My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, April 15, 2013

Nauli mpya za mabasi yaendayo mikoani

Dar -Iringa
Ordinary Bus Tsh18300, Semi Luxury Bus Tsh26300, Luxury Bus Tsh28900.

Dar -Mtwara 
Ordinary Bus Tsh21500, Semi Luxury Bus Tsh29700, Luxury Bus Tsh32600.

Dar -Arusha 
Ordinary Bus Tsh22700, Semi Luxury Bus Tsh32800, Luxury Bus Tsh36000.

Dar -Babati
Ordinary Bus Tsh29000, Semi Luxury Bus Tsh41800, Luxury Bus Tsh45900.

Dar -Bukoba
Ordinary Bus Tsh55100, Semi Luxury Bus Tsh77300, Luxury Bus Tsh85000.

Dar -Dodoma 
Ordinary Bus Tsh16700, Semi Luxury Bus Tsh24100, Luxury Bus Tsh26400.

Dar -Kigoma
Ordinary Bus Tsh58800, Semi Luxury Bus Tsh80900, Luxury Bus Tsh88900.

Dar -Lindi 
Ordinary Bus Tsh17800, Semi Luxury Bus Tsh24400, Luxury Bus Tsh26800.

Dar -Mbeya
Ordinary Bus Tsh30700, Semi Luxury Bus Tsh44300, Luxury Bus Tsh48700.

Dar -Moro
Ordinary Bus Tsh 7100, Semi Luxury Bus Tsh10300, Luxury Bus Tsh11300.

Dar -Moshi
Ordinary Bus Tsh19800, Semi Luxury Bus Tsh28500, Luxury Bus Tsh31300.

Dar -Musoma
Ordinary Bus Tsh50800, Semi Luxury Bus Tsh73200, Luxury Bus Tsh80500. 

Dar -Mwanza
Ordinary Bus Tsh42600, Semi Luxury Bus Tsh61400, Luxury Bus Tsh67500.

Dar -Shinyanga
Ordinary Bus Tsh36600, Semi Luxury Bus Tsh52700, Luxury Bus Tsh57900.

Dar -Singida
Ordinary Bus Tsh25500, Semi Luxury Bus Tsh36800, Luxury Bus Tsh40400.

Dar -Songea 
Ordinary Bus Tsh35000, Semi Luxury Bus Tsh50600, Luxury Bus Tsh55500. 

Dar -Sumbawanga
Ordinary Bus Tsh45100, Semi Luxury Bus Tsh62100, Luxury Bus Tsh68200. 

Dar -Tabora
Ordinary Bus Tsh39000, Semi Luxury Bus Tsh54700, Luxury Bus Tsh60100.

Dar -Tanga 
Ordinary Bus Tsh12800, Semi Luxury Bus Tsh18500, Luxury Bus Tsh20300.

Dar -Kibaha
Ordinary Bus Tsh1000, Semi Luxury Bus Tsh1500, Luxury Bus Tsh1600.

Mbowe, Slaa: Hatukubali Chadema kuhujumiwa

  
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akizungumza kwenye kongamano la chama hicho lililofanyika jana jijini Dar es Salaam. 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa wamesema “hawatakubali wala kuvumilia” hujuma dhidi ya chama chao.
Dar es Salaam.

Viongozi hao kwa nyakati tofauti jana walisema hujuma hizo zimekuwa zikifanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na Serikali ambayo imekuwa ikitumia vyombo vya dola na kwamba sasa wanapanga ugaidi wa kuwateka maofisa wa ngazi ya juu wa Chadema.
Suala la ugaidi liliibuka kwa nguvu katika wiki ya kwanza ya Bunge la Bajeti na sasa limehamia nje ya chombo hicho cha kutunga sheria kutokana na Chadema kuwatuhumu CCM na Serikali yake kwamba wanapanga njama za kuwateka maofisa wakuu wa chama hicho.
Jana Dk Slaa alipokuwa akimkaribisha Mbowe kufungua  Mkutano wa Mafunzo na Mipango ya Vuguvugu la Mabadiliko ‘M4C’ na Kongamano la Katiba Mpya kwa Kanda ya Dar es Salaam na Pwani, alisema taarifa walizonazo zinaonyesha kuwa CCM ndiyo wanaofanya vitendo vya kigaidi wakishirikiana na Serikali.
“Tuna taarifa zote zinazoonyesha kwamba CCM ndiyo magaidi wakishirikiana na  Serikali yake, lakini sisi tuko makini kuliko hata Serikali ya CCM na tuko makini kuliko hata Usalama wa Taifa na umakini huu ndiyo utakaotupeleka Ikulu mwaka 2015,”alisema Dk Slaa.
Hata hivyo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipotafutwa kujibu tuhuma hizo alisema hakuna jipya ambalo Chadema wamelisema.
“Kuna jipya katika hilo, ni yale yale ya kawaida na jana (juzi) Mwingulu alizungumza vizuri sana bungeni. Hiyo ni sawa na mchawi anapomwangia mtu na kufa anakuwa wa kwanza kwenda kulia msibani, nchi siku yoyotete haijengwi kwa ngonjera za maneno bali inajengwa kwa mipango,”alisema Nape.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alipotakiwa kutoa msimamo wa Serikali juu ya tuhuma hizo alisema, “Mimi siwezi kuzungumza ila mtafute Waziri (Dk Emmanuel Nchimbi),”alisema Silima.
Alipotafutwa Dk Nchimbi kupitia simu yake ya  mkononi, ilikuwa ikiita bila kupokewa.
Kauli ya Mbowe
Kwa upande wake Mbowe alisema, CCM imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali kuhakikisha inakisambaratisha chama hicho bila mafanikio.
“Watu wa Usalama wa Taifa wakishirikiana na CCM wamekuwa wakifanya mipango ya kutaka kuwateka maofisa wetu. Hawa watu ni wepesi sana na msiwaogope hata kidogo,”alisema Mbowe huku akishangiliwa na wanachama na makada waliofurika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl.
Mbowe alisema: “Ukiona chama chochote tawala kinatumia jeshi la polisi kutengeneza ushahidi wowote wa kihalifu hiyo ni dalili ya hatari kwa mustakabali wa usalama wa nchi.”
Mbowe alisema mbinu za sasa za CCM zinatokana na kushindwa kukivuruga chama hicho kwa propaganda kuwa ni chama cha familia, ukabila, ukanda na baadaye udini.
Katiba na Elimu
Kuhusu mchakato wa Katiba Mpya, Mbowe alisema ikiwa itafika Aprili 30 mwaka huu bila hatua zozote kuchukuliwa, watamwamuru mjumbe wa tume hiyo kutoka Chadema, Profesa Mwesiga Baregu kujiondoa

bilionea Sambeke; Ni mfanyabiashara maarufu aliyefariki kwa ajali ya ndege


Ndege aina ya Cessna  5H-QTT  ikiwa imeanguka eneo la Kisongo,  karibu na Uwanja wa Ndege Arusha  juzi jioni, baada ya kugonga mti wakati ikijiandaa kutua  na kusababisha kifo cha mmiliki wake na aliyekuwa rubani, Bob Sambeke(katika picha ndogo juu).
Huu ni msiba wa tatu katika muda wa mwezi mmoja kwani mwishoni mwa mwezi jana, Wakili na Mfanyabiashara maarufu mkoani Arusha, Nyaga Mawalla alifariki dunia, ikiwa ni siku moja tagu kufariki ghafla kwa mfanyabiashara mwingine wa madini wa mkoani humo
 
Arusha/Moshi.
Kwa mara nyingine, Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha imetikiswa, kutokana na kifo cha mfanyabiashara maarufu katika mikoa hiyo, Joseph Sambeke (49) maarufu kama Bob Sambeke.
Bob Sambeke alifariki dunia juzi jioni baada ya kuanguka na ndege ndogo aliyokuwa akiiendesha, kilomita moja kutoka Uwanja wa Ndege wa Arusha wakati akitokea mkoani Kilimanjaro.
Huu ni msiba wa tatu katika muda wa mwezi mmoja kwani mwishoni mwa mwezi jana, Wakili na Mfanyabiashara maarufu mkoani Arusha, Nyaga Mawalla alifariki dunia, ikiwa ni siku moja tagu kufariki ghafla kwa mfanyabiashara mwingine wa madini wa mkoani humo, Henry Nyiti.
Ndege ya Sambeke aina ya MT 7- namba 5H-QTT ilianguka saa 12.34 jioni baada ya bawa lake kugonga mti katika eneo la Magereza linalopakana na uwanja huo.
Alijeruhiwa na baadaye alifariki akiwa njiani wakati akiwahishwa hospitalini na askari wa Magereza ambao wanaishi katika kambi alipoanguka. Mazishi yake yamepangwa kufanyika Alhamisi eneo la Karanga, Moshi.
Meneja wa Uwanja wa Ndege Arusha, Ester Dede alithibitisha jana kutokea kwa ajali hiyo, na kueleza kuwa taarifa za awali zinaonyesha ndege hiyo ni mali ya marehemu Mawalla ambaye alikuwa mbia wa biashara na Bob Sambeki na imesajiliwa kupitia Kampuni ya Quality Tours & Travellers.
Hata hivyo, Wakili Alex Msando, ambaye pia alikuwa mshirika wa Mawalla, aliliambia gazeti hili kuwa Sambeke alikuwa ameinunua ndege hiyo kutoka kwa marehemu.
Dede alisema ndege hiyo, ilianguka mita 200 kutoka njia namba 8 ya kuruka ndege katika uwanja huo ikitokea Kilimanjaro, katika dakika 15 za muda wa nyongeza wa matumizi ya uwanja huo.
Alisema ndege hiyo ikiongozwa na rubani Bob Sambeki ina uwezo wa kubeba watu wanne akiwamo rubani. Baadhi ya walioshuhudia tukio hilo, walisema kabla ya kuanguka ndege hiyo, ilikuwa ikiyumba na iligonga mti mkubwa katika moja ya mabawa yake na kupoteza mwelekeo.
Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo, Julias Laizer alisema kwamba aliona ndege hiyo ikigonga mti na kuyumba, kisha kudondoka chini na ndipo askari wa magereza walipojitokeza kutoa msaada. Laizer alisema Sambeki alikuwa peke yake na alijeruhiwa kichwani.
 

Bashir aamuru mipaka Sudan kufunguliwa



Rais Omar al-Bashir na Salva Kiir

Marais wote wawili wameamua kushirikiana kwa maslahi ya mataifa yao
Rais Omar al-Bashir wa Sudan, katika ziara yake ya kwanza mjini Juba tangu nchi ya Sudan ya Kusini kuwa huru mwaka 2011, ametangaza mipaka kati ya nchi hizo mbili kufunguliwa.
Akizungumza akiwa na rais mwenzake, Salva Kiir, Bw Bashir alitaka pia mataifa hayo mawili kudumisha amani, na kuimarisha uhusiano wa kawaida tena.
Hali ya uhasama iliongezeka kati ya mataifa hayo mawili mwaka jana, huku kukiwa na wasiwasi wa kuzuka vita.
Uhasama huo umepungua, lakini tofauti kuhusiana na mafuta na ardhi bado upo kati ya nchi hizo mbili.
"Nimewaamuru maafisa wa serikali ya Sudan chama cha maslahi ya raia kushirikiana na ndugu zao katika Jamhuri ya Sudan ya Kusini", Bw Bashir alieleza katika hotuba yake katika mji mkuu wa Sudan ya Kusini, Juba.
"Kamwe hatutarudi katika vita," alieleza.
"Mimi na Bw Kiir tulikubaliana kwamba vita vilifanyika kwa muda mrefu mno."
Kwa upande wake, Bw Kiir alieleza kwamba yeye na Bw Bashir wamekubaliana kwamba watatekeleza masharti yote yaliyoafikiwa ya kuimarisha uhusiano kati ya mataifa yao mawili

New