My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, February 16, 2016

BUSARA KWA WANAWAKE. YAFUATE HAYA MAHUSIANO YAKO YADUMU


1. Degree yako ya fist class uliyoipata chuo kikuu haiwezi kukufanya uwe mke first class katika ndoa yako bali ni heshima yako na uthubutu wako.

2. Mwanamke anaemuheshimu mumewe ni mwanamke bora ambae kila mwanaume angetamani kuwa nae.

3. Tabia yako na misimamo yako ndio itakayomfanya mumeo ajute au afurahie kukuoa wewe.

4. Kuwa mke bora inakubidi uwe vizuri katika maarifa ya kutawala hasira zako na sio kuwa mtu wa kulipiza visasi.

5. Kuwa kiongozi huko kazini kwako lakini kuwa mtu wa kunyenyekea nyumbani kwako kwa mumeo. Hiyo ni busara.

6. Usiweke mashindano na mumeo, mpe hongea na mtie moyo kwa kila hatua anayopiga katika maisha.

7. Kuwa na ubinadamu, sio kosa dogo tu mumeo amefanya ukatamani kulipiza kisasi. It won't help u!

8. Kuwa mkarimu, kila mwanaume anamuheshimu mwanamke mkarimu na mwenye msimamo.

9. Usijaribu kumpa adhabu mumeo ya kumnyima chakula cha usiku kitandani, hii itamlazimu kutafuta chakula nje ya ndoa.

10. Hakuna kitu kibaya kama utakubali kuwa ulikosea kama kweli ulikosea. Kuwa mrahisi kukubali kama kweli ulikosea. Na omba radhi pale inapobidi.

11. Jiandae kumsamehe  mumeo pale anapokosea kwa maana mke atoae msamaha kwa mumewe ni mke mwema tofauti na yule aliejaa visasi.
 
12. Tengeneza maamuzi ya kuwa mke mwema, pasina kuwa na hofu yoyote na Mungu atakubariki.

13. La mwisho na la muhimu tambua kwamba mwanamke aliejaliwa umbo zuri na sura nzuri pasina maarifa kichwani anafaa kwa usiku mmoja, lakin yule mwenye maarifa na ufahamu yeya afaa kwa maisha yote!

MUNGU AWABARIKI WANAWAKE!

DONDOO KUMI KWA WANAUME ILI KUTENGENEZA MAHUSIANO YENYE AFYA.

 1. Usijisahau katika mahusiano ukawa comfortable kiasi kwamba zile mbwembwe zote za kipindi unamtongoza ukazipotezea. Mwanaume smart haachi kumfanya mwanamke wake ampende zaidi. Mwanaume anaemfanya mwanamke wake ampende zaidi mahusiano yao hudumu mpaka uchweo.

 2. Usisahau kufanya tabasamu kuwa kipaumbele cha mwanamke wako. Ole wao wanaume wanaowanyima tabasamu wapenzi wao wakaacha wanaume wengine ndio wawape tabasamu wanawake zao. Nawaambien mpo kwenye matatizo makubwa.

 3. Yatunze maneno yako kwa uaminifu mkubwa. Uaminifu ni msingi imara wa mahusiano yenye afya. Mwanaume wa kweli hakimbii majukumu.

 4. Usiwe mkoloni katika mahusiano. Kuna haki ya kusikiliza na kusikilizwa (natural justice). Kuwa mwanaume, admit kama umekosea. Kuwa na ujasiri wa kurekebisha pale ulipokosea

 5. Usimfanye mwanamke wako aone kama anashindana na muda wako, mfanye ajisikie na yeye anathamani katika muda wako. Sio sababu ya kuwa na muda au laa bali ni jitihada ya wewe kutengeneza muda wa pamoja.

 6. Usiwe mvivu. Kuna mtu mwingine pembeni ambaye anatamani kuwa na huyo mwanamke. Linda tunu yako kwa upendo, furaha na amani nae. Usiwe mvivu kumfurahisha, kumlinda, kumridhisha na kumsifia. Pombe na nyama choma zisije zikakuponza.

 7. Usihukumu. Kila mmoja anafanya makosa na anajifunza kwayo. Usihukumu makosa yake wala past yake. Na kitu cha muhimu usimhukumu kwa vile unafikiri tofauti na yeye. Binadamu tunatofautiana sana. Enjoy kuwa nae kwa jinsi alivyo. Usilazimishe awe kama wewe.

 8. Usi assume kwamba anajua kama unamjali, mwonyeshe kweli unajali. Mpe support katika shughuli zake i.e masomo, biashara, kilimo, etc. Mtumie sms, msikilize, msifie, muonyeshe mapenzi kwa maneno na vitendo na uwe mbunifu.

 9. Usiwe mwanaume jina, acha tabia ya kuzila na kususa ,onyesha kuwa wewe ni mtu wa majukumu na ni kichwa katika mahusiano, jenga mahusiano kwa busara zaidi na sio kwa ki imla (dictatorship). Maumuzi yako ya kijinga kijinga yatakutokea puani.

 10. Usikate tamaa kirahisi, najua maisha ni magumu ila mwanaume wa kweli anapotaka kitu, atafanya kila awezalo kukipata, unasubiri nini? fanya hivyo sasa.

Nawatakia week njema. 

Wewe ni nani? Karoti, yai au Mbegu ya kahawa



Binti alienda kwa bibi yake na kumuelezea jinsi anavyoishi na ugumu wa maisha katika ndoa yake. Mume wake amekua hamuheshimu ni ugomvi na malumbano kila siku iitwayo leo. Hakujua afanye nini na aliazimia kukata tamaa. Alichoka na ugomvi na manyanyaso. Ilionekana kila akitatua jambo hili linaibuka jambo jingine fasta.

Bibi yake alimchukua binti na kumpeleka jikoni. Bibi akajaza maji sufuria tatu na zote akaziweka katika moto. Punde maji ya kila sufuria yakachemka. Katika sufuria ya kwanza bibi akaweka karoti, sufuria ya pili akaweka yai, na la  tatu akaweka mbegu ya kahawa. Akaacha vichemke bila kusema neno.

Baada ya kama dakika ishirini akazima moto na kuepua sufuria zote tatu. Akatoa karoti na kuiweka katika bakuli, akatoa yai na kuweka kwenye bakuli pia na akamimina kahawa katika kikombe.

Baada ya hapo akamgeukia mjukuu wake na kumwambia "niambie sasa unaona nini?"

Binti akajibu "karoti, yai na kahawa"

Bibi akamsogezea vile vitu kwa karibu zaidi na akamwambia aiguse karoti na kuibinya. Akafanya hivyo na kugundua kuwa ilikuwa imelainika sana. Bibi akamwambia mjukuu wake alichukue lile yai na kujaribu kulivunja. Akagundua kuwa lilikuwa gumu mno.

Mwishoe bibi akamwambia ajaribu kuonja kahawa. Binti akatabasamu baada ya kujaribu ladha nzuri ya kahawa. Baada ya hivyo binti akamuuliza bibi "vitu hivi vinamaaninsha nini?"

Bibi akamfafanulia kwa kumuambia kwamba kila kitu yani kahawa, yai na karoti vimekabiliwa na tabu moja ya kuunguzwa na maji. Na kila kimoja kime react tofauti. Karoti kabla ya kuwekwa ktk maji ilikuwa ngumu kweli lakini baada ya kuunguzwa ikawa laini laini na kusinyaa.

Yai kabla ya kukutana na dhahama ya maji ya moto lilikuwa fragile kiasi kwamba ni rahisi kupasuka na ganda la nje lilikuwa likilinda kimiminika cha ndani ya yai. Lakini baada ya kuunguzwa na maji ya moto kimiminika cha ndani kikawa kigumu na si kimiminika tena.

Mbegu ya kahawa ilikuwa ya kipekee, lakini baada ya kuunguzwa na maji ya moto imeyabadilisha rangi maji yote.

Wewe upo wapi kati ya hivyo vitu vitatu? Bibi akamuuliza mjukuu wake. "pale unapokabiliana na matatizo ambayo kwa muktadha huu nimeyafananisha na maji ya moto huwa unareact vipi? Je wewe ni karoti, yai au mbegu ya kahawa?

Fikiria hivi: mimi ni nani? Je mimi ni karoti ambayo huwa ngumu, lakini pale ambapo ninakabiliana na maumivu na mateso makali nakuwa laini na kupoteza nguvu zangu?

Je mimi ni yai ambae nina moyo wa kimiminika lakini nabadilishwa na joto kali la maji. Nina moyo wa kimiminika ambapo baada ya kifo, kuachana, matatizo ya kiuchumi au majaribu mengine nakuwa mgumu na imara? Je ganda la nje linaonekana vile vile lakini ndani ni moyo jasiri, enye nguvu usioteteleka?

Au mimi ni kama mbegu ya kahawa? Ambayo kimsingi inayabadilisha maji ya moto rangi, je mimi ni jasiri kiasi kwamba ingawa nakabiliana na matatizo mengi lakini nakuwa jasiri kukabiliana nayo na kuyabadili? 

Mjukuu wangu ni vema ukawa kama kahawa au yai. Kamwe usiwe kama karoti, ukiwa hivyo utawanufaisha wale wakuumizao! Maana kwao watafurahi kukuona ukizidi kuwa mnyonge na mwenye kunyong'onyea pale wakuumizapo. Lakini kama utakuwa mgumu kama yai utawaacha wakijiuliza maswali mengi pasina majibu.

Hakuna tunu kubwa duniani kama furaha mjukuu wangu, wewe hata wakuumize kiasi gani! Usioneshe huzuni mbele yao! Wewe tabasamu tu. Kufanya hivyo utawaacha wakiwa na maswali yasiyo na majibu!

Unakabiliana vipi na majaribu yako? Je wewe ni karoti, yai au kahawa!! 

Jibu unalo wewe mwenyewe.

Monday, February 15, 2016

KOSA MOJA TENA DOGO LINAWEZA LIKAKUFANYA UWE MTUMWA WA KUDUMU.


Vijana wawili waliokuwa na hali ngumu ya maisha waliamua kwenda kuomba kazi kwa tajili mmoja aliyekuwa amejenga pembeni kidogo mwa mjii wenye watu masikini. Vijana hao mara baada ya kufika na kuonana na huyo tajili walijieleza namna maisha yao yalivyo magumu huku wakimuomba tajili huyo awape kazi yoyote, kwa kipato chochote, nao watafanya kwa moyo wote.

Yule tajili baada ya kuwasikiliza kwa umakini alijisikia kuwapa wale vijana kazi na akawaomba wafanye kazi kwa moyowote kama walivyojieleza huku akiwasisitiza wawe makini pindi wanapofanya kazi kwani alikuwa hapendi kuona kitu chochote kikihalibiwa kwa uzembe. Basi akatoa kazi mbili na kumsihii kila mmoja achague kazi anayoipenda.Kazi ya kwanza ilikuwa ni kazi ya jikoni yanii Kupika, pamoja na kufanya usafi wa ndani kama vile kudeki, kusafisha vyombo pamoja na kufua nguo na kazi ya pili ilikuwa inahusu shughuri zote za nje yani kufyeka majani, kupalilia bustani pamoja na kulisha mifugo.

Vijana walichagua kazi na kila mmoja aliipenda kazi yake, Hao vijana walijitaidi kufanya kazi vizuri ili wapendwe zaidi na boss wao. baada ya kumaliza kufanya kazi ya siku vijana walikuwa huru kucheza au kukaa tuu huku wakisubiri siku ipite. Kijana aliyekuwaanafanya kazi za nje alikuwa anamaliza kazi zake mapema kwani baadhi ya kazi zilikuwa sii za kufanya kila siku kwa mfano kupalilia bustani na kufyeka majani, kazi iliyokuwa kubwa kakwe ilikuwa ni kulisha mifugo asubhi, mchana na jioni.

Basi sikumoja kijana anayefanya kazi za nje baada ya kumaliza kazi zake alitengeneza manati na kuanza kulenga vindege vilivyokuwa vinatua kwenye mabanda ya mifupo, kwa bahati mbaya alikosea shabahaa na kupiga kuku aliyekufa papohapo. kijana yule alimkimbilia yule kuku na kumtia kwenye mfuko kisha alimzika haraka kabla boss wake hajaona, kwa bahati mbaya yule rafiki yake anayefanya kazi za jikoni alimuona akifanya kosa hilo. Basi yule Kijana anayefanya kazi za nje alimuomba kijana anayefanya kazi za ndani asiseme kwa boss kwani alikuwa anaogopa sana kufukuzwa kazi endapo boss angejua, yule kijana anayefanya kazi za ndani alikubaliana na ombi la rafiki yake kwa mashariti ya kusaidiwa kazi za ndani kwa siku hiyo. Hiyo siku kijana anayefanya kazi za nje aliambiwa aoshe vyombo, basi yule kijana anayefanya kazi za nje akaona siyo mbaya mara mia aoshe vyombo kuliko kufukuzwa kazi. Bahati mbaya ule utumwa uliendelea siku hadi sikuu na alipojalibu kukataa kufanya kazi za ndani basi yule mfanyakazi wa ndani alikuwa anamtishia na kusema kama unakataa naenda kwa boss na kumwambia habari za KUKU.

Basi zikapita siku, wiki, hatimaye miezi kadhaa, kijana anayefanya kazi za nje akajikuta amekuwa mtumwa wa kazi za ndani na nje, akakonda kwa kazi nzito huku jamaa yake akiendelea kunenepa maana ulifika wakati yule anayehusika na kazi za ndani hakuwa anafanya kazi yoyote. Siku moja yule kijana aliyekuwa anahusika na kazi za nje baada ya kupata taabu nyingi akakata shauri na akaamua kwenda kuonana na boss ili aombe msamaha kwa kosa alilofanya. Boss alimkalibisha yule kijana ili aweze kusikiliza mahitaji yake. Yule kijana alianza kulia kabla ya kujieleza hatimaye boss alijitaidi kumnyamazisha kisha alimsihii aelezee yanayomsibu. Kijana alipiga magoti na kuelezea kosa alilotenda ikiwa ni pamoja na taabu (utumwa) alizopata baada ya kufanya kosa lile la kuua kuku. Boss alishanga kuona lile jambo limemkondesha yule kijana kiasi kile na alisema mimi siku ile ile ya kwanza unamuua yule kuku nilikuona na nilisha kusamehe siku ile ile maana nilijua wazi kuwa hukukusudia kufanya hivyo lakini kwa bahati mbaya nilikuwa sijui kama lile jambo liliendelea kukutesa na kukufanya uwe mtumwa hadi ukakonda kiasi hiki. Basi yule kijana baada ya kusamehewa alishukuru ndipo boss akamwambia kila siku hakikisha unapikiwa mayai manne na rafiki yako ili mwili wako ujirudi haraka.

Kijana alimshukuru sana boss kwa msamaha aliopewa kisha akaondoka akiwa na furaha, bahati mbaya sana yule kijana aliyekuwa anahusika na kazi za jikoni alikuwa amelala akitegemea yule anayefanya kazi za nje atafanya kazi za ndani siku hiyo asijue kuwa kijana anayefanya kazi za nje ataenda kuomba msamahaa kwa boss. Basi aliamka na kukuta hamna kazi ya ndani iliyofanywa, Alimsihii kijana anayefanya kazi za nje aanze mara moja kufanya hizo kazi laa sivyo ataenda kusemelea habari za kuku kwa Boss. Kijana anayefanya kazi za nje akamjibu hunitishii kama vipi nenda ukaseme ndo kwanza kabisa nakusindikiza, basi yule kijana aliekuwa anahusika na kazi za ndani kwa hasira alitoka na kwenda kusemelea kwa boss habari za mauaji ya kuku. Boss alishangaa kuona jambo la zamani anaambiwa siku ile, akamuhoji yule mfanyakazi kwanini hukusema siku ile unaamua kusema leo? yule mfanyakazi alikosa maelezo ya kutosheleza kwani alisingizia kuwa alikuwa anaogopa kumbe boss ameshapata stori yote hata jinsi alivyomtumikisha mwenzake.

Ikabidi boss aelezee namna alivyofanya kosa la kuka na udhaifu wa mtu kwa mda mrefu huku akisikitishwa sana na jinsii alivyoutumia udhaifu huo kumtesa mwenzeke hadi kufikia hali ya kukonda kiasi kile, kisha akamwambia hawezi kukaa na mtu anayeficha maovu kwa mda mrefu na anaamua kuyaweka peupe hadi siku anayoona hanufaiki na uovu huo. Basi siku hiyohiyo yule kijana anayefanya kazi za ndani alisimamishwa kazi kisha yule boss akatafuta mfanyakazi mwingine.

USHAURI WANGU, CHINI YA JUA HAYUPO ALIYEKAMILIKA NA MUNGU ANAYETUJUA VEMA MDA  MWINGINE ANATUSAMEHE HATA KABRA YA KWENDA KUOMBA MSAMAHAA,JITAIDI KUSAMEHE BURE NAWE UTASAMEHEWA BURE.

MGOMBEA URAIS WA MAREKANI ..DONALD TRUMP ASEMA AFRIKA NI LAZIMA ITAWALIWE TENA KIKOLONI



Donald Trump: “There Is No Shortcut To Maturity, Africa Should Be Recolonized”
American business mogul Donald Trump has said that Africa needs to be recolonized. This time around he has directed his anger to African leaders who according to Trump, have failed to exercise leadership and are keeping their people in worse conditions.
Speaking yesterday in Nebraska, Trump said that Africans are slaves living like slaves in their own land yet they claim they are independent.
Trump was responding to a question by a South African journalist on whether he thinks African leaders were right to seek mass withdrawal from the Hague based International Criminal Court.
“It is shameful for African leaders to seek exit from ICC. In my view, these leaders want to have all the freedom to oppress their poor people without anyone asking them a question. I think there is no shortcut to maturity and in my view, Africa should be recolonized because Africans are still under slavery. Look at how those African leaders change constitutions in their favour so that they can be live presidents. They are all greedy and do not care about the common people” Said Trump
“When I saw them gang up against ICC yet they can’t even find an amicable solution for the ongoing quandary in Burundi, I thought to myself these people lack discipline and humane heart. They can’t lead by example. The only thing they are interested in is accumulating wealth from poor tax payers. Before they think of exiting from ICC, they should first restore peace in Burundi and other war-tone countries rather than gathering like hyenas with the aim of finishing the poor people” Added Trump.

New