Na Luqman Maloto
 VIONGOZI wakuu wa Dini ya Shetani, Freemasons, wamefanya kafara nzito  kuadhimisha kukamatwa, kuteswa kisha kuuawa kwa aliyekuwa Kiongozi wa  Libya, Muammar Gaddafi.
Vyanzo vimesema kuwa ni kawaida kwa  Freemasons kufanya sherehe yenye mrengo wa kafara kila mara, mpango wao  unapofanikiwa sehemu yoyote ile.
Kwa mujibu wa mitandao kadhaa inayojihusisha na utoaji wa habari za  jamii ya Freemasons, kafara ambayo hufanywa ni ile ya mnyama hususan  mbuzi mwenye pembe zinazofanana na zile za jini anayeitwa Lucifer (jini  mkuu) ambaye huabudiwa na wafuasi wa Dini ya…
Na Luqman Maloto
 VIONGOZI wakuu wa Dini ya Shetani, Freemasons, wamefanya kafara nzito  kuadhimisha kukamatwa, kuteswa kisha kuuawa kwa aliyekuwa Kiongozi wa  Libya, Muammar Gaddafi.
Vyanzo vimesema kuwa ni kawaida kwa Freemasons kufanya sherehe yenye  mrengo wa kafara kila mara, mpango wao unapofanikiwa sehemu yoyote ile.
Kwa mujibu wa mitandao kadhaa inayojihusisha na utoaji wa habari za  jamii ya Freemasons, kafara ambayo hufanywa ni ile ya mnyama hususan  mbuzi mwenye pembe zinazofanana na zile za jini anayeitwa Lucifer (jini  mkuu) ambaye huabudiwa na wafuasi wa Dini ya Shetani.
Mnyama huyo huchinjwa kisha damu na kichwa chake huhifadhiwa kwenye  chombo chochote chenye muundo wa ndoo ili pembe zitokeze kwa juu na  kutengeneza alama maarufu ya Freemasons ambayo wafuasi wake huitumia kwa  njia ya vidole kutoa salamu.
Habari zinasema Freemasons walifanya kafara hiyo usiku wa manane kwenye  hekalu moja kubwa lililojengwa kwenye eneo la jangwa lililopo ndani ya  Jiji la Misrata, Libya.
Inabainishwa kuwa viongozi mbalimbali wakubwa kwenye nchi zilizoendelea  kiuchumi ambao wana vyeo vikubwa ndani ya jamii ya Freemasons,  walihudhuria kafara hiyo.
MKAKATI HATARI
Habari zinabainisha kuwa Freemasons ipo kwenye mkakati thabiti wa kuitawala dunia kabla ya Desemba 2012.
Kutokana na mkakati huo, imebainishwa kuwa Freemasons wamekuwa  wakiratibu sera zao kwa kuangusha utawala wa nchi mbalimbali ambao  viongozi wake wameshindwa kuendana na matakwa yake.
Inaelezwa kuwa Gaddafi alikuwa kiongozi mwenye mrengo wa Kiislam japo  alikuwa haweki wazi kwenye utawala wake na kwamba alikuwa anapingana  vikali na Freemasons.
Kwa mujibu wa mnajimu msomi, Maalim Hassan Yahya Hussein, Jeshi la  Kujihami la Umoja wa Nchi za Magharibi (Nato), hutekeleza mipango ya  Freemasons kama lilivyofanya Libya kumng’oa Gaddafi.
Maalim Hassan ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mnajimu maarufu barani  Afrika, marehemu Sheikh Yahya Hussein, alisema kuwa dhumuni kuu la  Freemasons ni kuzipiga vita dini za Kiislam na Kikristo.
“Ipo wazi kuwa wao lengo lao ni kuitawala dunia, kwa hiyo wanahakikisha  hilo linawezekana kwa kudhoofisha Uislam na Ukristo ili ufe kisha  Shetani ashinde hapa duniani,” alisema Maalim Hassan ambaye ni mrithi wa  kazi za unajimu za marehemu Sheikh Yahya.
Aliongeza: “Mkakati mkubwa zaidi ni kuhakikisha dunia inaabudu Dini ya  Shetani, wanataka kila mtu awe chini ya mamlaka ya jini mkuu (Lucifer).  Dunia nzima itawaliwe na serikali moja na iwe na sarafu moja.”
Kauli ya Maalim Hassan inashabihiana na ile iliyopo kwenye maandiko  kwamba zama za Dini ya Shetani kuishika dunia, kutakuwa na mfumo ambao  utazuia mtu yeyote kupata huduma za kijamii mpaka awe mwanachama na  atatambulika kwa chapa 666.
Habari zaidi zinaeleza kuwa Freemasons wanatumia njia mbalimbali  kuhakikisha ulimwengu mzima hakuna anayeamini dini za Mungu na  wanapambana kuhakikisha hata Yesu (Nabii Isa) atakaporejea akute hakuna  aliye tayari kukombolewa.
Katika kuhakikisha wanapambana na nguvu ya Yesu, Freemasons wamekuwa  wakitumia damu ndiyo maana hutoa kafara kwa kuchinja mnyama hasa mbuzi  au kondoo wenye pembe kwa imani kwamba huwaongezea nguvu ya kuishika  dunia.
Kutokana na tishio la Freemasons, viongozi wa kidini hususan wale wa  Mashariki ya Kati, wamekuwa wakiwataka Waislam na Wakristo kwa imani  zao, kufunga na kusali ili Dini ya Shetani isipate mafanikio  inayoyataka.
SAKATA LA USHOGA
Habari zinasema kuwa Serikali ya Uingereza imekuwa ya kwanza kutumiwa na  Freemasons katika kuhakikisha nchi zote zinazounda Jumuiya ya Madola  zinapitisha sheria zinazokinzana na maandiko matakatifu yanayoaminiwa na  waumini wa Dini za Kiislam na Kikristo.
Ushoga na usagaji ni vitendo ambavyo vinakemewa na dini hizo lakini hivi  sasa, Freemasons wanadaiwa kuchochea mabadiliko ili watu wanaojihusisha  na hulka hizo wawe huru kikatiba duniani.
Hivi karibuni, Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, alitangaza kuwa  mwanachama wa Jumuiya ya Madola ili apate misaada inabidi kwanza aruhusu  ndoa za jinsi moja (ushoga na usagaji) kwenye katiba ya nchi yake.
Tanzania ikiwa moja ya wanachama wa Jumuiya ya Madola, inapitiwa kwenye  rungu hili, ingawa Balozi wa Uingereza nchini, Diana Corner alisema nchi  yetu haihusiki.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe  alishatoa tamko kwamba Tanzania haipo tayari kuruhusu ndoa za mashoga na  wasagaji kisha akaonya kuwa kauli ya Cameron inaweza kuivunja Jumuiya  ya Madola.
SIYO FREEMASONS PEKE YAKE
Mbali na Freemasons, dini nyingine zenye mrengo wa Shetani ni Illuminati na Skull & Bones ambazo zinavuma zaidi Marekani.
VIGOGO WA FREEMASONS
Viongozi wanaotajwa kuwa vigogo wa jamii hiyo ni marais wa 43 na 44 wa  Marekani, Barack Obama na George Bush, Rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy  ambao wanaonesha alama za vidole ukurasa wa kwanza. Yupo pia Cameron na  wengine wengi.
No comments:
Post a Comment