Kwa takribani muda wa juma moja 
sasa kumekuwepo na taarifa katika vyombo vya habari na njia mbalimbali 
za upashanaji habari, kuwa kampuni moja ya meli inayodaiwa kutoka Iran, 
inayojulikana kwa jina la NITC (National Iranian Tanker Company), 
inatumia bendera ya Tanzania, isivyo kihalali na kinyume kabisa na 
sheria za nchi na zile za kimataifa, kwa malengo ambayo hayajulikani.
Pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya 
Zanzibar kutoa taarifa kwenye Baraza la Wawakilishi tarehe 2 Julai 2012 
kukanusha taarifa hizo, Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) 
kinaitaka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania   kupitia kwa 
Waziri wa Mambo ya Nje na Waziri wa Uchukuzi kutoa taarifa kwa umma juu 
ya hatua ilizochukua kuchunguza madai hayo.
Aidha, Serikali ya Jamhuri ya Muungano
 wa Tanzania ieleze iwapo utaratibu huo umezingatia kwa ukamilifu United
 Nations Convention law of the Sea, kifungu cha 91,  Geneva Convention 
of Registration kifungu cha 6 na maazimio mengine ya kimataifa kuhusu 
usajili wa meli kubwa pamoja na usafirishaji wa mafuta.
Maelezo yaliyotolewa na Serikali ya 
Umoja wa Kitaifa Zanzibar inayoongozwa na CCM na CUF yanaibua maswali 
kutokana  na kampuni ya Philtex ya Dubai inayoelezwa kupewa uwakala na 
Mamlaka ya Usafiri wa Baharini- Zanzibar Maritime Authority (ZMA) 
kufanya kazi na makampuni mengine hivyo taarifa hizo hazijitoshelezi 
katika kuondoa uwezekano kwamba meli za NITC zilipeperusha bendera ya 
Tanzania.
Ili kujisafisha juu ya tuhuma hizo 
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ilipaswa kushirikiana na Serikali ya 
Muungano kufanya uchunguzi wa kubaini msingi wa tuhuma hizo na kuchukua 
hatua iwapo meli za NITC zilipeperusha bendera ya Tanzania bila 
ridhaa  ya serikali zote mbili.
Ikumbukwe kwamba hii si mara ya kwanza
 kwa baadhi ya maofisa wa ZMA kutuhumiwa kuruhusu vitendo vilivyo 
kinyume na sheria kama ilivyojitokeza wakati wa kashfa ya kuzama kwa 
meli ya Spice Islender.
Kwa upande mwingine, Serikali ya 
Muungano nayo haiwezi kukwepa kuwajibika kwa kuzingatia kuwa kuwa baadhi
 ya taarifa hizo katika vyombo vya habari vimewanukuu mawaziri wa 
serikali wakionekana kujikanyanga na kujikanganya juu ya suala hili 
nyeti la bendera ya taifa, ambayo ni moja ya utambulisho wetu rasmi kama
 Watanzania, kutumika kwa malengo yasiyojulikana na kampuni ya nje.
Moja ya vyombo vya habari hapa nchini,
 vimewanukuu mawaziri husika, Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe na 
Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe, juu ya 
suala hilo. 
Wakati Waziri Mwakyembe amenukuliwa 
akisema kuwa anazo taarifa za suala hilo, lakini asingeweza kulitolea 
kauli mpaka Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa Tanzania Zanzibar 
azungumze, Waziri Membe yeye mbali ya kukiri kuwa kitendo hicho ni kosa 
kisheria, anasema habari hizo zilikuwa za kushtushwa na ngeni kabisa, 
huku akisema kuwa vyombo husika vitalichunguza kwa makini.
Ukimya wa serikali yetu ambayo kwa 
hakika unatokana na udhaifu wake katika kuchukua maamuzi, sasa 
umesababisha kitendo hicho kutafsiriwa kuwa Tanzania inaibeba na 
kuisaidia Iran kukwepa vikwazo ambavyo nchi hiyo inatishiwa na mataifa 
ya Magharibi, hasa Marekani na Umoja wa Ulaya, kutokana na malumbano ya 
muda mrefu ambayo yanatokana na mataifa hayo kutumia mabavu na vitisho 
kuzichagulia baadhi ya nchi nyingine duniani, nini cha kufanya na 
rasilimali zake mathalani mzozo unaoendelea na Iran kuhusu urutubishaji 
wa madini ya urani. 
Si nia ya CHADEMA kuingia katika 
mgogoro wa Iran na Mataifa ya Magharibi hapa kupitia mjadala wa madai 
hayo yaliyoandikwa kwenye vyombo vya habari; lakini CHADEMA kinatoa 
tamko kufuatia ukimya na kigugumizi kinachoikumba Serikali ya CCM, kila 
inapohitajika kufanya maamuzi ya haraka, hasa kuwalinda watu wake na 
hadhi ya utaifa wao na nchi yao ndani na nje ya nchi.
Ni kutokana na udhaifu wa serikali 
hii, ambayo umekuwa ukijidhihirisha pia kwa kushindwa kupanga bajeti 
inayojitegemea hasa kwa kutumia utajiri mkubwa wa rasilimali ambazo nchi
 hii imebarikiwa, hali inayotufanya tuonekane taifa ombaomba na kupoteza
 heshima mbele ya mataifa makubwa na madogo, kuwa hatuna uwezo wa akili 
kuweza kujitegemea. 
Utegemezi huu umefanya baadhi ya raia 
wa Nchi nyingine mathalani Mbunge aitwaye Howard Berman wa Bunge la 
Marekani, akiwa kama Mwenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Nje, kupata 
uwezo wa kuandika barua ya dharau na kejeli kwa Rais Jakaya Kikwete, juu
 ya suala hilo la Meli za NIT kutuhumiwa kupeperusha bendera za 
Tanzania.
Kupitia tamko hili, CHADEMA tunaitaka 
serikali kutoa kauli madhubuti juu ya suala hilo ambalo tayari 
limechukua sura ya mjadala wa kimataifa usiokuwa na tija yoyote kwa 
mustakabali wa Watanzania. Suala la bendera ambayo ni utambulisho wa 
taifa letu, haliwezi kuwa suala la mchezo tu, ambapo mawaziri wazima 
hawawezi kutoa kauli za kina na kuchukua hatua zinazostahili.
Imetolewa tarehe 2 Julai 2012 na:
Hamad Mussa Yussuf
Naibu Katibu Mkuu Zanzibar
 
      
Tanzania
 is seriously investigating allegations that it re-flagged Iranian oil 
tankers in defiance of sanctions. A US congressman alleged last week 
that up to 10 Iranian oil tankers had been re-registered in 
Tanzania. But the East African nation's foreign minister said so far 
there was no evidence to suggest this was true and he appealed for help 
with the probe. The US and the European Union have just tightened 
sanctions on Iran over concerns about its nuclear programme.
On Sunday, a complete European Union oil
 embargo on Iran came into effect - in response to US legislation, which
 sanctions any entity that deals with Iran's Central Bank. Tanzania's 
neighbour Kenya on Wednesday said it had cancelled plans to import crude oil from Iran following threats of sanctions.
Flags of convenience
Howard Berman, who chairs the US House of Representative's Committee on Foreign Affairs, wrote to President Jakaya Kikwete last Fridayabout his concerns that Tanzania had allowed National Iranian Tanker Company vessels to re-flag. "If
 Tanzania were to allow Iranian vessels to remain under Tanzanian 
registry, we in the Congress would have no choice but to consider 
whether to continue the range of bilateral US programs with Tanzania," 
the US politician warned.
In a briefing to journalists on 
Thursday, Tanzania's Foreign Minister Bernard Membe said that if any 
Iranian ships had been re-flagged, they would be removed from Tanzania's
 shipping register. But he had received assurances from the Iranian 
embassy and a shipping agent in Dubai that no Iranian ships have been 
re-flagged. "We're calling on the international community, particularly 
the United States and European Union, to determine whether or not the 
statements... are correct or not," Mr Membe said. "If it is confirmed 
that the ships flying Tanzania's flag are indeed from Iran, we will take
 steps to deliberately obliterate the registration."
The BBC's international development 
correspondent Mark Doyle says the use of so-called flags of convenience 
is common, though controversial, for legitimate trade. But the flags are
 also sometimes flown as a way of trying to hide the origin of vessels 
and their cargo. On Wednesday, Sierra Leone's government said it would 
ban any ships flying its flag from violating international 
sanctions. The move came after reports that two ships, using a Sierra 
Leonean flag of convenience, had carried Syrian oil products against the
 aims of US and European sanctions imposed to try to prevent President 
Bashar al-Assad's access to foreign exchange.
No comments:
Post a Comment