My Web

Emmanuel

CONTACT

Thursday, December 17, 2015

Wananchi wa Kenya watamani kuwa na Rais kama Magufuli


Akamatwa Akitorosha Madini Ya Tanzaninte


Hela za Elimu Bure zapatikana Bilioni 131/- zatengwa elimu bure




RAIS John Magufuli amewahakikishia Watanzania kuwa fedha kwa ajili ya kutimiza ahadi ya kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari, zimetengwa Sh bilioni 131 mwezi huu na kupelekwa moja kwa moja katika shule husika.

Amesema Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa, watapatiwa nakala za taarifa za ugawaji wa fedha hizo na kuonya kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayethubutu kuzitumia vibaya.

Rais Magufuli alisema hayo Ikulu Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe aliyemtumia salamu za pongezi kwa kuchaguliwa kuiongoza Tanzania.

Dk Magufuli aliongeza kuwa fedha hizo ambazo ni pamoja na fedha za maendeleo, fedha za mitihani na fedha vifaa vya ku fundishia zitaanza kutumwa kila mwezi kuanzia mwezi huu.

Katika kipindi cha kampeni, Rais Magufuli aliahidi kutoa elimu bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari kidato cha nne na hivi karibuni kupitia Wizara ya Elimu ilitoa waraka maalumu wa kusisitiza agizo hilo la elimu bure.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amempongeza Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk Philip Mpango kwa kazi nzuri ya ukusanyaji wa mapato inayofanywa na mamlaka hiyo.

“Kwa mara ya kwanza mwezi huu ukusanyaji wa mapato hayo unatarajiwa kuwa zaidi ya shilingi trilioni moja na bilioni mia tatu,” alisema Rais Magufuli katika taarifa hiyo iliyotolewa jana na Ikulu.

Rais Magufuli pamoja na mambo mengine, jana alipokea ujumbe maalumu wa maandishi kutoka kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe uliowasilishwa na Waziri wa Nchi anayeshughu likia Mambo ya Nje ya Japan, Seiji Kihara.

Ujumbe huo umemueleza Rais Magufuli kuwa Japan imeridhishwa na hatua ambazo Serikali ya Tanzania inazichukua katika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuahidi kuongeza msukumo kwa upande wa Japan katika kuharakisha utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Japan nchini.

Mjumbe huyo juzi alishuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ujenzi wa njia ya umeme yenye urefu wa kilometa 441.5 kutoka Singida - Manyara - Namanga na kuunganisha hadi Kenya, ambapo Japan imetoa mkopo wa Dola za Marekani milioni 96 ili kufanikisha mradi huo.

WALIOJENGA PEMBEZONI YA BONDE LA MTO MSIMBAZI WAPITIWA NA BOMOA BOMOA

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Manispaa za jiji la Dar es salaam zitafanya zoezi la kuondoa wavamizi maeneo yote ya Mabondeni, kingo za mito  na za Bahari, maeneo ya wazi, maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi zaidi ya 150 katika  jiji la Dar es salaam. Bomoa bomoa ya leo inaendelea katika Bonde la mto msimbazi.Mkuu wa Kitengo cha Sheria Balaza la Taifa la usimamizi wa mazingira Tanzania (NEMC), Manchale Heche akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Bomoabomoa maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi nakuwataka wananchi waliojenga katika fukwe za bahari Kingo za mito na mikondo ya bahari kuhamisha mali zao mapema.
Wananchi wakitoa samani pamoja na vitu mbalimbali ndani ya nyumba zao ili kupisha ubomoaji wa nyumba zilizo maeneo hatarishi. 

WAZIRI KITWANGA AWAPA POLISI SIKU MOJA YA KUJIELEZA NI KWA NINI HAWALINDI BANDARI YA DAR ES SALAAM


Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga ametoa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza ni kwa nini askari hawalindi Bandari ya Dar es Salaam badala yake kazi hiyo inafanywa na kampuni binafsi za ulinzi.
Kitwanga amepanga kukutana na viongozi waandamizi wa Polisi kesho ili kujadili mipango na mikakati mbalimbali ya kuongeza ufanisi wa kazi ya kuwahudumia wananchi.
Akizungumza na maofisa waandamizi wa polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam baada ya kufanya ziara katika Chuo cha Taaluma ya Polisi na kuangalia makazi ya askari, Kurasini, Kitwanga alieleza kusikitishwa na hatua ya polisi kuacha kutoa ulinzi bandarini na kuita kitendo hicho kuwa ni udhaifu wa jeshi hilo.
Alisema kitendo hicho kimetoa mwanya kwa baadhi ya wafanyabiashara kukwepa kodi wakati wa kushusha bidhaa zao akisema Bandari ni eneo la mpaka ambalo linahitaji ulinzi wa polisi kama mipaka mingine ya nchi.
Akionekana kukerwa, Waziri Kitwanga alimkatisha Kamishna wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipojaribu kutoa sababu akimtaka kutumia siku nzima ya leo kuandaa majibu ili kesho wayazungumze kwenye kikao rasmi.
Waziri Kitwanga amelitaka pia jeshi la polisi kumweleza mipango ya kukabiliana na dawa za kulevya kwa sababu ndiyo zimekuwa chanzo cha matukio mengi ya uhalifu ikiwamo tishio la ugaidi.
Alisema haiwezekani kitengo cha kupambana na dawa za kulevya kikaachiwa jukumu hilo wakati jeshi la polisi liko kwenye operesheni zake kila siku.
Kuhusu msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam, waziri huyo alisema ni uzembe wa askari wa usalama barabarani kwa sababu wameshindwa kusimamia sheria na kuwachukulia hatua madereva wazembe.
Alisema zipo nchi za Afrika ambazo hazina askari wa barabarani kwa sababu kiwango cha nidhamu ya madereva wake ni kikubwa na wamekuwa wakifanya vizuri kuhakikisha kwamba suala la msongamano usio wa lazima unadhibitiwa kwa kufuata sheria.
Baadhi ya askari walimweleza Kitwanga kero zao. Mmoja wao, Alphonce Malowa alisema nyumba za askari ni chache na nyingi zimechakaa kiasi cha kuwafanya kudharaulika mbele ya wananchi.
Inspekta Novatus Makondowa alieleza juu ya umuhimu wa Serikali kuwasomesha walimu wa chuo cha taaluma za polisi ili kuwajengea uwezo zaidi wa kufundisha maofisa wengine chuoni hapo. 

Tuesday, October 20, 2015

Mkeo anahitaji talaka

Wewe bwana MASOUD mkeo kashakutangazia kukuacha na ameshaanza kuidai talaka.Ila mkeo alivyo muungwana akaamua kukupa na sababu za kukuacha ni wewe kutomjali mahitaji muhimu hapati na hata maendeleo ya familia hakuna miaka nenda miaka rudi toka mmefunga ndoa miaka kibao.
Mbaya zaidi si kwamba huna hela..lahasha! Pesa unazo ila mbinafsi saaaana hela zako wewe ni wewe na nduguzo na washkaji zako tu,hujui mkeo kavaa nini wala kala nini..Sasa bi Rehema kachoka anaidai talaka kwa nguvu zote kama kukuvumilia ashakuvumilia sana.
Rafiki yako mpenzi bwana Bashari Mussa Bashar ameona huruma unavyomfuja mkeo ameamua kukupindua sasa...
Bwana Masoud badala ya kuhakikisha unafanya yaleeee aliyokueleza mkeo kwamba ndio chanzo cha kuidai talaka eti na wewe unatoa ahadi kama bwana Bashari wakati mke bado unaye ndani na wewe ndio mume halali..
Kwanini usitende hayo anayoyataka badala ya kumpa ahadi "ooh usiniache ntaanza kukupa unyumba,usiniache ntaanza kukupeleka saluni,ooh usiponiacha ntaacha kujipendelea na ndugu zangu"
Kwa taarifa yako mkeo analalamika kwa watu kwamba anajuta kuolewa na wewe hakujua kama huna akili unazidiwa akili na rafiki yako Bashari ambaye anatoa ahadi za matumaini tofauti na wewe upo nae ndani badala ya kutenda unaahidi na wewe kama mwizi.
KWANINI UNAAHIDI KULALA NA MKEO ASIPOKUACHA KWANINI USILALE NAE WAKATI YUPO NDANI MWAKO?
NASIKIA ULIVYO MJINGA UMEANZA KUIGA MAVAZI YA BWANA BASHARI NA JINSI ANAVYOONGEA ILI MKEO ASIKUACHE..
HAHAHAHA KTK WANAUME MABWEGE DUNIANI BASI NI WEWE BWAN MASOUD YAANI UNAHANGAIKA KUHONGA WATU HELA WAMPAKE MATOPE BASHAR?BADALA HIYO HELA UNGEMPA MKEO AFUNGULIE SALUNI ANGALAU UMPUNGUZE MUNKARI WA KUKUMWAGA..
SASA MAVAZI NA SWAGA ZA KUONGEA ZA MBAYA WAKO ZITASAIDIA NINI WAKATI KIKUBWA ANACHOTAKA NI MAENDELEO KWA UJUMLA?

BWANA MASOUD UNAHITAJI BAGPARTY KUTOKA KWA MANYAKANGA WA USHELISHELI TENA WAKIONGOZWA NA MANYAKANGA WA KIMATAIFA MASHOGA WA MKEO WENYE UCHUNGU BI De Ambroze Nowme,Leah-Buzuka Derefa NA New Tina...NDOA IMEKUSHINDAAAA SUBIRI MKEO AENDE KWA BASHARI KIULAIIIINI.
ILA NASIKITIKA UMEIVUNJA NDOA ILIYOKUWA MFANO WA KUIGWA BARANI AFRICA..TENA UMEIVUNJA KWA MIKONO YAKO MWENYEWEE KWA KUPENDA NDUGUZO NA WASHKAJI KULIKO MKEO.


Kutoka Tanga.


Mkutano wa mgombea urais kupitia UKAWA Mh. Lowassa umevunjika baada ya watu kuzidi kufurika kwa wingi ktk uwanja wa Tangamano nakusababisha msukumano na mkanyagano usiokuwa wakawaida hali iliyotishia usalama wawatu waliofika kamsikiliza Mwanabadilikowao. 

Mh. Sumaye aliwatangazia watu kuwa kutokana na hali ilivyo uwanjani hapo wanalazimika kuufunga mkutano huo. Ndipo umati mzima ulipopaaza sauti ya kumshangilia kukubaliana nae. Hata hivyo mh. Lowassa aliusalimia umati huo kuupungia mkono.


















Mama katika ubora wake






































Monday, September 21, 2015

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya CHADEMA na UKAWA, Bw. Edward Lowassa

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya CHADEMA na UKAWA, Bw. Edward Lowassa ameendelea na kampeni zake za kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kuwa Rais  wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Bw. Lowassa jana aliendelea na kampeni zake katika majimbo matatu ya Mkoa wa Dar es Salaam ambayo ni Ukonga, Kigamboni na Mbagala 
  
Jimbo la Ukonga
Akiwa katika Uwanja wa Shule ya Msingi Tungine, Jimbo la Ukonga,Bw. Lowassa alisema katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, CCM wataisoma namba kwani Watanzania wanahitaji mabadiliko.
  
Alisema anataka kutimiza ndoto yake ya kuondoa umaskini wa Watanzania kwani ana utashi na ataweza kuuondoa kwa nguvu zote ili kuijenga Tanzania mpya wanayoitaka wananchi.
  
"Nimeamua kugombea urais ili niweze kuwatumikia Watanzania; hivyo  naomba mniamini niijenge Tanzania mpya ili kila mtu awezekuishi kwa amani na kujituma kwenye kazi," alisema.
  
Aliongeza kuwa, akiwa rais atafanya maamuzi magumu ili kuwaonesha Watanzania maana ya mabadiliko na maendeleo yanayohitajika ambapo anayekula mlo mmoja atakula mitatu, mwenye kanga tano awe na kumi lengo ni kuijenga Tanzania yenye maendeleo.
  
Bw. Lowassa aliahidi kuondoa ushuru kwenye zana za kilimo ili kila mkulima aweze kunufaika na kuuza mazao yake mahali popote iwe ndani au nje ya nchi ili aweze kujipatia kipato cha uhakika.
  
"Serikali yangu itatoa elimu bure kuanzia chekechea hadi Chuo Kikuu,nawashangaa viongozi wa CCM wanaposema hawawezi kutoa elimu burewakati wao wanatembelea mashangingi ya gharama kubwa.
  
"Nilikwenda Pugu kwa daladala ili kutembelea wananchi; wakaanza kuongea kwani hizi daladala za kazi gani, mbona wao wanapandisha twiga kwenye ndege na hawasemi?" alihoji Bw. Lowassa. 
  
Alisema atahakikisha matatizo ya wananchi kama alivyoyataja mgombea ubunge wa jimbo hilo, Mwita Waitara, ambapo atayatatua ambayo ni pamoja na tatizo la ukosefu wa umeme, umaskini, huduma mbovu za afya, ukosefu wa maji pamoja na hali ngumu ya maisha. 
  
Jimbo la Kigamboni
Bw. Lowassa akiwa kwenye Jimbo la Kigamboni, alisema akiwa rais wananchi watatumia Kivuko cha Kigamboni bure na kujenga upya mji huo ili uwe mfano wa kuigwa.
  
Jimbo la Mbagala
Akiwa Jimbo la Mbagala katika Uwanja wa Zakheem, alisema ataunda Serikali maalumu ambayo itashughulikia matatizo ya wakazi wa jiji hilo na kuleta maendeleo ya haraka ambayo hayajawahi kutokea.
  
Juma Duni Haji
Naye mgombea mwenza, Bw. Juma Duni Haji, alisema mwaka huu,CCM lazima waachie Serikali watake wasitake kwani miaka 50 waliyokaa madarakani imekuwa ya dhuluma na kuwanyanyasa wananchi. 
  
Alisema baada ya kuona wanashindwa, wameanza kuleta vurugu kwakuwaambia Watanzania kutakuwepo na vurugu baada ya uchaguzi. 
  
James Mbatia
Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Bw. James Mbatia, alisema pamoja na CCM kumpaka matope Bw. Lowassa, wataendelea kusonga mbele hadi waingie Ikulu, hivyo Rais Jakaya Kikwete na Serikali yake,waanze maandalizi ya kukabidhi Ikulu.
  
Mbowe amvaa Bulembo, Lubuva 
Akihutubia mkutano huo, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kauli iliyotolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa, Abdallah Bulembo kuwa UKAWA wataachiwa vitu vyote isipokuwa Ikulu ni ya kichochezi.
  
Alisema Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva, anatetea kauli hiyo akisema ni maneno ya kisiasa na kumtaka atoe tamko juu ya hilo kwani nchi inaweza kuwaka moto. 
  
"Mtu ambaye atashinda lazima apewe haki yake, Jaji Lubuva asifanye utani na kauli za akina Bulembo, nchi inaweza kuwaka moto, wananchi wapo tayari kwa mabadiliko hivyo wapewe haki yao,"alisema.
  
Aliongeza kuwa, NEC ilipaswa kukemea kauli za aina hiyo pamoja na kutoa tamko rasmi akitumia fursa hiyo kuwataka viongozi wa UKAWA, kukubaliana na maamuzi ya viongozi wakuu wa umoja huo juu ya kusimamisha mgombea mmoja katika kila jimbo na kata.
  
"Tuko katikati ya mabadiliko hatutaki mchezo, kiongozi wa NLD, CUF, CHADEMA au NCCR-Mageuzi katika ngazi za kata na wilaya ambaye atadharau maamuzi yetu tutamfukuza," alisema. 
  
Frederick Sumaye 
Kwa upande wake, Waziri Mkuu mstaafu, Bw. Frederick Sumaye, alisema hali anayoiona, hakuna sababu ya CCM kubaki madarakani ambapo wanachofanya sasa ni kuwabembeleza na kuwarubuni Watanzania ili wawape kura.
  
"CCM lazima iondoke madarakani, kote tulikozunguka watu wanataka mabadiliko wakisema Oktoba 25, mwaka huu, wachukue chao kila eneo wakidai CCM ina kiburi," alisema.
  
Alisema CCM imefilisika na kuishiwa sera ndiyo maana mgombea urais wao, Dkt. Magufuli anajinadi yeye badala ya chama akitumia nembo za CHADEMA; hivyo alimtaka aache kuwadanganya Watanzania.
  
Dkt. Makongoro Mahanga
Aliyekuwa Naibu Waziri wa Kazi na Ajira ambaye alitoka CCM na kuhamia upinzani, Dkt. Makongoro Mahanga, alisema Bw. Lowassa ndiye mwarobaini wa tatizo la ajira.
  
Alisema inashangaza kuona Dkt. Magufuli kudai ataanzisha mahakama ya mafisadi wakati idadi kubwa ya wagombea ubunge wa CCM wamepata nafasi hizo baada ya kutoa rushwa.

Tuesday, September 1, 2015

Wahamiaji 2 wajificha ndani ya injini

Image captionMtu aliyejificha ndani ya injini ya Gari
Mhamiaji mmoja kutoka Afrika Magharibi, alifanikiwa kuingia eneo la Ceuta nchini Uhispania kutoka Morocco, huku akiwa amejikunja ndani ya injini ya gari na mwingine akiwa amejificha nyuma ya kiti cha gari moja aina ya Mercedes-300.
Maafisa wa polisi wa Uhispania waliwapata wawili hao siku ya Jumapili wakati wa msako wao wa kawaida katika kituo cha El Tarajal, karibu na mpaka wa Morocco.
Watu hao wawili kutoka Guinea, kwanza walipewa huduma ya kwanza, kwa sababu walikuwa wamekosa hewa safi ya kupumua.
Image copyrightGetty
Image captionMtu aliyejificha ndani ya injini ya Gari
Raia wengi wa mataifa ya Afrika kujaribu kuingia Cueta kama njia moja ya kufika Ulaya.
Gari hilo linasemekana kuwa na nambari bandia ya usajili.
Polisi nchini Uhispania wanawazuilia watu wawili raia wa Morocco waliokuwa ndani ya gari hilo, wakati iliposimamishwa.
Haijabainika mtu aliyekuwa katika injini alikuwa katika hali hiyo kwa muda gani kwa sababu alikuwa akivuta hewa ya sumu.
Image captionMtu aliyejificha ndani ya injini ya Gari
Hata hivyo wahamiaji hao wawili hawakuwa na stakabadhi zozote za kuwatambulisha na kwa sasa wanachunguzwa na polisi.
Ceuta na Melilla ni himaya ndogo mbili za Uhispania karibu na pwani ya Kaskazini mwa Afrika na Uhispania imeweka ukuta mkubwa ili kuzuia wahamiaji kuingia nchini humo kinyume cha sheria.
Image copyrightBBC World Service
Image captionUkuta uliojengwa na Uhispania
Ukuta huo umewalazimisha wahamiaji wengi kutumia mbinu zingine kuingia Uhispania kama vile kuogelea hadi bandari nyakati za usiku na hata kujificha ndani ya mikoba.
Mwezi uliopita mto mmoja kutoka Morocco alifariki baada ya kukosa hewa safi ya kupumua pale nduguye alipojaribu kumsafirisha kwa mkoba wake.

Papa Francis alegeza msimamo wa Katoliki

Image copyrightAFP
Image captionPapa Francis
Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis, ameitikia shinikizo kutoka kwa wanawake wengi waumini wa kanisa hilo na kulegeza msimamo wa kanisa hilo kuhusu uavyaji mimba mwaka ujao wa jubilee.
Huwa ni marufuku kwa waumini wa kanisa Katoliki kuavya mimba, kitendo ambacho huchukuliwa kuwa kosa kubwa katika kanisa hilo.
Papa Francis amesema atawaruhusu mapadri kuwasamehe wanawake wanaoavya mimba na pia madaktari wanaowasaidia kutoa mimba.
Kinyume na watangulizi wake, Papa Francis, huchukulia fadhila na huruma kuwa nguzo kuu zinazozidi nyingine zote.
Image copyrightGetty
Image captionWaandamanaji nchini Marekani wakitaka serikali kuhalalisha uaviaji mimba
Papa huyo mzaliwa wa Argentina, alisema anafahamu shinikizo ambazo baadhi ya wanawake hukumbana nazo ndipo waavye mimba lakini akasema pia amekutana na wanawake wengi wanaobeba moyoni kovu la alichosema ni uamuzi wa kusikitisha na mchungu.
Ametangaza mwaka wa jubilee, ambao kawaida huhusishwa na msamaha, uadhimishwe na wakatoliki kote duniani kuanzia mwezi Desemba.
Maneno hasa aliyotumia Papa Francis yanaashiria kuwa anafahamu kuna wengi wa wanaojidai kutetea utamaduni wa kanisa hilo ambao hawatafurahishwa na uamuzi wake.
"Nimeamua," Papa Francis alisema. "Bila kujali pingamizi, kuwaruhusu mapadri kutoa msamaha wa dhambi wa kuavya mimba kwa wale wanafanya hivyo na wanaotafuta msamaha wakati wa mwaka wa jubilee."
Image copyrightGetty
Image captionRaia wa Ireland wakipinga uaviaji wa mimba

Wanariadha wa Kenya warejea nyumbani

Image captionJulius Yego akikaribishwa kwa kupewa maziwa katika uwanja wa JKIA
Mbwembwe zinaendelea katika jumba la mikutano ya Kimataifa la KICC, ambako wanariadha wa Kenya wamepokewa na kuandaliwa dhifa ya chakula cha mchana na shirikisho la mchezo wa riadha nchini Kenya AK.
Kikosi hicho kilichowasili leo asubuhi kutoka Beijing ambako kiliibuka mshindi wa mashindano ya riadha ya dunia, kililakiwa na maelfu ya wakenya na wakuu wengine wa serikali wakiongozwa na makamu wa rais William Ruto.
Akihutubia dhifa iliyoandaliwa na serikali, Ruto aliwapongeza mashujaa hao walioiweka Kenya katika nafasi ya duniani katika mashindani hayo ya riadha yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Beijing China.
Image captionMakamu wa rais akielekea kuwakaribisha wanariadha wa Kenya katika uwanja wa JKIA
Kenya imepata dhahabu saba, miongoni mwao urushaji mkuki na mita mia nne kuruka vizuizi, mashindano ambayo ni mara ya kwanza kwa Kenya kushinda medali katika mashindano ya Kimataifa.
Image captionWacheza danse waliowatumbukiza wanariadha wa Kenya
Dhahabu zingine zilinyakuliwa katika mbio za mita elfu kumi na kina dada, kwa upande wa wanaume ni mbio za mita mia nane , mita elfu tatu kuruka maji na viunzi na mita elfu moja mia tano.
Kenya pia ilinyakuwa medali sita ya fedha na tatu za shaba na kuweka rekodi hiyo ya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuwahi kuwa mshindi wa mashindano hayo ya riadha ya dunia.
Image captionMakamu wa rais William Ruto akiwa na mshindi wa mbio za mita 400 kuruka viunzi

New