My Web

Emmanuel

CONTACT

Thursday, August 29, 2013

MAMBO 4 YA KUFANYA KWA MPENZI WAKO ILI AKUOE HARAKA

Hoja kubwa ya msingi leo ni jinsi gani mwanamke anaweza kuolewa haraka na mpenzi wake. Ikumbukwe kwamba, hapa tunazungumza na wanawake ambao tayari wapo katika uhusiano, lakini wenzi wao hawana habari kabisa na mambo ya ndoa.


Leo nazungumzia juu ya wewe ambaye upo katika uhusiano ambao haueleweki, lakini ndoa unaitaka. Unajua cha kufanya? Soma hapa chini mambo ya kufanya ili mpenzi uliyenaye akuoe haraka...



1.EPUKA MAKUNDI MABAYA

Mwanaume anapenda kuwa na mke mwenye staha, ambaye hana tabia za hovyo. Kuwa na makundi ya ‘mashangingi’ ni alama ya kwanza kabisa kuwa unapenda au tayari una tabia za kishangingi. Wanaume wengi hawapendi kabisa wanawake wenye tabia za hovyo, wenye kampani ambazo si nzuri.

Lakini yawezekana, jamaa alishakuambia juu ya kilio chake hiki, lakini wewe umekuwa kama umeweka pamba masikioni mwako, hili ni tatizo. Linda heshima yako, kaa mbali na makundi hatari, ili umfanye jamaa akuone wewe ni mwanamke thabiti ambaye huigi, hushabikii na wala huna tabia mbaya. Utaonesha hili kwa kukaa mbali na makundi ya wanawake hatari! 



2. ZINGATIA MAVAZI YAKO

Kila mtu anamjua mtu wake alivyo, mwanamke hata wewe unamjua mpenzi wako alivyo. Sina shaka unafahamu anapenda nini na nini anachukia. Unajua kabisa, nina uhakika na hilo. Lakini pamoja na kwamba jamaa anaweza kuwa na vitu ambavyo vinamvutia zaidi, hata wewe kama mtoto wa kike, una mapendekezo yako au vitu ambavyo unapenda zaidi kuvifanya!

Huzuiwi, lakini swali la msingi, mwenzi wako anapenda? Kama wewe unapenda sana skin jeans na top inayoacha kitovu nje, yeye hapendi kwa sababu ana nia ya kukufanya mke hapo baadaye. Sasa utakuwa mke gani ambaye hata Salim anaona sehemu zako za faragha hadharani?

Ukiachana na chaguo la mwenzi wako, lakini lazima wewe mwenyewe kama mwanamke wa mtu, ujitambue! Jisitiri vyema. Kwani kuna urembo gani wa kuvaa nguo inayoonesha mwili wako ulivyo? Kuna burudani gani kuacha nyeti zako wazi? Unataka nani akuone ulivyo? Mke hana sifa hiyo dada yangu, sasa ili uweze kuwa na sifa hii muhimu, lazima uzingatie sana mavazi yako.



3. JIPE MOYO

Hili nilishawahi kulizungumza sana katika mada zilizopita, baadhi ya wanawake wamekuwa wakikatishwa tamaa na rafiki zao au watu wengine wanaowazunguka, eti hawana hadhi ya kuolewa au watahangaika sana lakini hawatapata mume, kisa eti HAVUTII!

Mwingine anajinyima mwenyewe nafasi akisema; “Mimi nina balaa, sina bahati ya kuolewa, ndiyo maana wadogo zangu wote wameolewa nimebaki mimi.”

Huu ni uvivu wa kuwaza. Lakini dada yangu, habari iliyo njema kwako ni kwamba, ndoa unaitengeneza wewe mwenyewe.

Unaitengeneza kwa misingi ya kwanza, kujipa moyo mwenyewe kwamba wewe ni mzuri na una sifa na haki za kuolewa kama wanawake wengine. Jipe moyo mwenyewe, huna nuksi wala balaa, wewe ni mzuri na una sifa za kuwa mke hapo baadaye.

Iko hivi, ukianza kujishusha mwenyewe, ni dhahiri kwamba hata mavazi yako hayatakuwa mazuri, uso wako hautakuwa na tabasamu na wala hutakuwa na matumani moyoni, hapo sasa ni mwanzo wa kuzorota afya yako. Utapata mchumba kweli? Utasubiri sana kwa mtindo huo.
4. ACHA PAPARA

Haizuiwi kuuliza kuhusu mustakabali wa uchumba wenu, lakini ni vizuri basi kuwa na kiasi. Kuuliza kila wakati au kuwa mtu wa kulaumu, hakutakusaidia kumfanya jamaa achukue maamuzi ya haraka ya kukuoa na badala yake yanaweza kumpa picha tofauti.

Ni rahisi kuwaza kwamba, unachohitaji kwake ni ndoa na baada ya hapo hutakuwa na staha tena. Kuwa mjanja, achana na papara. Usilogwe ukamfanyia jambo zuri mpenzi wako, halafu ndiyo umuulize; “Sasa honey, mbona hata huzungumzii ndoa yetu? Hivi utanioa kweli? Eeeh baby? Niambie basi mpenzi wangu

ATHARI ZA PICHA ZA NUSU UCHI NA TATTOO ZINAZO ZAGAA MITANDAONI

 
Mwezi wa kujistiri kwa wale wenzangu na mie ndiyo huo umeondoka, hapana shaka kuna wengine wanasoma hapa, huku wakiwa ndani ya yale mambo yetu. Siyo ishu, kila mtu ana uhuru wa kufanya kile akipendacho. Nchi yetu inaruhusu kuvaa chochote, ilimradi tu usiende utupu.

Nakumbuka miaka kama mitatu nyuma iliwahi kutokea hoja kuhusu mavazi, wengi walisema Serikali ilikuwa na mpango wa kupiga marufuku vimini na nguo za kubana.

Basi bwana siye tunaopenda mambo hayo roho zilikuwa juu, huku wengine tukitishia hata kuhama nchi ikiwa tutafikia huko kwa kukatazana mavazi.

Lakini kwa bahati nzuri rais wetu, Jakaya Kikwete alilitolea tamko suala hilo  na kusema kuwa kila mtu ana uhuru wa kuvaa kile anachojisikia, ili mradi tu asiende utupu. Hapo alimaliza kila kitu.

Tuachane na mambo ya mavazi, suala la msingi leo ni ‘mapicha’ na tattoo tunazochora mwilini na kuzitupia mtandaoni kila kukicha. Turudi kulekule kwenye uhuru wa kufanya kile unachojisikia, lakini usiku ukienda kulala jiulize mwisho wake nini?

Mimi na wewe hatujui kesho tutakuwa kina nani katika dunia hii, labda uniambie wewe huna ndoto za kufanya jambo litakalokufanya ukumbukwe, hata ukitoweka kwenye uso wa dunia.

Kila mtu, hasa wasichana waona fahari kuweka picha za nusu uchi  katika mitandao ya facebook, twitter na sasa instagram . Ujana, maji ya moto, kwa sasa hizo ‘likes’ na ‘comment’ unazopata zinakuvimbisha kichwa, lakini naamini baadhi yetu, miaka kumi ijayo tutatamani kurudi nyuma ili tuondoe historia mbaya tulioiweka mtandaoni.

Picha hizi zitatumika kukugandamiza kwa chochote unachokusudia kukufanya wakati huo. Ni nani atamchagua kiongozi mwenye picha kama zako unazotupia sasa.Kampuni gani yenye heshima itakayomwajiri mtu mwenye sifa mbaya kwa jamii.

Watu wengi wana uwezo kuona kinachoendelea kwenye mtandao, kumbuka miaka sita au saba kutoka leo siyo mbali, watu watakumbuka, wengine watakuwa na picha zako. Wasiokupenda watazitumia kama silaha ya kukuangamiza.

Kitu kingine ambacho unaweza kuja kukijutia ni hizo tattoo unazochora hivi sasa. Wapo watu hivi sasa wanalazimika kuvaa mashati yenye mikono mirefu, suruali au nguo zenye kuficha maeneo fulani ili waifiche michoro hiyo.

Itafika wakati unashindwa hata namna ya kuwaeleza watoto wako kwa kuwa wengi wanachora kwa kufuata mkumbo au kwa kuona Rihanna, Chris Brown kachora.

 

MAZOEZI 3 YA KUZUIA MATITI YA MWANAMKE YASILALE NA KUWA MALAPA

Ikiwa wewe umechelewa(ulikuwa hujui hili wakati matiti yako yanaota) basi msaidie mdogo wako au binti yako anaekuwa hivi sasa, ili asije kujisikia vibaya pale wanaume watakapokuwa wakiponda  matiti kwa kuyaita "malapa"....

Kwanza kabisa hakikisha mtindo wa kulala ni kifudifudi (kulalia tumbo), kwa kufanya hivyo kunasaidia kwa kiasi kikuwa kufanya matiti yako pumzike, kwamba hakutakuwa na kuning'inia kama utakuwa umelala chali(lalia mgongo) au kiubavu.


Zoezi...1
Asimame wima dhidi ya mlango au ukuta kisha aegeshe matiti yake mahali hapo kwa nguvu kisha aachie (ajitoe ukutani), zoezi hili hufanya matiti yaume sana lakini wewe kama dada  mpe moyo kuwa avumilie. Afanye hivyo mara 20 kila asubuhi.

Zoezi....2
Simama wima huku mikono yako ikiwa imenyooshwa huku na kule kisha ipeleke mbele nakukutanisha viganja vyako alafu irudishe nyumba kadiri uwezavyo (sio lazima ikutane) ila utahisi maumivu fulani sehemu ya matiti (misuli yafanya kazi hapo)....fanya hivyo mara 10 na ongeza hesabu njinsi unavyokua.

Zoezi...3
Ukiwa umesimama wima na mikono yako imenyooshwa huku na hule inanyue taratibu kuelekea juu na kutanisha vidole vyako huko juu kisha rudisha mikono ilipokuwa (imenyooka huku na kule).

JITIBU MAGONJWA HAYA KWA MAJI YA MOTO

                                                          Glasi  ya  maji  ya  moto. 
Ifuatayo  ni  orodha  ya  baadhi  ya  magonjwa  yanayo weza  kutibiwa  kwa  maji  ya  moto.
- pumu= asthma

- shinikizo la damu= hbp

- migraine / kichwa= migraine/ headache

- ugonjwa wa sukari= diabetes

- upungufu wa damu= anemia

- maumivu nyuma= back pain

- mawe katika figo= urinary calculus

- maambukizo wa haja ndogo= urinary tract infection

- cholesterol= cholesterol

- baridi yabisi & ugonjwa wa mifupa= rheumatism & arthritis

- kiharusi =stroke

- udhaifu wa mwili =sexual and body weakness

- kuchoka & uchovu = tiredness & fatigue

- tonsili =tonsillitis

- vijidudu vya tumbo = gastroenteritis (stomach virus)

- mafua/homa =colds, flu & fever

- kukosa usingizi= insomnia (lack of sleep)

- kichome kwenye roho= heartburn


- kidonda tumboni =stomach ulcer

- kuvimbiwa (ugumu kupata haja kubwa) =constipation

- kutetemeka mwili kutokana na umri= parkinsonism

- kupoteza nywele (upaa) =hair loss (baldness)

- magonjwa ya ngozi=skin diseases (psoriasis)

- kasoro ya ubongo =alzheimer (defects of the brain)

- maradhi ya moyo =heart disease

- saratani= cancer

- usafisha heidh ya kila mwezi ya wanawake= purifying women's monthly period


MATUMIZI:
Kunywa  angalau  glasi  moja  ya  maji  ya  moto  mara  mbili kwa  siku, asubuhi  kabla  ya  kula  chochote  na  usiku, kabla  ya  kulala

  Source:  Tafiti   za  taasisi  mbalimbali  za  tiba  asilia.

 

Hatua dhidi ya Syria


Mataifa ya magharibi yakiongozwa na Marekani, yatafakari kutumia nguvu dhidi ya Syria
Wasiwasi wa muungano wa mataifa ya Magharibi kuishambulia Syria umenukia, kufuatia Marekani, Uingereza na Ufaransa kusema kuwa itatoa adhabu kwa taifa hilo la kiarabu kwa kutumia silaha za kemikali katika mapigano dhidi ya waasi nchini humo juma lililopita.
Mataifa ya Magharibi, yakiongozwa na Marekani yanaunga mkono hatua ya kijeshi dhidi ya Syria huku mataifa ya Mashariki na Asia yakiongozwa na Urusi yakipinga.
Eneo karibu na mji mkuu Damascus lililoshambuliwa kwa silaha za kemikali
 
Katika shambulio hilo, ilikuwa dhahiri kuwa silaha hizo za kemikali zilitumiwa lakini kila upande katika mzozo huo ukilaumu mwenzake kwa kufanya hivyo.
Hapa uamuzi ulifanywa, kupitia Umoja wa Mataifa, kuwa wataalamu wa silaha za kemikali wa Umoja huo, wasafiri hadi Syria ili kuchunguza ukweli. Baada ya kushawishi Serikali ya Rais Assad kwa muda, idhini ilitolewa na pia wanajeshi wa Syria wakaahidi kuwa siku hiyo ya kuchunguza mapigano kati ya Serikali na waasi wanaoungwa na mataifa ya Magharibi watasitisha mapigano.
Juma lililopita wachunguzi hao walishambuliwa na wadenguaji mara mbili wakielekea kwenye eneo la kuchunguza, na isitoshe muda mfupi baadaye shambulio kubwa zaidi la silaha za kemikali likafanywa katika makaazi wa waasi, karibu sana na jiji la Damascus.
Kufuatia shambulio la pili ilikuwa wazi sasa kuwa Marekani, Uingereza na Ufaransa ziko tayari kushambulia.Suala la pekee ambalo hadi dakika hii watu wanajiuliza ni, lini?

Urusi yapinga azimio la kuiadhibu Syria

Marekani imeachana na jitihada za kutafuta uungwaji mkono wa baraza la usalama la umoja wa mataifa kuichukulia hatua Syria kwa utumiaji silaha za kemikali.
Hii ni kufuatia kukataa Urusi kwa rasimu ya maazimio yaliowasilishwa kwenye mkutano wa wanachama watano wa kudumu wa baraza hilo la usalama.

Akilaumu Urusi kwa kile alisema msimamo wake wa kutobadili maoni kwa chochote, Msemaji wa wizara ya mashauri ya kigeni, Maria Harf amsema kuwa Marekani haitaruhusu alichotaja kama uzembe wa kidiplomasia kutumiwa kama ngao ya kutetea Serikali ya Syria. Azimio lilioandikwa na Uingereza lingaliruhusu hatua za kuwalinda raia wa Syria lakini likapingwa na Urusi katika kikao cha wanachama watano wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.

Wataalamu wa Umoja wa mataifa wa silaha za kemikali

Urusi, ambayo hutoa silaha kwa Serikali ya Syria na pia mshirika wake mkuu kimataifa, ilisema kuwa kura ya azimio hilo inapaswa kuahirishwa hadi tume maalumu ya umoja wa mataifa ya kuchunguza matumizi ya silaha za kemikali nchini humo itakapokamilisha kazi yake.

Msemaji huyo alielezea hali ya Marekani ya kutoridhika na hali ya upole inayoendelea katika Umoja wa Mataifa, na akasisitiza kwamba kwa wakati huu Marekani haioni matumaini yoyote ya kuungwa mkono na Baraza la Usalama la umoja wa Mataifa na kwa sasa itatilia mkazo mashauriano na mataifa mengine washirika kabla ya kuchukua hatua yoyote inayofaa hivi karibuni.

Alisema kuwa hadi kufikia sasa Rais Obama hajafanya uamuzi wowote juu ya hatua inayopaswa kuchukuliwa, lakini akaongeza kuwa ni dhahiri kuwa silaha za kemikali zilitumiwa nchini Syria na kwamba wa kulaumiwa ni utawala wa Rais Assad.

Friday, August 23, 2013

NDEGE NDOGO YA TANZAIR KUNUSURU ABIRIA WAKE BAADA YA KUTIA HITIRAFU IKIWA ANGANI NA KUTUA LAKE MANYARA


Habari zilizoufikia mtandao huu hivi punde kutoka Mkoani Arusha zinaeleza kuwa Ndege Ndogo ya Shirika la Ndege la TANZAIR iliyokuwa ikitokea Mjini Bukoba kuelekea Jijini Dar es Salaam, imelazimika kutua katikati ya Ziwa Manyara lililopo Mkoani Arusha ili kunusuru abiria wake sita (6) waliokuwamo katika ndege hiyo baada ya kupatwa na hitilafu kwa kuzima ghafla kwa Injini moja wakati ikiwa hewani.
Aidha imeelezwa kuwa katika tukio hilo ni abiria watatu tu ambao wamepatwa na majeraha makubwa huku wakipelekwa kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Sirialni ya Mkoani Arusha, huku wengine wakitazamiwa na kuchunguzwa kabla ya kuruhusiwa kuweza kuendelea na safari.
Rubani wa ndege hiyo alilazimika kutaka kutua ghafla katika Uwanja wa Arusha, kutokana na Hitilafu hiyo, lakini alishindwa baada ya kuona mtikisiko ukizidi na kuamua kuielekeza ndege hiyo katikati ya Ziwa hilo, ambapo alifanikiwa kutua salama na baadhi ya Boti na mitumbwi iliyokuwa karibu iliweza kusogea na kutoa msaada wa kubeba abiria hao na kuwasogeza nchi kavu na baadaye ilifika Helkopta ambayo iliweza kutoa msaada zaidi.

Moto waunguza mitambo ya Songas Dar


Askari wa Kikosi cha zimamoto na Uokoaji wakizima moto uliokuwa unawaka katika mitambo ya kuzalisha umeme ya songas, Ubungo jijini Dar es Salaam jana. (Picha na Francis Dande) 
DAR ES SALAAM, Tanzania
Mitambo ya kuzalisha umeme ya Songas iliyopo Ubungo jijini dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo imeungua moto kabla ya kudhibitiwa na Kikosi cha Uokoaji na Zimamoto kwa kushirikiana na kikosi cha Kampuni ya Knight Support.
Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), Mhandisi Felichesim Mramba, alisema hitilafu hiyo imetokea katika kituo cha 33kv na kusababisha gridi ya taifa inayotumika jijini Dar es Salaam kuzimika, hivyo baadhi ya maeneo umeme ukawa umekatika.
“Tulipata taarifa saa 10 kuwa kuna hitilafu hapa na tukajaribu kuwasiliana na Idara ya Zimamoto kwa simu wakawa hawapatikani mpaka tulipowafuata ofisini kwao. Nashukuru baada ya taarifa walifika kwa wakati na wakafanikiwa kuudhibiti moto,” alisema.
Alisema kuwa kutokana na hitilafu hiyo maeneo mbalimbali ya jiji yaliyokuwa yakipata umeme kupitia kituo hicho yataathirika na kuyataja kuwa ni Kigogo, Mburahati, Magomeni, Tandale na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Meneneo mengine ni Changanyikeni, Kimara, Tabata na Riverside na kwamba juhudi zinafanyika kuangalia uwezekano wa maeneo hayo kuunganishwa katika njia nyingine kwa muda.
Aliongeza kuwa bado hawajajua thamani halisi ya hasara iliyopatikana na muda utakaotumika kufanya marekebisho huku akiainisha kuwa ukarabati wa vifaa hivyo unaweza kuchukua wiki moja mpaka mbili kutegemea na aina ya uharibifu.
Baadhi ya mashuhuda waliliambia gazeti hili kuwa moshi uliokuwa ukitoka katika mitambo hiyo ulikuwa mzito na uliwasababishia kushindwa kupumua vizuri.
“Niliwaona kina mama na watoto waliokuwa wanakwenda katika kituo cha mabasi Ubungo wakipata taabu kupumua hadi tukawa tunawasaidia kuwapeleka mbali na eneo la tukio,” alisema Gervas Lutabalize, ofisa wa Chama cha kutetea abiria.
Kamanda wa Kikosi cha Zima Moto na Uokoaji jijini Dar e s Salaam, ACP Jesward Ikonko, alisema walipata taarifa ya tukio saa 11:58 alfajiri na kufika katika tukio saa 12:5 ambapo waliwakuta wafanyakazi wa kikosi cha Knight Support wakiwa wameshaanza kazi ya kuzima moto.

New