Mwanadada Nguyen Thi Phuong alivyokuwa kabla ya kutumia dawa za asili.
Nguyen Thi Phuong alivyo baada ya kutumia dawa za asili.
NGUYEN Thi Phuong ni mwanadada mwenye asili  ya Vietnam, ukimuangalia huenda ukadhani ni bibi wa miaka 73 lakini ni  binti mdogo mwenye umri wa miaka 26.
Mrembo huyo, aligeuka mzee mwaka 2008 na kwa mujibu wa madaktari, tatizo hilo amelipata baada ya kutumia dawa za asili.
Wakati  anakutwa na tatizo hilo, Nguyen  alikuwa na umri wa miaka 23. Kipindi  hicho alikuwa mrembo mwenye sura ya kuvutia lakini hivi sasa hana raha,  kwani sura yake ni ya kikongwe.
Pamoja na madaktari kusema hivyo,  Nguyen  anaamini kuwa hali aliyonayo imesabishwa na aina ya samaki wa  baharini  aliokuwa anakula ambao  ndiyo  wamemsababishia mzio (aleji)  mwilini. 
Nguyen akiwa na mumewe, Thanh Tuyen.
Mume wa Nguyen, ambaye ni fundi seremala, Thanh Tuyen, alisisitiza kuwa pamoja na mkewe kuzeeka, bado anampenda kama zamani.
Tuyen  alisema, kinachomsikitisha ni kwamba yeye na mkewe hawajapata mtoto na  kutokana na hali ngumu kiuchumi aliyonayo, hajui kama Nguyen anaweza  kupona na kushika ujauzito, kwani hivi sasa ni kama amezeeka.
Kutokana na namna Nguyen alivyoharibika, amekuwa akitembea amevaa kinyago (maski) ili kuficha uso wake.
“Wakati naanza kuumwa nilikuwa najisikia maumivu mwili mzima, pia nilikuwa nawashwa wakati wa kulala,” alisema Nguyen.
Nguyen  aliendelea kusema kuwa baada ya maumivu aliamua kutafuta dawa kwenye  maduka ya madawa ya kawaida kwa sababu yeye na mume wake hawana uwezo wa  kununua dawa zinazofaa kwa sababu ya umaskini.
NI UGONJWA GANI?
Madaktari  wanafafanua kuwa ugonjwa alionao Nguyen unaitwa Lipodystrophy ambao  husababisha kuyeyuka kwa mafuta ya chini ya ngozi, hivyo kusinyaa na  mhusika kuonekana mzee.
Wataalamu hao wamesema kuwa mwili wa Nguyen una kiwango kikubwa sana cha cortisol iliyotokana na mitishamba.
Ugonjwa huo unatajwa kuwapata wanawake wengi ambao wana umri kati ya miaka 20 na 40.
Daktari Vo Thi Bach Suong wa Hospitali ya  HCMC, amejitolea kumsaidia Nguyen kwa kumpa matibabu yatakayomuwezesha kupona kabisa.
No comments:
Post a Comment