UGONJWA wa kisukari ni miongoni mwa magonjwa hatari na
yaliyoenea duniani. Ni ugonjwa ambao ukiupata hauna tiba na mara nyingi
huua iwapo utashindwa kujua kanuni za kuishi nao.
Wataalamu
wanauita ugonjwa huu kama ‘lifestyle disease’ kutokana na ukweli kwamba
staili yako ya maisha ndiyo inayoweza kusababisha ukaupata au
ukauepuka.
Taarifa mbaya zaidi kuhusu ugonjwa huu ni ukweli kwamba kisukari
kimekuwa si ugonjwa wa watu wazima pekee, bali sasa hata watoto na
vijana wadogo wanaugua.
Utafiti wa hivi karibuni uliochapishwa na
Jarida la Diabetes Care umeonesha kuwa vijana wengi wa kati ya miaka
10-29 wanaugua ugonjwa wa kisukari kwa kasi kubwa duniani na kwamba
unagharimu mabilioni ya dola kama gharama za matibabu kwa wagonjwa.
Hivyo, ili kujiondoa katika hatari ya kupatwa na ugonjwa huu, ni vyema
kuzingatia kanuni za ulaji na kula vyakula sahihi, kwani hiyo ndiyo
kinga pekee na hakuna kinga ya vidonge wala sindano. Yafutayo ni mambo
MATANO rahisi ya kubadili staili ya maisha yako ambayo yatapunguza
uwezekano wa kupata kisukari (type II) na pengine kutougua kabisa;
pendelea
kula vyakula vyenye kiwango kikubwa cha ufumwele au kambalishe (fibre)
na utumiapo mafuta, tumia yale yatokanayo na mimea na mboga
(polyunsaturated fats), kama vile alizeti, ufuta, nazi, n.k badala ya
kutumia mafuta yatokanayo na wanyama.
Vyakula vyenye kiwango kikubwa
cha kambalishe ni pamoja na maharagwe, mahindi, ngano, soya, ndizi
mbivu, maparachichi, matufaha (apples), n.k.
Kula kiasi kidogo sana
cha vyakula vilivyopikwa kwa mafuta, hasa yale yatokanayo na wanyama na
bidhaa zitokanazo na maziwa (transfats) ambayo kiafya siyo mazuri sana.
Ukila kwa tahadhari mafuta haya yanayoongeza kolestro mwilini,
utajiepusha pia na ugonjwa wa shinikizo la damu.
Kama wewe ni
mvutaji wa sigara, acha. Moja ya staili ya maisha inayochangia mtu
kupatwa na ugonjwa wa kisukari ni pamoja na uvutaji wa sigara. Licha ya
athari hiyo, athari nyingine ya sigara inajulikana kuwa ni ugonjwa wa
kansa.
Halikadhalika, kama wewe ni mnywaji wa kilevi (alcohol),
punguza kiwango unachokunywa. Wastani unaokubalika kiafya ni ule
usiozidi glasi mbili kwa siku, unywaji wa kupindukia ni hatari kwa afya
yako kwa ujumla na ukiweza kuacha kabisa unywaji wa pombe, ni bora
zaidi.
Mwisho
kabisa, dhibiti uzito wako na kama tayari ni mnene, punguza uzito hadi
ufikie kiwango kinachokubalika kulingana na urefu ulionao. Unaweza pia
kuujua wastani wa unene wako kama unakubalika ama la kwa kupima saizi ya
kiuno chako.
Kwa mwanamke mwenye uzito wa kawaida, saizi ya kiuno
chake hakitakiwi kuzidi inchi 34 na mwanaume hatakiwi kuzidi inchi 36.
Iwapo unavaa suruali au sketi zaidi ya saizi hiyo, basi unashauriwa
kuanza kuchukua hatua za kupunguza unene.
Lishe Kwa waliokwenye hatua ya kutumia dawa,
wanashauriwa kupendelea kutumia vidonge lishe vilivyothibitishwa
kutokuwa na madhara kwa mtumiaji, miongoni mwa hivyo kuna ‘Diabetic
Complex Support’ na inafanya kazi vizuri zaidi endapo mgonjwa atapata na
UngaLishe wake uitwao ‘Diabetic Replace’.
Hizi ni tibalishe ambazo
zinaaminika kuwa na uwezo mkubwa wa kuidhibiti sukari (Blood Sugar
level support), kuisafisha damu pamoja na kujenga upya seli za mwili
zilizoharibika (body degeneration) bila kuacha madhara (side effects)
kwa mtumiaji.