Katibu
 Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiwa na Mkewe, anayefuatia ni Naibu  Katibu 
Mkuu, Dkt. Asha-Rose Migiro akiwa na Mumewe,  Profesa Cleophas  Migiro 
wakisubiri kusalimiana na wageni waalikwa wakati wa hafla ambayo  Ban Ki
  Moon aliandaa maalum kwajili ya kumuaga msaidizi wake wa Karibu.
Profesa Migiro akiwa na Bint yake, Chansa- Jasmin wakifuatilia hafla hiyo kwa makini.
Ban
 Ki Moon akizungumza wakati wa hafla hiyo ambapo amempogeza na  
kushukurusu sana Migiro kwa namna alivyokuwa mshauri wake na mwalimu  
wake ambaye a anasema kwa  ualimu wake anampa alama ya plus plus plus. 
akatumia  hafla hiyo kutangaza kwamba anamteua   Dkt. Asha- Rose Migiro 
kuwa  mjumbe wake maalum katika  masuala ya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi  
  Barani  Afrika. Migiro anaondoka  baada ya kuutumikia Umoja wa 
 Mataifa  kwa miaka mitano na nusu.
Dkt.
 Asha-Rose Migiro akizungumza wakati wa hafla hiyo, akatoa shukrani  
zake kwa  Ban ki Moon kwa kumpatia heshima hiyo ya kihistoria ambayo  
haita kaa ifutike na kwamba  ameupokea uteuzi huo kwa mikoni miwili na  
hasa kutokana na kwamba tatizo la ugonjwa wa ukimwi ni tatizo ambalo  
analichukulia kwa uzito wa aina yake.
Na
 Chiaziiiiiiiiiiiiiiiii iligongeshwa, Katibu Mkuu akitakiana kila la  
kheri na Naibu  Katibu Mkuu, Dkt. -Asha Rose Migiro, kulia ni Mkurugenzi
  wa Ofisi ya Naibu Katibu Mkuu, Bw. Anyanga.
Dkt. Migiro akimtambulisha Mume wake kwa mmoja wa wageni waalikwa.
Bi Amina Mtengeti  akinywa kinywaji chake baada ya kigongeshana chiaziiiiii na Katibu Mkuu  Ban Ki Moon.
Dkt. Asha- Rose Migiro akiteta jambo na Katibu Mkuu Ban Ki Moon.
Hata
 kupiga picha naweza. Naibu Katibu Mkuu akinyaka  tukio hili la  picha 
wakati Katibu Mkuu Ban Ki Moon akizungumza na Bint wa mwisho wa  Migiro 
Chansa Jasmin.
Sehemu ya wageni waalikwa.
Na Mwandishi Maalum
Katibu
  Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, amemteua  Naibu Katibu Mkuu  
anayemaliza muda wake, Dkt, Asha-Rose Migiro kuwa  mjumbe wake maalum  
katika masuala ya ukimwi na ugonjwa wa ukimwi Barani Afrika.
Ban
  Ki Moon ametangaza uteuzi huo wakati wa hafla maalum aliyoiandaa  
mahsusi kwaajili ya kumuaga  Naibu Katibu Mkuu wake,ambaye anahitimisha  utumishi wake wa  miaka mitano na nusu   katika nafasi ya Unaibu katibu Mkuu. 
Hafla
  hiyo imefanyika   siku ya alhamisi katika viunga vya Umoja wa Mataifa,
  na kuhudhuriwa na wageni waalikwa  mbalimbali wakiwamo mabalozi na wakuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa.
“Ninatangaza rasmi kwamba ninamteua dkt.  Asha- Rose Migiro kuwa  mjumbe wangu maalum katika masuala ya ukimwi na ugonjwa wa Ukimwi Barani  Afrika. Akasema  Ban Ki Moon tangazo lililoshangiliwa kwa nguvu na wageni waalikwa.
Akiongea kwa hisia, Ban Ki Moon, ameeleza
  kwamba ingawa Migiro alikuwa naibu katibu mkuu wake, lakini amekuwa  
mwalimu wake, amejifunza mengi toka kwake na daima ataendelea kuenzi  
mchango wake mkubwa.
“ Kama
  ni kuvaa viatu vyake, naweza kusema ningechekesha sana,  kwa ufupi  
siwezi kuvaa viatu vya Migiro, amekuwa msaada mkubwa sana kwangu,  
ameniwakilisha vema kila mahali nilipomtuma  hata katika mazingira magumu na ya hatari,  kote ameniwakilisha vema sana, kama  mwalimu wangu, na kama profesa wangu anastahili alama ya juu sana” akasema  Ban Ki Moon na kushangiliwa.
Akamuelezea  Migiro kama kiongozi si tu mwadilifu, lakini mwanadiplomasia  aliyebobea, aliyefanya kazi kubwa,ngumu na nzito kwa moyo mkunjufu, uhodari , umakini, na uadilifu wa hali ya juu sana.
“  Siyo rahisi kuelezea yale aliyoyafanya nyuma ya pazia, namna gani alivyochapa kazi kwa nguvu, 
  yapo mengi makubwa ambayo Migiro ameyafanya na  kuyakamilisha kwa  
uadilifu wa hali ya juu. Migiro ni mwanadiplomasia aliyebobea lakini ni 
 mtu wa vitendo, vitendo ambavyo lazima utaona matunda yake” akabainisha
  Ban Ki Moon
Na kuongeza “  Migiro  amefanya kazi na viongozi wagumu,  kiwamo aliyekuwa  Rais wa Libya Muammar  Quadaff aliyethubutu hata kumrushia katiba ya Umoja wa Mataifa, amezikuna nyonyo za watu wengi wakiwamo watu wanyonge na wenye matatizo mbalimbali. Migoro  unaondoka, lakini Umoja wa  Mataifa  hauta sahau mchango wako. Hapa ni nyumbani kwako, na nitaendelea kuomba msaada wako na ushirikiano wako, bado nitaendelea kukuhitaji” akasisitiza Ban Ki Moon
  Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  akatumia fursa hiyo kuishukuru  
serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  kwa kumruhusu Migiro  
kwenda kuitumikia jumuia ya kimataifa.
“ Ninapenda  kutoa shukrani zangu za pekee kwa  jamhuri ya muungano wa Tanzania, kwa kumtoa Migiro katika utumishi wake wa Umma kuja kunisaidia , kwa serikali ya Tanzania na  watanzania nasema asanteni sana” akasema Ban Ki Moon..
Kwa
  upande wake, Naibu Katibu Mkuu dkt. Asha-Rose Migiro amesema anaupokea
  kwa mikono miwili uteuzi wa kuwa mjumbe maalum wa Katibu Mkuu katika  
masuala ya Ukimwi.
Akasema   masuala ya  ukimwi na ugonjwa wa ukimwi, ni eneo ambalo limo ndani ya moyo wake  na kwamba anashukuru kuona kwamba Katibu Mkuu anamuamini kwamba anaweza kumsaidia. Akaahidi kwam atalitekeleza  jukumu  hilo kwa  heshima  kubwa.
Akamshukuru
  Ban Ki Moon, kwa kumuamini kwamba anaweza kumsaidia kama naibu Katibu 
 Mkuu, na akamshukuru pia kwa ushirikiano mkubwa na uhusiano mkubwa  
uliojengeka kati yake na Ban Ki Moon lakini pia kati yake na wasaidizi  
wake.  Ushirikiano ambao anasema ulichagiza utendaji kazi  kufanikisha dira na matarajio ya  Katibu Mkuu.
“Katibu Mkuu amenipa heshima ya kihistoria, heshima ya kuwa msadizi wake,  ni heshima kubwa kwangu na kwa yeyote
  atakayekuja kuandika historia yangu, kwa namna yoyote ile hawezi  
kukwepa  kumtaja  Ban Ki Moon, naomba nikushukuru sana kwa heshima hii  
kubwa uliyonipa” akasema Migiro.
Hafla hiyo pia imehudhuriwa  na familia ya Naibu Katibu Mkuu ikijumuisha  mume wake, Profesa  Cleophas Migiro,  mdogo wa  Naibu Katibu Mkuu, Bi. Amina  Mtengeti na mtoto wa  mwisho wa Migiro Chansa Jasmin.
Naibu
  Katibu Migiro anakuwa mwanamke wa pili kushika wadhifa huo na mwanamke
  mwafrika wa kwanza. Lakini pia ni naibu katibu mkuu ambaye amehudumu  
katika wadhifa huo kwa miaka mitano na nusu.
No comments:
Post a Comment