My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, September 30, 2012

Shule ya kanisa yashambuliwa Nairobi

Shambulio la guruneti la mkononi dhidi ya shule ya Jumapili ya watoto wa Kikristo mjini Nairobi limeuwa mtoto mmoja na kujeruhi wengine kadha.


Polisi wa Kenya

Taarifa zinazohusianaKenya, GhasiaMkuu wa polisi wa Nairobi, Moses Ombati, ameliambia gazeti la Daily Nation kwamba watu watatu wamekamatwa, na kwamba watu hao walionekana wakipiga picha za kanisa la Saint Polycarp lilolengwa.

Msikiti ulio karibu na hapo ulishambuliwa na vijana waliokuwa na hasira.

Afisa wa polisi wa Nairobi aliwasihi watu wawe watulivu.

Shambulio lilitokea katika mtaa wa Juja Road, unaopakana na mtaa wa Eastleaigh.

Inaaminiwa kuwa guruneti lilirushiwa kanisa la Saint Polycap kama saa tano punde baada ya misa ya asubuhi.

Al-Shabaab waondoka Kismayo

Kundi la wapiganaji wa Kiislamu la Somalia, Al Shabaab linasema kuwa limeondoka katika ngome yao kubwa iliyobaki, yaani mji wa Kismayo.
Kismayo


Wakaazi wa Kismayo waliiambia BBC kwamba wapiganaji hao waliondoka usiku na kwamba mji sasa ni shuwari.

Majeshi ya Kenya na serikali ya Somalia, ambao walikuwa wakipigana na Al Shebaab kilomita kadha nje ya mji hapo jana, bado hawakuingia mjini.

Kismayo ni bandari ya pili ya Somalia kwa ukubwa na ikileta pato muhimu kwa al-Shabaab.

Wakaazi wa Kismayo wanasema waliamka leo asubuhi na kukuta Al Shebaab wameshaondoka.

Kwenye ukurasa wao wa mtandao wa internet wa twitter, kundi la al-Shabaab limetoa tangazo hili: "jana usiku, baada ya miaka mitano, utawala wa Kiislamu mjini Kismayo ulifunga ofisi zake".

Wanajeshi wa Kenya na serikali ya Somalia bado hawakuingia ndani ya mji.

Msemaji wa jeshi la Kenya aliiambia BBC kwamba ana wasiwasi kuwa kuondoka kwa al-Shabaab pengine ni mtego.

Kwa hivo kwa sasa, Kismayo haidhibitiwi na mtu yoyote.

Yote yanategemea vipi serikali ya Somalia na washirika wao wa Umoja wa Afrika watavosarifu maslahi yao yanayogongana, kudhibiti mji huo wenye bandari na unaoleta pato

Mkakati wa Kenya Somalia wasonga mbele

Wakati majeshi ya Kenya na Somalia yanakaribia mji wa Kismayo, sehemu ya mkakati wa miaka mingi wa Kenya karibu kukamilia.



Waziri wa uLinzi wa Kenya, Mohamed Yusuf Haji (kulia) na Waziri  Mkuu, Raila Odinga (kati)


Mpango wa kuwa na eneo la salama la kuzunguka mipaka ya Kenya karibu kukamilia:



Kwa miaka mingi, imekuwapo siri ambayo siyo siri tena, kwamba Kenya itapenda kuona taifa salama linaundwa nje ya mpaka wake na Somalia.



Huo ndio unaitwa makakati au mradi wa Jubaland.



Mpango huo unaungwa mkono na Wasomali wa Kenya.



Kati ya hao ni Waziri wa Ulinzi wa Kenya, Mohamed Yusuf Haji na mwanawe, Nuradin Yusuf, afisa wa ujasusi katika jeshi la Kenya.



Wote hao wanatokana na koo za Ogaden, ambazo zimetapakaa kaskazini mwa Kenya, kusini mwa Somalia na katika jimbo la Wasomali mashariki mwa Ethiopia.



Lakini kulikuwa na tatizo moja kubwa katika kuunda Jubaland, nalo ni upinzani wa Ethiopia.



Tangu miaka ya 1980, Waethiopia wamekuwa wakipigana vita na kundi la ONLF, wapiganaji wa jimbo la Ogaden.



Serikali ya Ethiopia inapinga kabisa wazo hilo la kuwa na Jubaland, ikiwa itaruhusu ONLF kuwa na kambi kupigana na majeshi ya Ethiopia.



Kwa hivo awali mwezi huu Waziri wa Ulinzi wa Kenya alipatanisha na kuleta makubaliano baina ya wapiganaji hao na serikali ya Ethiopia.



Kwa hivyo kikwazo cha mwisho dhidi ya mradi wa Jubaland sasa kimeondoka, na hivo kusukuma shambulio la hivi sasa dhidi ya Kismayo.



Tatizo moja limebaki: watu wa Kismayo siyo wa koo za Ogaden, na hiyo ndio sababu moja watu waliunga mkono al-Shabaab.



Kenya itabidi kusikiliza wasiwasi wao, ikiwa inataka kufanikiwa kukamilisha mradi wa Jubaland

Bajeti ya Ufaransa kukabiliana na deni

Waziri mkuu nchini Ufaransa, Jean-Marc Ayrault, ameitaja bajeti ya serikali yake ya mwaka 2013 kama silaha dhidi ya madeni ya nchi hiyo yanayo ongezeka kila kukicha.




Huku deni la nchi hiyo likikadiriwa kuwa asilimia tisini ya mapato ya nchi hiyo, bwana Ayrault alisema kuwa bajeti hiyo itajumuisha kuongezwa kwa kodi kwa watu wanaopokea mishahara mikubwa.



Tisa kati ya watu kumi hata hivyo hawataathirika kutokana na kupandishwa kwa viwango vya kodi.



Mpango huo wa serikali unasemekana utaweza kuchangisha dola bilioni ishirini na sita kwa pesa za serikali na kuzuia mipango ya kupunguza matumizi ya pesa za umma ambayo imeathiri nchi nyingi Ulaya.



Alisema kuwa serikali itahakikisha imetumia pesa kulingana na mahitaji ya nchi , yale muhimu yakipewa kipaombele kama elimu, ukosefu wa ajira , usalama na haki.



Katika wiki moja iliyopita, kiwango cha ukosefu wa ajira kimefika zaidi ya watu milioni tatu.

Deadly Kenya grenade attack hits children in church

One child has been killed and six critically hurt, the Red Cross says, in a grenade attack on a church's Sunday school in the Kenya capital, Nairobi.



The attacker targeted St Polycarp's church on Juja Road.


A police spokesman said they suspected sympathisers of Somalia's al-Shabab Islamist militants were to blame.


Kenyan troops are at present part of an African Union force that has forced al-Shabab from its last Somali urban stronghold of Kismayo.


The Daily Nation quoted local police as saying that a number of those hurt at the church were injured in a stampede after the attack.


The police spokesman, Charles Owino, told Reuters news agency: "We suspect this blast might have been carried out by sympathisers of al-Shabab.


The fact that Sunday's bombing has immediately been blamed on "Al-Shabab sympathisers" is hardly surprising, given events in Somalia in recent days.

The hand-grenade, thrown into a crowded public place, is becoming a grimly familiar tactic in Kenya. In the past six months, it has been used in bars in Mombasa, churches in Garissa near the Somali border, as well as churches and a bus station in Nairobi.



All of these attacks have initially been blamed on al-Shabab. But in at least some cases, subsequent reporting has suggested turf-wars between local gangs.



As Kenyan troops push al-Shabab out of its last Somali urban stronghold, Kismayo, there is nervousness about the possibility of a retaliation on Kenyan soil.



Many remember the bombings in Kampala in 2010, which killed 74 people, after Ugandan troops entered Somalia. Whatever the motive of Sunday's bombing, it is not on a comparable scale.

"These are the kicks of a dying horse since, of late, Kenyan police have arrested several suspects in connection with grenades."



Irene Wambui, who was in the church at the time of the attack, said: "We were just worshipping God in church when suddenly we heard an explosion and people started running for their lives.



"We came to realise that the explosion had injured some kids who were taken to hospital and unfortunately one succumbed."



Nairobi police chief Moses Ombati has appealed for calm after youths reportedly attacked the nearby Alamin mosque.


Nairobi and the port city of Mombasa have suffered a series of grenade attacks since Kenya sent troops into Somalia last October.

The attacks in Mombasa escalated after radical Islamist preacher Aboud Rogo Mohammed was killed in a drive-by shooting in August.


In July, 15 people were killed in raids on churches in Garissa, near Kenya's border with Somalia.


There was speculation that al-Shabab or its sympathisers were responsible.


Those attacks prompted the country's Inter-Religious Council chairman to urge a united front against sectarian division.


Adan Wachu told the BBC Network Africa programme at the time: "There are people out there who are determined to make Kenya another Nigeria.

"It's not going to be allowed to have a sectarian division in this country - whoever wants to do that will of course fail."


Attacks on churches in Nigeria have been frequent this year.

Many of them have been blamed on the Boko Haram group, which wants to establish Islamic law in a country where the north is largely Muslim and the south mainly Christian and animist.

Thursday, September 27, 2012

Mkutano maalum kuhusu Mali New York



Waasi wa Tuareg nchini Mali

Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa, Ban Ki Moon ameandaa mkutano maalum mjini New York kujadili mzozo unaokumba Mali ambako wapiganaji wa kiisilamu wameteka eneo la Kaskazini mwa nchi hiyo.
Nchi kadhaa za Afrika Magharibi pamoja na Ufaransa zinataka azimio la Baraza la usalama la umoja wa mataifa, litakalo wawezesha kuunga mkono hatua za kijeshi dhidi ya kile wanachokiita magaidi wa Kaskazini mwa Mali.
Rais wa Ufaransa, Francois Hollande, aliambia mkutano wa baraza kuu la umoja wa mataifa, Jumanne, kuwa Ufaransa iko tayari kuunga mkono juhudi za kuirejeshea Mali hadhi yake kama nchi huru.
Jeshi la pamoja la nchi za Magharibi mwa Afrika lijulikanalo kama ECOMOG, na ambalo limewahi kuingilia kati mizozo katika baadhi ya nchi za Afrika, linasema kuwa takriban wanajeshi elfu tatu, wana kibarua cha kutwaa eneo la Kaskazini kutoka kwa wapiganaji hao.
Lakini mwandishi wa BBC anasema kuwa viongozi wa Afrika wanatafuta uungwaji mkono kutoka kwa Baraza la usalama la umoja wa mataifa kabla ya kupeleka wanajeshi huko.

Malema ''Sitishiki na hatua ya mahakama''



Julius Melama akiwahutubia wafanyakazi wa migodi waliokuwa wanagoma
Julius Malema amewaambia wafuasi wake kuwa katu hatishiki na uamuzi wa mahakama kusema kuwa ana kesi ya kujibu.
Mahakama hii leo ilimwachilia kwa dhamana Malema anayekabiliwa na shtaka la kuhaulisha pesa.
Malema ambaye aliwahutubia wafuasi wake nje ya mahakama, pia anatuhumiwa kwa kutumia nafasi yake ya zamani kama kiongozi wa tawi la vijana la ANC kujitajirisha yeye na washirika wake wa biashara.
Washirika wake wengine wanne nao walikabiliwa na mashtaka sawa na hiyo katika kesi yao iliyosikilizwa hapo jana.
Katika hotuba yake kwa mamia ya wafuasi wake nje ya mahakama mjini Polokwane, bwana Malema alisema ataendelea na juhudi zake za kutetea maelefu wanaoishi katika umaskini nchini humo.
Seng'enge zilizungushwa katika eneo la mahakama hiyo iliyopo Polokwane, mji mkubwa wa jimbo analotokea mwanasiasa huyo,Limpopo.
Wafuasi wake wanasema mashtaka hayo yameshinikizwa kisiasa.
Wakiimba na kucheza nje ya mahakama hiyo wafuasi wengi wa chama hicho cha ANC tawi la vijana walishikilia mabango yaliosema 'Muacheni kiongozi wetu'.
Maafisa wa usalaman walidhibiti ulinzi na kulikuwa na utulivu mkubwa.
Julius Malema na washirika wake wa kibiashara wanashutumiwa kwa kufaidi kutokanana na mikataba ya serikali katika jimbo la Limpopo, tuhuma ambazo anazikana. Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 31 pia anachunguzwa katika kesi tofauti ya ukwepaji kulipa ushuru.
Malema ni maarufu sana Afrika Kusini kwa ukakamavu wake wa kutetea maslahi ya wananchi na maisha yake ya kifahari, huku akijitambulisha kama mpiganiaji uhuru wa uchumi.
Alitimuliwa kwenye chama hicho tawala mnamo mwezi Aprili akishutumiwa kwa kuzusha migawanyiko katika chama hicho.
Ni mkosoaji mkali wa a Jacob Zuma, hivi karibuni akimshutumu rais huyo kwa alivyoushughulikia mgomo wa wachimba migodi wa Marikana.
Kwa mujibu wa mwandishi wa masuala ya Afrika, Andrew Harding, baadhi ya watu Afrika kusini wanaamini anafikishwa haraka mahakamani, ikiwa ni chini ya wiki moja baada ya kutolewa waranti ya kukamatwa kwake, ili kuimarisha nafasi ya kisiasa ya Zuma.
Mwandishi wetu anaeleza kwamba huenda ikawa ni kesi ya muda mrefu, ambayo huenda ikatoa nafasi ya kujulikana ukweli kuhusu suala hilo la rushwa, ambalo watu wengi wanaamini inaitia nchi hiyo doa

Sudan na S.Kusini zakubaliana



Mazungumzo kati ya nchi hizo mbili yalifanyika nchini Ethiopia

Sudan na Sudan Kusini zimeafikia makubaliano kuhusu mgogoro wa mpaka na uzalishaji wa mafuta.
Baada ya mazungumzo ya siku ya nne, nchi hizo mbili zimeafikiana kuruhusu usafirishaji wa mafuta kutoka kusini kupitia mabomba ya Kaskazini na kuondoa wanajeshi mpakani.
Viongozi wa nchi hizo mbili hatimaye walikubaliana baada ya mazungumzo ya siku nne mjini Addis Ababa Ethiopia.
Lakin maswala kadhaa muhimu yangali kutatuliwa ikiwemo kuafikia makubaliano kuhusu mipaka inayozozaniwa ikiwa ni mojawpao ya kilichosababisha mgogoro ambao nusura utumbukize nchi hizo kwenye vita mapema mwaka huu.
Baada ya mapigano kuzuka kuhusu mzozo wa mafuta na mipaka, Umoja wa mataifa ulitishia kuziwekea pande zote mbili vikwazo ikiwa hazitaafikia makubaliano ya kina.
Wapatanishi wa Muungano wa Afrika wangali kuthibitisha kuwa makubaliano yameafikiwa lakini rais wa Sudan Omar al-Bashir na mwenzake wa Kusini Salva Kiir, wanatarajiwa kutia saini makubaliano hayo hii leo.
Maelezo yametolewa tu kwa mukhtasari lakini wapatanishi wa pande zote mbili, walisema kuwa wamekubaliana kuhusu eneo la nchi hizo mbili ambalo halina ulinzi wa kijeshi.
Pia makubaliano ya kiuchumi yaliafikiwa kuruhusu Sudan Kusini kuanza tena shughuli zake za kuzalisha mafuta.
Lakini mwafaka haukupatikana kuhusu eneo linalozozaniwa la Abyei wala mipaka mingine mingi ambayo nchi hizo zinazozania.
Kwa hivyo makubalino hayo hayajaweza kutimiza masharti ya Umoja wa Mataifa kwa nchi hizo kuafikia mkataba unaotatua mzozo huo kwa kina.

Utoaji mimba wahalalishwa Uruguay

Bunge la Congress nchini Uruguay limepitisha sheria ya kuhalalisha utoaji mimba katika hali zinazokubalika.
Bunge hilo limepitisha sheria hiyo kufuatia majadiliano makali yaliyoishia kwa wabunge hao wa Congress kuipitisha kwa kura 50 dhidi ya 49.
Sasa hoja hiyo itawasilishwa katika bunge la juu la Senate ambalo linatazamiwa kuiidhinisha.
Sheria hiyo itawaruhusu wanawake kutoa mimba kabla haijafika wiki 12 ilimradi wamepata ushauri nasaha kutoka kwa madaktari wasiopungua 3 ili kufahamishwa hatari za kuavya mimba.
Mbali na Cuba, Uruguay itakuwa nchi ya kwanza katika ukanda wa Amerika kusini kuruhusu mwanamke yeyote anayetaka kutoa mimba fursa ya kufanya hivyo.

Tuesday, September 25, 2012

MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP)



Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila.

MWENYEKITI wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.
Inadaiwa kuwa Oktoba 21 mwaka jana katika  maeneo ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ilala, jijini Dar es Salaam Mchungaji Mtikila alitoa maneno ya uchochezi, dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.
Akizungumza na mtandao huu baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema "Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa amenijibu".
Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili lingine baada ya mtu mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) akimtuhumu Mchungaji Mtikila kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa viwanja. Baada ya kutaka kukamatwa na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo, Mchungaji alikataa kwa madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa hivyo hawezi kukamatwa na polisi mwenye cheo cha Koplo, labda polisi mwenye cheo cha SSP (Senior Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo polisi alishindwa kumtia nguvuni.

Trafigura lazima ishtakiwe



Maefu ya watu waliugua kutokana na taka hizo za simu

Wanaharakati nchini Uingereza wanataka kampuni ya Trafigura kufunguliwa mashtaka kwa hatua yake ya kutupa taka yenye sumu nchini Ivory Coast mwaka 2006.
Uchunguzi wa miaka mitatu wa mashirika ya Amnesty International na Greenpeace umeonyesha udhaifu wa serikali za Magharibi kushindwa kuzuia kumwagwa kwa taka yenye sumu nchini Ivory Coast mwaka 2006.
Trafigura, kampuni ya uchukuzi ya Uholanzi iliyo na matawi yake jijini London, iliilipa kampuni ya Ivory Coast kumwaga uchafu huo karibu na bandari ya Abidjan.
Watu elfu mia moja walikwenda hospitali kwa matibabu. Wanaharakati hao wanateta kuwa serikali za Uingereza na Uholanzi zimeshindwa kuzuia kumwagwa kwa sumu au kuwawajibisha Trafigura.
Kampuni hiyo imekanusha madai hayo na kusema kuwa ripoti hiyo ina taarifa zisizo za kweli.
Kampuni hiyo ni mojawapo ya kampouni kubwa duniani za usafiri na imekuwa ikijitetea ikisema kuwa taka hiyo haikuwa na na sumu na wala haikuhatarisha maisha ya watu.
Mnamo mwezi agosti mwaka 2006, familia kadhaa mjini Abidjan ziliamka na kukumbana na harufu mbaya yenye mvuke wa sumu.
Taka hizo za kemikali zilikuwa zimeletwa katika eneo hilo kwa meli ya kampuni iliyokuwa imekodiwa na kampuni ya Trafigura na kisha kutupa taka hizo katika eneo lenye taka.
Kampuni hiyo imekana kuwa taka hizo zingeweza kusababisha ugonjwa na kuelezea kuwa ilikuwa imelipa kampuni moja mwenyeji kuweza kutupa taka hiyo kwa njia sawa kisheria.

Afueni kwa wanafunzi wa Kenya



Wanafunzi darasani Kenya 

Shule za umma nchini Kenya zimefungua hii leo baada ya wiki tatu za mgomo wa walimu.
Walimu hao hatimaye waliweza kuafikia makubaliano na serikali kuhusu matakwa yao ya nyongeza ya mishahara.
Serikali ilitishia kuwafuta kazi walimu hao Ijumaa wiki jana wakati walipokataa pendekezo la asilimia 4 ya mishahara ambalo serikali ilitoa.
Lakini makubaliano hatimaye yaliafikiwa mwishoni mwa wiki ya nyongeza ya asilimia arobaini.
Sasa mwalimu atakayepokea mshahara mdogo zaidi kuliko wote atalipwa dola 140 huku mwenye kulipwa mshahara mkubwa akipata dola 1,700 .
Sekta ya umma nchini Kenya imekumbwa na migomo katika wiki chache zilizopita. Hospitali za umma ambazo pia zilishuhudia mgomo wa madaktari, zinawahudumia tu wagonjwa walio katika hali ya dharura.
Vyuo vikuu vya umma navyo vilifungua siku ya Jumatatu baada ya wahadhiri ambao pia walikuwa wanagoma kurejea kazini.
Kupanda kwa gharama ya maisha na mkakati duni wa serikali kuweza kushughulikia matatizo ya wananchi hususan swala la mishahara ndio mojawapo ya sababu ya kutokea kwa migomo hii.
Walimu hao 200,000 walitaka nyongeza ya asilimia miamoja hadi miatatu .
Kulingana na makubaliano hayo yaliyotiwa saini na waziri wa fedha Njeru Githae na chama cha kitaifa cha walimu, marupurupu ya walimu pia yataongezeka hasa kwa wale wanaofanya kazi katika mazingira magumu na wale wanaowahudumia wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Mitihani ya mwisho wa kidato cha nne na darasa la nane ilitaakhirishwa kwa wiki tatu ili kuwawezesha wanafunzi kuajindaa vilivyo.

Msako dhidi ya Boko haram



Waathiriwa wa mashambulizi ya Boko Haram 

Takriban wapiganaji 35 wa kundi la kiisilamu la Boko Haram, wameuawa katika msako mkali dhidi ya kundi hilo Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Kwa mujibu wa jeshi la Nigeria, wapiganaji wengine sitini walikamatwa wakati wa msako huo kwenye majimbo ya Adamawa na Yobe.
Kundi hilo la kiisilamu, linapinga mifumo ya kimagharibi na athari zake nchini Nigeria na wamekuwa wakifanya mashambulizi yanayolenga maslahi ya nchi za Magharibi pamoja na makanisa.
Mnamo siku ya Jumapili, kulitokea shambulizi dhidi ya kanisa moja katoliki na ambalo lilisababisha mauaji ya watu wawili. Boko Haram ndilo limelaumiwa kwa kufanya shambulizi hilo.
Msemaji wa jeshi nchini humo, alifahamisha shirika la habari la AFP kuwa msako huo ulifanyika usiku kucha kati ya siku ya Jumapili na Jumatatu.
Wanajeshi walifanya msako wa nyumba hadi nyumba, katika mitaa mitatu na wakati mwingine kufyatuliana risasi na wapiganaji hao, usiku kucha.
Wanajeshi wawili walijeruhiwa katika makabiliano hayo.
Bunduki na mabomu vilipatikana katika maficho ya wanamgambo hao pamoja na silaha zengine ikiwemo mishale 32 na panga.
Mji huo umekuwa mojawapo ya miji iliyoathirika sana kutokana na harakati za Boko Harama ambalo linataka kutumika kwa sheria za kiisilamu kote nchini humo.

Masaibu ya watoto wa Syria



Masaibu ya watoto wa Syria walionaswa katika vita 

Shirika la kutetea haki za watoto Save the Children, limekusanya maelezo ya kutisha na kuogofya kuhusu visa vinavyowakumba watoto katika vita vinavyoendelea nchini Syria.
Shirika hilo limekusanya ushahidi kutoka kwa watoto waliotoroka vita na ambao wameelezea dhulma na mateso waliyokumbana nayo.
Kwa mujibu wa shirika hilo, kila mtoto aliyehojiwa na ambaye ameweza kutoroka Syria, ameelezea kuona jamaa wake angalau mmoja akiuawa.
Shirika hilo linasema kuwa limehoji mtoto mwenye umri wa miaka 15, aliyechomwa kwa sigara,wakati alipokuwa amefungwa katika iliyokuwa shule yake.
Mtoto mwingine alizungumzia kupigwa na umeme huku akiishi katika chumba kimoja na maiti.
Ingawa shirika hilo halikutoa taarifa rasmi kuhusu nani aliyetenda mateso hayo, limeisisitizia Umoja wa Mataifa kuchukua hatua dhidi ya wanaotenda dhulma hizo.

Friday, September 21, 2012

Waziri mkuu mpya wa Ethiopia



Hailemariam Desalegn

Waziri mkuu mpya wa Ethiopia Hailemariam Desalegn, ameapishwa kuchukua wadhifa wa hayati Meles Zenawi aliyeitawala nchi hiyo kwa miaka 21.
Mwingine aliyeapishwa ni naibu wake Demeke Mekonen, ambaye alikuwa anashikilia wadhifa wa waziri wa elimu.
Bwana Hailemariam Desalegn, amenukuliwa na shirika la habari la AFP akisema kuwa ana furaha kuchukua wadhifa huo na yuko tayari kufanya majukumu yake kwa kujitolea.
Hailemariam aliungwa mkono bila pingamizi na bunge la waakilishi ambalo lina wanachama wengi wa muungano tawala kuchukua wadhifa huo
Sherehe ya kumuapisha waziri mkuu huyo iliendeshwa na rais wa mahakama ya juu zaidi nchini humo, Tegene Getaneh na kuonyeshwa moja kwa moja kupitia televisheni ya taifa.
Hayati Zenawi alifariki mwezi jana mjini Brussels baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Watanzania mabingwa wa kiswahili

Kwa mpenzi yeyote wa Kiswahili ni sharti azingatie stadi nne za lugha hiyo. Yaani kuzungumza, kusoma kuandika na kuelewa lugha ya Kiswahili. Hata hivyo baadhi ya wakenya wamekuwa wakilamika kuwa vitabu vingi vya Watanazani vimekuwa vikitahiniwa nchini Kenya hususan katika vidato vya tatu na vinne.
Ukweli ni kuwa Watanzania wamewabwaga wakenya na ipo mifano ya kutajika kuhusiana na hilo katika vitabu hususan vya fasihi. Swali ni je Wakenya wamepewa fursa ya kuandika au la? Ni nani anastahili kuwaambia waandike vitabu vya Kiswahili, na je wachapishaji vitabu wako radhi kuzichapisha kazi za Wakenya?
Kuanzia miaka ya themanini hadi sasa, idadi ya vitabu vya Watanzania vilivyotahiniwa katika kunga za riwaya, tamthilia na ushairi ni kubwa kushinda vya Wakenya. Riwaya ya Kusadikika ya Shaaban Robbert(Mtanzania) ilitahiniwa mwanzoni mwa miaka ya tisini hadi mwaka 1994. Wakati huo hadi mwaka 1997 tamthilia ya Mashetani ya Ebarahim N. Hussein(Mtanzania) ilitahiniwa. Mwaka wa 1994 hadi mwaka 1998 riwaya ya Kisima cha Giningi ya Mohamed Said Abdullah(Mtanzania) ilitahiniwa. Katika miaka hiyo kuanzia mwaka 1998 tamthilia ya Amezidi ya Said Ahmed Mohamed (Mpemba) ikaanza kutahiniwa kuchukua mahali ya tamthilia ya Buriani ya A. S Yahya na David Mulwa(Wakenya). Wakati huo Mkenya Khaemba Ongeti alijipenyeza na tamthilia yake ya Visiki.
Hayakuishia hapo, baada ya tamthilia za Visiki na Amezidi kuondolewa katika ratiba ya shule za upili nchii Kenya ikaingia riwaya nyigine ya Mohamed Said Ahmed (Mpemba) ya Kitumbua kimeingia mchanga. Na hiyo ilipoondoka ikaja riwaya ya Utengano ambayo inatahiniwa hadi sasa.
Ukweli unaojitokeza hapa ni kuwa taasisi ya elimu nchini haiviteui vitabu hivyo kwa sababu ni vya Watanzania. Ni kutokana namna vilivyosukwa kimaudhui na kifani. Isitoshe waandishi wa vitabu hivyo wameandika wameandika vitabu vingi tu. Kwa mfano Said Ahmed Mohemed ameandika zaidi ya vitabu 40 vya Kiswahili. Mohamed Said Abdullah ameandika vitabu vingi tu kama vile Kisima cha Giningi, Duniani kuna watu, Mizimu ya watu wa kale na Kadhalika.
Hata hivyo ni vyema kutambua kuwa baadhi ya Wakenya wamejitokeza na kuandika kazi nzuri za fasihi ya Kiswahili kama vile Siku Njema ya Ken Walibora, Mstahiki Meya ya Timothy Arege na Kifo Kisimani ya Kithaka Wamberia. Kwa ufupi wapenzi wa Kiswahili katika kanda ya Afrika Mashariki wakijumuisha mataifa ya Rwanda, Sudan Kusini, Sudan, Somalia na Uganda waandike vitabu zaidi vya Kiswahili. Twasubiri siku watanzania watavitahini vitabu vya Kiswahili vya wakenya, Vivyo hivyo si dhambi kitabu cha Kiswahili kilichoandikwa na Mrundi ama Mnyarwanda kikitahiniwa Uganda na vinginevyo.

Saturday, September 8, 2012

Obama apigiwa debe na Bill Clinton



Rais mstaafu Bill Clinton na Barack Obama

Rais wa zamani wa Marekani, Bill Clinton amemtetea vikali mgombea urais wa chama cha Democrats nchini Marekani Barack Obama.
Katika hotuba iliyochukua muda wa dakika 50 katika kongamano la chama hicho linalofanyika mjini Charlotte, North Carolina, Clinton alikosoa sera za uchumi za chama pinzani cha Republican.
Bill alisisitiza kuwa sera ya uchumi ya Barack Obama imeweza kuimarisha uchumi wa nchi hiyo ambao ulikuwa umedorora. Bwana Clinton alimaliza hotuba yake kwa kumteua rais Obama kuwa mgombea rasmi wa urais wa chama.
Rais Obama atamenyana na mgombea wa chama cha Republican Mitt Romney katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwezi Novemba.
Hotuba ya Clinton ni dalili ya kuimarika kwa uhusiano kati yake na Obama na pia kama juhudi za kupiga jeki mvuto wa obama miongoni mwa wazungu wanaofanya kazi.
Kura za maoni zinaonyesha kuwa wapiga kura wa chama hicho wamekuwa waangalifu sana kuhusu sera za Obama lakini Clinton ana rekodi nzuri ya kuwashawishi watu kumuunga mkono Obama.
Clinton aliambia wafuasi wa chama '' Amueni nchi mnayotaka kuishi. Ikiwa mnataka viongozi wasio wajali basi pigieni kura chama cha Republican. Mkitaka nchi yenye nafasi nyingi na ambayo majukumu yanagawanywa, basi sote tuko pamoja. Lazima mumpigie kura Barack Obama na makamu wake Joe Biden."
Bwana Clinton alikosoa vikali chama cha republican kwa kuzuia juhudi za uchepuzi wa uchumi na badala yake kujihusisha na mijadala kuhusu sera.
Kura za maoni zinaonyesha Barack Obama akiongoza kwa asilimia 47 huku mpinzani wake Mit Romney akimfuata kwa asilimia arobaini na sita.

Michelle Obama amuombea mumewe kura



Mkewe rais Obama , Michelle akihutubia kongamano la Democrats 

Mkewe Rais wa Marekani, Barack Obama, Michelle, amehutubia kongamano la chama tawala cha Democratic ambapo alitetea haki ya mumewe kupewa nafasi kutawala taifa hilo kwa muhula wa pili.
Akiongea Kaskazini mwa Jimbo la Carolina, alimtaja mumewe kama mtu anayeelewa matatizo yanayowakumba wamarekani.
Alitetea hatua ya mumewe ya kuanzisha mpango maalumu wa bima ya afya ulioleta utata mwingi sana hasa miongoni mwa wanachama wa chama cha upinzani cha Republican walioupinga.
Alisema kuwa mumewe alinuia kutoa nafasi sawa ya matibabu kwa wote. Hata hivyo alikiri kuwa mageuzi aliyoahidi mumewe miaka minne iliyopita yalikuwa magumu kuyatekeleza lakini akasisitiza kuwa yatafaulu baadaye.
Rais Obama atahutubia kongamano hilo baadaye juma hili, ambapo atakubali rasmi kuwa mgombea wa Urais wa chama cha Democratic.

Apple yaipiku Samsung mahakamani

Jopo la mahakama moja ya Marekani limeamua kuwa kampuni kubwa ya teknolojia ya Korea Kusini, Samsung, iliiga baadhi ya ufundi mpya wa kampuni ya Marekani ya Apple kuunda simu zake wenyewe za kisasa za smartphone na kumputa ndogo - tablet.
Simu za Apple na Samsung
Baada ya kesi iliyoendelea kwa mwaka mzima, ambayo ilichunguza mashtaka kama 700 ya aina ya ufundi ulioigwa, mahakama ya California yaliiamrisha Samsung iilipe Apple fidia ya dola zaidi ya bilioni moja.
Samsung imelalamika kuwa Apple inajaribu kuhodhi soko zima la smartphone, na imesema itakata rufaa.
Zaidi ya nusu ya simu za smartphone zinazouzwa duniani ni ama za Apple au Samsung, na kampuni hizo mbili zinashtakiana katika mahakama ya nchi mbali mbali duniani.

Ombi la Rais Obama kwa wamarekani



Rais wa Marekani Barack Obama

Rais wa Marekani Barack Obama, amewaomba wamarekani kumpa fursa nyingine kuiongoza nchi hiyo.
Ombi lake amelitoa katika kilele cha kongamano la chama cha Democratic mjini North Carolina.
Akijiwasilisha kama mgombea wa urais mwenye kuleta matumaini kwa wamarekani, Rais Obama alisema kuwa uchaguzi utakaofanyika mwezi Novemba, utatoa fursa kwa wapiga kura kuchagua kati ya maono mawili tofauti kuhusu hatma ya Marekani.
Aliwataka Wamarekani kuwa wavumilivu akisema kuwa matatizo yanayokabili Marekani yamekuwa yakiongezeka kwa miaka mingi na kuwa itachukua muda kuweza kuyatatua.
Lakini aliongeza kuwa ikiwa watamchagua tena, ataweza kubuni nafasi mpya za kazi, kupunguza madeni na kuimarisha uchumi wa Marekani.
Rais Obama alisema anajiona kama kiongozi aliyekuwa amewekwa kwa mizani kujaribiwa uongozi wake na kuwa amefaulu. Alisema mpinzani wake wa Republican, Mitt Romney, hayuko tayari kwa mashauriano ya kidiplomasia.
Alitofautisha malengo yake na yale ya chama pinzani na kurejelea kauli mbiu yake ya mwaka 2008 , kuwataka watu kuwa na matumaini.
"sikuwahi kusema kuwa safari hii itakuwa rahisi na sitatoa ahadi hiyo hii leo'' Obama aliambia kongamano la wajumbe wa Democrat.
Mitt Romney wa chama cha Republican atapambana na Rais Obama kuwania urais huku kura za maoni zikionyesha wawili hao wakikaribiana.

Hofu ya vita kuhusu mpaka wa Sudan na S. Kusini



Mkutano wa Umoja wa mataifa kuhusu mzozo wa Sudan mbili
Balozi wa Marekani katika umoja wa mataifa Susan Rice, amesema mzozo kuhusu mpaka kati ya Sudan na Sudan Kusini huenda ukasababisha vita kuzuka tena kati ya nchi hizo mbili.
Bi Rice ametoa matamshi yake katika mkutano wa baraza la usalama la umoja wa mataifa kuhusu mzozo wa mpaka kati ya nchi hizo nchini Marekani.
Sudan Kusini imekubali mpango wa amani uliopendekezwa na Muungano wa nchi za Afrika ingawa Sudan imeukataa.
Nchi hizo mbili nusura zipigane mapema mwaka huu sababu kuu ikiwa mzozo wa mpaka na ugawanaji wa mapato ya mafuta .
Sudan Kusini ilipata uhuru wake kutoka kwa Sudan mwaka jana na kumaliza miaka mingi ya mapigano kati yake na Sudan.
Akiongea mjini New York, Bi Rice alisema kuwa hatua ya serikali ya Khartoum kukataa kusaini mpango wa amani inaweka nchi hizo katika hatari ya kurejelea vita.
Alisisitiza kuwa hatua ya kujikokota ya Khartoum inazua wasiwasi kuhusu kujitolea kwake kutatua mzozo huo.
Licha ya Sudan Kusini kukubali mpango wa amani, Bi Rice amekariri kuwa Marekani ina wasiwasi kwamba nchi hizo hazichukulii kwa uzito swala hilo kama ambalo linapaswa kushughulikiwa kwa dharura.
Muda wa mwisho uliowekwa na Umoja wa mataifa wa kuafikia makubaliano mwezi Agosti tarehe mbili, haukuweza kufikiwa na nchi hizo mbili.
Hata hivyo, pande hizo mbili zinashinikizwa kutia saini mpango huo wa amani ifikapo tarehe 22 mwezi Septemba.
Mwezi jana serikali za Khartoum na Juba zilifanya mkutano wa wiki tatu mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Kwenye mazungumzo hayo, mwafaka ulifikiwa wa kugawana mapato ya mauzo ya mafuta ingawa bado mazungumzo zaidi yanahitajika kuhusu usalama.
Mazungumzo hayo yataendelea mwishoni mwa mwezi Agosti.
Majeshi ya Sudan yamepigana mara kadhaa na yale ya Sudan kusini tangu Sudan kusini kujipatia uhuru mwaka jana.
Huenda baraza la usalama la umoja wa mataifa likaziwekea vikwazo nchi hizo iwapo zitashindwa kukubaliana kusitisha mzozo huo katika eneo la mpakani.

Kanisa la Anglikana lataka kuwa na rais

Askofu Mkuu wa kanisa la Anglikana, Rowan Williams, amefichua kuwa kanisa hilo linaandaa mpango wa kumteua rais wa kanisa, ambaye atabeba sehemu ya jukumu la kuongoza kanisa duniani.
Askofu Rowan Williams
Alisema mtu atayechukua nafasi hiyo ataweza kusafiri kwa urahisi, na hivo kumuacha Askofu Mkuu kushughulika zaidi na kuongoza kanisa.
Doctor Williams, ambaye anastaafu mwezi wa Disemba baada ya uongozi wa miaka 10, alikiri kuwa hakuweza kufanya mengi kuzuwia mgawanyiko kanisani juu ya swala la uhusiano wa jinsia moja.

John Tendwa


Makundi mbalimbali ya jamii yamesema kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, hana ubavu wa kukifuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na kwamba kauli aliyoitoa juzi ilikuwa ya jazba na ya kisiasa. Wamesema kauli hiyo haina mashiko kwa sababu makosa ya jinai hayafanywi na taasisi bali watu binafsi. Walisema suala hilo ni gumu kwa kuwa anapaswa kuangalia sera za chama na kwamba hadi sasa hakuna chama ambacho kina sera za mauaji ama uvunjifu wa amani.

DK. BANA: TENDWA ANATAKA KUWASHA MOTO 

Mkuu wa Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana alisema si rahisi Tendwa kufuta Chadema, kwa kuwa hatua hiyo inaweza kuzua moto mkubwa, ambao ni vigumu kuuzima. Alisema kauli ya Tendwa ni ya kijazba na pia ni ya kisiasa, kwani ofisi yake haina uwezo wa kukifuta chama chochote cha siasa, kwa kuwa suala hilo ni la kisheria. “Sijawahi kuona msajili anafuta chama chochote japo baadhi ya vyama vimekuwa vikikiuka sheria. Kwa hiyo, si rahisi msajili kufuta Chadema. Anataka kuzua moto, ambao huwezi kuuzima,” alisema Dk. Bana.

Alisema kwa mujibu wa sheria, chama kinatakiwa kifutwe iwapo kitakiuka sheria na kwamba, hatua hiyo itachukuliwa hadi hapo vyombo vya sheria vitakapothibitisha ukiukwaji wa sheria uliofanyika. Hata hivyo, alivitaka vyama vya siasa kujenga maadili mema, ikiwa ni pamoja na kuheshimu mamlaka halali iliyopo.

Tuesday, September 4, 2012

Historia ya Charles Taylor

 
Charles
Charles Taylor amekutwa na hatia

Mahakama inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imempata na hatia aliyekua Rais wa Liberia, Charles Taylor, kwa kosa la kushiriki na kusaidia uhalifu dhidi ya binadamu, mauaji, ubakaji na ugaidi.
Mahakama ya huko The Hague imesema kua Bw Taylor anawajibika kwa kuunga mkono waasi wa kundi lililojulikana kama RUF yaani Revolutionary United Front katika nchi jirani ya Sierra Leone wakati wa vita vikali vya wenyewe kwa wenyewe katika miaka 1990.
Bw Taylor ndiye kiongozi wa kwanza kutoka Afrika kukabiliwa na hukumu mbele ya Mahakama ya Kimataifa tangu kesi maarufu za Nuremburg baada ya vita vikuu vya pili vya Dunia. Atahukumiwa mwezi ujao.
Maelezo yafuatayo yalikusanywa na kuandikwa na mwandishi wa BBC aliye nchini Liberia na mara kadhaa alikutana na Charles Taylor.
Charles Taylor alikua Rais wa Liberia kuanzia mwaka 1997 hadi alipojiuzulu mnamo mwaka 2003 kufuatia shinikizo kali za kimataifa. Alianza shughuli za siasa wakati wa ziara yake nchini Liberia kama kiongozi wa msafara wa mashirika ya Waliberia yaliyo barani Amerika mapema katika muongo wa 1980, mapinduzi ya kijeshi yalipofanyika naye kupewa kazi katika serikali ya Samuel Doe.
Baada ya kuteuliwa kama Naibu waziri katika Wizara ya biashara ya serikali ya Rais Doe, Taylor aliikimbilia Marekani kufuatia madai kwamba amepoteza takriban dola za kimarekani milioni moja.
Alifungwa huko Marekani lakini akatoroka jela katika mazingira ambayo hadi leo bado ni ya kutatanisha. Hatimaye aliunda kundi lake la waasi, lililojulikana kama National Patriotic Front of Liberia, ambalo liliiondoa serikali ya Samuel Doe madarakani.
Taylor
Alikuwa kiongozi wa waasi
Taylor ana kipaji cha kua mtu mchangamfu ambaye aliweza kumbadili adui na kumpenda kiasi cha kumfanya kua mfuasi sugu. Kwa mfano alipoingia mji wa Monrovia mnamo mwaka 1995 makumi kwa mamia ya watu waliompinga walijitokeza kumpokea na kumuimbia nyimbo za kumsifu kama shujaa.
Licha ya kuwateua watu wengi kama washauri wake lakini hiyo ilikua danganya toto'' kwa sababu hakufuata ushauri wao hata siku moja. Mmoja wa washauri wake wa karibu aliwahi kuniambia kua yaliyomfika Taylor yangeweza kuepukika kama angewasikiliza washauri hao.
Taylor alipenda sana kujifananisha na watawala wa enzi ya karne ya kumi na tisa kwa jinsi alivyowazawadia fukara akifahamu kua fadhila zake zitamjengea sifa na kumfaa siku moja.
Akiwa mpenda madaha alifahami vyema nguvu ya vyombo vya habari na jinsi ya kuvitumilia. Kupitia miaka ya 1990 alishiriki mahijiano mengi ya kipindi cha BBC cha Focus on Africa.
Katika kipindi cha kwanza, akiwa ni kiongozi wa kundi la waasi asiyefahamika, alitangaza mpango wake wa kuivamia Liberia.
Miaka michache baadaye, alipodokezewa na mtangazaji kwamba watu wengi wanamuonelea kua muuwaji, alilipuka na kusema ''Hata Yesu Kristu alituhumiwa kua ni muuwaji enzi zake.
Katika mahojiano mengi tuliyofanya naye daima alijitahidi kudhibiti mahojiano ili kutoa sura inayompendeza yeye. Mfano uilipomrushia suali lililomchukiza alijitahidi kulibadili liweze kusikika kwa manufaa yake.
Kama mpiganaji mahiri alijivunia uwezo wake wa kiume na uwezo wa kuzaa watoto wengi. Hakuficha siri yake ya kupenda wanawake, akidokeza wakati mmoja kua kama kiongozi wa Kiafrika ana haki ya hadi wake wanne.

Naomi
Mwanamitindo Naomi Campbell alihusishwa katika kesi ya Taylor

Wakosoaji wake walipokashifu tabia yake ya uzinzi, alijibu kwa kuwakemea wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia moja na kujibu ''Bora mimi nawapenda wanawake.''
Mnamo mwaka 1996 alidokezea kua angetaka kujaliwa na watoto wengine watano na wote watakua wanaume. Hata hivyo hakujaliwa na ndoto yake hio watoto wake wawili waliofuata walikua wa kike.
Labda kama ishara ya kujiliwaza majaliwa hayo, aliwahi kuniambia kua kama mzazi anayewapenda wanawe, mume yeyote atakayewaoa wanangu, itabidi akubali watoto wake warithi jina la Taylor liendelee kudumu katika familia yao.

Wadai kuachishwa kazi kwa ajili ya imani zao

Watu wanne nchini Uingereza wanaodai kuwa waliachishwa kazi baada ya kubaguliwa kwa misingi ya dini yao, wanapeleka kesi yao katika mahakama ya haki za binadamu ya ulaya baadaye leo.
Kesi ya wanne hao ambayo waliwahi kuiwasilisha kwa jopo maalum kuhusu maswala ya ajira ilishindwa.

Mwandishi wa BBC Robert Pigott anasema kuwa uamuzi utakaotolewa kuhusu kesi hiyo katika mahakama hiyo , utakuwa muhimu sana hasa ikizingatiwa swala la mabadiliko ya mawazo kuhusu dinni ya kikristo kwa jamii.
Waliofikisha kesi hiyo mahakamani ni pamoja na mfanyakazi wa shirika la ndege la uingereza, Nadia Eweida, muuguzi Shirley Chaplin, mshauri nasaha na mtaalamu wa maswala ya mapenzi, Gary McFarlane na msajili wa watu Lilian Ladele.
Bi Eweida, mkristo wa madhehebu ya Pentecostal kutoka London,aliachishwa kazi mwaka 2006 baada ya kukataa amri ya kuvua mkufu wake uliokuwa na msalaba.

Kanisa nchini Uingereza
Muuguzi Chaplin pia aliachishwa kazi katika hospitali ya Royal Devon kwa sababu sawa na hiyo.
Bwana McFarlane, mshauri nasaha kutoka Bristol alifutwa kazi na kampuni ya Relate baada ya kusema kuwa aliona ugumu kutoa ushauri kwa wapenzi wa jinsia moja.
Naye Bi Ladele aliadhibiwa baada ya kukataa kuwafungisha ndoa wapenzi wa jinsia moja kaskazini mwa London.
Mapema mwaka huu, kilio cha wanne hao kiliungwa mkono na tume ya usawa na haki za binadamu nchini Uingereza, ambayo ilisema kuwa majaji walitafsiri kwa udhaifu sheria za usawa kwa madai ya udini.
Tume hiyo ilisema kuwa hatua hiyo iliwafanya waajiri kuweka sheria tata jinsi wakristo wanavyoweza kuishi kutokana na imani zao.
Katika kisa kilichomkumba muuguzi Chaplin, mwajiri wake alimwambia kuwa mkufu wa msalaba aliokuwa ameuvaa ulikiuka miongozo ya afya na usalama. Hata hivyo alishindwa kesi yake mwaka 2010

Walimu waanza mgomo wa kitaifa Kenya


Mabango ya walimu Kenya wakitaka kuongezwa mishahara
Maelfu ya walimu nchini Kenya wameanza mgomo wao rasmi wakidai kuwa serikali imekuwa ikipuuza kilio chao kuongezwa mishahara kwa miaka mingi.
Walimu hao ni wa shule za misingi na zile za upili na leo wamesusia kazi wakitaka nyongeza ya mishahara huku shule nyingi nchini humo zikiathirika.
Walimu hao wamekiuka agizo la mahakama lililoharamisha mgomo huo. Shule nyingi katika miji mikubwa mfano Mombasa, Nairobi na Nakuru zilisalia kufungwa.
Walimu hao wanadai nyongeza ya kati ya asilimia miamoja na miatatu.
Walimu wa shule za upili pamoja na wahadhiri wa vyuo vikuu wamesema watajiunga na mgomo huo baadaye wiki hii.
Mgomo huu unajiri wakati shule zikifungua kwa muhula wa tatu kitu ambacho walimu hao wanasema sio hoja kwani wamekuwa wakigoma kila muhula wa tatu unapofungua kwa zaidi ya miaka kumi iliyopita wakidai hiyo nyongeza.
Wanasema kuwa serikali haina usawa katika mishahara kwa wafanyakazi wa sekta ya umma kwani ni hivi maajuzi tu wauguzi na wafanyakazi wengine wa umma walipoongezwa mishara baada ya kugoma. Wanadai kuwa walimu wamepuuzwa.
Mgomo huu umeonekana kufanikiwa kwani shule nyingi zimesalia kuwa bila walimu wanafunzi wengi wakibaki nyumbani.
Walikuwa wamebeba mabango yenye ujumbe kwa serikali kuwa wao hawawezi kula panya kwa mishahara midogo ambayo wanapata. Na vile vile walisema kuwa wamechoka na ahadi za uongo za serikali.
Mgomo huo uliitishwa na mashirika ya wafanyakazi yanayowakilisha takriban walimu laki mbili na nusu.
Wameahidi kuendelea na mgomo hadi matakwa yao yatakapotimizwa.

Wachimba Migodi 122 waachiliwa Afrika Kusini

 
Wachimba migodi walioachiliwa

Wachimba migodi mia moja ishirini na wawili wa kampuni ya Lonmin yenye kuchimba madini ya Platinum wameachiliwa huru na Mahakama ya Kharankuwa iliyoko kaskazini mwa Pretoria.
Mara tu baada ya kuachiliwa wachimba migodi hao walikaribishwa nje ya mahakama na wenzao ambao walionekana kuimba nyimbo za kushangilia na kuwaelekeza katika eneo kulikotokea mauaji
Hatua ya kuachiliwa kwa wachimba migodi inakuja baada ya viongozi wa mashtaka kufutilia mbali mashtaka dhidi ya wachimba migodi 270 kufutia shinikizo za umma.
Wachimba migodi wa kwanza hao walikamatwa na kushtakiwa kwa mauaji ya wenzao 34 waliouawa kwa kupigwa risasi na maafisa wa polisi.
Wakili wa wachimba migodi hao Bi Mapuli Kesi, alifurahia uamuzi huo wa mahakama na kunukuliwa akisema, "mimi ninayo furaha kubwa na ni ushindi mkubwa kwa kundi letu. Tumefanya kazi kubwa kufikia hapa tulipo."
Mwandishi wetu wa Afrika Kusini, Omar Mutasa, aliyekuweko mahakamani wakati kundi la kwanza la wachimba migodi lilipoachiliwa huru, alisema wachimba madini hao walilalamikia kile walitaja kuwa mateso mikononi mwa maafisa wa polisi.
Mmoja wao ambaye hakutaka kusema jina lake aliambia BBC, "polisi walikuwa wakali sana wakisema tusiwatazame na wakati mwingine walikuwa wakitutoa nguo na kutupiga marungu."
Hapo jana polisi waliwapiga riasasi na kuwajeruhi wachimba migodi wanne katika tukio tofauti .
Inadaiwa kuwa polisi walitumia risasi za mipira kuwatawanya waandamanaji katika Mgodi mwingine wa Gold Miners wanaogoma wakidai nyongeza ya mishahara ndipo wanne hao walipojeruhiwa.
Kisa hiki kinafuatia kuuwawa kwa wachimba migodi wengine 34 wakati walipopigwa risasi na polisi wiki mbili zilizopita.
Mazungumzo yanayolenga kusitisha mgomo wa wachimba migodi hao wa mgodi wa madini ya Platinum wa Marikana, vile vile yalitarajiwa kuanza hapo jana.
Polisi wanadai kuwa walilazimika kuwafyatulia risasi wachimba migodi hao kama hatua ya kujilinda kwani na wao walikuwa wamejihami kwa mapanga wakati wakikabiliana nao.
Mgomo wao ulioitishwa kulalamikia nyongeza ya mishahara pamoja na kutaka chama chao kipya cha wafanyakazi kutambuliwa, ungali unaendelea huku mgodi ukisalia kufungwa kwa wiki tatu sasa.
Hata hivyo kampuni inayomiliki mgodi huo, Lonmin, ambayo ndio ya tatu kwa ukubwa wa uzalishaji wa madini hayo, imesema kuwa mgomo huo ni haramu.
Lakini imetupilia mbali matakwa yake kuwa ikiwa wafanyakazi hao hawatarejea kazini , watafutwa kazi.
Baada ya ufyatuliaji risasi, viongozi wa mashtaka wa serikali, walitumia kanuni ya enzi ya ubaguzi wa rangi ya kosa la ujumla kuweza kuwafungulia mashtaka wachimba migodi 270 waliokamatwa wakati wa vurugu baada ya mgomo wao kuwalazimisha polisi kuwafyatulia risasi.
Kanuni hiyo ilitumika na walowezi wa kizungu wakati wa enzi ya ubaguzi wa rangi kuwanyanyasa wapinzani wao waafrika weusi.

New