My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, September 30, 2012

Bajeti ya Ufaransa kukabiliana na deni

Waziri mkuu nchini Ufaransa, Jean-Marc Ayrault, ameitaja bajeti ya serikali yake ya mwaka 2013 kama silaha dhidi ya madeni ya nchi hiyo yanayo ongezeka kila kukicha.




Huku deni la nchi hiyo likikadiriwa kuwa asilimia tisini ya mapato ya nchi hiyo, bwana Ayrault alisema kuwa bajeti hiyo itajumuisha kuongezwa kwa kodi kwa watu wanaopokea mishahara mikubwa.



Tisa kati ya watu kumi hata hivyo hawataathirika kutokana na kupandishwa kwa viwango vya kodi.



Mpango huo wa serikali unasemekana utaweza kuchangisha dola bilioni ishirini na sita kwa pesa za serikali na kuzuia mipango ya kupunguza matumizi ya pesa za umma ambayo imeathiri nchi nyingi Ulaya.



Alisema kuwa serikali itahakikisha imetumia pesa kulingana na mahitaji ya nchi , yale muhimu yakipewa kipaombele kama elimu, ukosefu wa ajira , usalama na haki.



Katika wiki moja iliyopita, kiwango cha ukosefu wa ajira kimefika zaidi ya watu milioni tatu.

Deadly Kenya grenade attack hits children in church

One child has been killed and six critically hurt, the Red Cross says, in a grenade attack on a church's Sunday school in the Kenya capital, Nairobi.



The attacker targeted St Polycarp's church on Juja Road.


A police spokesman said they suspected sympathisers of Somalia's al-Shabab Islamist militants were to blame.


Kenyan troops are at present part of an African Union force that has forced al-Shabab from its last Somali urban stronghold of Kismayo.


The Daily Nation quoted local police as saying that a number of those hurt at the church were injured in a stampede after the attack.


The police spokesman, Charles Owino, told Reuters news agency: "We suspect this blast might have been carried out by sympathisers of al-Shabab.


The fact that Sunday's bombing has immediately been blamed on "Al-Shabab sympathisers" is hardly surprising, given events in Somalia in recent days.

The hand-grenade, thrown into a crowded public place, is becoming a grimly familiar tactic in Kenya. In the past six months, it has been used in bars in Mombasa, churches in Garissa near the Somali border, as well as churches and a bus station in Nairobi.



All of these attacks have initially been blamed on al-Shabab. But in at least some cases, subsequent reporting has suggested turf-wars between local gangs.



As Kenyan troops push al-Shabab out of its last Somali urban stronghold, Kismayo, there is nervousness about the possibility of a retaliation on Kenyan soil.



Many remember the bombings in Kampala in 2010, which killed 74 people, after Ugandan troops entered Somalia. Whatever the motive of Sunday's bombing, it is not on a comparable scale.

"These are the kicks of a dying horse since, of late, Kenyan police have arrested several suspects in connection with grenades."



Irene Wambui, who was in the church at the time of the attack, said: "We were just worshipping God in church when suddenly we heard an explosion and people started running for their lives.



"We came to realise that the explosion had injured some kids who were taken to hospital and unfortunately one succumbed."



Nairobi police chief Moses Ombati has appealed for calm after youths reportedly attacked the nearby Alamin mosque.


Nairobi and the port city of Mombasa have suffered a series of grenade attacks since Kenya sent troops into Somalia last October.

The attacks in Mombasa escalated after radical Islamist preacher Aboud Rogo Mohammed was killed in a drive-by shooting in August.


In July, 15 people were killed in raids on churches in Garissa, near Kenya's border with Somalia.


There was speculation that al-Shabab or its sympathisers were responsible.


Those attacks prompted the country's Inter-Religious Council chairman to urge a united front against sectarian division.


Adan Wachu told the BBC Network Africa programme at the time: "There are people out there who are determined to make Kenya another Nigeria.

"It's not going to be allowed to have a sectarian division in this country - whoever wants to do that will of course fail."


Attacks on churches in Nigeria have been frequent this year.

Many of them have been blamed on the Boko Haram group, which wants to establish Islamic law in a country where the north is largely Muslim and the south mainly Christian and animist.

Thursday, September 27, 2012

Mkutano maalum kuhusu Mali New York



Waasi wa Tuareg nchini Mali

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa, Ban Ki Moon ameandaa mkutano maalum mjini New York kujadili mzozo unaokumba Mali ambako wapiganaji wa kiisilamu wameteka eneo la Kaskazini mwa nchi hiyo.
Nchi kadhaa za Afrika Magharibi pamoja na Ufaransa zinataka azimio la Baraza la usalama la umoja wa mataifa, litakalo wawezesha kuunga mkono hatua za kijeshi dhidi ya kile wanachokiita magaidi wa Kaskazini mwa Mali.
Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, aliambia mkutano wa baraza kuu la umoja wa mataifa, Jumanne, kuwa Ufaransa iko tayari kuunga mkono juhudi za kuirejeshea Mali hadhi yake kama nchi huru.
Jeshi la pamoja la nchi za Magharibi mwa Afrika lijulikanalo kama ECOMOG, na ambalo limewahi kuingilia kati mizozo katika baadhi ya nchi za Afrika, linasema kuwa takriban wanajeshi elfu tatu, wana kibarua cha kutwaa eneo la Kaskazini kutoka kwa wapiganaji hao.
Lakini mwandishi wa BBC anasema kuwa viongozi wa Afrika wanatafuta uungwaji mkono kutoka kwa Baraza la usalama la umoja wa mataifa kabla ya kupeleka wanajeshi huko.

Malema ''Sitishiki na hatua ya mahakama''



Julius Melama akiwahutubia wafanyakazi wa migodi waliokuwa wanagoma
Julius Malema amewaambia wafuasi wake kuwa katu hatishiki na uamuzi wa mahakama kusema kuwa ana kesi ya kujibu.
Mahakama hii leo ilimwachilia kwa dhamana Malema anayekabiliwa na shtaka la kuhaulisha pesa.
Malema ambaye aliwahutubia wafuasi wake nje ya mahakama, pia anatuhumiwa kwa kutumia nafasi yake ya zamani kama kiongozi wa tawi la vijana la ANC kujitajirisha yeye na washirika wake wa biashara.
Washirika wake wengine wanne nao walikabiliwa na mashtaka sawa na hiyo katika kesi yao iliyosikilizwa hapo jana.
Katika hotuba yake kwa mamia ya wafuasi wake nje ya mahakama mjini Polokwane, bwana Malema alisema ataendelea na juhudi zake za kutetea maelefu wanaoishi katika umaskini nchini humo.
Seng'enge zilizungushwa katika eneo la mahakama hiyo iliyopo Polokwane, mji mkubwa wa jimbo analotokea mwanasiasa huyo,Limpopo.
Wafuasi wake wanasema mashtaka hayo yameshinikizwa kisiasa.
Wakiimba na kucheza nje ya mahakama hiyo wafuasi wengi wa chama hicho cha ANC tawi la vijana walishikilia mabango yaliosema 'Muacheni kiongozi wetu'.
Maafisa wa usalaman walidhibiti ulinzi na kulikuwa na utulivu mkubwa.
Julius Malema na washirika wake wa kibiashara wanashutumiwa kwa kufaidi kutokanana na mikataba ya serikali katika jimbo la Limpopo, tuhuma ambazo anazikana. Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 31 pia anachunguzwa katika kesi tofauti ya ukwepaji kulipa ushuru.
Malema ni maarufu sana Afrika Kusini kwa ukakamavu wake wa kutetea maslahi ya wananchi na maisha yake ya kifahari, huku akijitambulisha kama mpiganiaji uhuru wa uchumi.
Alitimuliwa kwenye chama hicho tawala mnamo mwezi Aprili akishutumiwa kwa kuzusha migawanyiko katika chama hicho.
Ni mkosoaji mkali wa a Jacob Zuma, hivi karibuni akimshutumu rais huyo kwa alivyoushughulikia mgomo wa wachimba migodi wa Marikana.
Kwa mujibu wa mwandishi wa masuala ya Afrika, Andrew Harding, baadhi ya watu Afrika kusini wanaamini anafikishwa haraka mahakamani, ikiwa ni chini ya wiki moja baada ya kutolewa waranti ya kukamatwa kwake, ili kuimarisha nafasi ya kisiasa ya Zuma.
Mwandishi wetu anaeleza kwamba huenda ikawa ni kesi ya muda mrefu, ambayo huenda ikatoa nafasi ya kujulikana ukweli kuhusu suala hilo la rushwa, ambalo watu wengi wanaamini inaitia nchi hiyo doa

Sudan na S.Kusini zakubaliana



Mazungumzo kati ya nchi hizo mbili yalifanyika nchini Ethiopia

Sudan na Sudan Kusini zimeafikia makubaliano kuhusu mgogoro wa mpaka na uzalishaji wa mafuta.
Baada ya mazungumzo ya siku ya nne, nchi hizo mbili zimeafikiana kuruhusu usafirishaji wa mafuta kutoka kusini kupitia mabomba ya Kaskazini na kuondoa wanajeshi mpakani.
Viongozi wa nchi hizo mbili hatimaye walikubaliana baada ya mazungumzo ya siku nne mjini Addis Ababa Ethiopia.
Lakin maswala kadhaa muhimu yangali kutatuliwa ikiwemo kuafikia makubaliano kuhusu mipaka inayozozaniwa ikiwa ni mojawpao ya kilichosababisha mgogoro ambao nusura utumbukize nchi hizo kwenye vita mapema mwaka huu.
Baada ya mapigano kuzuka kuhusu mzozo wa mafuta na mipaka, Umoja wa mataifa ulitishia kuziwekea pande zote mbili vikwazo ikiwa hazitaafikia makubaliano ya kina.
Wapatanishi wa Muungano wa Afrika wangali kuthibitisha kuwa makubaliano yameafikiwa lakini rais wa Sudan Omar al-Bashir na mwenzake wa Kusini Salva Kiir, wanatarajiwa kutia saini makubaliano hayo hii leo.
Maelezo yametolewa tu kwa mukhtasari lakini wapatanishi wa pande zote mbili, walisema kuwa wamekubaliana kuhusu eneo la nchi hizo mbili ambalo halina ulinzi wa kijeshi.
Pia makubaliano ya kiuchumi yaliafikiwa kuruhusu Sudan Kusini kuanza tena shughuli zake za kuzalisha mafuta.
Lakini mwafaka haukupatikana kuhusu eneo linalozozaniwa la Abyei wala mipaka mingine mingi ambayo nchi hizo zinazozania.
Kwa hivyo makubalino hayo hayajaweza kutimiza masharti ya Umoja wa Mataifa kwa nchi hizo kuafikia mkataba unaotatua mzozo huo kwa kina.

Utoaji mimba wahalalishwa Uruguay

Bunge la Congress nchini Uruguay limepitisha sheria ya kuhalalisha utoaji mimba katika hali zinazokubalika.
Bunge hilo limepitisha sheria hiyo kufuatia majadiliano makali yaliyoishia kwa wabunge hao wa Congress kuipitisha kwa kura 50 dhidi ya 49.
Sasa hoja hiyo itawasilishwa katika bunge la juu la Senate ambalo linatazamiwa kuiidhinisha.
Sheria hiyo itawaruhusu wanawake kutoa mimba kabla haijafika wiki 12 ilimradi wamepata ushauri nasaha kutoka kwa madaktari wasiopungua 3 ili kufahamishwa hatari za kuavya mimba.
Mbali na Cuba, Uruguay itakuwa nchi ya kwanza katika ukanda wa Amerika kusini kuruhusu mwanamke yeyote anayetaka kutoa mimba fursa ya kufanya hivyo.

Tuesday, September 25, 2012

MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP)



Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.

MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.
Inadaiwa kuwa Oktoba 21 mwaka jana katika  maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala, jijini Dar es Salaam Mchungaji Mtikila alitoa maneno ya uchochezi, dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.
Akizungumza na mtandao huu baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema "Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa amenijibu".
Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili lingine baada ya mtu mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) akimtuhumu Mchungaji Mtikila kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa viwanja. Baada ya kutaka kukamatwa na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo, Mchungaji alikataa kwa madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa hivyo hawezi kukamatwa na polisi mwenye cheo cha Koplo, labda polisi mwenye cheo cha SSP (Senior Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo polisi alishindwa kumtia nguvuni.

Trafigura lazima ishtakiwe



Maefu ya watu waliugua kutokana na taka hizo za simu

Wanaharakati nchini Uingereza wanataka kampuni ya Trafigura kufunguliwa mashtaka kwa hatua yake ya kutupa taka yenye sumu nchini Ivory Coast mwaka 2006.
Uchunguzi wa miaka mitatu wa mashirika ya Amnesty International na Greenpeace umeonyesha udhaifu wa serikali za Magharibi kushindwa kuzuia kumwagwa kwa taka yenye sumu nchini Ivory Coast mwaka 2006.
Trafigura, kampuni ya uchukuzi ya Uholanzi iliyo na matawi yake jijini London, iliilipa kampuni ya Ivory Coast kumwaga uchafu huo karibu na bandari ya Abidjan.
Watu elfu mia moja walikwenda hospitali kwa matibabu. Wanaharakati hao wanateta kuwa serikali za Uingereza na Uholanzi zimeshindwa kuzuia kumwagwa kwa sumu au kuwawajibisha Trafigura.
Kampuni hiyo imekanusha madai hayo na kusema kuwa ripoti hiyo ina taarifa zisizo za kweli.
Kampuni hiyo ni mojawapo ya kampouni kubwa duniani za usafiri na imekuwa ikijitetea ikisema kuwa taka hiyo haikuwa na na sumu na wala haikuhatarisha maisha ya watu.
Mnamo mwezi agosti mwaka 2006, familia kadhaa mjini Abidjan ziliamka na kukumbana na harufu mbaya yenye mvuke wa sumu.
Taka hizo za kemikali zilikuwa zimeletwa katika eneo hilo kwa meli ya kampuni iliyokuwa imekodiwa na kampuni ya Trafigura na kisha kutupa taka hizo katika eneo lenye taka.
Kampuni hiyo imekana kuwa taka hizo zingeweza kusababisha ugonjwa na kuelezea kuwa ilikuwa imelipa kampuni moja mwenyeji kuweza kutupa taka hiyo kwa njia sawa kisheria.

Afueni kwa wanafunzi wa Kenya



Wanafunzi darasani Kenya 

Shule za umma nchini Kenya zimefungua hii leo baada ya wiki tatu za mgomo wa walimu.
Walimu hao hatimaye waliweza kuafikia makubaliano na serikali kuhusu matakwa yao ya nyongeza ya mishahara.
Serikali ilitishia kuwafuta kazi walimu hao Ijumaa wiki jana wakati walipokataa pendekezo la asilimia 4 ya mishahara ambalo serikali ilitoa.
Lakini makubaliano hatimaye yaliafikiwa mwishoni mwa wiki ya nyongeza ya asilimia arobaini.
Sasa mwalimu atakayepokea mshahara mdogo zaidi kuliko wote atalipwa dola 140 huku mwenye kulipwa mshahara mkubwa akipata dola 1,700 .
Sekta ya umma nchini Kenya imekumbwa na migomo katika wiki chache zilizopita. Hospitali za umma ambazo pia zilishuhudia mgomo wa madaktari, zinawahudumia tu wagonjwa walio katika hali ya dharura.
Vyuo vikuu vya umma navyo vilifungua siku ya Jumatatu baada ya wahadhiri ambao pia walikuwa wanagoma kurejea kazini.
Kupanda kwa gharama ya maisha na mkakati duni wa serikali kuweza kushughulikia matatizo ya wananchi hususan swala la mishahara ndio mojawapo ya sababu ya kutokea kwa migomo hii.
Walimu hao 200,000 walitaka nyongeza ya asilimia miamoja hadi miatatu .
Kulingana na makubaliano hayo yaliyotiwa saini na waziri wa fedha Njeru Githae na chama cha kitaifa cha walimu, marupurupu ya walimu pia yataongezeka hasa kwa wale wanaofanya kazi katika mazingira magumu na wale wanaowahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Mitihani ya mwisho wa kidato cha nne na darasa la nane ilitaakhirishwa kwa wiki tatu ili kuwawezesha wanafunzi kuajindaa vilivyo.

Msako dhidi ya Boko haram



Waathiriwa wa mashambulizi ya Boko Haram 

Takriban wapiganaji 35 wa kundi la kiisilamu la Boko Haram, wameuawa katika msako mkali dhidi ya kundi hilo Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa jeshi la Nigeria, wapiganaji wengine sitini walikamatwa wakati wa msako huo kwenye majimbo ya Adamawa na Yobe.
Kundi hilo la kiisilamu, linapinga mifumo ya kimagharibi na athari zake nchini Nigeria na wamekuwa wakifanya mashambulizi yanayolenga maslahi ya nchi za Magharibi pamoja na makanisa.
Mnamo siku ya Jumapili, kulitokea shambulizi dhidi ya kanisa moja katoliki na ambalo lilisababisha mauaji ya watu wawili. Boko Haram ndilo limelaumiwa kwa kufanya shambulizi hilo.
Msemaji wa jeshi nchini humo, alifahamisha shirika la habari la AFP kuwa msako huo ulifanyika usiku kucha kati ya siku ya Jumapili na Jumatatu.
Wanajeshi walifanya msako wa nyumba hadi nyumba, katika mitaa mitatu na wakati mwingine kufyatuliana risasi na wapiganaji hao, usiku kucha.
Wanajeshi wawili walijeruhiwa katika makabiliano hayo.
Bunduki na mabomu vilipatikana katika maficho ya wanamgambo hao pamoja na silaha zengine ikiwemo mishale 32 na panga.
Mji huo umekuwa mojawapo ya miji iliyoathirika sana kutokana na harakati za Boko Harama ambalo linataka kutumika kwa sheria za kiisilamu kote nchini humo.

Masaibu ya watoto wa Syria



Masaibu ya watoto wa Syria walionaswa katika vita 

Shirika la kutetea haki za watoto Save the Children, limekusanya maelezo ya kutisha na kuogofya kuhusu visa vinavyowakumba watoto katika vita vinavyoendelea nchini Syria.
Shirika hilo limekusanya ushahidi kutoka kwa watoto waliotoroka vita na ambao wameelezea dhulma na mateso waliyokumbana nayo.
Kwa mujibu wa shirika hilo, kila mtoto aliyehojiwa na ambaye ameweza kutoroka Syria, ameelezea kuona jamaa wake angalau mmoja akiuawa.
Shirika hilo linasema kuwa limehoji mtoto mwenye umri wa miaka 15, aliyechomwa kwa sigara,wakati alipokuwa amefungwa katika iliyokuwa shule yake.
Mtoto mwingine alizungumzia kupigwa na umeme huku akiishi katika chumba kimoja na maiti.
Ingawa shirika hilo halikutoa taarifa rasmi kuhusu nani aliyetenda mateso hayo, limeisisitizia Umoja wa Mataifa kuchukua hatua dhidi ya wanaotenda dhulma hizo.

Friday, September 21, 2012

Waziri mkuu mpya wa Ethiopia



Hailemariam Desalegn

Waziri mkuu mpya wa Ethiopia Hailemariam Desalegn, ameapishwa kuchukua wadhifa wa hayati Meles Zenawi aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 21.
Mwingine aliyeapishwa ni naibu wake Demeke Mekonen, ambaye alikuwa anashikilia wadhifa wa waziri wa elimu.
Bwana Hailemariam Desalegn, amenukuliwa na shirika la habari la AFP akisema kuwa ana furaha kuchukua wadhifa huo na yuko tayari kufanya majukumu yake kwa kujitolea.
Hailemariam aliungwa mkono bila pingamizi na bunge la waakilishi ambalo lina wanachama wengi wa muungano tawala kuchukua wadhifa huo
Sherehe ya kumuapisha waziri mkuu huyo iliendeshwa na rais wa mahakama ya juu zaidi nchini humo, Tegene Getaneh na kuonyeshwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa.
Hayati Zenawi alifariki mwezi jana mjini Brussels baada ya kuugua kwa muda mrefu.

New