
Timu
 ya England ya soka imeondolewa katika mashindano ya Euro 2012, baada ya
 kufungwa na Italia usiku wa Jumapili katika robo fainali, kwa kufungwa 
magoli 4-2 ya penalti mjini Kiev, Ukraine, kufuatia muda wa kawaida na 
dakika 30 zaidi kumalizika kwa timu hizo mbili kutofungana.
Italia sasa itapambana na Ujerumani katika mechi ya nusu fainali.
Alessandro
 Diamanti alifunga bao la kuamua mshindi katika mikwaju hiyo ya penalti,
 baada ya Ashley Young na Ashley Cole kukosa kufunga mabao kupitia 
mikwaju waliyopiga.
Vijana
 wa meneja Roy Hodgson ilikuwa wazi walilemewa katika mchezo mzima, 
lakini ni hali ya imani na uvumilivu iliwafanya kuwa na matazamio ya 
kuishinda Italia.
Italia iliweza kugonga mwamba, na bao la Antonio Nocerino lilikataliwa baada ya mwamuzi kusema aliotea mpira.
Kadri
 mechi ilivyoendelea, ndivyo wachezaji wa England nao walionekana 
wachovu, na ikielekea walitazamia bahati zaidi kuliko kujitahidi 
kuimarisha kiwango cha mchezo wao, na penalti kwao bila shaka ikawa sio 
za kutegemewa tena.
Baada
 ya mechi, nahodha Steven Gerrard alisema: "Wachezaji walicheza kadri ya
 uwezo wao wote. Nilidhani tungelipata bahati katika mikwaju ya penalti,
 lakini mambo hayakuwa hivyo. Ukiongoza katika penalti, unashikilia 
matumaini kwamba mambo yatasalia hivyo, lakini Italia ndio waliokuwa na 
bahati. Vijana waliokuwa walinzi walifanya kazi nzuri mno, na kuiletea 
nchi fahari, lakini tunarudi nyumbani na mioyo ya huzuni, na hili ni 
jambo gumu kulikubali."
No comments:
Post a Comment