Habari zilizoufikia mtandao huu hivi punde kutoka Mkoani Arusha 
zinaeleza kuwa Ndege Ndogo ya Shirika la Ndege la TANZAIR iliyokuwa 
ikitokea Mjini Bukoba kuelekea Jijini Dar es Salaam, imelazimika kutua 
katikati ya Ziwa Manyara lililopo Mkoani Arusha ili kunusuru abiria wake
 sita (6) waliokuwamo katika ndege hiyo baada ya kupatwa na hitilafu kwa
 kuzima ghafla kwa Injini moja wakati ikiwa hewani.
Aidha imeelezwa kuwa katika tukio hilo ni abiria watatu tu ambao 
wamepatwa na majeraha makubwa huku wakipelekwa kupatiwa matibabu katika 
Hospitali ya Sirialni ya Mkoani Arusha, huku wengine wakitazamiwa na 
kuchunguzwa kabla ya kuruhusiwa kuweza kuendelea na safari.
Rubani wa ndege hiyo alilazimika kutaka kutua ghafla katika Uwanja wa 
Arusha, kutokana na Hitilafu hiyo, lakini alishindwa baada ya kuona 
mtikisiko ukizidi na kuamua kuielekeza ndege hiyo katikati ya Ziwa hilo,
 ambapo alifanikiwa kutua salama na baadhi ya Boti na mitumbwi iliyokuwa
 karibu iliweza kusogea na kutoa msaada wa kubeba abiria hao na 
kuwasogeza nchi kavu na baadaye ilifika Helkopta ambayo iliweza kutoa 
msaada zaidi.

No comments:
Post a Comment