My Web

Emmanuel

CONTACT

Thursday, March 29, 2012

MWANAFUNZI ALIYETOA MANENO YA KIBAGUZI DHIDI YA FABRICE MUAMBA AENDA JELA SIKU 56

Mtuhumiwa Liam Stacey (kulia) akiwa chini ya ulinzi.

A student who posted a series of racist comments on Twitter following footballer Fabrice Muamba’s cardiac arrest has begun a prison sentence of 56 days.

Liam Stacey, 21, caused widespread revulsion by reacting to Muamba’s mid-game collapse by writing: ‘LOL [laughing out loud], **** Muamba. He’s dead!!! #haha.’ He responded to criticism of that message with vile racist tweets.
The messages were forwarded to the police by several members of the social network, including former England striker Stan Collymore, himself a victim of abuse on Twitter...


As he spent his first night behind bars, the two teams most shaken by Muamba's collapse replayed the fixture that was called off when the midfielder came close to death.

Tottenham Hotspur and Bolton Wanderers met again at White Hart Lane, with the home team cruising to a 3-1 victory.

It means Muamba's club are now out of the FA Cup, but this hardly seemed to matter to the fans and players treating the match as a chance to pay tribute to him.

Stacey, seen arriving at the court earlier in the morning, posted a series of vile tweets about footballer Fabrice Muamba

Stacey, seen arriving at the court earlier in the morning, posted a series of vile tweets about footballer Fabrice Muamba

At the ground where the 23-year-old's heart stopped, his teammate Sam Ricketts was seen to wipe a tear from his eye before kick-off. It was a difficult return for the entire Bolton squad, and manager Owen Coyle commended them for their bravery.

Players from both sides wore T-shirts bearing messages of thanks to those who supported Muamba, while the whole of the Tottenham stadium erupted in applause for him.

Stacey, meanwhile, faces expulsion from Swansea University. The third-year biology student had hoped to become a forensic scientist. Describing his tweets, prosecutor Louise Barron told the court: ‘The offence is clearly racially aggravated.

‘There was sustained and gratuitous racism. These were unprovoked comments and persistent abuse. The recipients were disgusted.’

Jailing the student at Swansea Magistrates’ Court, District Judge John Charles said: ‘Not just the footballer’s family, not just the footballing world, but the whole world were literally praying for Muamba’s life. Your comments aggravated this situation.

‘I have no choice but to impose an immediate custodial sentence to reflect the public outrage at what you have done.’

Stacey made his comments about the Bolton Wanderers midfielder while celebrating the Welsh rugby team’s Six Nations grand slam victory earlier this month.

The judge added: ‘You committed this offence while you were drunk and it is clear you immediately regretted it.

'But you must learn how to handle your alcohol better.’

Stacey, from Pontypridd, South Wales, told police following his arrest at his student home in Swansea: ‘I was at the bar when I heard what had happened to Muamba.

'I don’t know why I posted [the comments]. I’m not racist and some of my friends are from different cultural backgrounds.’

He later sent a text message to a friend saying: ‘I said something about Muamba that I shouldn’t have and tweeted back to some people who abused me.

'Getting police on me now which isn’t good at all.’

Another read: ‘Been bawling my eyes out on the phone to my mother for the last hour, really can’t be dealing with this.’

Applause: Everybody clapped for Muamba at the start of the match (and below)

Applause: Everybody clapped for Muamba at the start of the match (and below)

muamba

Gareth Jones, defending, said Stacey ‘does not bear [Muamba] any grudge and is glad he is making a good recovery’.

He continued: ‘My client simply lost his head and posted these disgusting comments to the bitter shame of himself and his parents.

'For a moment of madness, his career has now gone.’

Stacey’s father Neale, 49, and mother Hayley, 46, were visibly shocked when the details of his comments were read aloud yesterday.

Solidarity: Bolton's Nigel Reo-Coker (left) and Tottenham's Jermain Defoe shake hands

Solidarity: Bolton's Nigel Reo-Coker (left) and Tottenham's Jermain Defoe shake hands

Jim Brisbane, chief crown prosecutor for CPS Cymru-Wales, said: ‘Racist language is inappropriate in any setting and through any media.

'We hope this case will serve as a warning to anyone who may think that comments made online are somehow beyond the law.’

Muamba is said to be continuing to make good progress at the London Chest Hospital, where he was visited by his Bolton teammates ahead of their rescheduled match against Tottenham.

The game was abandoned on March 17 following Muamba’s collapse.

Upsetting: Fabrice Muamba's is treated by medical staff on Saturday after collapsing. A court heard that Liam Stacey, 21, posted mocking tweets as the midfielder was treated on the pitch

Upsetting: Fabrice Muamba is treated by medical staff after collapsing. Liam Stacey, 21, posted mocking tweets as the midfielder was treated on the pitch

'God is in control': Shauna Magunda, right, Fabrice Muamba's fiancee urged her Twitter followers to keep the Bolton player in their prayers as he fights for lifeHappier time: Shauna Magunda, right, Fabrice Muamba's fiancee, has urged fans to keep the Bolton player in their prayers as he continues to recover from a life-threatening condition


Read more: http://www.dailymail.co.uk/news/article-2121003/Liam-Stacey-jail-tweeting-abuse-Fabrice-Muamba.html#ixzz1qRrFN7p7

Wednesday, March 28, 2012

JIHADHARINI NA UTAPELI HUU, UMERUDI TENA JIJINI

Wana Global naomba kushea na nyinyi stori ya jaribio la utapeli lililonitokea jana tarehe 26/03/2012,

majira ya saa sita na nusu mchana nilipigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Patric Makombe ambaye alidai kuwa anafanyakazi shirika la chakula duniani katika kambi moja huko Kigoma. Mtu huyo alilitaja jina langu kwa ufasaha kazi yangu namba ya gari na mtaa ninaoishi.

Mtu huyo alidai kuwa amewahi kufanyakazi katika benki ya NMB Tanga baadae akahamia WFP Kigoma namba ya simu ya mtu huyu ni 0712127749. Alinijulisha kuwa hapo ofisini kwake wanahitaji dawa fulani ya kuhifadhia chakula na kwamba baada ya muda bosi wake atanipigia kwa kuwa kwa wakati ule alikuwa kwenye kikao lakini akaniomba nikubali kushirikana nae kwa kuwa ananifahamu kuwa ni mtu mwaminifu na nisingeweza kuwadhulumu baada ya biashara.

Baada ya masaa matatu hivi alinipigia simu mtu aliyejitambulisha kwa jina la Thomas Michael ambaye alidai kuwa ni coordinator wa WFP Kigoma na alinieleza kuwa anahitaji product inaitwa DAMOLINE LIQUID BEST IN FOOD PAIR 50. Na akaniambia nimtafute mtu anaitwa Dr. Msuya Peter namba ya simu 0656367291 ni muulize wanauzaje pea moja ya hiyo dawa kisha nimjulishe lakini nisimwambie chochote huyo Dr. Msuya kwa kuwa mwaka jana aliwadhulumu walipo fanya dili kama hiyo. Aliendelea kudai kuwa bei nitakayo ambiwa atanielekeza niongeze kiasi fulani kisha bosi wake ambaye ni mzungu atakapokuja kununua nimpige hicho cha juu na hiyo ndio itakuwa faida yetu. Ingawa nilishaanza kustuka lakini nilifanya kama nilivyoelekezwa kumpigia Dr. Msuya naye akanijibu dawa kwa pea moja ni dola 3100 za Marekani ambazo ni karibu ya shilingi za Kitanzania milioni tano. Nilipo mrudishia jibu akasema huyo Mzungu akija ni muuzie dola 4000 na kwamba faida yetu kwa kila pea itakuwa dola 900 sawa na shilingi milioni moja na laki nne hivi. Na kwamba Mzungu atakapokuja atachukuwa pea hamsini. kwa kuwa ilikuwa jioni tulikubaliana tuwasiliane siku inayofuata ili tuanze dili. Usiku huo nilamua kufuatilia kwenye mtandao maana ya hiyo DALOMINE LIQUID. Hamaaad nilipofungua tu nikakutana na ujumbe jihadhari na utapeli huu kwenye blogu mbili tofauti za bongo. Kwa mujibu wa maelezo yao kama ningeenda kwenye dili ningeambiwa na matapeli kuwa niende kwa Dr. Msuya ninunue sample moja ya dawa kisha niende nayo Golden Tulip au uwanja wa ndege kumsubiri bosi wake ambaye angekuwa anatokea Kigoma kisha ningeondoka na mtu mwingine kwenda kuchukua pea 49 zilizobaki pamoja na kulipwa kitita changu kisha tugawane. Kumbuka kuwa kama ningeenda kwa Dr. Msuya ningetakiwa kwenda na dola 3100 ili nipewe hiyo sample na kwa kufanya hivyo ningeenda Golden Tulip kuwatafuta hao waungwana nisingekuta mtu. Baada ya kujua ujanja wao niliwasubiri wanipigie siku iliyofuta na walifanya hivyo majira ya saa nne asubuhi. Niliwaomba wanitumie nauli toka nilipo hadi Dar ili tuendelee na dili ndipo walipostuka na hawajapiga simu tena. Hivyo nawaomba sana wana Global muwatahadahrishe ndugu zetu wote kuhusu utapeli huu mpya. Watu wameibiwa mamilioni ya shilingi mkitaka kuhakikisha fungueni GOOGLE kisha andika DALOMINE LIQUID BEST IN FOOD halafu fuatilia trend za jamaa wa mablog wanavyoshusha hata mwenye blogu mmoja anaitwa Michuzi limemfika jambo hili tahadharini sana ndugu zangu.

Monday, March 26, 2012

Kitu usichokijua kuhusu ‘juisi ya boksi’- 2

WIKI iliyopita tulianza makala haya kwa kueleza ukweli kuhusu juisi ya boksi ambayo huandikwa asilimia 100 ‘pure fruit juice’ na kusema kwamba haya ni maneno ya kibiashara ambayo hayana ukweli wowote. Sasa endelea...

Aidha, Hamilton anaendelea kueleza mchezo mchafu unaochezwa na watengeneza juisi viwandani kwamba ladha ya juisi hiyo ya machungwa hutofautiana pia kati ya nchi na nchi, kwani viwanda huweka aina ya ladha kwenye chungwa kulingana na vile ambavyo wanapenda watu wa eneo inakokwenda.

Juisi inayotengenezwa kwa ajili ya nchi za Amerika Kaskazini huwa na kiwango kikibuwa cha kirutubisho aina ya ‘ethyl butyrate’, ambacho ni moja ya kemikali inayotumika sana kwenye utengenezaji wa manukato na ladha. Mbali ya kirutubisho hicho kuwa na uwezo wa kutengeneza aina mbalimbali za ladha za matunda, lakini pia hakina gharama (cheap).

HATUA GANI ZA KUCHUKUA SASA?
Kama makala haya yatakuwa yamekushitua na kukushangaza, jua hauko peke yako. Hata hivyo, lengo kubwa la makala haya ni kukufumbua macho ujue juisi unayokunywa siyo salama kiasi gani na uwe na uamuzi wa kuicha au kuendelea kuitumia kwa hiyari yako mwenyewe, lakini siyo kwa kudanganywa na maelezo ya uongo ya kibiashara yanayowekwa juu yake.

Kama ambavyo mwandishi wa kitabu hicho Bi. Hamilton anavyosema: “Lengo la kitabu changu siyo kukataza watu kunywa juisi, isipokuwa kuwafanya wakijue vizuri wanachokinywa. Watu wana haki ya kujua ni kwa kiasi gani utengenezaji wa juisi hivi sasa umekuwa wa kibiashara zaidi, hii itawafanya wawe na maamuzi sahihi kuhusu afya zao.”

Ingawa ni vigumu sana kuepuka ‘kuingizwa mkenge’, lakini unaweza kujiepusha na madhara ya kiafya yatokanayo na unywaji wa juisi hizi ‘feki’ kwa kupendelea kunywa juisi uliyoitayarisha mwenywe nyumbani na kuacha kununua vyakula au vinywaji ‘ready made’, hasa kwa vile ambavyo vinapatikana kwa wingi sokoni.

TAHADHARI
Kwa ujumla matunda na juisi zake zina virutubisho vingi muhimu kwa ustawi wa afya ya binadamu, lakini tahadhari inatolewa kwa wanaopenda kunywa kiasi kingi cha juisi za matunda, hasa juisi ya machungwa ambayo inaelezwa kuwa na sukari nyingi.

Kiasi cha glasi moja ya juisi ya machungwa ina wastani wa gramu 25 za ‘fructose’, (sukari), kiwango ambacho ni cha mwisho kabisa anachotakiwa mtu kutumia kwa siku moja. Hii ina maana kama utakunywa zaidi ya glasi moja pamoja na vinywaji vingine vinavyotumia sukari, kama vile chai, tayari utakuwa umezidisha kiwango kinachopendekezwa kwa siku.

Iwapo utakuwa na tatizo la unene na unahitaji kupunguza uzito, ni vyema ukapunguza sana au ukajiepusha kabisa na uywaji wa juisi za matunda, kwa sababu kiwango cha sukari kilichomo ni zaidi ya wastani unaotakiwa.

Ili upate faida za virutubisho vinavyopatikana kwenye matunda, yakiwemo machungwa, unashauriwa kula matunda hayo kama yalivyo kuliko kukamua juisi na kutupa makapi yake. Inaelezwa kwamba sukari iliyomo kwenye chungwa inapoliwa pamoja na nyama zake (fibre), sukari hiyo huwa haina madhara kwani huweza kujichanganya kwenye mfumo wa damu bila kuleta athari zozote kwa mlaji.

Hivyo ushauri wa ujumla unatolewa kwamba pendelea zaidi kula matunda na mboga za majani kama zilivyo kuliko kunywa juisi zake. Kwa kufanya hivyo utajiepusha na uwezekano wa kusumbuliwa na ugonjwa wa kisukari. Iwapo utakunywa, basi kunywa nusu glasi au isizidi glasi moja kwa siku. Asanteni.

JUISI YA KITUNGUU: HUPONYA YALIYOSHINDIKANA HOSPITALI!

Katika makala ya leo nawaeleza faida za juisi ya kitunguu maji katika mwili wako, ikiwemo uwezo wake wa kuzuia na kutibu magonjwa sugu na yaliyoshindikana kwa kutumia dawa za hospitali.

Tunapaswa kutambua kwamba viungo vingi tunavyotumia jikoni kwenye vyakula vyetu kila siku vina uwezo mkubwa wa kuponya magonjwa yanayotusumbua. Sina shaka kama kuna mtu ambaye hakijui kitunguu, nyanya, au kitunguu saumu.

Kitunguu maji ni kiungo cha mboga, ambacho aghalabu hutumika katika mapishi ili kuongeza ladha katika chakula na wakati mwingine hutumika kutengenezea kachumbari. Baadhi ya watu hawapendi kula kachumbari kwa kutokujua umuhimu wake mwilini.

KITUNGUU KINATIBU YAFUATAYO
Katika orodha ndefu ya magonjwa yanayotibika PASIPO SHAKA kwa kutumia juisi ya kitunguu, ni pamoja na ugonjwa unaowasumbua watu wengi wa kutokwa na damu sehemu ya haja kubwa wakati wa kujisadidia.

Ugonjwa huu, ambao kwa kitaalamu unajulikana kama ‘hemorrhoids’ au ‘Piles’, unawatokea watu wengi ambao kama mtu hukupata nafuu kwa kula vidonge, suluhisho la mwisho huwa ni kufanyiwa upasuaji mdogo katika njia ya haja kubwa, upasuaji ambao huambatana na maumivu makali.

Kwa wale ambao wameshakutwa na tatizo hili au wanalo hadi sasa, dawa kama vile ANUL SUPPOSITORIES, SECNIDAZOLE, n.k zinajulikana sana kwao, kwa sababu ndiyo dawa zinazopendekezwa na madaktari wengi kutumiwa ili kutibu PILES. Unaweza ukapona kwa muda na tatizo likajirudia baadaye au unaweza usipone na ukalazimika kufanyiwa upasuaji.

Lakini kwa kutumia juisi ya kitunguu, unaweza ukapona kabisa na inawezekana tatizo lisijirudie, kwani mzizi wa tatizo huondoka kabisa kutoka tumboni.

SIFA YA KITUNGUU
Kitunguu kina virutubisho vyenye uwezo wa kuua bakteria (antibacterial) na fangasi mwilini. (anti fungus). Pia kina virutubisho vyenye uwezo wa kuzuia wadudu wanaosababisha magonjwa nyemelezi (anti free radicals) na magonjwa ya uvimbe (anti informatory).

Mbali na sifa hizo, kitunguu kina kiwango kikubwa cha madini kama vile ‘calcium’, ‘magnesium’, ‘sodium’, ‘potassium’, ‘selenium’, ‘phosphorus’ na bila kusahauu kiasi kidogo cha aina fulani ya mafuta ambayo huimarisha kinga ya mwili.
JINSI YA KUJITIBU ‘HEMORRHOIDS.’

Kama nilivyoanza kusema awali, pamoja na magonjwa mengine yanayotibika kwa kitunguu, leo tutaanza kwanza na ugonjwa huu unaosumbua watu wengi. Dawa hii ni ya uhakika kwa mtu atakayeweza kuitumia kama inavyotakiwa.

Kunywa juisi ya kitunguu kila siku asubuhi kwa muda wa siku saba hadi siku 14, ikitegemea na ukubwa wa tatizo lako. Juisi hiyo lazima uinywe asubuhi kabla ya kula kitu chochote (on empty stomach) na utaruhusiwa kunywa kifungua kinywa chako saa moja baada ya kunywa juisi hiyo.

Dozi hii ni maalum kwa ajili ya kutibu ‘hemorrhoids’, ingawa wakati ukitibu tatizo hilo, matatizo mengine yaliyomo mwilini yatakuwa yakijiondoa, kama tutakavyoona katika makala haya wiki ijayo. Napenda kukuhakikishia kuwa tiba hii ni ya uhakika na haina madhara yoyote.

TAHADHARI
Mara baada ya kuinywa juisi hii kwa mara ya kwanza na siku chache zitakazofuata, utajisikia vibaya na tumbo kuchafuka. Hali hii ni ya kawaida, unachotakiwa kufanya mara baada ya kunywa, ni kukaa au kulala kwa muda, baada ya muda hali yako itarejea kama kawaida. Baada ya siku tatu, ukinywa mwili utaizoea na utajisikia kawaida tu.

ZIJUE FAIDA 10 ZA TENDE KIAFYA

Katika mwezi mtukufu wa Ramadhani, tende ndiyo tunda linaloliwa kwa wingi, pengine kuliko tunda lingine. Pamoja na kuwa ni tunda lenye ladha tamu na nzuri mdomoni,

lakini kisayansi pia limethibitika kusheheni madini na vitamini lukuki, hivyo kuwa na faida nyingi kiafya. Katika makala ya leo, nimekuorodhoshea faida zake 10:


1. Ukila tende mara kwa mara, mwili wako utapata aina mbalimbali za madini na vitamin za kutosha, ambazo zinapatikana kwenye tunda hili maarufu duniani. Katika tende kuna kiasi kidogo tu cha mafuta (fat) na haina lehemu (kolestrol).


2. Ukila tende, utajipatia kiasi cha kutosha cha protini na vitamin B1, B2, B3, B5, A1, na C, virutubisho ambavyo ni muhimu kwa ustawi wa afya ya mwili wako kwa ujumla.


3. Ulaji wa tende huimarisha na kuboresha mfumo wa usagaji chakula tumboni, hivyo utaondokana na matatizo ya ukosefu wa choo, au matatizo ya kupata choo kigumu kinachosababisha maumivu wakati wa kujisaidia. Pia ndani ya tende kuna virutubisho vya ‘amino acids’ ambavyo ni muhimu mwilini.


4. Ukila tende, mwili utapata nguvu na kukuondolea uchovu ndani ya nusu saa tu, kwa sababu tende ina virutubisho vya sukari asilia kama vile ‘glucose’, ‘sucrose’ na ‘fructose’. Ili kupata faida zaidi za tende,

changanya na maziwa fresh kisha kula. Unapojisikia mchovu, badala ya kunywa vinywaji baridi vinavyodai kuongeza nguvu, kula tende, hata kiasi cha punje tatu kinatosha. Kwa wafunga saumu, ndiyo maana inashauriwa kuanza kufungua kwa kula tende ili kuurejeshea mwili wako nguvu iliyopotea siku nzima.


5. Tende ina madini pia aina ya ‘potassium’ na kiasi kidogo cha chumvi (sodium). Madini haya husaidia uimarishaji wa mishipa ya fahamu. Watafiti wamegundua kwamba ulaji kiasi wa ‘potassium’ huweza kumuepusha mtu na kupatwa na kiharusi (stroke). Pia tende husaidia kupunguza lehemu (cholesterol) mwilini (LDL Cholesterol).


6. Kwa wale wenye matatizo ya ugonjwa wa kukauka damu mwilini (anemia), wanaweza kupata ahueni kwa kula tende kwa wingi ambayo ina kiwango cha kutosha cha madini ya chuma ambayo huhitajika katika utengenezaji wa damu mwilini. Wakati vitu vitamu vingine huozesha meno, utamu wa tende huzuia uozaji wa meno.
7. Kwa tatizo sugu na la muda mrefu la ukosefu wa choo, loweka tende za kutosha kwenye maji kiasi cha lita moja usiku kucha, kisha asubuhi changanya maji hayo pamoja na hizo tende ili upate juisi nzito, kunywa na choo kitafunguka na kuwa laini.

8. Kwa matatizo ya ukosefu wa nguvu za kiume, mchanganyiko maalum wa tende, maziwa, asali na unga wa hiriki vinaweza kuondoa tatizo lako. Chukua kiasi cha kiganja kimoja cha tende, loweka kwenye maziwa ya mbuzi kiasi cha lita moja na yakae usiku kucha.

Asubuhi, zisage tende hizo kwenye maziwa hayo hadi zichangayike, kisha weka asali kiasi cha vijiko vitatu au vinne vikubwa pamoja na unga wa hiriki, kiasi cha nusu kijiko kidogo. Kisha kunywa mchangayiko huo kila siku hadi utakapoona mabadiliko ya kuridhisha.


9. Tende ni dawa ya unene, kwa wale wenye matatizo ya wembamba wa kupindukia na wanataka kuongeza uzito, ulaji wa tende kila siku unaweza kuwasaidia. Lakini hii ina maana kwamba, wale wanaohitaji kupunguza uzito, ulaji wa tende kwa wingi hauwezi kuwafaa. Pia tende husaidia uondoaji wa kilevi mwilini.


10. Tende inatibu saratani ya tumbo. Habari njema kuhusu tende kama tiba ni kwamba, haina madhara yoyote kwa sababu ni dawa asilia na inafanyakazi vizuri kuliko dawa za ‘kizungu’. Tende vile vile ina imarisha nuru ya macho na tatizo la kutokuona usiku (night blindness).


Kwa ujumla faida za tende ni nyingi na unaweza kuila tende kwa namna mbalimbali, kama vile kuchanganya na maziwa, kuchanganya na mkate au vitafunwa vingine. Ifanye tende kuwa sehemu ya mlo wako wa kila siku ili ujipatie faida hizi 10 na nyingine.

KAMA HULI NAFAKA, MBOGA, MATUNDA, UKO HATARINI

ILI mwanadamu awe na afya bora, anapaswa kula kwa wingi vyakula vitokanavyo na nafaka, ale mboga za majani pamoja na matunda, angalau mara kwa mara kama siyo kila siku. Kwa sababu vyakula hivi ndiyo msingi wa afya bora ya kila binadamu.

Kwa mujibu wa wanasayansi wetu, mwili wa binadamu una chembechembe hai (cells) zaidi ya trioni 70. Katika chembechembe hizo ndipo ulipo uhai, zikifa na binadamu naye hufa, zikiwa dhaifu na binadamu naye huwa hivyo hivyo.

Ili chembechembe hizo ziwe hai, zinahitaji kula na chakula chake ni virutubisho tu ambavyo asilimia kubwa na muhimu inapatikana katika vyakula vya nafaka (ambayo haijaondolewa viini lishe). Ndani ya nafaka, kama vile mchele, ngano, mahindi, maharage, n.k., ndiko kunakopatikana virutubisho hivyo.

Madhara ya kuwa na chembechembe dhaifu ni makubwa na unaweza kuyasikia mwenyewe. Kwanza mwili huwa mchovu, usio na nguvu, unapotumia dawa hazifanyi kazi upesi mwilini, kama ni dozi ya malaria, ni lazima utumie zaidi ya moja au dawa kali zaidi! Katika hili baadhi husema fulani ana malaria sugu, lakini ukweli ni kwamba chembechembe zako zimekauka, hazina tena uwezo wa kupenyeza dawa na kutoa sumu mwilini.

MATUNDA NA MBOGAMBOGA
Hili ni kundi la chakula ambalo nalo ni muhimu sana. Baada ya kujenga mwili (chembechembe hai), sasa unahitaji kuulinda ili uwe imara na unaofanya kazi yake sawasawa. Kazi hiyo inafanywa kwa kula matunda na mbogamboga kwa wingi, chakula hiki ndicho kinachojenga mfumo wa kinga ya mwili (Body Immunity System), inayouwezesha mwili wako kujikinga wenyewe dhidi ya maradhi mbalimbali na kukufanya uishi kwa muda mrefu bila kuugua hata malaria.

Kwa mujibu wa Shirika la Afya la Dunia (WHO), binadamu anatakiwa kula milo ya matunda na mboga kati ya 5-9 kila siku. Mboga na matunda yana virutubisho muhimu vinavyotoa kinga mwilini (Anti-oxidant) ambayo hupambana na kuondoa viini vya magonjwa (free radicals).

Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya watu hula matunda kwa nadra sana na wengine hawali kabisa! Msimu wa matunda unaingia mpaka unaisha, mtu hajala hata tunda moja au kama kala, basi ya kuhesabu, wengine mpaka waagizwe na daktari, hii ni hatari kwa afya yako na hauutendei haki mwili wako.

Kwa upande wa mboga za majani, hali ni mbaya zaidi, watu hawapendi kula mboga za majani, zinachukuliwa kama chakula cha kimasikini, bila kujua kwamba kwa kuacha kula mboga za majani unayakaribisha maradhi hatari, kama vile saratani, magonjwa ya moyo, n.k.

Ni vizuri ikaeleweka kwamba binadamu hatuwezi kula kama zinavyotaka nafsi zetu, bali tunapaswa kula kama miili yetu inavyotaka. Sisi hatuwezi kuwa muhimu kuliko miili yetu. Kwa mfano, unapopatwa na kiharusi na kupooza mwili, hapo mwili huwa umegoma kufanyakazi na chanzo huwa ni wewe mwenyewe ulishindwa kuupa chakula unachokihitaji ili ujiendeshe wenyewe.

Mwili umeumbwa kama mnyororo, unategemeana sehemu moja na nyingine, sehemu moja inapopatwa na tatizo, mwili mzima unataabika. Maradhi yamekuwa mengi hivi sasa kwa sababu vyakula vinavyouzwa na kuliwa na watu wengi kila siku, hasa mijini, siyo vile vinavyotakiwa na miili yetu. Chukua tahadhari mapema kwa kuzingatia kanuni za ulaji sahihi.

CHUNGWA: UNAZIJUA FAIDI HIZI 13 ZA TUNDA HILI?

Ni msimu mwingine wa machungwa, yamejaa tele kila kona. Shilingi 100 tu unapata chungwa. Lakini siyo ajabu kama kuna watu msimu unaisha hawajala hata chungwa moja, wala suala la matunda halipo kabisa katika orodha ya milo yao!

Inawezekana pia hata kwa wale wanaokula, japo kidogo, hula kama kiburudisho tu bila kujua faida zake mwilini. Katika makala ya leo nitakujuza faida 13 unazoweza kuzipata unapokula chungwa, ambalo limesheheni virutubisho kibao.

Kumbuka kuwa hata chungwa moja tu ukila lina kidhi yale mahitaji muhimu ya mwili ya kila siku (daily requirement), iwe chungwa lenyewe au juisi yake halisi.

1. UKOSEFU WA CHOO
Kutokana kuwa na kiwango kikubwa cha kirutubisho aina ya kambalishe (fibre), chungwa husaidia usagaji wa chakula tumbuni na hutoa ahueni kwa mtu mwenye matatizo ya ukosefu wa choo. Aidha, kambalishe huondoa kolestro na huimarisha kiwango cha sukari mwilini, hivyo chungwa ni zuri kwa wagonjwa wa kisukari.

2.UGONJWA WA MOYO
Kiwango kikubwa cha Vitamin C na virutubisho vya ‘flavonoids’, ‘phytonutrients’ vilivyomo kwenye chungwa, huondoa kwa mlaji hatari ya kupatwa na magonjwa ya moyo (Cardiovascular disease)!

3. SHINIKIZO LA DAMU
Virutubisho vya Magnesi (Magnesium) na ‘hesperidin’ vilivyomo kwenye chungwa, husaidia kuondoa tatizo la shinikizo la damu la juu (high blood pressure), hivyo machungwa ni mazuri kwa wagonjwa wa presha.

4. UGONJWA WA MAPAFU
Chungwa pia lina kiasi kikubwa cha Vitamin B6 na Madini ya Chuma (iron), virubisho ambavyo ni muhimu kwa uzalishaji wa seli nyekundu za damu, ambazo hufanya kazi ya kusafirisha hewa ya oksjeni mwilini, hivyo kuwa muhimu kwa kujikinga na ugonjwa wa mapafu.

5. MIFUPA NA MENO
Chungwa lina kiasi kingi cha madini ya kalisi (calcium) ambayo ni muhimu kwa uimarishaji wa mifupa na meno.

6. AFYA YA NGOZI
‘Anti oxidants’ iliyomo kwenye chungwa, hutoa kinga kwenye ngozi ili isiharibike au kushambuliwa na magonjwa ya ngozi yanayoweza kujitokeza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa. Pia huifanya ngozi ‘isizeeke’.

7. KOLESTRO
Virutubisho vilivyomo kwenye chungwa, hasa kwenye maganda yake, hupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (bad cholesterol). Hivyo kwa wenye tatizo la lehemu wanashauriwa kula machungwa pamoja na nyama zake.

8. UKUAJI WA UBONGO
Chungwa moja lina kiasi cha asilimia 10 ya ‘folic acid’ inayohitajika mwilini kila siku. Madini haya ni muhimu kwa afya ya ngozi na ukuaji wa ubongo kwa ajili ya kuimarisha kumbukumbu na uwezo wa mtu wa kufikiri.

9. KINGA YA MWILI
Vitamin C iliyomo kwenye chungwa huimarisha uzalishaji wa seli nyeupe ambazo ni muhimu kwa uimarishaji wa kinga ya mwili. Unapokuwa na kinga imara, huwezi kusumbuliwa na magonjwa mara kwa mara, yakiwemo malaria.

10. UGONJWA WA FIGO
Ulaji wa machungwa mara kwa mara, ukusaidia kujiepusha na ugonjwa wa figo kwa kiasi kikubwa.

11. VIDONDA VYA TUMBO
Unapokuwa na kiwango cha kutosha cha Vitamin C mwilini, una uhakika na kinga dhidi ya ugonjwa wa vidonda vya tumbo, na kama tayari unavyo, ulaji wa machungwa utakupa ahueni.

12. UGONJWA WA MAFUA
Kutokana na wingi wa virutubisho vya kinga vilivyomo kwenye chungwa, ulaji wake mara kwa mara utakuepusha na magonjwa ya kuambukiza na vairasi (virus), kama vile mafua ambayo hivi sasa yanawasumbua watu wengi. Hivyo kula machungwa mengi kadii uwezavyo ili ujiepushe na mafua.

13. KINGA YA MAGONJWA MENGI
Chungwa, siyo tu linatoa kinga kwa magonjwa yaliyoainishwa hapo juu, bali pia hutoa kinga hata kwa magonjwa mengine kama vile baridi yabisi (arthritis, rheumatism), pumu, kikohozi, kifua kikuu, nimonia na kisukari. Nakushauri kula machungwa au juisi yake halisi kuanzia leo ili kupata faida hizo.

Nyanya: Dawa kiboko ya minyoo

Minyoo ni wadudu hatari ambao huingia tumboni mwa binadamu na kusababisha matatizo kadhaa ya kiafya. Ukubwa wa minyoo tumboni hutofautiana, kuna minyoo yenye urefu wa kuanzia inchi sita hadi inchi 26, ikitegemea imekaa kwa muda gani tumboni.

Kwa kawaida minyoo huingia tumboni kwa njia kuu mbili, ingawa zipo njia nyingine. Minyoo huingia tumboni kwa kula chakula kisicho salama au kwa njia ya ngozi, hasa kwa watu wanaopenda kutembea na kucheza bila viatu miguuni.

Watoto ndiyo wanao ambukizwa zaidi minyoo kwa njia ya ngozi kutokana na tabia yao ya kupenda kucheza bila viatu, tena wakiwa sehemu zisizo safi. Vile vile mtu anaweza kupata minyoo kwa kunywa maji yasiyo salama au kwa kuumwa na mbu, inzi na hata kwa njia ya kujamiana bila kinga.

Dalili za mtu mwenye minyoo ni pamoja na mtu kuwa na utapiamlo, kuonekana dhaifu na ngozi kupauka, kusumbuliwa na tumbo, kula sana na kusikia njaa muda mfupi baada ya kumaliza kula. Pia mtu mwenye minyoo huwa mwenye hasira kila mara.

TIBA YA NYANYA
Pamoja na tiba mbadala nyingine unazoweza kuzijua, nyanya imepewa nafasi ya kwanza katika kutibu tatizo hili kwa mafanikio makubwa na bila kuleta madhara kwa mtumiaji baada ya kumaliza tiba.

JINSI YA KUTUMIA NYANYA KAMA TIBA
Tayarisha nyanya mbili za ukubwa wa kawaida kwa kuziosha vizuri (inashauriwa uzioshe kwa maji ya moto ili kuua vijidudu, ikiwemo minyoo), zikatekate
Kisha changanya na chumvi pamoja na unga kiasi wa pilipili manga.

Kula mchanganyiko huo wa nyanya, chumvi kidogo na pilipili manga asubuhi kabla ya kunywa chai au kitu chochote. Fanya zoezi hilo mara moja kwa siku, kwa muda wa siku 15 au wiki mbili. Kwa kula nyanya hizo, minyoo wote waliyomo mwilini mwako wataondoka na kuacha tumbo lako safi.

Tiba hii inaweza pia kutumiwa na watoto, lakini kwa watoto wenye umri wa KUANZIA MIAKA MITATU TU na kuendelea, haishauriwi kutumiwa na watoto wadogo chini ya umri huo.

FAIDA NYINGINE ZA NYANYA
Wakati ukitumia nyanya hiyo kama tiba ya minyoo, utakuwa pia unanufaika na faida zingine za kiafya zitokanazo na nyanya, ambazo ni kutoa kinga dhidi ya magonjwa ya saratani.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zilizokwisha fanyika, pamoja na virutubisho vingine ilivyonavyo, nyanya ina kirutubisho muhimu na cha kipekee kinachojulikana kwa jina la Lycopene. Kirutubisho hiki kina uwezo mkubwa wa kutoa kinga dhidi ya saratani.

Aina mbalimbali za saratani zinazoweza kuzuilika kwa kula nyanya zimeorodheshwa kuwa ni saratani ya kibofu, saratani ya kizazi, saratani ya njia ya haja kubwa, saratani zote za tumbo, mdomo na saratani ya koo. Nyanya mbichi ndiyo yenye sifa ya kutoa matokeo mazuri.

Ili kujiepusha na kupatwa na minyoo, zingatia usafi, epuka ulaji wa vyakula vya kwenye makopo (refined food), kupenda kunywa juisi zilizowekewa rangi za ladha ya matunda, biskuti, pipi na vyakula vibichi, zikiwemo nyama zisizoiva vizuri.

Ili kujitengenezea kinga dhidi ya minyoo, pendelea kula vitunguu saumu na karoti mara kwa mara, kwani vyakula hivi vina virutubisho ambavyo ni adui mkubwa wa minyoo tumboni. Pia pendelea kunywa maji mengi sana kila siku, maji husaidia kusafisha tumbo, ikiwemo kuondoa minyoo.

Rais Kikwete awaapisha Makatikbu Tawala wa Mikoa ikulu jijini Dar Es Salaam

Katibu Tawala mpya wa mkoa wa Mbeya Bibi.Mariam Mtunguja akila kiapo mbele ya Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ikulu jijini Dar es salaam leo.Katika hafla hiyo Rais aliwaapisha pia makatibu Tawala wa mikoa mingine kama ifuatavyo,Dkt. Faisal Issa (Kilimanjaro),Bwana Eliya Ntandu (Morogoro), Bwana Severine Kahitwa (Geita),Bwana Emmanuel Kalobelo (Katavi), Bwana Hassan Bendeyeko (Ruvuma) na Dkt. Anselem Tarimo (Shinyanga).

Friday, March 23, 2012

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TOKA TFF

KUONA MORO UNITED, AFRICAN LYON 1,000/-
Viingilio kwenye mechi namba 149 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Moro United na African Lyon itakayochezwa kesho (Machi 24 mwaka huu) Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam ni sh. 1,000 kwa mzunguko na sh. 5,000 kwa jukwaa kuu.

Mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar es Salaam ndiye atakayechezesha mechi hiyo akisaidiwa na Ephraim Ndissa na Abdallah Selega wakati mwamuzi wa akiba ni Oden Mbaga. Wote pia wanatoka Dar es Salaam. Kamishna wa mechi hiyo ni James Mhagama kutoka mkoani Ruvuma.

Pia viingilio hivyo ndivyo vinavyotumika kwa mechi zote za Ligi Kuu ya Vodacom zinazochezwa Uwanja wa Chamazi zisizohusisha timu za Simba na Yanga.

VPL itaendelea tena Machi 28 mwaka huu kwa mechi kati ya Ruvu Shooting Stars itakayocheza na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi wakati Moro United itakuwa mwenyeji wa Villa Squad katika mechi namba 153 itakayofanyika Uwanja wa Chamazi.

MMOJA AONGEZWA TWIGA STARS
Kocha Charles Boniface Mkwasa wa Twiga Stars amemuongeza mshambuliaji Rehema Salum wa Shule ya Sekondari Lord Baden ya mkoani Pwani kwenye kikosi hicho kitakachoingia kambini Machi 25 mwaka huu.
Rehema aliibuka mfungaji bora kwenye mashindano maalumu ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyoshirikisha shule nane za sekondari za Mkoa wa Dar es Salaam na kuhitimishwa Machi 8 mwaka huu.

Twiga Stars itaingia kambini kwenye kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) iliyoko Ruvu mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya maandalizi kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Fainali za Wanawake Afrika (AWC) zitakazofanyika Novemba mwaka huu nchini Equatorial Guinea.

Timu hiyo itacheza na Ethiopia kusaka tiketi ya kwenda Equatorial Guinea ikianzia ugenini Addis Ababa kwa mechi itakayochezwa Mei 26 mwaka huu. Timu hizo zitarudiana wiki mbili baadaye jijini Dar es Salaam.

Katika raundi ya kwanza, Twiga Stars iliitoa Namibia kwa jumla ya mabao 7-2. Ilishinda ugenini 2-0 na kuibuka na ushindi mnono nyumbani wa mabao 5-2.

Machi 10 mwaka huu, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara alizindua akaunti ya Twiga Stars kupitia Tigo Pesa kuichangia timu hiyo ili ishiriki vyema michuano ya AWC.

Wachangiaji wa Twiga Stars wanatakiwa kutuma mchango wao kwenda namba 13389 ambapo kiwango cha juu kinachoweza kutumwa kwa muhamala (transaction) mmoja ni sh. 500,000. Katika uzinduzi huo, Waziri Dk. Mukangara alichangia sh. milioni moja.

MTIHANI WA MAWAKALA WA WACHEZAJI

Mtihani kwa kwa ajili ya watu wanaotaka kuwa mawakala wa wachezaji na mechi wanaotambuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) utafanyika Machi 31 mwaka huu saa 4 kamili asubuhi ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (FIFA).

Kwa wanaotaka uwakala huo wanatakiwa kujisajili ambapo watapewa kanuni mbalimbali za FIFA na TFF ili waweze kujiandaa kikamilifu kwa mtihani huo utakaokuwa na sehemu mbili. Sehemu ya kwanza ya mtihani huo ni maswali kutoka FIFA wakati nyingine ni kutoka TFF.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

NYUMBA ZA SHIRIKA LA RELI, BANDARI MSIMBAZI DAR ZABOMOLEWA

Tingatinga likibomoa nyumba hizo.

Vikosi vya zimamoto vikiwa tayari kutoa msaada wowote.

Mabaki ya nyumba iliyobomolewa.

Moja ya familia zilizoathirika na bomoabomoa hiyo.

Askari wakisimamia ubomoaji huo.

Eneo hilo lilikuwa limefungwa kwa wapita njia.

Moja ya nyumba ambazo zimebomolewa.

MAMLAKA ya jiji la Dar es Salaam leo alfajiri ilianza kubomoa nyumba zilizokuwa za Shirika la Reli nchini na Bandari katika Mtaa wa Msimbazi, Kariakoo, karibu na Shule ya Msingi ya Uhuru, ili kupisha ujenzi wa kituo cha mabasi yaendayo kasi. Kazi hiyo iliyofanywa chini ya ulinzi mkali wa vyombo vya usalama, iliwaacha watu wengi waliokuwa wakiishi katika nyumba hizo kwa miaka mingi wakiwa katika majonzi makubwa ya kukosa mahali pa kukaa na kile walichosema ni kupoteza mali zao.

Hadi mtandao huu unakwenda mitamboni, kazi hiyo ilikuwa bado inaendelea, ikiwa imevuta watu wengi waliokuwa wakipita eneo hilo ambalo lina maduka na vituo vingi vya mabasi.

PICHA NA IKULURAIS KIKWETE AZUNGUMZA NA NAIBU WAZIRI WA BIASHARA WA CHINA IKULU LEO

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Mh Li Jonzhao
baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kumtembelea Ikulu Dar es salaam leo March 23, 2012 kwa mazungumzo.

Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Mh Li Jonzhao na ujumbe wake walipomtembelea Ikulu Dar es salaam leo March 23, 2012 kwa mazungumzo. Mawaziri wa Fedha Mh Mustafa Mkullo, Uchukuzi Dr Omar Nundu na Nishati na Madini Mh William Ngeleja walihudhuria mazungumzo hayo.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete katika mazungumzo na Naibu Waziri wa Biashara wa Jamhuri ya Watu wa China Mh Li Jonzhao baada ya mgeni huyo na ujumbe wake kumtembelea Ikulu Dar es salaam leo March 23, 2012 kwa mazungumzo. Katikati yao ni mkalimani na wengine ni ujumbe wa Mh Jonzhao.

Tuesday, March 20, 2012

TANZANIA REPRESENTED AT THE COMMONWEALTH DAY IN LONDON

Tanzania flag being flown at the Abbey
Her Majesty Queen Elizabeth II
Mr and Mrs Peter kallaghe arriving for service
--
By Ayoub mzee

Commonwealth Day is an opportunity to promote understanding on global issues, international co-operation and the work of the Commonwealth’s organisations, which aim to improve the lives of its citizens.
It is celebrated on the second Monday in March every year.
The theme for Commonwealth Day 2012 is Connecting Cultures
The observance is the largest uk annual multi faith gathering which is always honoured by the presence of the head of the commonwealth HER MAJESTY QUEEN ELIZABETH II ,The Duke of Edinburgh ,Prince Charles and the duchess of Cornwall.Tanzania was represented by H.E Peter Kallaghe

Waziri wa Ofisi ya Rais Utawala Bora, Mathias Chikawe Azungumza na Waandishi Wa Habari

Waziri wa Ofisi ya Rais Utawala Bora Mathias Chikawe akitoa taarifa mbele ya waandishi wa habari Ofisini kwake Machi 19, 2012 kuhusu Haki za binadamu katika nchi yetu, baada ya kuhurudhuria mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Geneva –Uswiss hivi करिबुनी,

ADUI WA MWAKYEMBE ATAJWA

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harisson Mwakyembe.

Na Elvan Stambuli
ADUI namba moja wa Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harisson Mwakyembe ametajwa kuwa ni yule aliyevumisha na kusambaza ujumbe kwa watu mbalimbali kuwa kiongozi huyo amefariki dunia.
Chanzo chetu cha habari ambacho ni mmoja wa wanafamilia wa Dk. Mwakyembe kimeliambia gazeti hili kuwa adui huyo wa ndugu yao, familia inamjua lakini hivi sasa ni mapema mno kumtaja.
“Tunamjua tena ni mbunge kupitia Chama Cha Mapinduzi. Hatuwezi kumtaja kwa sasa lakini nakuhakikishia tunamjua,” kilisema chanzo hicho.
Hata hivyo, msemaji wa Dk. Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela, Victor Mwambalaswa alimwambia mwandishi wetu kuwa ni kweli kuna mtu alizusha na kusambaza habari za kifo cha mpendwa wao.
“Hawa wanaoeneza uvumi huo wanasikitisha, kuishi au kufa ni mipango ya Mungu. Sijui anayeeneza hayo ana makusudi gani?” alihoji Mwambalaswa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Lupa.
Alisema Dk. Mwakyembe ni mzima wa afya na angezungumza na waandishi wa habari jana (Jumatatu) baada ya kurejea kutoka India mwishoni mwa wiki iliyopita.
Dk. Mwakyembe amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya ngozi ambayo Oktoba 9, mwaka jana yalimlazimu kupelekwa katika Hospitali ya Apollo, India kwa matibabu zaidi.
Maradhi hayo yamezua utata mkubwa baada ya kudaiwa kuwa yametokana na kulishwa sumu huku kukiwa na kauli zinazotofautiana kutoka kwake na baadhi ya watendaji wengine wa serikali.
Kauli tete ziliibuka baada ya baadhi ya viongozi akiwamo Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kudai kuwa maradhi yanayomsumbua Dk. Mwakyembe yametokana na kulishwa sumu.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Robert Manumba alijibu madai hayo aliposema kuwa uchunguzi wa polisi umebaini kuwa Dk. Mwakyembe hajaugua kwa sababu ya kulishwa sumu bali ana maradhi ya ngozi na kutishia kuwachukulia hatua waliotoa kauli hizo.
Ripoti ya uchunguzi aliyoisoma Manumba katika mkutano wake na waandishi wa habari Februari 16, mwaka huu Dar es Salaam, inaonyesha kuwa Dk.Mwakyembe hakulishwa sumu huku akisema kwamba pia ulijumuisha taarifa kutoka hospitalini India ambako alikuwa anatibiwa.
Alisema uchunguzi huo unalipa jeshi la polisi picha kuwa waliotoa taarifa hizo hadharani wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria.
Baada ya kauli hiyo, Dk. Mwakyembe aliibuka na kutoa kauli nzito iliyoonekana kumjibu Kamishna Manumba akielezea kushangazwa kwake na majibu hayo na kudai kuwa hayakuwa sahihi.
Mbali ya Dk. Mwakyembe, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Mponda na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha, kwa nyakati tofauti walikana kuijua ripoti hiyo ya Kamishna Manumba na kila wanapobanwa anamtupia ‘mzigo’ kachero huyo mkuu wa upelelezi nchini.
Hata hivyo, katika kile kilichoonekana kudhamiria kuchukua hatua, inadaiwa kuwa Kamishna Manumba aliwasilisha jalada la mashtaka kwa watu anaodai wanaeneza habari ya kulishwa sumu Mwakyembe kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Eliezer Feleshi ambaye alithibitisha kulipokea lakini akasema ni vigumu kufahamu ni lini atalipeleka mahakamani jalada la kesi hiyo.

MKAPA, SLAA WACHAFUKA ARUMERU

Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa.

Na Mwandishi Wetu, Arumeru
WAKATI kampeni za Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki zikishika kasi, tathmini ya jumla inaonesha kwamba viongozi wakubwa wa kitaifa nchini, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, wamechafuka.
Viongozi hao wenye heshima kubwa kitaifa, wamechafuliwa kutokana na makombora yanayoendelea kurushwa wakati huu wa kampeni, hivyo kuwafanya wananchi watumie muda mwingi kuwajadili Mkapa na Slaa badala ya wagombea husika.
Mwandishi wetu, pamoja na kufuatilia sera za wagombea amekuwa akipita mitaani kupata maoni ya wananchi kuhusu uchaguzi huo na alichobaini kwa wiki nzima iliyopita ni mjadala mzito kuhusu madongo yaliyotupwa kwa Mkapa na Slaa.

MKAPA
Kauli yake kuwa Mbunge wa Musoma Mjini (Chadema), Vincent Nyerere si familia ya Baba wa Taifa, Hayati Julius Kambarage Nyerere, imemchafua hasa baada ya majibu ya mtoto mkubwa wa rais huyo wa kwanza wa Tanzania, Madaraka Nyerere.
Madaraka alitoa majibu kuwa Vincent ni ndugu yao, kauli ambayo imechukuliwa na wananchi wengi wa Arumeru Mashariki kwamba imemzodoa Mkapa, hivyo kupunguza heshima yake.
Kauli ya Vincent kuwa Mkapa alilazimisha Baba wa Taifa apelekwe Uingereza, kinyume cha ushauri wa daktari wake, Profesa David Mwakyusa, nayo imeibua mjadala mzito Arumeru Mashariki, huku wananchi wengi wakihoji kunani kifo cha Nyerere?
Vincent alidai kuwa kifo cha Nyerere ni tata akataka Mkapa aeleza siri aliyonayo.

SLAA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Steven Wassira ndiye anayetajwa kumchafua Slaa kutokana na dongo alilomrushia kuwa alifukuzwa ukasisi wa Kanisa Katoliki baada ya kufanya ufisadi kwenye fedha za mapokezi ya Papa John Paul II (hayati) alipokuja nchini Septemba Mosi 1990.
Wassira amedai kuwa mbali na Slaa kufanya ufisadi kwenye fedha za Kanisa Katoliki mpaka akafukuzwa pia ana kashfa ya kumfukuza mhasibu wa Chadema kwa sababu alikataa kumpa fedha, shilingi milioni 10, mchumba wake, Josephine Mushumbusi.
Japo inaelezwa kwamba Slaa anayo majibu kuhusu madongo hayo ya Wassira lakini mtaani kwa sasa amechafuka kutokana na jinsi wananchi wanavyomzungumzia.

KUHUSU UCHAGUZI
Uchaguzi Mdogo Arumeru Mashariki, unafanyika kujaza nafasi ya aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Jeremiah Sumari aliyefariki dunia Januari 19, 2012.
Katika uchaguzi huo, mchuano mkali upo kati ya mgombea wa tiketi ya CCM, Sioi Sumari dhidi ya Joshua Nassari wa Chadema.

WAJUA KAMA VYAKULA HATARI NDIYO VINAVYOLIWA KWA WINGI?

WENGI wetu tunafanya kosa kubwa kila siku kwa kula kwa wingi vyakula ambavyo tulipaswa kuvila kwa kiasi kidogo, hii ni kutokana na kutopata elimu ya kutosha kuhusu jambo hili au kwa wengine kupuuzia licha ya kuujua ukweli.
Aina hizo ni zile za Protini (Proteins), mafuta na wanga (Fats & Carbohydrates). Hili ni kundi la vyakula HATARI sana lakini ndilo linalopendwa na watu wengi, unapotumia vyakula vyake unapaswa kuvitumia kwa uchache na uangalifu mkubwa. Kundi hili ndilo linalowaletea matatizo ya kiafya watu wengi.
Vyakula vilivyo katika kundi la protien ni kama vile nyama, mayai, maziwa, n.k na vyakula vilivyo katika kundi la Fats ni vile vyenye mafuta na vinavyopikwa kwa mafuta mengi, kama vile chips, n. k. Vyakula vilivyo katika kundi la wanga (Carbohydrate) ni pamoja na sukari na vyakula vingine vitamu vitamu.

SUALA LA KUZINGATIA
Katika aina za vyakula zilizotajwa hapo juu, tahadhari kubwa inatakiwa ichukuliwe kwa sababu hutakiwi kuacha kabisa kuvila na pia hutakiwi kuvila sana. Binadamu anahitaji Protini mwilini ili kuuwezesha mwili kupata virutubisho muhimu vya kuuendesha mwili wake, halikadhalika mafuta na wanga.
Lakini ni vizuri ukaelewa kwamba kila aina ya chakula iliyotajwa katika kundi hilo la hatari, unaweza pia kuipata kutoka katika kundi lingine la vyakula salama na ukapata virutubisho vyote muhimu.
Katika kundi la nyama, pendelea kula samaki au kuku badala ya nyama ya ng’ombe au nyama yoyote nyekundu (red meat) na usipende kula ngozi, iwe ya samaki au ya kuku, kwani huwa zina mafuta mengi ambayo siyo mazuri kiafya.
Badala ya kula sukari, pendelea kula mboga na matunda ambayo yana sukari ya asili na isiyo na madhara. Au pendelea kutumia asali pahali panapohitaji sukari na ukilazimika kutumia sukari, pendelea sukari nyeusi (brown sugar) kuliko nyeupe na kwa kiasi kidogo sana.
Kundi la chakula cha mafuta, wanga na protini, hutakiwa kuliwa kwa uchache sana na kwa tahadhari kubwa, lakini kwa bahati mbaya sana kundi hili ndilo ambalo linaliwa sana kuliko makundi yenyewe (nafaka, matunda na mboga) na matokeo yake watu wengi wamepatwa na matatizo ya kiafya kama vile kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya moyo na matatizo ya unene wa kupindukia.
Baada ya kupatwa na matatizo hayo ya kiafya, wengi wao hivi sasa wameshakatazwa na daktari kuendelea kuvitumia vyakula hivyo na wanapokaidi maagizo wanayopewa, matatizo yao ya kiafya huwa mabaya zaidi na hatimaye kifo. Hivyo wewe kama hujafika huko, badili mfumo wako wa kula kuanzia sasa.
Katika hali halisi na kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), tunapaswa kula zaidi vyakula vitokanavyo na nafaka, matunda na mboga, kisha kula kiwango kidogo sana cha vyakula vitokanavyo na nyama, mafuta na sukari. Kama mgawanyo huo ukiwekwa katika asilimia 100, basi unaweza kuugawa kama ifuatavyo:
Nafaka: 40%
Matunda, Mboga: 35%
Nyama, mayai, maziwa: 15%
Mafuta, Sukari,n.k: 10%
Lakini hali halisi haiko hivyo, maisha wanayoishi watu wengi yamegeuzwa, wanakula sana vyakula vya mafuta, sukari, nyama, mayai. Matokeo yake hivi sasa wanakabiliwa na magonjwa yasiyotibika na kama hawajapatwa, wanajiweka katika hatari ya kupatwa wakati wowote.
Kama ulikuwa hulijui hilo, basi ni vyema ukaanza kubadilika na kuviangalia vyakula katika mtizamo tofauti, achana na vyakula vilivyo katika kundi la hatari na badala yake pendelea kula vyakula vya asili na vilivyosalama, kama kweli unajali afya yako.
Daima kumbukeni, jinsi ulivyo leo, kunatokana na ulivyokula jana na utakavyokuwa kesho, kutatokana na unavyokula leo!

New