My Web

Emmanuel

CONTACT

Saturday, October 29, 2011

Wema anaswa kifakamia nguna

Na Imelda Mtema
IKIWA ni siku chache tangu aonje joto ya jiwe kwenye mapenzi, msanii wa filamu Wema Sepetu juzikati alinaswa akifakamia ugali kwa mlenda nyumbani kwa Mtangazaji wa Clouds TV, Zamaradi Mketema maeneo ya Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Ijumaa hivi karibuni lilifika nyumbani kwa Zamaradi kwa lengo la kufanya naye mahojiano lakini bila kutarajia lilimnasa Wema akiwa katulia akijenga mwili kwa mlo huo.

Akizungumza na mwandishi wetu Wema alisema, ana muda mrefu hajala chakula hicho hivyo alivyokikuta kwa shosti wake huyo hakuona sababu ya kujivunga.

“Mimi na mlenda usinipimie kabisa, ndiyo maana unaniona sijivungi,” alisema Wema huku akipeleka tonge mdomoni kisha kulumangia na samaki wa kukaanga.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa tangu mpenzi wake Naseeb Abdul ‘Diamond’ atishie kumuacha, afya ya Wema ambaye inaelezwa kuwa mjamzito imetingishika hivyo ameamua kutokuwa mvivu katika suala la kula ili kufukia mashimo.

No comments:

Post a Comment

New