Rais Jakaya Kikwete kushoto akiwa na Rais Barack Obama
....................................................................................
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, SAID MECK
 SADICK, amesema serikali imechukua tahadhari zote katika kuhakikisha 
shughuli zote za wananchi za kibiashara zinaendelea kama kawaida wakati 
wa ziara ya rais wa Marekani Barack Obama.
Aidha mkuu huyo wa mkoa amesema katika kipindi hicho wafanyabiashara 
kutoka mikoani na ndani ya jiji wataendelea kuingiza bidhaa zao katika 
masoko kama kawaida bila kuzuiliwa, na kwamba si barabara zote 
zitakazofungwa na kutolea mfano wa barabara itakayofungwa kuwa ni 
barabara ya Nyerere ambayo wageni wengi hutumia na kwamba ziara hiyo 
haitaathiri maonesho ya 37 biashara maarufu kama sabasaba yanayoendelea 
katika viwanja vya Mwl. JULIUS NYERERE.
Rais wa Marekani Barack Obama anatarajia kuzuru Tanzania siku ya 
jumatatu ambapo miongoni mwa masuala atakayoangazia ni pamoja na 
kuhamasisha demokrasia na kukuza fursa za kiuchumi.
Maandalizi ya mapokezi ya Rais Obama yamezidi kupamba moto hasa katika 
jiji la Dar-es salaam ambapo ndipo kituo chake cha kwanza kwa rais huyo 
nchini Tanzania huku suala la usafi na matengenezo katika barabara 
nyingi Jijini likionekana kupewa kipaumbele tofauti na siku zote.
Pia  abiria  wa  ndege na  wale wa 
mabasi ya mikoani  wametakiwa  kuripoti mapema  katika  vituo vyao  ili 
 kuepuka kukosa  usafiri siku  hiyo ,huku akitaka mabasi ya mikoani 
ambayo yanaondoka baada ya  saa 3  kuzingatia muda kwani baada ya saa 3 
barabara zitafungwa  hivyo  kukosa kusafiri hadi ugeni utakapoondoka 

No comments:
Post a Comment