tutazungumzia jinsi ya kuwa na msingi imara kwa biashara yako 
ili idumu kwa muda mrefu na ikuletee faida kwa sasa na siku zijazo!Jambo la kwanza kabla hujaanza ni kuangalia Uwiano wa Thamani wa Biashara yako (The Value Equation).Watu
 wengi sana huanzisha biashara kabla ya kufanya uwiano mzuri wa thamani 
kati ya mtaji utakaotumika na faida wanayotarajia kuipata. Kila mtu huwa
 analifahamu hili akilini mwake kwa kiwango fulani, lakini ni watu 
wachache ambao hujitaabisha vya kutosha kuangalia uwiano kati ya hizi 
pande mbili. Mfano, mama anayetaka kuanza biashara ya maandazi kama 
kitafunwa cha chai asubuhi, huanza kwanza kwa kukokotoa hesabu ya 
gharama ya unga wa ngano, amira, sukari, mafuta, umeme au mkaa 
utakaotumika kuivisha maandazi hayo n.k. Baada ya hapo, mama huyu 
hukokotoa tena mahesabu ya idadi ya maandazi anayoweza kupika, bei 
atakayouzia na faida atakayoipata kwa kila andazi. Kisha kutokana na 
utafiti ambao mama huyu atakuwa ameufanya, maamuzi hufanyika, ama kuanza
 biashara hii au la. Mara nyingi hivi ndivyo ilivyo hata kwa biashara 
nyingine nyingi.
 Watu huangalia japo juujuu gharama za uendeshaji na
 hulinganisha na faida inayoweza kupatikana kisha huingia moja kwa moja 
kwenye biashara.Tatizo kubwa ninaloliona kwa wajasiriamali wengi ni 
kwamba huwa hawauchukulii uwiano huu kiumakini zaidi. Na hii hufanya 
wengi kufunga au kushindwa biashara zao baada ya muda mfupi! Kwa kuwa 
mara nyingi utakuta kuwa mategemeo yao ni tofauti sana na uhalisia 
wenyewe.
 Kwa mfano mtu anayeanzisha shule huwa anakuwa hajaangalia 
ukweli kwamba kuna miezi ambayo shule zinafungwa lakini waalimu hawaendi
 likizo, ikiwa ina maana kwamba japo wanafunzi watakuwa majumbani na 
hawalipi ada, lakini walimu watatakiwa walipwe mishahara kama kawaida. 
Hii huwasababisha wamiliki wa shule kuhamaki hususan mwaka wa kwanza wa 
uendeshaji wa shule.Hivyo kuwa na uwiano mzuri wa thamani ni 
kuyaangalia yote haya. Je, pesa itakuwa inaingia kila siku, kila mwezi 
au kila baada ya miezi mitatu, sita, tisa au mwaka? Je, kiasi 
kinachopatikana kitatosha kulipa mishahara na kulipia gharama za 
uendeshaji?
 Baada ya hapo, je, kutakuwa na akiba kwa ajili ya kukuza
 mtaji na wewe mwenyewe mjasiriamali kulipwa? Mara nyingi ninashangazwa 
na watu wanaokuja kuniomba ushauri wakiwa tayari na pesa mkononi jinsi 
ambavyo wanakuwa hawajayaangalia mambo haya kwa kina. Jiulize maswali 
magumu mengi kadiri uwezavyo kabla hujaamua kuanzisha biashara yako.
 1.
 Je, utanunua bidhaa yako au malighafi kwa kiasi gani? Ni wapi  unaweza 
kupata kiasi kingi au kikubwa kwa gharama ndogo kadiri uwezavyo?2. Gharama za usafiri ni kiasi gani (kama usafiri unahusika) na utapataje kwa bei ndogo kadiri iwezekanavyo?4.
 Sehemu yako ya kuendeshea biashara itagharimu kiasi gani? Malipo 
yatakuwaje? Utakodi? Utapewa bure kwa muda gani (kama inawezekana). 
Itahitaji matengezo au ukarabati kiasi gani?
 5. Utahitaji 
wafanyakazi wangapi wa kuanza nao? Utawalipa kiasi gani? Au utaanza 
mwenyewe na mkeo/mumeo/mwanao/nduguyo n.k? Watanufaika vipi na biashara 
yako? Watafanya kazi kwa muda gani kila siku? Je, watahitaji pesa ya 
chakula cha mchana au itajumlishwa kwenye mshahara?6. Utahitaji vitendea kazi vipi? Mashine (kama utahitaji)? Kompyuta je? Meza? Viti? Vitagharimu kiasi gani?7. Malipo ya kodi yatakuwa kiasi gani? Utalipa kodi za aina ngapi na kwenye mamlaka aina ngapi?8. Gharama za uendeshaji wa biashara yako kila siku ni kiasi gani? Kama vile umeme, usafiri, maji, usafi, simu n.k?
 9. Gharama za uzalishaji/utengezaji au utoaji wa huduma wa siku itakuwa kiasi gani?10. Je, wewe mwenyewe utajilipa kiasi gani kwa wiki, mwezi n.k?
 
No comments:
Post a Comment