hatua ya polisi kuacha kutoa ulinzi bandarini na kuita kitendo hicho kuwa ni udhaifu wa jeshi hilo.
Alisema kitendo hicho kimetoa mwanya kwa baadhi ya wafanyabiashara kukwepa kodi wakati wa kushusha bidhaa zao akisema Bandari ni eneo la mpaka ambalo linahitaji ulinzi wa polisi kama mipaka mingine ya nchi.
Akionekana kukerwa, Waziri Kitwanga alimkatisha Kamishna wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipojaribu kutoa sababu akimtaka kutumia siku nzima ya leo kuandaa majibu ili kesho wayazungumze kwenye kikao rasmi.
Waziri Kitwanga amelitaka pia jeshi la polisi kumweleza mipango ya kukabiliana na dawa za kulevya kwa sababu ndiyo zimekuwa chanzo cha matukio mengi ya uhalifu ikiwamo tishio la ugaidi.
Alisema haiwezekani kitengo cha kupambana na dawa za kulevya kikaachiwa jukumu hilo wakati jeshi la polisi liko kwenye operesheni zake kila siku.
Kuhusu msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam, waziri huyo alisema ni uzembe wa askari wa usalama barabarani kwa sababu wameshindwa kusimamia sheria na kuwachukulia hatua madereva wazembe.
Alisema zipo nchi za Afrika ambazo hazina askari wa barabarani kwa sababu kiwango cha nidhamu ya madereva wake ni kikubwa na wamekuwa wakifanya vizuri kuhakikisha kwamba suala la msongamano usio wa lazima unadhibitiwa kwa kufuata sheria.
Baadhi ya askari walimweleza Kitwanga kero zao. Mmoja wao, Alphonce Malowa alisema nyumba za askari ni chache na nyingi zimechakaa kiasi cha kuwafanya kudharaulika mbele ya wananchi.
Inspekta Novatus Makondowa alieleza juu ya umuhimu wa Serikali kuwasomesha walimu wa chuo cha taaluma za polisi ili kuwajengea uwezo zaidi wa kufundisha maofisa wengine chuoni hapo. 

New