My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, October 31, 2011

Mimba ya Wema yawa kero

Na Brighton Masalu.
WEMA Isaac Sepetu (pichani), mwenye kibendi cha miezi miwili kasoro alichopachikwa na ‘kidume’ Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’, amegeuka kero kwa baadhi ya mastaa Bongo hasa wa kike kutokana na kutema mate ovyo, kujichetua na kuinadi mimba yake kupita maelezo.

Akizungumza na The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda ndani ya Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, Wema alisema kuwa kinachosababisha awe kero ni dalili za wazi za mjamzito alizonazo ikiwemo kutema mate ovyo, kubagua vyakula na kudeka kupitiliza.

Alifunguka: “Wanasema nawakera, lakini nahisi wananionea gere na mimba yangu. Mimi sina chuki na mtu yeyote na naomba…

Na Brighton Masalu.
WEMA Isaac Sepetu (pichani), mwenye kibendi cha miezi miwili kasoro alichopachikwa na ‘kidume’ Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’, amegeuka kero kwa baadhi ya mastaa Bongo hasa wa kike kutokana na kutema mate ovyo, kujichetua na kuinadi mimba yake kupita maelezo.

Akizungumza na The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda ndani ya Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, Wema alisema kuwa kinachosababisha awe kero ni dalili za wazi za mjamzito alizonazo ikiwemo kutema mate ovyo, kubagua vyakula na kudeka kupitiliza.

Alifunguka: “Wanasema nawakera, lakini nahisi wananionea gere na mimba yangu. Mimi sina chuki na mtu yeyote na naomba wanivumilie.”


Bi harusi mtarajiwa


Na Musa Mateja

PICHA za Bi Harusi mtarajiwa ambaye ni modo sexy Bongo, Jacqueline Patrick ‘Jack’ hivi karibuni zimenaswa akiwa katika mapozi ya kimahaba na mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Martin.

Picha hizo ambazo zipo kwenye mtandao zinawaonesha wawili hao wakijiachia kwenye Ufukwe wa Mbalamwezi uliopo Mikocheni jijini Dar es Salaam, mazingira yaliyosababisha baadhi ya watu kuhoji juu ya ukaribu wao huo.

“Mh! Huyu si ndiyo anatarajiwa kuolewa hivi karibuni? Sasa huyu mwanaume ni nani tena, au ndiyo mchumba wake?” alihoji mdau mmoja baada ya kuziona picha hizo.

Katika kujua uhusiano uliopo kati ya wawili hao, mwandishi wetu alimtafuta Jack kupitia simu yake ya mkononi lakini hakuweza kupatikana mara moja.

Martin alipopatikana alisema: “Picha hizo tulizipiga siku tuliyokuwa tunaandaa matangazo flani hivi, ila hazina maana yoyote mbaya, Jack ni mshikaji wangu wa kawaida tu.”

Jack ambaye ni Miss Ilala namba 3, 2005 anatarajiwa kuolewa hivi karibuni ambapo vikao vya harusi vimeshaanza.


Wosia wa Gaddafi

Kanali Muammar Gaddafi.
Sifael Paul na Mashirika ya Habari
SIKU chache baada ya kuuawa kwa aliyekuwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, bado kuna mitazamo tofauti kuhusu tukio hilo huku wosia aliouacha ukiwatoa watu machozi, Ijumaa Wikienda linauanika.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari vya kimataifa, wosia huo uliosambazwa na waliokuwa wakimuunga mkono Kanali Gaddafi umejaa ujasiri, msimamo wa ajabu na utabiri wa aina ya kifo chake.

WOSIA WASISITIZA MAPAMBANO BILA KUJALI KIFO
Pia wosia huo uliwatia moyo wafuasi wake kuendelea kupambana bila kujali kama yeye yuko hai au kafa, hivyo kuuawa kwake inasadikiwa kuwa ndiyo…

Kanali Muammar Gaddafi.
Sifael Paul na Mashirika ya Habari
SIKU chache baada ya kuuawa kwa aliyekuwa kiongozi wa Libya, Kanali Muammar Gaddafi, bado kuna mitazamo tofauti kuhusu tukio hilo huku wosia aliouacha ukiwatoa watu machozi, Ijumaa Wikienda linauanika.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari vya kimataifa, wosia huo uliosambazwa na waliokuwa wakimuunga mkono Kanali Gaddafi umejaa ujasiri, msimamo wa ajabu na utabiri wa aina ya kifo chake.

WOSIA WASISITIZA MAPAMBANO BILA KUJALI KIFO
Pia wosia huo uliwatia moyo wafuasi wake kuendelea kupambana bila kujali kama yeye yuko hai au kafa, hivyo kuuawa kwake inasadikiwa kuwa ndiyo mwanzo wa chuki na kutafutana ili kulipa kisasi.

Wosia huo uliotafsiriwa kutoka katika lugha ya Kiarabu kwenda Kiingereza unaweka wazi kuwa Kanali Gaddafi alichagua kupigana kiume hadi nukta ya mwisho ya uhai wake na kufia katika ardhi ya Libya.

Ulieleza kuwa kukimbilia uhamishoni nje ya nchi yake kilikuwa ni kitendo cha kujidhalilisha, kisichokuwa na heshima pamoja na kwamba alishapata ahadi za ulinzi.

HUU NDIYO WOSIA WENYEWE
Katika tafsiri isiyo rasmi ya Kiswahili, wosia huo ulisomeka:
“Hii ni hiyari yangu. Mimi Muammar bin Mohammad bin Abdussalam bin Humayd bin Abu Manyar bin Humayd bin Nayil al Fuhsi Gaddafi, ninaapa kwamba hakuna Mungu mwingine zaidi ya Allah na Muhammad ni Mtume wake, amani ipo kwake. Ninaahidi nitakufa nikiwa Muislam.

ALIJUA ATAUAWA
“Najua siku siyo nyingi nitauawa, nawaomba mnizike nikiwa nimetapakaa damu zangu kwa mujibu wa taratibu za Kiislam, nikiwa na mavazi nitakayokuwa nimevaa wakati kifo changu kikitokea, bila mwili wangu kuoshwa.

ALITAKA AZIKWE HAPA, MKE NA FAMILIA WALINDWE
“Nizikwe katika makaburi ya Sirte, (Benghazi, Libya) jirani na familia na jamaa zangu.
“Nitapenda kwamba familia yangu, hasa wanawake na watoto, watunzwe vyema baada ya kifo changu.

“Watu wa Libya wana wajibu wa kulinda sifa, mafanikio, historia na heshima ya waasisi na mashujaa wa taifa lao.
“Walibya hawatakiwi kupuuza kujitapa na lazima wawe watu huru wa kuthaminiwa.

UJASIRI
“Ninawataka wale wanaoniunga mkono kuendelea kupambana, kuwakabili wote wanaosimama kutoka nje dhidi ya Libya, leo, kesho na siku zote. Msikubali hata siku moja kuuza utu wenu kwa wageni.

FUNZO
“Hata kama hatutashinda mapema, tutatoa funzo kwa vizazi vyetu vijavyo, kwamba kuchagua kulinda utaifa ni heshima na kuliuza ni uasi mkubwa ambao historia haitausahau milele, pamoja na juhudi za wengine kuwaeleza kinyume cha hayo”.

TAFSIRI NYINGINE
Kwa mujibu wa wachambuzi wa mambo ya kisiasa barani Afrika, Kanali Gaddafi na mwanaye Mutassim walikuwa na udhaifu wao, lakini hawakustahili kifo cha ‘sampuli’ walichokutana nacho.

Kanali Gaddafi anaelezewa kuwa ni aina ya viongozi wa Afrika wenye misimamo mikali kama ilivyo kwa Nelson Mandela na Robert Mugabe.

BADO KIMENUKA LIBYA
Jiji la Sirte alikozaliwa Kanali Gaddafi, watu wa kabila lake wanaendeleza mapambano ambapo mwishoni mwa wiki iliyopita viliripotiwa vifo vya watu 100.

Saturday, October 29, 2011

Dawa za asili zamzeesha mrembo

Mwanadada Nguyen Thi Phuong alivyokuwa kabla ya kutumia dawa za asili.

Nguyen Thi Phuong alivyo baada ya kutumia dawa za asili.

NGUYEN Thi Phuong ni mwanadada mwenye asili ya Vietnam, ukimuangalia huenda ukadhani ni bibi wa miaka 73 lakini ni binti mdogo mwenye umri wa miaka 26.

Mrembo huyo, aligeuka mzee mwaka 2008 na kwa mujibu wa madaktari, tatizo hilo amelipata baada ya kutumia dawa za asili.

Wakati anakutwa na tatizo hilo, Nguyen alikuwa na umri wa miaka 23. Kipindi hicho alikuwa mrembo mwenye sura ya kuvutia lakini hivi sasa hana raha, kwani sura yake ni ya kikongwe.

Pamoja na madaktari kusema hivyo, Nguyen anaamini kuwa hali aliyonayo imesabishwa na aina ya samaki wa baharini aliokuwa anakula ambao ndiyo wamemsababishia mzio (aleji) mwilini.


Nguyen akiwa na mumewe, Thanh Tuyen.


Mume wa Nguyen, ambaye ni fundi seremala, Thanh Tuyen, alisisitiza kuwa pamoja na mkewe kuzeeka, bado anampenda kama zamani.

Tuyen alisema, kinachomsikitisha ni kwamba yeye na mkewe hawajapata mtoto na kutokana na hali ngumu kiuchumi aliyonayo, hajui kama Nguyen anaweza kupona na kushika ujauzito, kwani hivi sasa ni kama amezeeka.

Kutokana na namna Nguyen alivyoharibika, amekuwa akitembea amevaa kinyago (maski) ili kuficha uso wake.
“Wakati naanza kuumwa nilikuwa najisikia maumivu mwili mzima, pia nilikuwa nawashwa wakati wa kulala,” alisema Nguyen.

Nguyen aliendelea kusema kuwa baada ya maumivu aliamua kutafuta dawa kwenye maduka ya madawa ya kawaida kwa sababu yeye na mume wake hawana uwezo wa kununua dawa zinazofaa kwa sababu ya umaskini.

NI UGONJWA GANI?
Madaktari wanafafanua kuwa ugonjwa alionao Nguyen unaitwa Lipodystrophy ambao husababisha kuyeyuka kwa mafuta ya chini ya ngozi, hivyo kusinyaa na mhusika kuonekana mzee.

Wataalamu hao wamesema kuwa mwili wa Nguyen una kiwango kikubwa sana cha cortisol iliyotokana na mitishamba.
Ugonjwa huo unatajwa kuwapata wanawake wengi ambao wana umri kati ya miaka 20 na 40.

Daktari Vo Thi Bach Suong wa Hospitali ya HCMC, amejitolea kumsaidia Nguyen kwa kumpa matibabu yatakayomuwezesha kupona kabisa.

Unaishi mbali na Mpenzi wako

WENZI kuishi mbalimbali ni mtihani mkubwa kwa wengi. Jambo hilo linapotokea, fikra huhamia kwenye kuwapoteza wapenzi wao, kusalitiwa au kugombana. Kwa namna fulani, mawazo hayo huwa sahihi, lakini leo nitakupa mbinu.

Kama mtakumbuka vyema, wiki chache zilizopita niliwahi kuandika mada inayozungumzia faida za wapenzi kuishi mbalimbali, leo nitasogea mbele zaidi, nikilenga namna ya kuboresha uhusiano huo na kumfanya mwenzi asipate wazo la usaliti.

Tatizo hapa ni kukosa mbinu za kuboresha penzi, hapo ndiyo mwanzo wa kuchochea kuachana. Tafiti mbalimbali zinaonyesha kwamba wapenzi ambao wanaishi mbali mbali, kama wasipokuwa makini ni rahisi sana kuachana au kuwa na ugomvi ambao mwisho wake ni kutengana kuliko wale ambao wanaishi pamoja au eneo moja.

Waswahili wanasema, fimbo ya mbali haiui nyoka, hivyo ukitokea ugomvi mdogo, hasa ukizingatia kwamba wanaishi mbali inakuwa rahisi kwa mmoja wao kuamua kulipiza kisasi kwa kutoka na patna mwingine.

Katika mada hii, nitakupa njia mbadala za kuufanya uhusiano wako uendelee kuwa hai, pamoja na kwamba mnaishi mbali na mpenzi wako. Hebu twende pamoja.

MAWASILIANO
Kuwasiliana na mpenzi wako mara kwa mara kunatajwa kama njia mojawapo kati ya nyingi zinazoweza kukusogeza karibu zaidi na mwandani wako, hivyo kumfanya azidi kukupenda na kushindwa kukusahau.

Hata hivyo, wengi hushindwa kujua aina ya mawasiliano na jinsi ya kutumia ili kuteka akili za wapenzi wao na kuwafanya waendelee nao siku zote za maisha yao, pamoja na kwamba wapo mbali nao.

Hapa chini ni vijisehemu vichache ambavyo vinaainisha mambo ambayo ukiyazingatia, utaendelea kuulinda uhusiano wako hata kama mwenzi wako yupo mbali.

(i) Barua pepe
Njia hii ya mawasiliano kwa wapenzi walio mbali ni nzuri sana. Hata hivyo inategemea mpenzi wako yupo wapi, maana kuna maeneo mengine yanakuwa hayana huduma za Mtandao wa Intaneti.

Kutokana na kukua kwa Teknolojia, wengi humiliki kompyuta za mikononi (lap top) ambazo huwarahisishia mawasiliano ya moja kwa moja na watu wengi. Kama mpenzi wako ni mmoja wao, hii ni nafasi nzuri sana kwako.

Mtumie kadi nzuri zenye ujumbe mwanana wa mapenzi kwa ajili ya kuhamasisha penzi. Mwandikie tungo za mapenzi ukionesha ubunifu wako. Pia waweza kumtumia vichekesho kwa ajili ya kumburudisha na kumfanya mwenye furaha.

Haya unaweza kufanya kwa wingi kadri uwezavyo na kwa nafasi yako, huku ukizingatia upatikanaji wa huduma hiyo na uwezo wa kumudu gharama. Kadhalika unapaswa kuzingatia uwiano wa kumfikia mpenzi wako.

Hapa namaanisha kwamba kama anamiliki lap top yake ni rahisi zaidi maana unaweza kumtumia nyingi kadiri uwezavyo, lakini kama ni wa kwenda Internet Cafe mara moja kwa wiki, basi unapaswa kumtumia mara moja kwa wiki. Umenipata?

(ii) Simu
Kuwasiliana kwa njia ya simu za mkononi ni moja kati ya njia bora za mawasiliano na kuboresha uhusiano wa wapenzi. Mwenzi wako anapokuwa mbali na wewe, kwa kutumia njia hii, unaweza kumsogeza karibu yako na kufurahia sana uwepo wako, ingawa upo naye mbali.

Epuka neno ‘habari yako?’ baada ya kumpigia simu. Lazima kauli yako iwe laini, uzungumze naye kwa unyenyekevu na kumtia hamasa ya kuzidi kuzungumza na wewe. Kadhalika unapomwandikia meseji, kaa chini na utunge, siyo unamwandikia ‘sema mwenzangu, uko poa? Umeshakula?’ Hii ni meseji mbaya kwani haina hamasa yoyote ya kimahaba.

Unapaswa kumtumia sms za mapenzi, tungo za mahaba, maneno ya utani, vichekesho na kejeli. Hivi ni kati ya vitu vya kufurahisha ambavyo kwa hakika vikifanywa, humfanya mwenzi wako kuwa na hofu ya kukusaliti.

Unaweza kumtumia meseji nyingi kadiri uwezavyo kulingana na uwezo wako wa kifedha, ingawa mitandao mingi ya simu za mikononi siku hizi huwa na ofa maalumu ya kutuma sms nyingi kwa gharama ya chini. Unaweza kujisajili kila siku kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano na mpenzi wako.

Pamoja na kwamba uwezo wako kifedha, muda na majukumu vinaweza kukufanya uamue idadi ya meseji utakazomtumia mpenzi wako, lakini ni lazima umtumie angalau meseji tano kwa siku.

Meseji hizo hutumwa kwa muda maalum, mathalani baada ya kuamka asubuhi unapaswa kumtumia ujumbe mzuri, uliojaa mashairi na tungo za mapenzi, ukimtakia asubuhi njema na mafanikio katika kazi zake za kutwa hiyo.

Mchana, mtakie mlo mwema na kazi njema, alasiri mtumie ujumbe wa kichekesho. Usiku, mtumie ujumbe wa kumpa pole kwa kazi, kisha malizia kwa kumtumia ujumbe mwanana wakati wa kulala.

Kama nilivyoeleza awali, unaweza kutuma meseji nyingi zaidi kulingana na uwezo wako na muda huku ukizingatia majukumu yako ya kazi.

Inawezekana mwenzi wako huko alipo, ana kazi nyingi na ratiba zake zinambana sana, kama ndivyo unapaswa kuhakikisha humtumii meseji nyingi sana, kwani unaweza kumkera kwa milio ya simu kila wakati, muda ambao yeye hutumia kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuboresha maisha yenu ya baadaye.

Ni vyema kuangalia sana ratiba yake ya mchana, kwa suala la kumpigia simu na kumwandikia meseji. Unaweza kumpigia simu angalau mara mbili kwa siku, kisha baada ya hapo ukamwachia muda wa kufanya kazi, kwani si busara kumsumbua sana anapokuwa ana majukumu kazini.

Usiku ni muda mzuri kwako ‘kumlinda’ mpenzi wako. Zungumza naye kwa sauti laini ambayo inaweza kuamsha hisia zenu na kujikuta kila mmoja akiwa anaridhika kwa kusikia tu sauti ya mwenzi wake.

Haya ni mambo yanayowezekana na kwa hakika kama ukijaribu utaona mafanikio yake makubwa. Inawezekana, jaribu utaona.

Watu wafurika kwa Nabii Flora kupata uponyaji

Nabii Flora (aliyeshika maiki) akiendesha maombezi kwa wenye matatizo.
Watu wenye matatizo wakishiriki maombi ya kuponywa kanisani kwa Nabii Flora.
WATU wengi wamekuwa wakifurika kutafuta uponyaji kwa njia ya maombezi kutoka kwa Nabii Flora ambaye mashuhuda wanasema anaponya magonjwa mbalimbali kama vile Ukimwi, kansa, kupoteza fahamu, magonjwa ya moyo, upofu, ulemavu na kadhalika.

Maombi hayo yaendeshwa na Nabii Flora huko Mbezi Beach maeneo ya Tangi Bovu jijini Dar es Salaam ambapo watu wenye kufuata huduma hiyo wamekuwa wakiwasiliana naye kwa kutumia namba za simu 0657 442699.

Zifuatazo ni picha zaidi za uponyaji katika kanisa la Nabii Flora:

Ugumu wa maisha usipunguze raha ya mapenzi


MUHALI gani mabibi na mabwana wale wote ambao huwa tupo sambamba katika kuhakikisha hamuikosi safu hii. Kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu natumaini wote mu wazima wa afya njema, kwa wale walio wagonjwa Muumba awape nafuu ili mpone upesi.

Naam leo najua kina baba mmekaa tayari kujua kwa nini niwaite wavivu, nina maana yangu, ni ukweli ulio dhahili kuwa kina baba wengi kutokana na ugumu wa kazi na mawazo mengi kichwani au ugumu wa maisha ya maana kila kukicha hali inakuwa ni afadhali ya jana.

Mmejikuta muda mwingi hamfikirii masuala ya mapenzi zaidi ya kufikiria baada ya kula leo, ungoje kesho yake itakuwaje.
Hata mkeo akitaka haki yake utampa tu ili mradi, kwako huwa ni karaha na kuona kama usumbufu. Kama ulimzoesha kumliza kilio cha mbwa, anakuwa hakipati tena, basi zinakuwa lawama kila kukicha.

Siku zote ili ufurahie penzi lazima moyo wako uwe umetulia na mawazo yako yaweze kuwaza kile ukifanyacho. Lakini unawaza ugumu wa maisha mkeo naye anataka haki yake asilimia 100.

Lakini ugumu wa maisha upo hata ufanyeje, la muhimu japo hukufanikiwa kupata chochote urudipo nyumbani muone mkeo kama tulizo lako. Usifikiri ni wewe unayeumia bali hata yeye vile vile anaumia kwa kuona unataabika bila mafanikio.

Hivyo basi, unaporudi hujitahidi kumliwaza kwa mapenzi motomoto kwa kuwa starehe ile huilipii, angalau mioyo yenu muipe chakula chake. Usiwe mkosa yote, fedha hukupata na hata mkeo hukumridhisha.

Hata kazi nzito hupoteza hamu ya kufanya mapenzi, kwa mwanamke lazima umjue mwenzio yupo kwenye hali gani, najua umeshikika na wa kukutuliza ni mumeo mpe nafasi angalau apumzike kidogo, kisha ruksa kuurudisha mwili wake kwenye hali ya mapenzi kwa kuuandaa mwili, kwa kumshika zile sehemu zinazoupa mwili msisimko kwa haraka.

Lazima atajisikia hamu ya mapenzi, hapo lazima uwe makini kwa kujua mwenzio pamoja na kumrudisha katika hali ya mapenzi bado mwili wake hautakiwi kazi nzito tena bali unatakiwa kumpa penzi laini ambalo halitamchosha sana na kuuchosha mwili wake zaidi.

Hapa lazima mwanaume awe mbunifu kwa mtindo wa njia ya mkato ambao utawahisha kumfikisha kileleni haraka mwanamke bila kuuchosha sana mwili wako.
Siku zote mwanaume unatakiwa kumsoma mkeo ili kujua njia ipi ya haraka kumfikisha mwenzako au penzi la muda mrefu la kuinjoi unapokuwa na nguvu za kutosha.

Kwa utaratibu huu nina imani malalamiko ndani ya nyumba zetu yatakwisha, mwisho namalizia kwa kusema kuwa ugumu wa maisha usipunguze upendo ndani ya nyumba kwa kumnyima mwenzio haki yake, nawe mwanamke ukimuandaa mwenzio raha zako utazipata.

Dotnata awachana wavaa nusu utupu

Na Mwandishi Wetu
Staa wa filamu, muziki na mjasiriamali Bongo, Husna Posh ‘Dotnata’ (pichani) ameibuka na kuwaponda wasanii hususan wacheza filamu wanaovaa nusu uchi na kuwaambia kwamba kufanya hivyo ni zaidi ya kujidhalilisha.

Dotnata anayekimbiza sokoni na filamu yake ya Chupa Nyeusi aliyowashikirisha wasanii wa Burundi, akichonga na paparazi wetu hivi karibuni katika viunga vya Msasani Beach Club Kinondoni, alisema anawashangaa mastaa wanaopenda kuvaa nguo fupi sana na kukatiza mitaani bila kujali kama wao ni kioo cha jamii.

“Unajua sisi wasanii hasa wanawake tunapaswa kuwa mstari wa mbele kusimamamia maadili kwa sababu ni kioo cha jamii, sasa tunapovaa nguo fupi zinazotuacha nusu uchi na kukatiza mitaani jamii ituelewaje?” alihoji Dotnata.

Msanii huyo aliongeza kuwa thamani ya ustaa ni kujiheshimu na kuvaa nguo za heshima jambo linaloweza kuigwa na jamii kuliko mambo yasiyofaa kama ulevi, uasherati na kutembea nusu uchi.

MWANAMKE BORA ANAPATIKANA MJINI AU KIJIJINI - 2

NI siku nyingine tena tunakutana katika safu yetu bora ambayo inazungumzia mambo ya mapenzi. Inapanua uelewa na kujenga kujiamini zaidi katika uwanja wa mapenzi. Wengi wamenufaika kupitia hapa.

Ndoa nyingi zilizopoteza muelekeo zimekaa sawa baada ya kusoma ukurasa huu. Kadhalika kuna vijana wengi ambao wamefanya maamuzi sahihi na kuoa/kuolewa na wenzi sahihi baada ya kupata muongozo hapa.

Naam! Ni kisima cha ujuzi wa mambo ya mapenzi. Mada inayoendelea ni kama inavyosomeka hapo juu. Tupo katika juma la pili la kuangalia ni wapi hasa mwanamke bora anapopatikana.

Wiki iliyopita tulianza kwa kuona faida na hasara za mwanamke wa kijijini. Pia tulianza kuona faida za mwanamke wa mjini. Leo tuanze na kuona hasara za mwanamke wa mjini kabla ya kusonga mbele zaidi.

HASARA
Inaelezwa kwamba wanawake wa mijini, hutumia vibaya utandawazi na hujikuta wameharibika na hivyo kuwa na tabia chafu. Mitandano ya simu za mikononi na intaneti zinatajwa kama vyombo vinavyotumiwa na baadhi ya wanawake hao kufanya ufuska.

Ni wanawake wa gharama sana, wanapenda kutolewa ‘out’, disko na kumbi mbalimbali za burudani kila mwisho wa wiki. Kama akizoeshwa ndiyo huwa hatari zaidi, kwani siku asipotolewa, huwa ugomvi mkubwa, maana ameshachukulia kama sehemu ya maisha yao ya kimapenzi.

Wakati mwingine ni wabishi, wanaweka fedha mbele, wakiamini fedha ni kila kitu katika mapenzi. Baadhi yao huwa na wanaume kwa ajili ya kujipatia fedha tu, na siyo ajabu siku fedha ikiisha ikawa ndiyo mwisho wa mapenzi.

Mara nyingi wanawake hawa wamezoea maisha mepesi, siyo rahisi sana kukabiliana na mikikimikiki ya maisha. Kwa maneno mengine, huwa hawawezi kuishi katika mazingira ya shida au mabadiliko ya mazingira.

Tatizo lingine kwa wanawake hawa ni mavazi yao, mara nyingi hayana staha na hata kama ukimweleza juu ya hilo, huwa mgumu sana kubadilika.

Siyo werevu wa kukabiliana na vishawishi (hasa waliopo maofisini). Ni wepesi sana kushawishiwa kwa ahadi ndogo ndogo au mvuto wa kimahaba wa wanaume watanashati. Kama hutakuwa makini na mwanamke huyu, unaweza kuwa kwenye foleni ya mapenzi bila kujua.

Ni mjanja sana wa kutengeneza mambo, anaweza kuwa amefanya kitu, lakini akakudanganya kwamba hajafanya, hata kama ni kwa kutoa machozi! Huyu ni mkali wa kufanya usanii na usishtukie kirahisi.

Kwa uchache tu, hizo ndiyo hasara za kuwa na mwanamke huyu wa mjini. Hata hivyo, usisahau kwamba, siyo kila mwanamke anaweza kuwa na tabia nilizoanisha hapo juu. Wengine wana baadhi, zaidi au pungufu lakini kwa wastani wengi wana tabia hizo.

Sina shaka sasa, umeanza kuelewa japo kidogo sana kuhusu wanawake hawa wanaoishi katika mazingira tofauti. Swali la msingi sasa ni je, nani kati ya hawa anaweza kuwa mke bora zaidi ya mwenzake?

Je, kuna ukweli kwamba wanawake wa kijijini wakiolewa na wanaume wa mjini hubadilika? Je, mwanaume wa kijijini anaweza kuoa mjini na kumchukua mwanamke huyo kwenda kuishi naye kijijini? Tuendelee kuona.

VIPI MAZINGIRA?
Wengi wanaamini wanawake wa vijijini wana mapenzi ya kweli, wazuri, wakarimu na wenye sifa zote nzuri za kuwa wake bora, lakini wakiolewa na kupelekwa mjini hubadilika! Sababu ambazo zinatajwa kusababisha kubadilika huku ni pamoja na kuathiriwa na mazingira.

Inaelezwa kuwa, msichana ambaye amekulia kijijini ambapo hakuna mambo mengi kama mjini, akifika mjini anabadilishwa na mazingira. Hili siyo la kweli. Sikatai kwamba hakuna wanawake ambao wakifika mjini wanabadilika, lakini nataka kukuambia kwamba,
kinachombadilisha siyo mazingira bali tabia yake.

Kama mwanamke ana tabia chafu, hata akiwa kijijini anaweza kuendelea na uchafu wake vizuri sana. Lakini tunapotizama suala la mazingira, siku hizi za Sayansi ya Teknolojia, kuna vitu vingi sana vipo vijijini.
Nishati ya umeme, mawasiliano yameondoa matabaka yaliyokuwepo zamani, angalau kwa kiasi kidogo, hivyo mwanamke wa kijijini hatakuwa na mageni sana atakapoenda mjini.

Kama umeamua kuoa kijijini na kumchukua mkeo huyo kwenda naye mjini, ni vizuri sana kumwangalia kwa karibu, mweleweshe mji ulivyo, mtahadharishe na walaghai, mwambie jinsi unavyompenda na ulivyomuona wa thamani.

Mtake aithamini thamani hiyo kwa kumchagua yeye, mambo haya na mengine yanayofanana na hayo yanaweza kumbabadilisha mwanamke wako na kuwa mwenye heshima na asiyebabaishwa na mabadiliko hayo.

Kubwa zaidi ni vyema kama utapata muda wa kuzungumza naye kabla ya kumpeleka mjini, yaani picha nzima ya maisha ya mjini awe nayo kabla ya kufika mjini, hii nayo inaweza kumsaidia na kumfanya aishi kwa umakini bila kushawishika.

Kumbuka kwamba, makosa mengi yanayofanywa na wanawake ni kwa sababu ya kuhadaiwa, sasa kama utakuwa umeshamfumbua macho mapema, siyo rahisi kudanganyika!
Mada bado inaendelea, wiki ijayo nitakuja kumalizia sehemu ya mwisho, USIKOSE!

Wema anaswa kifakamia nguna

Na Imelda Mtema
IKIWA ni siku chache tangu aonje joto ya jiwe kwenye mapenzi, msanii wa filamu Wema Sepetu juzikati alinaswa akifakamia ugali kwa mlenda nyumbani kwa Mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi Mketema maeneo ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Ijumaa hivi karibuni lilifika nyumbani kwa Zamaradi kwa lengo la kufanya naye mahojiano lakini bila kutarajia lilimnasa Wema akiwa katulia akijenga mwili kwa mlo huo.

Akizungumza na mwandishi wetu Wema alisema, ana muda mrefu hajala chakula hicho hivyo alivyokikuta kwa shosti wake huyo hakuona sababu ya kujivunga.

“Mimi na mlenda usinipimie kabisa, ndiyo maana unaniona sijivungi,” alisema Wema huku akipeleka tonge mdomoni kisha kulumangia na samaki wa kukaanga.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa tangu mpenzi wake Naseeb Abdul ‘Diamond’ atishie kumuacha, afya ya Wema ambaye inaelezwa kuwa mjamzito imetingishika hivyo ameamua kutokuwa mvivu katika suala la kula ili kufukia mashimo.

KUKAMATWA KUUAWA KWA GADDAFI

Luquman Maloto na Mitandao
KUNA mvutano kuhusu mazishi ya marehemu Kanali Muammar Gaddafi, watu wa kabila la kiongozi huyo wa zamani wa Libya, wanadai mwili wa ndugu yao ili wauzike kwa heshima, wakati Baraza la Mpito linaweka ngumu na kusisitiza kwamba atazikwa kwa siri kubwa.
Ijumaa Wikienda, limenasa maisha ya Gaddafi saa 18 kabla ya kifo chake pamoja na danadana za mwili wa kiongozi huyo ambaye neno lake, harakati zake na fedha alizomwaga katika ufadhili, ndivyo viliwezesha kuundwa kwa Umoja wa Afrika.

Jumamosi iliyopita, Mwenyekiti wa Baraza la Mpito (NTC), Mustafa Mohammed Abdul Jalil alitarajiwa kwenda jijini Misrata kutoa tamko kuhusu mazishi hayo.

Kwa mujibu wa mtu anayedaiwa alikuwa mlinzi wa Gaddafi kabla ya kumgeuka dakika za mwisho, saa 18 kabla kiongozi huyo wa zamani wa Libya kufariki dunia, alizitumia kusali na kuweka mikakati ya kuhama Jiji la Sirte.

Mlinzi huyo (jina limehifadhiwa) alisema kuwa katika saa hizo 18, Gaddafi alizungumza na wanajeshi wachache waliokuwa wamebaki wanamlinda na kuwaambia kwamba hategemei kurudi kutawala Libya na hadhani kama ana maisha marefu.
Hata hivyo, jina la mlinzi huyo limefichwa ili kukwepa hasira za watu wanaompenda Gaddafi kulipa kisasi.

Aliongeza kusema: “Aliwaambia wapigaji kwamba wakipata nafasi warudi kuitetea Libya na wasikubali vibaraka wa Marekani na Uingereza wafilisi mali za Walibya.”

Alisema kuwa saa tatu kabla Gaddafi na timu yake, hawajaanza kutoroka, alizungumza na wanaye kwa muda mrefu lakini akawasisitiza: “Msiumie wala msifedheheke, wakati mwingine Shetani hutumia nguvu na kufunika haki dhidi ya batili.”

NENO LA MWISHO
Mlinzi huyo alisema, Gaddafi alijitetea kwa maneno mengi ili asiuawe lakini kauli maarufu aliitoa kwa njia ya kuuliza, “je, ninyi wanangu, mnaifahamu haki kwenye uongo?”

SAFARI YA KIFO
Alhamisi iliyopita (Oktoba 20, 2011), Gaddafi na timu yake, wakiwa kwenye magari ya kifahari, walikuwa wanahama kutoka Jiji la Sirte kuelekea mpakani. Inadaiwa walitaka kutorokea nje ya nchi, ingawa taarifa nyingine zinadai kiongozi huyo aligoma kuondoka na kusisitiza anangoja kufa kwenye ardhi aliyozaliwa.

Saa 2:30 asubuhi (saa za Libya), vikosi vya Nato na Ufaransa viliyashambulia kwa mabomu magari ya msafara wa Gaddafi. Magari 15 yaliharibiwa kwenye mashambulizi hayo, Gaddafi na timu yake walikwenda kujificha kwenye daraja la mtaro.

5:05 asubuhi, NTC ilitangaza kuwa ngome ya Gaddafi imekwisha na kilichobaki ni kutafuta masalia.
8:00 mchana, baada ya mapambano ya risasi kwisha, Gaddafi aligundulika yupo kwenye daraja la mtaro wa maji machafu amejificha.

8:45 mchana mwanaume mmoja mkazi wa Sirte aliliambia Shirika la Utangazaji la Reuters kuwa alimuona Gaddafi akipigwa risasi tumboni kwa bastola yenye ukumwa wa 9mm.

8:56 mchana, Reuters ilitangaza kuwa Gaddafi alifariki dunia kutokana na majeraha baada ya mapigano ya risasi.

9:00 mchana, wapiganaji wa NTC walianza kuzunguka mitaani wanashangilia kukamatwa na kuuawa kwa Gaddafi.
10:31 alasiri, AFP ilitangaza kuwa mtoto wa Gaddafi, Muttasim amekutwa ameuawa jijini Sirte.

11:52 jioni, mwili wa Gaddafi ulifikishwa Misrata.


1:50 jioni, Aljazeera ilitangaza kuwa mtoto wa Gaddafi, Saif al Islam naye ameuawa kwenye mashambulizi hayo. Ingawa taarifa za baadaye zinasema kuwa Saif mikono yake ilikatika katika mashambulizi.

AMAZING FACTS ABOUT GADDAFI

Muammar Abu Minyar al-Gaddafi.

1. There is *no electricity bill* in Libya; electricity is free for all its citizens.
2. There is *no interest on loans*, banks in Libya are state-owned and loans given to all its citizens at 0% interest by law.
3. *Home* considered a human right in Libya – Gaddafi vowed that his parents would not get a house until everyone in Libya had a home. Gaddafi’s father has died while him, his wife and his mother are still living in a tent.
4. All newlyweds in Libya receive *$60,000 Dinar* (US$50,000) by the government to buy their first apartment so to help start up the family.
5. Education and medical treatments are free in Libya. Before Gaddafi only 25% of Libyans are literate. Today the figure is 83%.
6. Should Libyans want to take up *farming* career, they would receive farming land, a farming house, equipments, seeds and livestock to kick-start their farms – all for free.
7. If Libyans cannot find the education or medical facilities they need in Libya, the government funds them to *go abroad* for it – not only free but they get US$2,300/mth accommodation and car allowance.
8. In Libyan, if a Libyan buys a *car*, the government subsidized 50% of the price.
9. The price of *petrol* in Libya is $0.14 per liter.

10. Libya has *no external debt* and its reserves amount to $150 billion – now frozen globally.
11. If a Libyan is unable to get *employment* after graduation the state would pay the average salary of the profession as if he or she is employed until employment is found.
12. A portion of Libyan *oil sale* is, credited directly to the bank accounts of all Libyan citizens.
13. A mother who *gave birth* to a child receive US$5,000
14. 40 loaves of *bread* in Libya costs $ 0.15
15. 25% of Libyans have a *university degree*
16. Gaddafi carried out the world’s largest *irrigation* project, known as the Great Man-Made River project, to make water readily available throughout the desert country.

Which other dictator has done much good to his people besides.

*P.S. If this is the dictator Gaddafi is, then give us one like him here in Bolehland

lulu amfuata Mwanaume Marekani

Na Imelda Mtema

Mcheza filamu mdogo ambaye hivi karibuni alipenda aitwe ‘mrs Bieber’, Elizabeth Michael ‘Lulu’ yupo kwenye maandalizi ya kwenda Marekani kwa ajili ya kumfuata mwanamuziki anayetamba kwa sasa nchini humo, Justine Bieber.

Lulu alizungumza hayo kupitia mtandao wa mtangazaji mahiri wa Televisheni ya Clouds ya jijini Dar, Zamaradi Mketema.

Alisema kwamba endapo atakwama katika suala la nauli, atatengeneza kadi kwa ajili ya kuchangisha michango kwa maana kitendo hicho alichoamua ni cha kijasiri sana kwa vile ni nadra binadamu kujitoa ‘mhanga’ kwenda kumtafuta mtu nje ya nchi.

“Mimi lazima nimfuate, hata kama nauli itanishinda nimeshaandaa mpango wa kuchangisha kwa kupitia kadi ambazo nitazitengeneza, kitendo hiki ni cha kijasiri sana, hakuna mtu ambaye aliwahi kufanya,” alisema Lulu.

Staa huyo aliongeza kuwa endapo atafanikiwa kumuona ‘laivu’ mwanamuziki huyo ndipo mchezo mzima utakapoishia na Watanzania waamini kuwa lazima atamleta Bongo kwa sababu anajua akionana naye hawezi kuchomoa.

“Nitakapoonana naye lazima nitamleta hapa nyumbani kuonesha ushindi wangu kwani najua akionana na mimi kamwe hawezi kuchomoa kwangu,” aliweka wazi Lulu kupitia mtandao huo.
mwisho wa GADDAFI


Mwandishi Wetu na intaneti

Wanajeshi wa Serikali ya Baraza la Mpito la Libya (NTC), walitamba wakishangilia, wakati asilimia kubwa ya raia walizizima kwa vilio juzi (Alhamisi) baada ya kupokea taarifa kwamba Muammar Gaddafi amefariki dunia.

Gaddafi aliyeiongoza Libya kwa zaidi ya miongo minne, enzi yake ilifika mwisho baada ya kuuawa na wapiganaji wa NTC kwenye jiji alilozaliwa la Sirte, Libya.

Habari zinasema kuwa wapiganaji wa NTC walimshambulia Gaddafi miguuni, hivyo kumfanya ashindwe kukimbia kabla ya ‘kumshuti’ na kummaliza kabisa.

Waziri wa Habari wa NTC, Mahmoud Shammam alithibitisha kuuawa kwa Gaddafi aliyeanza kuitawala Libya kuanzia mwaka 1969 kabla ya utawala wake kuangushwa mwaka huu.

Hata hivyo, picha za awali zilizotolewa zikimuonesha kiongozi huyo akiwa amefariki dunia, zilikosolewa kwa maelezo kwamba zilitengenezwa kwa lengo la kuuzuga ulimwengu.

Ubishi uliisha baada ya kutolewa kwa video inayowaonesha wapiganaji wa NTC wakiuburuza barabarani mwili wa Gaddafi uliokuwa umejaa damu huku wakimpiga na kumdhihaki.

Kutokana na hilo, wanaharakati wa haki za binadamu wamevishutumu vikosi vya NTC kwa kitendo cha kuuzungusha mwili wa Gaddafi barabarani na kumpiga.

Kwa mujibu wa NTC, yalitokea mapigano makali kati ya wapiganaji waliokuwa wanamlinda Gaddafi dhidi ya wanajeshi wa baraza hilo la mpito.

NI ZAIDI YA MATESO
Video zinazomuonesha Gaddafi baada ya kuuawa, zinaonesha jinsi kiongozi huyo wa zamani wa Libya alivyokumbwa na mateso makali katika saa za mwisho za uhai wake.

Katika moja ya video, wapiganaji wa NTC walionekana wakiuchanachana mwili wa Gaddafi, kitendo ambacho kimelaaniwa vikali na wanaharakati wa haki za binadamu.

Baadhi ya wananchi wa Libya hasa Waislamu, baada ya hali kuchafuka juzi kutokana na kifo cha mtawala wao wa zamani, walijumuika misikitini na kusali kumuombea apumzike kwa amani.

Walisema kuwa kwa mateso ambayo wapiganaji wa NTC walimpa Gaddafi, ni afadhali sasa apumzike na Mungu atamkadiria yale aliyotenda duniani kama yanafaa kumpeleka peponi au motoni.

YALIYOMSIBU SAA 24 KABLA YA KIFO
Baada ya Gaddafi kuuawa, NTC walifanikiwa kumtia nguvuni mmoja wa watoto wake wa kiume ambaye hata hivyo hawakumtaja jina.

Imeelezwa kuwa mtoto huyo aliwaambia wapiganaji wa NTC kwamba 24 kabla ya kifo cha Gaddafi, alikuwa akisumbuliwa na mawazo ya kutenganishwa na familia yake ingawa hakujua kama na kifo kimemkariba.

Habari zinaeleza kuwa Gaddafi alishachoka kupambana lakini alikuwa haelewi hatima yake ni nini ndiyo maana alibakiza wafuasi wachache wa kumlinda.

Ilielezwa pia kuwa katika kipindi cha saa hizo, alikuwa akionesha dalili za kufika mwisho wa maisha yake ya hapa duniani.

Ilifika wakati alikuwa akishindwa kula kama zamani, muda mwingi akionesha kukata tamaa, kumbe wapiganaji wa NTC walishamkaribia.

Friday, October 28, 2011

FOUR KILLED IN MANDERA GRENADE ATTACK

Al-Shabaab soldiers.

By KBC reporters
FOUR people have died in a grenade attack on a government vehicle transporting exam materials in Lafey area, in Mandera.

Military Spokesman Emmanuel Chirchir said a rocket propelled grenade was thrown at a LandCruiser in Sino area.

Those who died were the principal of Lafey secondary school in Mandera district, the Lafey divisional district education officer, a former councillor and a mechanic.

Two homeguards who were escorting the victims survived the attacks.

This is the third grenade attack this week, after two other explosions rocked separate locations in Nairobi on Monday morning and evening.

Video showing a man who killed in second Nairobi grenade attack on Monday.

The four casualties were among six people travelling to Mandera town early in the morning, in a Toyota Surf vehicle that belonged to the principal.

They were ambushed when they were about 50km from Mandera by militia who emerged from bushes and started spraying the car with bullets.

An administration police officer in Mandera said the homeguards jumped out of the vehicle firing back at the bandits, who responded by hurling the explosive device on the vehicle.

The two homeguards were said to have escape in a hail of bullets ad were reported to have sustained injuries.

The headmaster, the DEO and the councillor were said to have been well-known figures in Mandera town.

They had been driving to the town daily to pick exam papers since the tests began almost two weeks ago.

Confirming the incident, North Eastern Provincial Commissioner James ole Serian linked the attack to the Al shabaab militia group currently being pursued by the Kenya army inside Somalia.

He said security agents are pursuing the group across the border .

The PC said that a Provincial security committee had met following the incident and more police had been deployed along the porous Somalia border.

He said patrol will be intensified across the province so as to protect life and property of innocent mwananchi who he said are an easy prey to members of militia group.

He cautioned people visiting social places such as bars to be vigilant and report suspicious looking individuals to police.

The administrator said that a search will be conducted in the province to wipe out foreigners causing chaos in the name of retaliation.

The provincial boss cautioned residents to avoid traveling at night saying that the gang would use darkness as a mask to attack.

He directed the provincial administrators hold security meetings for the next three days to sensitize members of the public on security measures.

He advised travelers from Mandera County to use Mandera -ramu-elwaq and avoid mandera-lafey-elwak route as it was prone to militia attacks

Meanwhile, Police Spokesman Erick Kiraith described it as a "banditry attack" that happened about 110 km (70 miles) from Mandera town.

In a brief statement to newsrooms, Kiraithe said his officers are heading to the scene and will give more details in due course.

"We have received a report of a banditry attack in Mandera District about 110 kilometers from Mandera town involving a vehicle carrying government officials among others . The District Police Commander and his security team are proceeding to the scene , we shall give details in due course".

Kenya sent hundreds of troops into Somalia on 16 October to attack al-Shabab, which is linked to al-Qaeda.

Al-Shabab has repeatedly threatened retaliatory attacks on Kenya.

On Wednesday, a man arrested after two grenade blasts in Nairobi, admitted in court to being a member of the group.

Elgiva Bwire Oliacha pleaded guilty to carrying out the attacks on a nightclub and bus stop.

One person was killed and 29 others were wounded in the attacks on 24 October.

Security has been stepped up in Nairobi since the blasts.

Thursday, October 27, 2011

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AHUDHURIAAHUDHURIA MKUTANO WA MAWASILIANO WA KIMATAIFA HUKO GENEVA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza katika mkutano wa Mawasiliano wa Kimataifa, uliofanyika Geneva, Switzerland, Oktoba 25.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihojiwa na mtangazaji wa Televisheni ya CNN, Becky Underson, baada ya kuhudhuria katika mkutano wa Mawasiliano wa kimataifa uliofanyika Geneva, Switzerland, Oktoba 25.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri wa Mawasiliano wa India, Kapil Jibal, wakati walipokutana katika ufunguzi wa mkutano wa Mawasiliano wa Kimataifa, uliofanyika Oktoba 25, Geneva, Switzerland.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akichangia hoja wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Mawasiliano wa Kimataifa, uliofanyika Oktoba 25, 2011.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika ufunguzi wa mkutano wa Mawasiliano wa Kimataifa, uliofanyika Oktoba 25, Geneva Switzerland, ambapo Tanzania ilikuwa ni moja kati ya nchi zilizoshiriki katika maonyesho ya mkutano huo.

New