Mkurugenzi
 Mtendaji wa Tanesco Bw. William Mhando, amesimamishwa kazi leo kupisha 
uchunguzi juu ya tuhuma dhidi yake za ubadhirifu na matumizi mabaya ya 
madaraka.
 Bodi
 ya wakurugenzi ya  Shirika la Umeme Nchini -TANESCO- imemsimamisha kazi
 Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO Mhandisi WILLIAM MHANDO ili kupisha 
uchunguzi wa tuhuma mbalimbali zinazoelekezwa dhidi ya Menejimenti ya  
TANESCO.  
          Taarifa
 hiyo imetolewa  na mwenyekiti wa bodi hiyo Jenerali Mstaafu ROBERT 
MBOMA ambapo katika taarifa yake amesema maamuzi hayo  yamefikiwa katika
 kikao cha dharura kilichofanyika jana kujadili masuala mbalimbali 
ikiwemo tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.
Taarifa
 zinasema katika kikao hicho, Bodi iliona tuhuma hizo ni nzito hivyo ni 
 vyema zikafanyiwa uchunguzi huru na wa kina mara moja.
Jenerali MBOMA katika taarifa hiyo amesema uchunguzi huo utaanza mara moja kwa  kutumia mchunguzi huru.
Aidha
 Bodi hiyo, leo imefanya kikao kingine cha dharura ambapo imeamua  
kuwasimamisha kazi mara moja wafanyakazi wengine wakiwemo naibu 
mkurugenzi mtendaji,  huduma za Shirika Ndugu ROBERT SHEMHILU, afisa 
mkuu wa fedha Ndugu LUSEKELO  KASSANGA na meneja mwandamizi, manunuzi 
Ndugu HARUN MATTAMBO.
Jenerali
 MBOMA amesema kufuatia hatua hizo zilizochukuliwa, Bodi imechukua hatua
  stahiki ili kuhakikisha shughuli za kiutendaji na uendeshaj wa TANESCO
  zinaendelea kama kawaida.
No comments:
Post a Comment