My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, October 20, 2015

Mkeo anahitaji talaka

Wewe bwana MASOUD mkeo kashakutangazia kukuacha na ameshaanza kuidai talaka.Ila mkeo alivyo muungwana akaamua kukupa na sababu za kukuacha ni wewe kutomjali mahitaji muhimu hapati na hata maendeleo ya familia hakuna miaka nenda miaka rudi toka mmefunga ndoa miaka kibao.
Mbaya zaidi si kwamba huna hela..lahasha! Pesa unazo ila mbinafsi saaaana hela zako wewe ni wewe na nduguzo na washkaji zako tu,hujui mkeo kavaa nini wala kala nini..Sasa bi Rehema kachoka anaidai talaka kwa nguvu zote kama kukuvumilia ashakuvumilia sana.
Rafiki yako mpenzi bwana Bashari Mussa Bashar ameona huruma unavyomfuja mkeo ameamua kukupindua sasa...
Bwana Masoud badala ya kuhakikisha unafanya yaleeee aliyokueleza mkeo kwamba ndio chanzo cha kuidai talaka eti na wewe unatoa ahadi kama bwana Bashari wakati mke bado unaye ndani na wewe ndio mume halali..
Kwanini usitende hayo anayoyataka badala ya kumpa ahadi "ooh usiniache ntaanza kukupa unyumba,usiniache ntaanza kukupeleka saluni,ooh usiponiacha ntaacha kujipendelea na ndugu zangu"
Kwa taarifa yako mkeo analalamika kwa watu kwamba anajuta kuolewa na wewe hakujua kama huna akili unazidiwa akili na rafiki yako Bashari ambaye anatoa ahadi za matumaini tofauti na wewe upo nae ndani badala ya kutenda unaahidi na wewe kama mwizi.
KWANINI UNAAHIDI KULALA NA MKEO ASIPOKUACHA KWANINI USILALE NAE WAKATI YUPO NDANI MWAKO?
NASIKIA ULIVYO MJINGA UMEANZA KUIGA MAVAZI YA BWANA BASHARI NA JINSI ANAVYOONGEA ILI MKEO ASIKUACHE..
HAHAHAHA KTK WANAUME MABWEGE DUNIANI BASI NI WEWE BWAN MASOUD YAANI UNAHANGAIKA KUHONGA WATU HELA WAMPAKE MATOPE BASHAR?BADALA HIYO HELA UNGEMPA MKEO AFUNGULIE SALUNI ANGALAU UMPUNGUZE MUNKARI WA KUKUMWAGA..
SASA MAVAZI NA SWAGA ZA KUONGEA ZA MBAYA WAKO ZITASAIDIA NINI WAKATI KIKUBWA ANACHOTAKA NI MAENDELEO KWA UJUMLA?

BWANA MASOUD UNAHITAJI BAGPARTY KUTOKA KWA MANYAKANGA WA USHELISHELI TENA WAKIONGOZWA NA MANYAKANGA WA KIMATAIFA MASHOGA WA MKEO WENYE UCHUNGU BI De Ambroze Nowme,Leah-Buzuka Derefa NA New Tina...NDOA IMEKUSHINDAAAA SUBIRI MKEO AENDE KWA BASHARI KIULAIIIINI.
ILA NASIKITIKA UMEIVUNJA NDOA ILIYOKUWA MFANO WA KUIGWA BARANI AFRICA..TENA UMEIVUNJA KWA MIKONO YAKO MWENYEWEE KWA KUPENDA NDUGUZO NA WASHKAJI KULIKO MKEO.


Kutoka Tanga.


Mkutano wa mgombea urais kupitia UKAWA Mh. Lowassa umevunjika baada ya watu kuzidi kufurika kwa wingi ktk uwanja wa Tangamano nakusababisha msukumano na mkanyagano usiokuwa wakawaida hali iliyotishia usalama wawatu waliofika kamsikiliza Mwanabadilikowao. 

Mh. Sumaye aliwatangazia watu kuwa kutokana na hali ilivyo uwanjani hapo wanalazimika kuufunga mkutano huo. Ndipo umati mzima ulipopaaza sauti ya kumshangilia kukubaliana nae. Hata hivyo mh. Lowassa aliusalimia umati huo kuupungia mkono.


















Mama katika ubora wake






































New