Waziri Mkuu Mstaafu Bw. Frederick 
Sumaye akimsisitiza jambo Bw.Martin Sanya mara baada ya kumkabidhi tunzo
 pamoja na kitita cha shilingi Mil 3.8 ya mwamuzi bora wa ligi kuu ya 
Vodacom 2011/2012, Anaeshuhudia kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na
 Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bw. Kelvin Twisa.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick 
Sumaye katikati akishuhudia Mh.Mbunge wa Tabora mjini ambae ni 
Mwenyekiti wa Simba Sports Club Elden Rage akipongezwa na Mkuu wa 
kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bw.Kelvin Twisa mara baada ya kupokea 
tunzo ya golikipa bora kwa niaba ya Juma Kaseja,wakati wa hafla ya kutoa
 tunzo kwa msimu ulioisha wa ligi kuu ya Vodacom.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick Sumaye akiongea wakati wa hafla ya kutoa tunzo kwa msimu ulioisha wa ligi kuu ya Vodacom.
Meneja Mahusiano ya nje wa Vodacom 
Tanzania Bw.Salum Mwalim (kushoto) na Meneja Mahusiano wa kampuni hiyo 
Matina Nkurlu wakifuatilia hotuba ya Waziri Mkuu Mstaafu Bw. Frederick 
Sumaye ambae alikuwa mgeni rasmi kwenye hafla ya kutoa tunzo kwa msimu 
ulioisha wa ligi kuu ya Vodacom.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick 
Sumaye akimpongeza Msemaji msaidizi wa Azam FC Jaffer Iddi Maganga 
alipoenda kupokea tunzo ya vijana kwa niaba ya Rashid Mandawa wa Coastal
 Union wakati wa hafla ya kutoa tunzo kwa msimu ulioisha wa ligi kuu ya 
Vodacom,iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania katika Hoteli ya Dobble Tree, 
anaeshuhudia kulia ni Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa 
Vodacom Bw.Kelvin Twisa.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick 
Sumaye katikati akishuhudia Mwenyekiti wa Azam FC Mohamed Said 
akipongezwa na Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bw.Kelvin Twisa
 mara baada ya kupokea tunzo ya mfungaji bora na timu ya nidhamu na 
kocha bora kwa niaba ya klabu yake wakati wa hafla ya kutoa tunzo kwa 
msimu ulioisha wa ligi kuu ya Vodacom, iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania
 katika hoteli ya Dobble Tree jijini Dar e Salaam.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick 
Sumaye akimkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Milioni kumi na tano 
na laki tano Katibu wa Yanga Bw.Selestini Msigwa wakati wa hafla ya 
kutoa tunzo kwa msimu ulioisha wa ligi kuu ya Vodacom, iliyoandaliwa na 
Vodacom Tanzania katika hoteli ya Dobble Tree jijini Dar e 
Salaam,anaeshudia katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano 
wa Vodacom Tanzania Bw.Kelvin Twisa.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick 
Sumaye kushoto akishuhudia Mwenyekiti wa Azam FC Mohamed Said 
akipongezwa na Mkuu wa kitengo cha Masoko na Mawasiliano Bw.Kelvin Twisa
 mara baada ya kupokea hundi yenye thamani ya shilingi Milioni ishirini 
na mbili kwa kuibuka washindi wa pili katika msimu 2011/2012 wa ligi kuu
 ya Vodacom wakati wa hafla ya kutoa tunzo kwa msimu ulioisha wa ligi 
kuu ya Vodacom,iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania katika hoteli ya Dobble
 Tree jijini Dar e Salaam.
Waziri
 Mkuu Mstaafu Bw.Frederick Sumaye kushoto akimkabidhi hundi yenye 
thamani ya shilingi milioni hamsini Mh.Mbunge wa Tabora mjini ambae ni 
Mwenyekiti wa Simba Sports Club wakati wa hafla ya kutoa tunzo kwa msimu
 ulioisha wa ligi kuu ya Vodacom,katikati ni Mkuu wa kitengo cha Masoko 
na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania Bw.Kelvin Twisa.
Waziri Mkuu Mstaafu Bw.Frederick 
Sumaye akipiga picha ya ukumbusho na baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom 
Tanzania wakati wa hafla ya kutoa tunzo kwa msimu ulioisha wa ligi kuu 
ya Vodacom.Iliyoandaliwa na Vodacom Tanzania katika hoteli ya Dobble 
Tree Jijini Dar e Salaam.
MWANDISHI WETU
WAZIRI Mkuu mstaafu Frederick Sumaye 
ameeleza kusikitishwa kwake na kupoteza umaarufu wa soka la Tanzania kwa
 sasa ukilinganisha na miaka ya 1970.
Sumaye alisema hayo juzi 
katika hoteli ya Double Tree By Hilton ya jijini Dar es Salaam katika 
hafla ya kuwatunuku washindi mbalimbali waliofanya vema kwenye ligi kuu 
ya Vodacom msimu wa 2011/2012.
Alisema hali hiyo inatokana na timu vilabu 
nguli vya Simba na Yanga kubweteka kwa moja kuifunga nyenzake na kujiona
 zimefika peponi kitu ambacho si dalili nzuri katika maendeleo ya soka.
“Simba kuifunga Yanga au Yanga kuifunga 
Simba si kigezo kizuri cha kujiona ni timu nzuri, timu inatakiwa 
iangalie ushindani kimataifa …ndiyo maana hata wakipangiwa timu kutoka 
Misri, Ivory Coast n.k mnaingiwa na hofu kubwa,”alisema.
“zamani vilabu vya nje vilikuwa vikipangwa 
na timu za Tanzania zinatetemeka lakini sisi sasa…kama tunataka kurudi 
katika heshima yetu ya zamani tujipange kimataifa, “aliongeza Sumaye.
Aidha, Sumaye alisikitishwa na migogoro 
katika vilabu na kusema inachangia pia kudidimiza soka hivyo amewataka 
viongozi kuhakikisha wanafanya kazi kwa ushirikiano sambamba na 
kuvihudumia ipasavyo vilabu vyao.
Sumaye ambaye ni mpenzi mkubwa wa mabingwa 
wa ligi kuu soka Tanzania Bara Simba, alitumia fursa hiyo kuwaasa 
mashabiki na wanachama wa timu za Simba na Yanga kuzomeana uwanja pindi 
moja ya timu inapokuwa uwanjani.
“Muwe wapinzani katika michezo lakini si 
uhasama, lazima tuwe na urafiki baina yetu na kuonyesha uzalendo zaidi 
kwa Simba kuishangilia Yanga ikicheza na timu ya nje au Yanga 
kuishangili Simba ikicheza na timu ya nje,”aliongeza.
Sumaye pia alitumia nafasi hiyo kuwapongeza
 washindi wote na kuwataka kutovimbishwa vichwa na zawadi hizo badala 
yake wazitumie kama kichocheo cha kujibiidiisha zaidi.
Awali Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa 
Vodacom Kelvin Twisa alisema kampuni yake imetoa zaidi ya shilingi 
milioni 113 kama zawadi za washindi hao na hivyo kufanya mwaka huu zwadi
 kuongezeka tofauti na mwaka jana zilikuwa shilingi milioni 90.8.
“Tunajivunia kuwa wadhamini wa ligi kuu 
bara ambapo vipaji vingi vimeonekana na viwango vya kuvutia pia katika 
mechi zote na ndio maana hii leo tupo katika kutoa zawadi kwa 
washindi,”alisema.
Katika halfa hiyo, ilitambulishwa tuzo mpya
 inayohusisha wachezaji vijana waliofanya vema kwenye timu hizo ambapo 
waliotwaa ni pamoja na Rashid Mandawa (Coastal Union), Hassan Dilunga 
(Ruvu Shooting) na Frank Damayo aliyekuwa anaichezea JKT Ruvu na sasa 
amesajiliwa Yanga ambapo kila mmoja alizawadiwa shilingi milioni moja.
Azam Fc ilifanikiwa kuongoza kwa kutwaa 
tuzo tano ikiwemo ile ya nafasi ya pili iliyowapatia sh.mil.22, timu 
yenye nidhamu (mil.7.8), kocha bora-Stewart Hall (mil.3.8), mfungaji 
bora- John Bocco (mil.3.9) na mchezaji bora- Aggrey Morris (mil.3.3).
Aidha mabingwa Simba walitwaa mil.50, huku 
kipa wake Juma Kaseja alitwaa tuzo ya kipa bora na kuzawadiwa Mil.3.3, 
wakati Yanga ilizawadiwa mil.15 kwa kushika nafasi ya tatu na Martin 
Sanya alitwaa tuzo ya mwamuzi bora na kuzawadiwa mil.3.8.
Ligi kuu ya Vodacom msimu wa 2011/2012 
ilianza kutimua vumbi Agosti 20,2011 na kumalizikia Mei 6, 2012 na 
kuvishirikisha vilabu 14 vikiwemo Simba, Yanga, Azam Fc, African Lyon, 
Kagera Sugar, Mtibwa Sugara, Toto Africans, Moro United, JKT Ruvu, Ruvu 
Shooting, Coastal Union, Polisi Dodoma na Oljoro JKT.
  
  | 
| Mgeni rasmi, Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye kushoto akiwa na Meneja Masoko wa Vodacom Kevin Twisa 'Kifaa' | 
  | 
| Katikati
  ni Sumaye, kulia Twisa na kuhsoto Mwenyekiti wa Simba SC, Alhaj Ismail
  Aden Rage Mbunge wa Tabora Mjini (CCM) na mmiliki wa kituo cha Redio 
cha  Voice Of Tabora | 
  | 
| Ofisa Habari wa TFF, Boniphace Wambura kulia | 
  | 
| Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala kushoto na rafiki zake | 
  | 
| Twisa akihutubia | 
  | 
| Mwenyekiki wa Simba, Rage kulia, Mwenyekiti wa Azam, Mzee Mohamed Said katikati na Katibu Mkuu wa Yanga, Celestine Mwesigwa   | 
  | 
| Waziri Mkuu wa zamani, kipenzi cha Watanzania, Sumaye | 
  | 
| Msaidizi wa Sumaye, Chombo kulia akizungumza na bosi wake | 
  | 
| Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah kulia, katikati Twisa wakiwa na Sumaye | 
  | 
| Wadau, Dina Ismail kushoto na Mohamed Mharizo | 
  | 
| Warembo wa Vodacom | 
  | 
| Maswahiba
  wa miaka nenda, rudi, Grace Hoka, Mhariri wa BINGWA na Dina Ismail, wa
  dinaismail.blogspot.com ambaye pia ni Mwandashi wa Habari za Michezo  
Mwandamizi wa gazeti la Tanzania Daima | 
  | 
| Twisa kulia na Sumaye  | 
  | 
| Rage na Sumaye wakiteta | 
  | 
| Sumaye | 
  | 
| Sumaye | 
  | 
| Sumaye | 
  | 
| Sumaye | 
  | 
| BIN ZUBEIRY | 
  | 
| Mzee Said kulia, Mwesigwa na Jaffar Iddi, Msemaji wa Azam  | 
  | 
| Vimwana wa Vodacom na mataji, tuzo mbalimbali walizokabidhiwa washindi | 
  | 
| Refa bora, Martine Sanya kulia akipokea tuzo yake kutoka kwa Mh Sumaye. Kushoto ni Twisa  | 
  | 
| Rage amkimpokelea tuzo Kaseja | 
  | 
| Mzee Said akipokea tuzo | 
  | 
| Mwesigwa akipokea hundi ya Yanga | 
  | 
| Mzee Said akipokea tuzo ya Azam FC | 
  | 
| Rage akipokea hundi ya Simba SC | 
  | 
| Angetile akipongezana na Mh Sumaye | 
  | 
| Wadau wa Yanga, katika picha ya pamoja na Mh Sumaye | 
  | 
| Wadau wa Simba SC katika picha ya pamoja na Mh Sumaye | 
  | 
| Angetile kulia na kushoto Wambura katika picha ya pamoja na Sumaye | 
  | 
| Frank damayo | 
  | 
| Mlimbwende | 
  | 
| Damayo akipokea tuzo yake | 
  | 
| Damayo akichukua msosi | 
  | 
| Mh Mbunge na kiungo wa zamani wa Simba SC, Rage 'akifakamia'  | 
  
 JUMA
 Kaseja, kipa wa Simba SC usiku huu ameibuka kipa bora wa Ligi Kuu ya 
Vodacom Tanzania Bara na kujinyakulia kitita cha Sh. Milioni 3.3 kutoka 
kwa wadhamini Vodacom.
 Katika
 hafla ya kukabidhi tuzo za washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom 
zilizofanyika kwenye hoteli ya Double Tree By Hilton, Masaki, Dar es 
Salaam, beki wa Azam FC, Aggrey Morris alishinda tuzo ya Mchezaji Bora 
wa msimu wa Ligi Kuu.
 Aidha,
 Azam FC washindi wa pili wa Ligi Kuu walitwaa pia tuzo za timu yenye 
nidhamu, wakati kocha waom, Stewart Hall kutoka Uingereza, aliibuka 
kocha bora, mshambuliaji wake John Bocco ‘Adebayor’ aliibuka mfungaji 
bora. 
 Katibu
 Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Angetile Osiah pia 
alitambulisha tuzo maalum kwa wachezaji chipukizi waliopandishwa kutoka 
timu za vijana na kufanya vizuri katika timu za wakubwa.
 Katika
 tuzo hizo, kiungo mpya wa Yanga, Frank Damayo sambamba na Rashid 
Mandawa wa Coastal Union na Hassan Dilunga wa Ruvu Shooting, kila mmoja 
alitwaa Sh. Milioni 1.
 Katika
 hafla hiyo, ambayo mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa zamani, Frederick
 Sumaye, mwamuzi Martin Sanya alishinda tuzo ya refa bora, wakati bingwa
 Simba alizawadiwa Milioni 50, mshindi wa pili Azam Milioni 22 na Yanga 
aliyekuwa wa tatu Milioni 15.5.
 
 
 
No comments:
Post a Comment