Mataifa ya Afrika Magharibi 
yanajitayarisha kukamilisha mipango yao ya kuingilia kijeshi nchini 
Mali, kuwaondoa wapiganaji wa Kiislamu walioteka zaidi ya nusu ya nchi 
hiyo kufuatia jaribio la kupindua serikali mwezi Machi.
Lakini hadi sasa ni mataifa machache tu ya Afrika Magharibi ambayo yamejitolea kutoa wanajeshi kwa kikosi hicho.
Baadae juma hili, Umoja wa Mataiafa, wakuu wa Ulaya na Umoja wa Afrika watajumuika na wawaikilishi wa Mali mjini Bamako, kujaribu kutafuta mkakati imara wa kuingia Mali kijeshi.
No comments:
Post a Comment