My Web

Emmanuel

CONTACT

Wednesday, December 12, 2012

VODACOM YASHAURI VILABU LIGI KUU KUIMARISHA VIKOSI KUPITIA DIRISHA DOGO


 
Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa akiongea na wanahabari (hawapo pichani).
Dar es Salaam, 12. Des. 2012 … Mdhamini wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara, Kampuni ya simu ya Vodacom Tanzania imezishauri klabu zinazokipiga ligi kuu kutumia nafasi ya usajili wa dirisha ndogo kuimarisha vikosi ili kuongeza kasi ya ushindani katika mzunguko wa lala salama wa ligi hiyo.
Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kampuni hiyo, Vodacom imesema vuilabu vina nafasi ya kutumia fursa ya dirisha dogo la usajili kujihakikishia kufanya vema kuelekea ubingwa wa ligi kuu.
“Msimamo wa ligi sasa unaonyesha dhahiri kuwa hata timu iliyo katika nafasi ya tano ina nafasi ya kuchukua ubingwa ikitambua mapema mapungufu yaliyosababisha usifanye vizuri katika mzunguko wa kwanza kupitia dirisha dogo klabu inaweza kujisahihisha.” Amesema Kelvin Twissa, Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania.
“Kabla ya usajili wa dirisha ndogo haujafanyika ni vyema klabu zikafanya tathmini ya aina ya wachezaji wanaohitaji na kufanya usajili wa kisayansi ambao utazijenga timu na kukabiliana na mikiki ya msimu ujao ambao ni mgumu zaidi,” amesema Twissa.
“Tumeshuhudia ushindani wa kiwango cha juu katika mzunguko wa kwanza hili linaweza kuufanya mzunguko wa pili ukawa mgumu zaidi kuusaka ubingwa na kujinusuru kushuka daraja hivyo ni vema kila timu ikajiandaa kimkakati kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili wa ligi”Aliongeza Twissa
Mkuu huyo wa Masoko amesema kuwa kampuni yake inaendelea kutekeleza dhamira yake ya kuinua michezo na wao kama wadhamini wa ligi kuu ni vyema kushirikiana na timu ili kujenga uwezo na kiwango cha soka nchini.
“Timu zetu zimekuwa gumzo katika michuano ya Chalange kwa kufunga magoli mengi zaidi na kuonyesha kiwango cha hali ya juu. Ni Wachezaji hao hao wanaocheza katika Ligi kuu ya Vodacom pamoja na wale wa ligi kuu Zanzibar ndio wamezua gumzo katika michuano hiyo,” amesema Twissa, na kuongeza kuwa, “Ukitazama hilo kwa kina lazima utawapa makocha wetu wa Tanzania sifa kwani ndio wanao waandaa wachezaji katika ngazi ya vilabu na wanapokuja kucheza katika timu ya taifa wanakuwa na mafanikio makubwa,”
Twissa amehitimisha kwa kuzisihi timu za Simba na Azam kufanya maandalizi ya michuano ya kimataifa inayo wakabili na kuzitakia kila la kheri.
“Tunazitakia kila la kheri timu zitakazoiwakilisha nchi yetu katika michuano ya kimataifa. Tunaamini tutafika mbali kwani ligi yetu inaendelea kuwa bora zaidi,” amesema Twissa.
Klabu ya Simba itachuana na timu ya C.R Libolo ya Angola katika michuano na Klabu bingwa Afrika na Azam FC itachuana na Ali Nasir Juba ya Sudan Kusini katika kombe la Shirikisho.

RAIS WA ZAMANI WA MADAGASKA MARC RAVALOMANANA AMEKUBARI KURUDI NCHINI KWAKE




  
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiwa na Rais wa zamani wa Madagascar , Marc Ravalomanana wakati wa mkutano na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es Salaam jana Desemba 11, 2012.
(PICHA NA IKULU)
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete amefanikiwa kufanya mazungumzo na Rais wa zamani wa Madagaska Marc Ravalomanana ambaye amekubari kurudi nchini kwake baada ya kuwa uhamishoni  nchini  Afrika Kusini tangu mwaka 2009.
Akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari Ikulu jijini Dar es Salaam leo,  Raisi Kikwete amesema Ravalomanana amekubali pia kutokugombea katika uchanguzi utakaofanyika nchini humo mwezi Mei 2013 ili kuleta amani na utulivu.
“Nimezungumza na Rais Ravalomanana na amekubali kurudi nchini kwake madagaska  na kukubali kutokukugombea  uchaguzi ujao kama maamuzi ya  Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) yalivyofikiwa katika vikao vyake vya hivi karibuni”, amesisitiza Rais Kikwete.
Raisi kikwete amefafanua  kuwa Ravalomanana  anarudi nchini Madagaska bila masharti yoyote na atapewa ulizi na Serikali ya nchi hiyo ikisaidiana na Jumuiya ya SADC.
Kwa upande wake Rais Ravalomanana amemshukuru Rais kikwete kwa kufanikisha mazungumzo hayo  na  amesema anaheshimu maamuzi yaliyotolewa na SADC kwa lengo la kuisaidia Madagaska kuwa katika hali ya amani.
“Ninamshukuru Rais Kikwete kwa kufanikisha mazungumzo haya na niko tayari kurudi nchini kwangu kujenga, kuimarisha na kushirikiana na wananachi  ili kuleta amani na utulivu,” amesema  Ravalomanana.
Rais kikwete alipewa jukumu na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika  la kufanya mazungumzo na Marais wote wa wawili,  Rais wa sasa wa Madagaska Andry Rajoelina na Rais wa zamani Marc Ravalomanana ambapo mazungumzo bado yanaendelea kwa upande wa Rais Rajoelina.
Dar es Salaam
11/12/2012.

Monday, December 10, 2012

Utafiti: Nguo za ndani zachangia ugumba

 

 

“Kwa kawaida mwanamume anayeishi maeneo ya joto anapaswa kuwa makini sana, ili kuhifadhi vizuri manii yake anatakiwa kutumia mavazi yenye kupitisha hewa,” alisema Dk Massawe.

TAFITI za kisayansi zimebaini kuwa nguo za ndani hasa zinazobana kwa wanaume na zile za aina ya nailoni (nylon) zinaathiri uwezo wa mbegu za kiume, hivyo kushindwa kutunga mimba.

Utafiti huo uliofanyika katika nchi za Ufaransa na Uingereza na kuchapishwa katika Gazeti la Daily Mail la Uingereza unabainisha kuwa, wanaume wanaovaa nguo za ndani zinazobana na zile zilizotengezwa kwa malighafi ya nailoni, mbegu zao za kiume (manii) huwa nyepesi na kupoteza uwezo wa kutunga mimba.

Vazi la ndani la wanaume linalojulikana kama boksa na nguo nyingine za ndani za kubana zenye asili ya nailoni, zinakuwa na athari kubwa zaidi hasa zinapovaliwa katika sehemu zenye joto, kama Dar es Salaam.

Kutokana na matokeo hayo, wanasayansi wameonya kuwa wanaume wanapaswa kuchukua tahadhari, hasa kutokana na tafiti nyingi za karibuni kuthibitisha kuongezeka kwa matatizo ya mbegu za kukosa uwezo wa kutunga ujauzito katika nyumba ya uzazi ya mwanamke.
Akizungumzia utafiti huo jana, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi katika Hosipitali ya Taifa Muhimbili, Dk Cyril Massawe, alisema una ukweli kutokana na mbegu za kiume kuwa nje ya mwili wa mwanamume tofauti na mwanamke ambaye kizazi chake kipo ndani.

“Kwa kawaida mwanamume anayeishi maeneo ya joto anapaswa kuwa makini sana, ili kuhifadhi vizuri manii yake anatakiwa kutumia mavazi yenye kupitisha hewa,” alisema Dk Massawe.

Ufaransa na Uingereza
Utafiti uliofanywa Ufaransa umebaini kuwa, upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume wengi ulianza kutokea tangu mwanzoni mwa 1990.

Awali, ilikuwa ikiaminika kuwa kupungua kwa uwezo wa mbegu za kiume kulitokana na sababu kama vile mtindo wa maisha, ulaji na matumizi ya dawa kupindukia na matumizi ya vyakula vyenye kemikali nyingi, lakini safari hii utafiti umebaini kuwa matumizi ya nguo za ndani yamekuwa yakiwaathiri wanaume wengi.

Mtafiti wa Uingereza, Profesa Richard Sharpe anasema tatizo hilo linaweza kuepukwa ikiwa mhusika atajitahidi kuvaa nguo zinazokubalika na mahala alipo. Hata hivyo, anapendekeza uchunguzi zaidi ufanywe ili kulinda kizazi cha sasa na kijacho.

Mtafiti huyo kutoka Chuo Kikuu cha Edinburgh anasema: “Uingereza suala hili halijawahi kuonekana wala kutiliwa mkazo na kuwa kipaumbele katika afya, labda kwa sababu ya wasiwasi kwamba sehemu za mwanamume zinatakiwa kubanwa. Hivi sasa hakuna shaka kwamba suala hilo ambalo liliongelewa hapo awali lina ukweli ndani yake, hivyo ni wakati kwa watu wote kuchukua hatua.”

“Kutokuchukua hatua kutasababisha familia nyingi kukosa watoto na hivyo idadi ya watu itapungua, lakini katika hali ya kawaida, ni vyema watu wakaelimishwa namna ya uvaaji. Sehemu za joto mtu anatakiwa kuvaa pamba na si nailoni ili kulinda mbegu zake.”

Profesa Sharpe anasema bado wanasayansi wana kazi kubwa kwani mpaka sasa karibu kila eneo ambalo wanasayanasi wamelichunguza limebainisha kuchangia tatizo hilo, lakini mpaka sasa wanafikiri kuwa vyakula vyenye mafuta na vile vyenye kemikali nyingi vina mchango mkubwa zaidi katika tatizo hilo.

Watafiti ambao walitumia takwimu kutoka katika vituo vya afya 126, waligundua kuwa tangu mwaka 1989 mpaka 2005, kulikuwa upungufu wa uwezo wa manii kwa mwanamume kufanya kazi kwa asilimia 32.2, kiwango ambacho ni karibu asilimia mbili kwa mwaka.

Watafiti walisema: “Kwa ufahamu wetu, ni utafiti wa kwanza kufanyika na umehusisha mbegu za kiume hai na uwezo wa manii katika nchi nzima kwa kipindi kirefu.”
“Huu ni utafiti mkubwa na unatoa onyo kali kiafya kwa jamii. Lakini huwezi kumlazimisha mtu kuhusu matumizi ya nguo za ndani,” wanasema.

Rungu la Mulugo lawashukia wakuu wa shule saba

 

Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,Philip Mulugo 

Walimu hao ni wale ambao shule zao wanafunzi wake walibainika majibu yao kufanana katika mitihani ya darasa la saba iliyofanyika mwaka jana hivyo kusababisha kufutiwa matokeo ambao wanafunzi husika walipewa adhabu ya kurudia mitihani mwaka huu

RUNGU la Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,  Philipo Mulugo limewashukia wakuu saba wa shule za msingi wilayani hapa kwa kupewa adhabu za kuteremshwa vyeo baada ya shule zao kujihusisha na udanganyifu kwenye mitihani.
Walimu hao ni wale ambao shule zao wanafunzi wake walibainika majibu yao kufanana katika mitihani ya darasa la saba iliyofanyika mwaka jana hivyo kusababisha kufutiwa matokeo ambao wanafunzi husika walipewa adhabu ya kurudia mitihani mwaka huu.
Naibu Waziri Mulugo alitoa agizo la walimu hao kuteremshwa vyeo kwa maofisa elimu wa halmashauri za wilaya na Mji wa Korogwe juzi, alipokuwa wilayani humo kwa ajili ya shughuli za kikazi ambapo alipata fursa ya kuzungumza na watumishi wa sekta ya elimu.
Walimu waliokumbwa na sakata hilo na shule wanazotoka kwenye mabano kwa upande wa halmashauri ya wilaya ni Karimu Awadhi (Hale), Eliakim Mbise (Kerenge), Ramadhani Kisairo (Rwengera Estate), Dastan Daudi (Pambei) na Mohamed Kombo (Vuluni).
Wengine ni Elisante Elibariki wa Shule ya Msingi Welei aliyehamishiwa Wilaya ya Kilindi ambaye hata hivyo imeelezwa kwamba tayari anatumikia adhabu hiyo ya kuteremshwa daraja huko aliko na Rashid Shekigenda wa Shule ya Msingi Antakaye Korogwe Mjini.
Katika mkutano na walimu wa eneo la Korogwe Mjini, Mulugo alielezea masikitiko yake juu ya hali ya ufaulu wa wanafunzi ambapo alisema ingawaje kimaandishi inaelezwa kuwa kiwango cha ufaulu kimeongezeka lakini uhalisia hauelezi hivyo kwa mazingira yaliyopo.
Naibu Waziri Mulugo aliyasema hayo baada ya kupokea taarifa toka kwa ofisa elimu wa halmashauri ya mji kuwa kiwango cha ufaulu kimeongezeka kwa wanafunzi wa darasa la saba, hapo aliweza kuzikumbuka baadhi ya shule zilizofutiwa matokeo kwa udanganyifu.
Baada ya naibu waziri huyo kuuliza swali hilo Ofisa Elimu, Maajabu Nkanyemka alijibu kuwa bado na kuitaja shule iliyofutiwa matokeo kuwa ni Antakaye ambapo mwalimu mkuu aliyekuwepo mkutanoni aliitwa mbele na waziri akiulizwa maswali kadhaa na baadaye na afisa elimu wa halmashauri hiyo ya mji alitakiwa kutekeleza agizo la kumteremsha cheo.
Kuhusu majibu juu ya suala la upungufu wa vitabu shuleni taarifa ambayo alisomewa, Mulugo aliwatoa hofu walimu kwamba serikali imetenga fedha za kutosha kukabili tatizo hilo

Gamboshi, ‘makao makuu ya uchawi na wachawi’

 

Gari linalokokotwa na ng'ombe katika barabara ya kuelekea kijijini Gamboshi.

USIKU YAONEKANA KAMA JIJI LA NEW YORK AU LONDON. WENYEWE WAMWOMBA RAIS KIKWETE, MZEE WA VIJISENTI AKAWASAFISHE

WAKAZI wa Kijiji cha Gamboshi, kilichopo wilayani Bariadi, Mkoa wa Shinyanga, wamemuomba Rais Jakaya Kikwete awasaidie kusafisha kijiji chao kutokana na jina baya lililoenezwa duniani kwamba  hapo ni makao makuu ya maovu ya uchawi  ulioshindikana.
Kijiji hicho ambacho ni nadra sana kutembelewa, kimepata umaaurufu mkubwa ndani na nje ya nchi kikielezwa kuwa ni kitovu cha uchawi na wachawi wanaoweza kufanya miujuza, hali ambayo imekifanya kijiji hicho kupitwa na mkondo wa kimaendeleo.
“Sisi ni wakulima wakarimu wa pamba, mahindi na mpunga. Yote mnayoyasikia kwamba sisi ni magwiji wa uchawi ni uvumi uliotiwa chumvi nyingi. Tunamwomba Rais wetu kwa kushirikiana na Mbunge wetu, Andrew Chenge watusadie kulisafisha jina letu,”alisihi  Zephania Maduhu, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Gamboshi.
Maduhu pamoja na wanakijiji wenzake walidai kuwa, hofu iliyoenezwa ndani na nje ya nchi kuhusua uchawi uliovuka mipaka wa Kijiji cha Gamboshi umesababisha madhara makubwa kwa kijiji chao kiasi chakutengwa na jamii yote ya Watanzania.
“Hakuna aliyetembelea kijiji hiki kwa miaka mingi sana. Hata sisi tunapotoka nje ya kijiji, wengi hawataki kutusogelea wakiamini tutawadhuru, ”  alisema Musa Deus (26), mmoja wa wakulima walionufaika kilimo cha mkataba kijijini Gamboshi.
Kwa mujibu wa Ofisa Mtendaji wa Kijiji hicho, tangu Uhuru mwaka 1961, hakuna kiongozi yoyote wakitaifa aliyewahi kukanyaga kijijini hapo.
Anaongeza kuwa mtu wa pekee aliyewahi kuzuru kijijini hapo ni mbunge wa Bariadi Mashariki, Andrew Chenge, aliyefika kijijini hapo mwaka 2010, wakati akifanya kampeni za ubunge.
“Tume ya Katiba ilitupita, mwenge wa Uhuru nao haujawahi kupita hapa.Tuko kisiwani mbali na Watanzania wengine,” anasema Maduhu.
Kikiwa mafichoni kabisa, kiasi cha kilometa 44 kutoka mjini Bariadi, Kijiji cha Gamboshi si rafiki wa watu wa Kanda ya Ziwa kama ambavyo Mwananchi Jumapili ilibaini katika utafiti wake wa muda mrefu.
Mijini na vijijini, kumekwepo na ubishani mkali kuhusu ni mkoa gani unaokimiliki kijiji hicho, ambacho baadhi ya wakazi wake wanadai kuwa miongoni mwa vioja vyake ni mauzauza yanayoweza kuifanya Gamboshi ionekane kama Jiji la New York, Marekani au London, Uingereza wakati wa usiku.
Pamoja na umaarufu wake, bado uwepo wa Gamboshi umekuwa ni kitendawili kikubwa kwa jamii ya Wasukuma kutoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga na Simiyu.
Mbali na ubishani mkali kuhusu kuhusu mahali hasa kilipo kijiji hicho cha miujiza, wengi wamekuwa wakidai wakazi wake siyo jamii ya Kisukuma.
Wakazi wa Shinyanga wanadai kuwa Gamboshi iko wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza, wakati wale Mwanza wakidai kuwa iko mkoani Shinyanga.
Kwa mujibu wa Maduhu, Gamboshi iko katika Wilaya Bariadi, karibu na mpaka unaotenganisha na Wilaya ya Magu iliyoko mkoani Mwanza.
“Tunaomba sana ndugu mwandishi, waambie Watanzania kuwa mengi wanayoyasikia kuhusu Gamboshi siyo kweli kabisa. Tunawakaribisha wote waje hapa kufanya biashara na sisi, waoleane na vijana wa Gamboshi kama wafanyavyo katika vijiji vingine. Sisi ni binadamu wema,” anasema mkazi wa kijiji hicho, Malimi Kidimi ambaye ni mkulima.
Ofisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Pamba(TCB), Ramadhani Dissa, anaielezea Gamboshi kuwa ni moja ya vijiji vilivyouza pamba nyingi msimu huu.

Polisi yakiri wizi bandarini ni mtandao

  

Waziri waUchukuzi,Dk Harrison Mwakyembe

 Jamani tupo kazini, wizi uliotumika siyo wizi huu wa kawaida bali ni wizi wa mtandao, wapo walioghushi  nyaraka ndizo zimetumika  kufanikisha wizi, hivyo tunafanya uchunguzi kubaini wahusika wote,” alisema.

KAMANDA wa Polisi Kikosi cha Bandari, Foturnatus Muslim amesema katika uchunguzi wa awali wamebaini  wizi uliotumika kuiba shaba na mafuta ni wa mtandao.
Akizungumza kwa simu jana,  Muslim alisema ili kuhakikisha wanafanya kazi ya kukomesha vitendo vya wizi bandarini, wanalazimika kufanya uchunguzi wa kina wa tukio hilo.
“ Jamani tupo kazini, wizi uliotumika siyo wizi huu wa kawaida bali ni wizi wa mtandao, wapo walioghushi  nyaraka ndizo zimetumika  kufanikisha wizi, hivyo tunafanya uchunguzi kubaini wahusika wote,” alisema.
Waziri wa Uchukuzi, Harrison Mwakyembe hivi karibuni alihoji kuhusu maendeleo ya kesi ya wizi wa shaba lenye kumbukumbu namba KLB /IR/3067 /2012 na ya wizi wa mafuta yenye namba KLR 3068/2012.
Kesi hizo hadi sasa zinajumuisha washtakiwa 13.
Hata hivyo, imeeleza kuna polisi ambao wanatuhumiwa kuhusika kusimamia wizi huo, hawajaunganishwa na wenzao.  
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alikaririwa na vyombo vya habari juzi akieleza kwamba upelelezi wa kubaini polisi waliohusika unaendelea.

JK:Wenye hila na chuki wanabeza maendeleo yetu

  

 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kushoto) Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein (kushoto), Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange,Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal, Wakiwa makini wakati wimbo wa Taifa ulipokuwa ukiimbwa kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru jana.Picha na Salhim Shao

 “Utaratibu uliopo ni kuzungumza kila baada ya miaka mitano, lakini mwaka huu ninazungumza na wananchi kutokana na kuwapo kwa viongozi wa mataifa ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc). Nataka wasikie mafanikio yetu ya miaka 51 ya Uhuru,” alisema Rais Kikwete.

RAIS Jakaya Kikwete amesema wenye hila na chuki pekee ndiyo wanaosema kuwa Tanzania hakuna maendeleo.
Alisema hayo jana alipolihutubia Taifa kwenye maadhimisho ya miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
“Utaratibu uliopo ni kuzungumza kila baada ya miaka mitano, lakini mwaka huu ninazungumza na wananchi kutokana na kuwapo kwa viongozi wa mataifa ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc). Nataka wasikie mafanikio yetu ya miaka 51 ya Uhuru,” alisema Rais Kikwete.
Viongozi walioshiriki maadhimisho hayo ni marais Armando Guebuza wa Msumbiji, Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) na Hifikepunye Pohamba wa Namibia.
Nchi zilizotuma wawakilishi katika sherehe hizo zilizohudhuriwa na umati wa watu ni Lesotho, Zambia, Angola, Swaziland, Shelisheli, Rwanda, Zimbabwe, Mauritius na Malawi.
Rais Kikwete alisema mwenye macho hawezi kusema lolote, lakini kwa mwenye hila hakosi maneno na kutoa dosari kwa maendeleo yaliyofikiwa.
“Watu waliobahatika kuiona Tanzania ya mwaka 1961 wakija sasa hivi, wataona mabadiliko makubwa. Kuna mabadiliko makubwa na hii inatokana na kuboresha nyanja mbalimbali za kiuchumi, ulinzi na usalama na miundombinu... kwa wenye hila hawakosi la kusema ila mwenye macho haambiwi tazama,” alisema.
Aliwashukuru viongozi walioshiriki mkutano SADC… “Tumepata bahati ya uwepo wa viongozi waandamizi wa SADC baada ya kukubali ombi langu la kuhudhuria sherehe hizi japo wengine wametoa udhuru na kutuma wawakilishi,” alisema.
Viongozi mashuhuri wakosekana
Baadhi ya viongozi wa kitaifa wakiwamo wastaafu, hawakuwamo katika sherehe hizo.
Miongoni mwa viongozi hao ni pamoja na mtangulizi wa Kikwete, Benjamin Mkapa ambaye yuko Lushoto mkoani Tanga.
Wengine ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Idd ambao hata hivyo, haikuelezwa sababu za kukosekana kwa

Misri: Rais aliamuru jeshi kudumisha amani



Vifaru vyadumisha amani
Vifaru vyadumisha amani

Rais Morsi wa Misri ameliamuru jeshi kudumisha amani na kuzilinda taasisi za serikali katika kipindi kinachotangulia kura ya maoni kuhusu katiba.
Viongozi wa upinzani wameshutumu kitendo hicho, na wameitisha maandamano yafanyike Jumanne.
Jon Leyne wa BBC, aliyeko mjini Cairo, anasema kwamba kitendo hicho kitakuza wasiwasi uliopo kwamba hali nchini Misri inarudi tena katika siku za uongozi wa kijeshi.
Bwana Morsi amejaribu kutuliza maandamano ambayo yamekuwepo kwa siku kadhaa sasa, kwa kubatilisha amri iliyokuwa imempa mamlaka makubwa, lakini hata hivyo kura ya maoni ya 15 Desemba kuhusu katiba mpya bado itapigwa.

Maandamano
Vyama vya Kiisilamu vimesema kuwa nao pia wataandamana, jambo ambalo limezua wasiwasi kwamba makabiliano yanayotokea mara kwa mara katika barabara za mji mkuu wa Misri yatazidi kuwa makali.
Haijajulikana wazi kama upinzani utasusia kura hiyo ya maoni, mwandishi wetu anasema, ingawaje hali inaashiria kuwa wanaweza wakafanya hivyo.

Rais Mohammed Morsi
Rais Mohammed Morsi

Wanasema kwamba jopo lililorasimu katiba lilikuwa limejaa wapambe wa Morsi.
Katika taarifa iliyotolewa baada ya mazumgumzo ya Jumapili, chama cha National Salvation Front kilisema kisingetambua katiba rasimu "kwa sababu katiba hiyo haiwawakilishi wananchi wa Misri".
Kura ya maoni
Mnamo siku ya Jumapili, mamia ya wafuasi wa upinzani walikusanyika nje ya kasri la rais wakishtumu mpango wa kufanya kura hiyo ya maoni.
Huku wakiikashifu Muslim Brotherhood, waliimba barabarani na kubeba mabango yaliyosema "Morsi, wazuie majambazi wako" na "Wananchi wanataka serikali iondolewe ".
Amri hii mpya ya rais itaanza kutekelezwa mnamo siku ya Jumatatu. Jeshi limeombwa lifanye kazi pamoja na polisi ili kudumisha amani na usalama. Jeshi pia lina uwezo wa kuwakamata wananchi.
Jeshi limeshajenga ukuta wa saruji amabo umezingira kasri la rais, eneo ambalo wapinzani wanapenda kuandamana.

Amri

Waandamanaji nchini Misri
Waandamanaji nchini Misri

Rais anasema kwamba anajaribu kulinda mapinduzi yaliyompindua Hosni Mubarak mwaka uliopita, lakini wapinzani wake wanamnyooshea kidole cha lawama na kumuita dikteta.
Amri ya Bwana Morsi ya 22 Novemba iliinyang'nya mahakama haki ya kupinga maamuzi ya Morsi, na ikazua maandamano yaliyokuwa na vurugu.
Ingawaje amri hii imebatilishwa, maamuzi fulani yaliyochukuliwa awali yangali yapo.

John Mahama ashinda uchaguzi Ghana


Wapiga kura nchini Ghana

Wapiga kura nchini Ghana
Tume ya Uchaguzi nchini Ghana imetangaza John Mahama kama mshindi wa uchaguzi wa urais. Mahama alikuwa rais kabla ya uchaguzi.
Tume hiyo ilisema kwamba Bwana Mahama alishinda kwa asilimia 50.7 dhidi ya mpinzani wake Nana Akufo-Addo aliyepata 47.74%.
Hata hivyo chama cha upinzani cha NPP kimesema kwamba kitayapinga matokeo hayo, huku kikilaumu chama tawala cha NDC kwa kupanga njama na tume hiyo ili kubadilisha matokeo ya uchaguzi uliofanyika Ijumaa.
Rais Mahama aliwasihi "viongozi wote wa vyama vyote vya kisiasa kuheshimu uamuzi wa wananchi".
"Sauti ya wananchi ni sauti ya Mungu," alisema.
Polisi mjini Accra walilazimika kufyatua vitoa machozi ili kuwatawanya wafuasi wa upinzani waliokuwa wamekusanyika nje ya ofisi za tume hiyo.
Wakati matokeo yakitangazwa, vifaru vilikuwa vikilinda ofisi za tume hiyo, na barabara zilizoizunguka zilikuwa zimewekwa vizingiti na polisi.
"Mabibi na mabwana, kulingana na matokeo tuliyopata, namtangaza John Dramani Mahama kama rais-mteule," mkuu wa tume Kwadwo Afari-Gyan aliwaambia waandishi habari.

Bwana Akufo-Addo
Bwana Akufo-Addo

Alisema asilimia 80 ya wapigaji kura walijitokeza.
Matokeo yakataliwa
Katika taarifa rasimu iliyotumwa kwa waandishi habari mnamo Jumapili kupitia barua pepe, upinzani ulisema kwamba utayapinga matokeo hayo.
"Hali hii ikikubaliwa kuendelea bila kupingawa au kusahihishwa italeta madhara makubwa kwa misingi ya taratibu za uchaguzi na hali halisi ya demokrasia nchini Ghana," NPP ilisema.
"Kukubali matokeo haya ni kuidharau demokrasia nchini Ghana, na, kwa hali hiyo hiyo, kuvuruga taratibu za kukuza demokrasia barani Afrika. Kwa minajili hii, New Patriotic Party haitayakubali matokeo ya uchaguzi wa urais kama yalivyotolewa na Tume ya Uchaguzi jioni hii."
Awali, NPP ilikuwa imesema kuwa ilikuwa na “ushahidi wa kutosha” kuthibitisha kwamba Bwana Akufo-Addo alikuwa ameshinda uchaguzi huo.
"Chama tawala cha NDC kilipanga njama na baadhi ya wafanyikazi wa EC katika maeneo bunge fulani kote nchini ili kubadilisha matokeo, na hivyo kudharau uamuzi wa wananchi wa Ghana," chama hicho kilisema.
John Dramani Mahama
John Dramani Mahama

"Ni kitendo hiki cha kuiba kura makusudi katika ngazi kulikokuwa kunafanywa mahesabu ndicho kiligundilika mapema."
Uchaguzi wa amani
Mshauri wa maswala ya kirais wa Bwana Mahama, Tony Aidoo, alisema madai hayo yalikuwa hayana ukweli wowote.
Bwana Akufo-Addo alishindwa katika uchaguzi urais wa 2008 kwa asilimia moja tu, lakini akakubali matokeo.
Matatizo ya mashine mpya za kupiga picha alama za vidole, katika maeneo kadhaa nchini, yalilazimisha uchaguzi uoendelee hadi Jumamosi.
Hata hivyo, wachunguzi walisema kwamba uchaguzi huo, kwa ujumla, ulifanyika kwa amani.
Bwana Mahama alikuwa makamu wa rais hadi rais John Atta Mills alipofariki ghafla mwezi Julai mwaka huu, ndipo akawa rais.

Korea Kaskazini yaahirisha urushaji roketi

Korea Kaskazini inasema kwamba imeongeza muda wa uzinduzi wa roketi yake ya masafa marefu ili kukabiliana na hitilafu za kimitambo katika injini ya roketi hiyo.
Uzinduzi huo, uliokuwa uanze leo, sasa umesogezwa na kupewa muda hadi 29 Desemba.
Jaribio la awali ili kujaribu kurusha roketi hiyo mnamo mwezi Aprili halikufaulu.
Korea Kaskazini inasisitiza kuwa roketi hiyo ni ya amani ili kutuma setilaiti angani, lakini Marekani na mataifa mengine yanasema kuwa hilo ni jaribio la kurusha kombora la masafa marefu kutoka bara moja hadi jingine.

Monday, December 3, 2012

Papa Benedict kwenye Twitter

Papa anatarajiwa kuanza kutumia mtandao wa kijamii Twitter kuwasiliana na waumini
Papa Benedict anafungua akaunti katika mtandao wa kijamii,Twitter, katika jitihada ya kusambaza ujumbe wa kanisa katoliki.
Taarifa kuhusu akaunti hiyo itatolewa baadaye hii leo katika mkutano na waandishi habari, lakini duru kutoka Vatican zinasema huenda asiandike mwenyewe ujumbe kwenye akaunti hiyo.
Wanasema Papa Benedict anapendelea kuandika kwa mkono kuliko kutumia tarakilishi.
Kanisa hilo la katoliki tayari linatumia mitandao kadhaa ya kijamii na hivi karibuni limezindua mtandao mkuu unaounganisha mitandao ya kanisa hilo kote ulimwenguni.
Wakatoliki kote duniani, wataweza kuwasilina na Papa kupitia Twitter wakati akaunti hiyo itakapozinduliwa rasmi.
Papa Benedict anataka kuitumia akaunti hiyo kuwasiliana na wakatoliki kote duniani.

Majaji kususia kura ya maoni Misri


Wafuasi wa rais Morsi wakisherehekea mjini Cairo
Shirika linalowawakilisha mahakimu wa Misri limetangaza kuwa wanachama wake hawatoisimamia kura ya maoni ya rasimu ya katiba itakayofanyika wiki mbili zijazo.
Taarifa hiyo ya muungano huo wa mahakimu, inajiri baada ya kuwepo mvutano kati ya mahakama ya juu nchini Misri na wafuasi wa rais Morsi wenye itikadi kali za dini ya kiislamu.
Mahakama ya kikatiba imetangaza kuwa inasitisha shughuli zake kwa muda usiojulikana baada ya mahakimu wa mahakama hiyo kuzuiwa kutoa uamuzi kuhusu uhalali wa baraza rasimu hiyo ya katiba.
Upinzani unasema rasimu inashusha hadhi ya uhuru wa watu.
Makundi ya upinzani yaliitisha maandamano dhidi ya kura ya maoni juu ya katiba hiyo itakayofanyika siku ya Jumanne.
Walisema kuwa Rais Morsi alivunja ahadi ya kutoitisha kura ya maoni bila ya makubaliano ya wengi kuukubali wito huo.
"vuguvugu la National Salvation Front, linapinga kitendo kilichofanywa na ambachio hakikubaliki katu cha kuitisha kura ya maoni juu ya rasimu ya katiba ambayo imekataliwa na watu wengi''ilisema taarifa ya muungano wa vyama vaya upinzani kwa umma.
Upinzani unaamini kuwa rasimu hiyo inabana uhuru muhimu wa watu kikatiba.

Wasiwasi wa UN kuhusu mpango wa Israel




Walowezi wa kiyahudi wanaoishi katika Ukingo wa Magharibi
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa, Ban Ki Moon, ameonya kuwa mpango wa Israeli wa ujenzi wa makao mapya ya walowezi utakuwa na athari mbaya kwa nafasi ya kupatikana amani na Palestina.
Israeli inasema inapanga kuongeza nyumba elfu tatu kwa makaazi yaliopo tayari na inatarajia kuongeza makaazi mapya kuunganisha yale yaliopo katika ukingo wa Magharibi na Jerusalem Mashariki.
Ilitangaza mpango huo kufuatia kura iliyopigwa katika Umoja wa mataifa iliyoipandisha Palestina hadhi kuwa dola muangalizi katika umoja huo.
Hapo jana kiongozi wa Palestina Mahmoud Abbas alipokewa kwa shangwe mjini Ramallah katika ukingo wa Magharibi aliporudi nyumbani kutoka kwenye mkutano huo.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ameahidi kuendelea na mpango wake wa ujenzi.
Katika taarifa yake Jumapili, Bwana Ban alielezea wasiwasi mkubwa kuhusu mpango ulioidhinishwa wa nyumba mpya elfu tatu zinazotarajiwa kujengwa Mashariki mwa Jerusalem na katika ukingo wa Magharibi.
Lakini alisisitiza kuwa mpango wowote wa kujenga makaazi katika sehemu inayojulikana kama E1, kati ya
Jerusalem na makaazi yaliyoko Ukingo wa Magharibi ya Maaleh Adumim, lazima usitishwe. "Hatua hii itakuwa pigo kubwa kwa fursa iliyopo ya mazungumzo ya amani'' alisema bwana Ban.
Marekani ilisema kuwa mpango huo hausaidii chochote bali utaathiri hatua zilizofikiwa za amani. Naye Mkuu wa sera katika Muungano wa Ulaya Catherene Ashton, alielezea wasiwasi kuhusu mpango wa ujenzi wa makaazi mengine ya walowezi

Tuesday, November 20, 2012

Askofu wa kwanza wa Kike ateuliwa



Ellinah Wamukoya  
 
Ellinah Wamukoya
Ellinah Wamukoya ameteuliwa kuwa askofu wa kwanza wa kike wa kanisa la Kianglikana barani Afrika.
Akiongea muda mfupi baada ya kuteuliwa, Bi. Ellinah Wamukoya amesema uamuzi huo heshima kwa kina mama.
Ellinah Wamukoya, 61, sasa atahudumu kama askofu mpya wa kanisa hilo katika ufakme wa Swaziland, moja wapo ya nchi zinazokisiwa kufuata siasaa za kihafidina.
Kutawazwa kwake kumejiri huku kanisa la Kianglikana, likitarajiwa kujadili ikiwa kina mama wataruhusiwa kuapishwa kuwa maaskofu wa kanisa hilo.
Askofu wa jimbo la Capte Town, nchini Afrika Kusini, amesema kuwa wamechukua uamuzi huo ili wawe mfano kwa wengine na pia kuwatakia, viongozi wa kanisa hilo, faraja na hekima ili kujadilia sauala hilo kwa haraka.
Kwa mujibu wa ripoti aliyotuma kwa vyo,bo vya habari, askofu huyo wa jimbo la Cape Town, Revd. Thabo Makgoba, amesema wimbi kwa sasa linavuma na kuwa wameshuhudia tukio la kihistoria ambao ni sawa na bingu kufunguka.
David Dinkebogile aliongoza sherehe hizo na kukariri kuwa nia yao kuwa ilikuwa kumuapisha askofu na wale sio mtu mweusi, muafrika na raia wa Swaziland.
Askofu Wamukoya ni meya wa zamani wa mji mkuu wa Swaziland Manzini.

Barack Obama's victory speech

Thank you. Thank you. Thank you so much. (Sustained cheers, applause.)

Tonight, more than 200 years after a former colony won the right to determine its own destiny, the task of perfecting our union moves forward. (Cheers, applause.)

It moves forward because of you. It moves forward because you reaffirmed the spirit that has triumphed over war and depression, the spirit that has lifted this country from the depths of despair to the great heights of hope, the belief that while each of us will pursue our own individual dreams, we are an American family, and we rise or fall together as one nation and as one people. (Cheers, applause.)

Tonight, in this election, you, the American people, reminded us that while our road has been hard, while our journey has been long, we have picked ourselves up, we have fought our way back, and we know in our hearts that for the United States of America, the best is yet to come.

(Cheers, applause.) I want to thank every American who participated in this election. (Cheers, applause.) Whether you voted for the very first time (cheers) or waited in line for a very long time (cheers) – by the way, we have to fix that – (cheers, applause) – whether you pounded the pavement or picked up the phone (cheers, applause), whether you held an Obama sign or a Romney sign, you made your voice heard and you made a difference. (Cheers, applause.)

I just spoke with Governor Romney and I congratulated him and Paul Ryan on a hard-fought campaign. (Cheers, applause.) We may have battled fiercely, but it's only because we love this country deeply and we care so strongly about its future. From George to Lenore to their son Mitt, the Romney family has chosen to give back to America through public service. And that is a legacy that we honour and applaud tonight. (Cheers, applause.) In the weeks ahead, I also look forward to sitting down with Governor Romney to talk about where we can work together to move this country forward.

(Cheers, applause.)

I want to thank my friend and partner of the last four years, America's happy warrior, the best vice-president anybody could ever hope for, Joe Biden. (Cheers, applause.)

And I wouldn't be the man I am today without the woman who agreed to marry me 20 years ago. (Cheers, applause.) Let me say this publicly. Michelle, I have never loved you more. (Cheers, applause.) I have never been prouder to watch the rest of America fall in love with you too as our nation's first lady. (Cheers, applause.)

Sasha and Malia – (cheers, applause) – before our very eyes, you're growing up to become two strong, smart, beautiful young women, just like your mom. (Cheers, applause.) And I am so proud of you guys. But I will say that, for now, one dog's probably enough. (Laughter.)

To the best campaign team and volunteers in the history of politics – (cheers, applause) – the best – the best ever – (cheers, applause) – some of you were new this time around, and some of you have been at my side since the very beginning.

(Cheers, applause.) But all of you are family. No matter what you do or where you go from here, you will carry the memory of the history we made together. (Cheers, applause.) And you will have the lifelong appreciation of a grateful president. Thank you for believing all the way – (cheers, applause) – to every hill, to every valley. (Cheers, applause.) You lifted me up the whole day, and I will always be grateful for everything that you've done and all the incredible work that you've put in. (Cheers, applause.)

I know that political campaigns can sometimes seem small, even silly. And that provides plenty of fodder for the cynics who tell us that politics is nothing more than a contest of egos or the domain of special interests. But if you ever get the chance to talk to folks who turned out at our rallies and crowded along a rope line in a high school gym or – or saw folks working late at a campaign office in some tiny county far away from home, you'll discover something else.

You'll hear the determination in the voice of a young field organiser who's working his way through college and wants to make sure every child has that same opportunity. (Cheers, applause.) You'll hear the pride in the voice of a volunteer who's going door to door because her brother was finally hired when the local auto plant added another shift. (Cheers, applause.)

You'll hear the deep patriotism in the voice of a military spouse who's working the phones late at night to make sure that no one who fights for this country ever has to fight for a job or a roof over their head when they come home. (Cheers, applause.)

That's why we do this. That's what politics can be. That's why elections matter. It's not small, it's big. It's important. Democracy in a nation of 300 million can be noisy and messy and complicated. We have our own opinions. Each of us has deeply held beliefs. And when we go through tough times, when we make big decisions as a country, it necessarily stirs passions, stirs up controversy. That won't change after tonight. And it shouldn't. These arguments we have are a mark of our liberty, and we can never forget that as we speak, people in distant nations are risking their lives right now just for a chance to argue about the issues that matter – (cheers, applause) – the chance to cast their ballots like we did today.

But despite all our differences, most of us share certain hopes for America's future.

We want our kids to grow up in a country where they have access to the best schools and the best teachers – (cheers, applause) – a country that lives up to its legacy as the global leader in technology and discovery and innovation – (scattered cheers, applause) – with all of the good jobs and new businesses that follow.

We want our children to live in an America that isn't burdened by debt, that isn't weakened up by inequality, that isn't threatened by the destructive power of a warming planet. (Cheers, applause.)

We want to pass on a country that's safe and respected and admired around the world, a nation that is defended by the strongest military on Earth and the best troops this – this world has ever known – (cheers, applause) – but also a country that moves with confidence beyond this time of war to shape a peace that is built on the promise of freedom and dignity for every human being.

We believe in a generous America, in a compassionate America, in a tolerant America open to the dreams of an immigrant's daughter who studies in our schools and pledges to our flag – (cheers, applause) – to the young boy on the south side of Chicago who sees a life beyond the nearest street corner – (cheers, applause) – to the furniture worker's child in North Carolina who wants to become a doctor or a scientist, an engineer or an entrepreneur, a diplomat or even a president.

That's the – (cheers, applause) – that's the future we hope for.

(Cheers, applause.) That's the vision we share. That's where we need to go – forward. (Cheers, applause.) That's where we need to go. (Cheers, applause.)

Now, we will disagree, sometimes fiercely, about how to get there. As it has for more than two centuries, progress will come in fits and starts. It's not always a straight line. It's not always a smooth path. By itself, the recognition that we have common hopes and dreams won't end all the gridlock, resolve all our problems or substitute for the painstaking work of building consensus and making the difficult compromises needed to move this country forward.

But that common bond is where we must begin. Our economy is recovering. A decade of war is ending. (Cheers, applause.) A long campaign is now over. (Cheers, applause.) And whether I earned your vote or not, I have listened to you. I have learned from you. And you've made me a better president. And with your stories and your struggles, I return to the White House more determined and more inspired than ever about the work there is to do and the future that lies ahead. (Cheers, applause.)

Tonight you voted for action, not politics as usual. (Cheers, applause.) You elected us to focus on your jobs, not ours.

And in the coming weeks and months, I am looking forward to reaching out and working with leaders of both parties to meet the challenges we can only solve together – reducing our deficit, reforming our tax code, fixing our immigration system, freeing ourselves from foreign oil. We've got more work to do. (Cheers, applause.)

But that doesn't mean your work is done. The role of citizens in our democracy does not end with your vote. America's never been about what can be done for us; it's about what can be done by us together, through the hard and frustrating but necessary work of self-government. (Cheers, applause.) That's the principle we were founded on.

This country has more wealth than any nation, but that's not what makes us rich. We have the most powerful military in history, but that's not what makes us strong. Our university, our culture are all the envy of the world, but that's not what keeps the world coming to our shores. What makes America exceptional are the bonds that hold together the most diverse nation on Earth, the belief that our destiny is shared – (cheers, applause) – that this country only works when we accept certain obligations to one another and to future generations, so that the freedom which so many Americans have fought for and died for come with responsibilities as well as rights, and among those are love and charity and duty and patriotism. That's what makes America great. (Cheers, applause.)

I am hopeful tonight because I have seen this spirit at work in America. I've seen it in the family business whose owners would rather cut their own pay than lay off their neighbours and in the workers who would rather cut back their hours than see a friend lose a job. I've seen it in the soldiers who re-enlist after losing a limb and in those Seals who charged up the stairs into darkness and danger because they knew there was a buddy behind them watching their back. (Cheers, applause.) I've seen it on the shores of New Jersey and New York, where leaders from every party and level of government have swept aside their differences to help a community rebuild from the wreckage of a terrible storm. (Cheers, applause.)

And I saw it just the other day in Mentor, Ohio, where a father told the story of his eight-year-old daughter whose long battle with leukaemia nearly cost their family everything had it not been for healthcare reform passing just a few months before the insurance company was about to stop paying for her care. (Cheers, applause.) I had an opportunity to not just talk to the father but meet this incredible daughter of his. And when he spoke to the crowd, listening to that father's story, every parent in that room had tears in their eyes because we knew that little girl could be our own.

And I know that every American wants her future to be just as bright. That's who we are. That's the country I'm so proud to lead as your president. (Cheers, applause.)

And tonight, despite all the hardship we've been through, despite all the frustrations of Washington, I've never been more hopeful about our future. (Cheers, applause.) I have never been more hopeful about America. And I ask you to sustain that hope.

[Audience member: "We got your back, Mr President!"]

I'm not talking about blind optimism, the kind of hope that just ignores the enormity of the tasks ahead or the road blocks that stand in our path. I'm not talking about the wishful idealism that allows us to just sit on the sidelines or shirk from a fight. I have always believed that hope is that stubborn thing inside us that insists, despite all the evidence to the contrary, that something better awaits us so long as we have the courage to keep reaching, to keep working, to keep fighting. (Cheers, applause.)

America, I believe we can build on the progress we've made and continue to fight for new jobs and new opportunities and new security for the middle class. I believe we can keep the promise of our founding, the idea that if you're willing to work hard, it doesn't matter who you are or where you come from or what you look like or where you love. It doesn't matter whether you're black or white or Hispanic or Asian or Native American or young or old or rich or poor, abled, disabled, gay or straight. (Cheers, applause.) You can make it here in America if you're willing to try.

Hotuba ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete

Utangulizi

Mheshimiwa Dkt. Amani Abeid Karume, Makamu Mwenyekiti  wa CCM na Rais Mstaafu wa Zanzibar;
Ndugu Pius Msekwa, Makamu Mwenykiti wa CCM wa Bara;
Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Ndugu Benjamin William Mkapa;
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Waziri Mkuu;
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ;
Viongozi Wakuu Wastaafu;
Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Wilson Mukama;
Ndugu  Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM;
Wageni wetu waalikwa kutoka vyama rafiki,
 Ndugu zetu wa Vyama vya Siasa Nchini;
Waheshimiwa Mabalozi,
Viongozi wa Dini,
Wageni Waalikwa,
Mabibi na Mabwana; 

 

kuna mada ndogo ndogo hapa

1. Msichana akitaka kukutafutia sababu ya kukukataa wala hatumii nguvu,ana full of option,na majibu yao makuu ni haya yafuatayo:
1.We kwanza mweusi na mi mweusi mtoto atakuwa so dark,mi napenda wanaume weupe ili mtoto atoke mzuri..Anaongea kwa kujiamini utadhani kwenye kutunga mimba huwa anamsadidia Mungu kukoroga kopo la rangi ya mtoto...
2.We sio type yangu,sasa sijui type ipi anataka Nokia au Samsung
3.Am not ready,moyo wangu umepasuka...moyo upasuke bado unatembea??Tairi lenyewe likipasuka watu wanaziba pancha...
Kuwa Mwanaume shida,tunapambana na majibu unaweza kumzaba vibao mtu na Love inaisha hapohapo!



 2. Kutokuwa na Trust kwa mpenzi wako ni Kansa mbaya sana,itakumaliza! Kama humuamini unaendelea kuwa naye wa kazi gani??
Mpenzi anaaga anaenda harusini,kiroho kinakusimama,kila muda unampigia simu,asipopokea umenuna,sasa ulitaka aende kutoa zawadi kwa maharusi simu sikioni??
Anatoka Outing usiku,hulali,kila baada ya robo saa unampigia,eti uko na nani hapo,kama kweli uko salama hebu nibusu kwa nguvu,au sema I love you kwa nguvu...Huo ni Wazimu!
Nyie ndo mnakufaga na Presha za kushuka,Huwezi kumpenda mtu usiyemuamini,thats a big lie...
Big up kwa wote mnaowaamini wapenzi wenu,kama wako wako tu,na kama sio wako sio,acheni ukukumaji



3. Ni heri uishi kwenye nyumba ndogo sana lakini ni ya kwako na imetokana na jasho lako,kuliko kujisikia fahari kukaa kwenye nyumba kubwa ya kupanga ambayo si yako..
Ni heri uwe na Msichana wa kawaida,mwenye upendo wa kweli ambaye unammiliki peke yako kuliko kuwa na demu mkali,shape hinhaa,lakini ana wamiliki wengi kama Hisa za Facebook New York Stock Exchange..
Ni heri uwe na Mwanaume wa kawaida mwenye hela za kawaida tu za kubadilishia mboga,lakini mwenye upendo wa dhati kwako kuliko kuwa na Mwanaume tajiri lakini jeuri na anayedhani pesa ni kila kitu kwake,utakuwa mtumwa



4. Akiringa huna haja ya kumbembeleza,kama ni udongo wote mmeumbwa kwa udongo asijifanye kuact kama ameumbwa special na utomvu wa mpapai....
One who loves you will listen and not cause drama for you to get hurt.Be strong and show him/her that you can manage yourself without him/her...Machozi yako ndio power yake ya kuendelea kukunyanyasa.Kujishusha kwako ndio mtaji wake kukuona wewe kama kinyago na takataka.Dont let anyone treat you lesser than what God made you to be.WAKE UP



5. 'baby come home',baby utaniletea chocolate?'babe nimekumiss'..
Kabisa mtu na akili zako unaandika status ya namna hii..Sijui ndo mahaba mapya au mapenzi ya kichina,si umtumie message???mpaka marafiki 5000 na dunia nzima wajue umemmiss babe kwenye wall?
Mapenzi ya simu ya kichina haya,Vibration ina kelele mpaka inafyeka nyasi...wape wiki 8 tu,'love sucks,''being single is better,''never mind i'll find someone lke you,Chinese love doesnt last long



6. Nyie wanawake,kuna baadhi yenu huwa mnajitafutia kuachwa nyie wenyewe!Mwanaume sio ATM ya Umoja Switch,unamtangazia shida zako zoteeeee mpaka anajuta kwanini alikutongoza.Yaani unadate na mtu anakutumia msg,Babe naomba unisaidie kitu kimoja,unajua Baba ameishiwa hela kabisa hapa home hapaeleweki please nisaidie hela'
Khaa!sasa mimi nilikutongoza wewe au nilitongoza ukoo wenu mzima???Babako kuishiwa hela mimi inanihusu nini??Mwambie akadai mafao ya Wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki!Kesho utasema unaomba hela shangazi anunue cherehani...Girls muwe serious,Mizinga kwa sasa ni adui namba moja wa mapenzi!!


7. Mapenzi ya Facebook
DAY 1-Mamboo
DAY 2-Mambo Dear.
DAY 3-Umeamkaje Baby
DAY 4-Babe kuna kitu ntakuomba
DAY 5-Baby can you help me with 200,000,nna shida ntakurudishia kabla ya Ijumaa..Mwanafunzi huyo,na hamjawahi kuonana...Laki 2,airudishe ndani ya mwezi,hata UPATU haizai fasta hivi..Ukijitusu umeumia.Unauchuna
DAY 6-Babe ulipata meseji yangu?Unapiga kimya
DAY 7-Nishagundua we Mwanaume suruali,hata laki 2 huna...We unayo??Ulidhani Mi Mwanaume Sketi???
Mnaonana humu,Mnapendana humu,Mnaachana humuhumu,tena kwa Kashfa..Yeu bora urudi tu,maana watoto wetu hawana wa kuwalea,wanaume na wanawake wote akili kushney



8. Miaka michache nyuma,Wanaume walikuwa wanalalamika sana vibomu vya kuombwa vocha,vocha ilikuwa gharama inayokera sana na kuboa maana kila siku iendayo kwa Mungu ni vocha..
Kumbe bora ingebakia Vocha,maana ina afadhali...Siku hizi,unapigwa mzinga hadi Simu yako inazimika kwanza maana haiamini kilichoandikwa..''Baby naomba laki8 ninunue iPhone simu yangu imeibiwa..dah,laki8 ni mshahara wa Walinzi 5 wa KK security wenye wake na watoto!Mama zao wenyewe wanaisikia tu iPhone wanajua ni Aina mpya ya Kitenge cha Wax...Balaa,hatuhemi,hatujengi,Love has become Article of Oenstation,kui-afford ni ngumu,come on DIVAS give us a break!



9. Mimi sikukatazi KUVAA MINI SKIRT,ila kabla hujaivaa ebu waulizee hata MAJIRANI kama kweli unaMGUU wa mini SKIRT coz wengine wanaovaa mpaka unawaonea huruma,au jiangalie basi hata kwenye KIOO KUBWA...!!      

Wednesday, November 7, 2012

Haki zaidi kwa wapenzi wa jinsia moja Ufaransa

Mipango ya sheria mpya itakayowaruhusu wapenzi wa jinsia moja nchini Ufaransa kuoana na kupata watoto inajadiliwa katika mkutano muhimu wa baraza la mawaziri la Rais Francois Hollande.
Ufaransa inaruhusu uhusiano wa pamoja kati ya wapenzi wa jinsia moja lakini rais wa nchi hiyo alioongoza jitihda za kuwaongezea haki zao kama sehemu ya kampeini yake ya uchaguzi mapema mwaka huu.
Sasa anakabiliwa na upinzani mkali kuhusu fikira hiyo kufuatia maandamano kote nchini na shutuma kutoka kwa kanisa katoliki.
Kwa wapenzi wengi wa jinsia moja, mabadiliko katika sheria hii yalipaswa kufanyika kitambo. Wanataka nafasi sawa kuwa na familia kama ilivyo kwa wapenzi wengine wa kawaida.
Katika sheria hiyo iliyopendekezwa, wapenzi wa jinsia moja wataruhusiwa kuasili watoto kwa pamoja.
Na kutakuwa na mabadiliko katika stakabadhi rasmi, ambapo mama na baba wataondolewa na badala yake kuwekwa mzazi wa kwanza na mzazi wa pili.
Lakini mabadiliko hayo yaliyopangwa yameshutumiwa vikali na wanasiasa wa mrengo wa kulia ambapo mmoja alisema huenda hili likachangia ndoa za wake au waume wengi.
Mswada huu utakapowasilishwa kwenye baraza la mawaziri, utajadiliwa bungeni ifikapo Januari.
Chama cha kisoshalisti cha Rais Hollande kina wingi wa wabunge wanaohitajika lakini kutokana na kuwepo mzozo huenda akawa anategemea kura zote kuhakikisha kuwa mswada huo utapitishwa na kuwa sheria

President Barack Obama wins re-election




President Barack Obama handily defeated Gov. Mitt Romney and won himself a second term Tuesday after a bitter and historically expensive race that was primarily fought in just a handful of battleground states. Networks project that Obama beat Romney after nabbing the crucial state of Ohio.

The Romney campaign's last-ditch attempt to put blue-leaning Midwestern swing states in play failed as Obama's Midwestern firewall sent the president back to the White House for four more years. Obama picked up the swing states of New Hampshire, Michigan, New Mexico, Iowa, Wisconsin, Pennsylvania, Minnesota, and Ohio. Florida and Virginia are still too close to call, but even if he won them, they would not give Romney enough Electoral College votes to put him over the top. Romney looks poised to do better in the overall popular vote.

The Obama victory marks an end to a years-long campaign that saw historic advertisement spending levels, countless rallies and speeches, and three much-watched debates.
The Romney campaign cast the election as a referendum on Obama's economic policies, frequently comparing him to former President Jimmy Carter and asking voters the Reagan-esque question of whether they are better off than they were four years ago. 

But the Obama campaign pushed back on the referendum framing, blanketing key states such as Ohio early on with ads painting him as a multimillionaire more concerned with profits than people. The Obama campaign also aggressively attacked Romney on reproductive rights issues, tying Romney to a handful of Republican candidates who made controversial comments about rape and abortion.

These ads were one reason Romney faced a steep likeability problem for most of the race, until his expert performance at the first presidential debate in Denver in October. After that debate, and a near universal panning of Obama's performance, Romney caught up with Obama in national polls, and almost closed his favoribility gap with the president. In polls, voters consistently gave him an edge over Obama on who would handle the economy better and create more jobs, even as they rated Obama higher on caring about the middle class.

But the president's Midwestern firewall--and the campaign's impressive grassroots operation--carried him through. Ohio tends to vote a bit more Republican than the nation as a whole, but Obama was able to stave off that trend and hold an edge there over Romney, perhaps due to the president's support of the auto bailout three years ago. Romney and his running mate Paul Ryan all but moved to Ohio in the last weeks of the campaign, trying and ultimately failing to erase Obama's lead there.

A shrinking electoral battleground this year meant that only 14 states were really seen as in play, and both candidates spent most of their time and money in those states. Though national polls showed the two candidates in a dead heat, Obama consistently held a lead in the states that mattered. That, and his campaign's much-touted get out the vote efforts and overall ground game, may be what pushed Obama over the finish line.

The loss may provoke some soul searching in the Republican Party. This election was seen as a prime opportunity to unseat Obama, as polls showed Americans were unhappy with a sluggish economy, sky-high unemployment, and a health care reform bill that remained widely unpopular. Romney took hardline positions on immigration, federal spending, and taxes during the long Republican primary when he faced multiple challenges from the right. 

He later shifted to the center in tone on many of those issues, but it's possible the primary painted him into a too-conservative corner to appeal to moderates during the general election. The candidate also at times seemed unable to effectively counter Democratic attacks on his business experience and personal wealth

OBAMA ASHINDA KWA KIPINDI KINGINE CHA MIAKA MINNE

 
 
Michelle Obama akionyesha upendo kwa mumewe baada ya ushindi wake.
 
Obama akitoa hotuba baada ya ushindi wake leo huko Chicago.
 
Akiwa na mkewe, Michelle, na binti zake Sasha (wa pili kulia) na Malia Obama wakisherehekea ushindi wake.
 
Obama ambaye pia ni Mkuu wa Majeshi, akiwa Ikulu ambako atakaa kwa miaka minne tena.
 
Familia nzima ya Obama ikifurahia ushindi.
 
Obama akitoa hotuba yake mbele ya umati wa watu huko Chicago.
 
Michelle Obama akiwa amepandwa ‘mzuka’ kwa ushindi wa Obama.
 
Mkutano wa Obama ulivyokuwa umepambwa kwa rangi mbalimbali za taifa hilo.
 
Mke wa Romney aitwaye Ann Romney, akimliwaza mumewe baada ya kushindwa.
                                                      Romney akiwashukuru waliompigia kura.
ALIYEKUWA mgombea wa urais wa Marekani kupitia chama cha Democratic, Barack Obama, amemshinda mpinzani wake kutoka chama cha Republican, Mitt Romney, katika uchaguzi uliofanyika jana.
Obama ambaye alishinda urais wa nchi hiyo miaka minne iliyopita, amesema hivi sasa ana dhamira ya hali ya juu zaidi na nguvu zaidi za kufanya kazi zake.  Aliyasema hayo huko Chicago wakati wa hotuba yake ya kupokea ushindi huo.
Hata hivyo, wagombea wote  wawili wa kinyang’anyiro hicho walitoa wito wa umoja kwa watu wa nchi hiyo kwa ajili ya maendeleo.
Katika hotuba hiyo alimshukuru mkewe na mabinti zake , Sasha na Malia, ambao alisema ni “wasichana wawili jasiri kama mama yao.”
Katika uchaguzi huo Obama alipata kura nyingi hususani katika majimbo ya  Ohio, Iowa, Wisconsin, Pennsylvania, New Hampshire na Virginia.
Kiongozi huyo alipongezwa haraka na viongozi wengine duniani wakiwemo David Cameron wa Uingereza na Benjamin Netanyahu.
PICHA KWA HISANI YA : REUTERS, AP, EPA, AFP/GETTY IMAGES , KEYSTONEUS-ZUMA/REX FEATURES

Matokeo ya uchaguzi wa urais nchini Marekani yameanza kutolewa kutoka maeneo mbali mbali ya nchi.
Rais Barack Obama ameshinda katika majimbo ambayo yalikuwa muhimu sana kubaini mshindi wa uchaguzi huu ambayo ni Michigan na Pennsylvania, pamoja na mengine ambayo alishinda katika uchaguzi wa mwaka 2008.
Mwenzake wa Republican Mitt Romney ameshinda katika majimbo mengine muhimu pia ya Republican pamoja na kushinda Indiana ambalo lilimuunga mkono Obama mwaka 2008.
Mamilioni ya watu walijitokeza kupiga kura siku ya Jumanne. Mshindi huenda akajulikana baada ya masaa kadhaa kuanzia sasa hususan huku matokeo katika majimbo mengine muhimu yakitolewa.
Kura za maoni kabla ya kufanyika uchaguzi huu zilionyesha kinyang'anyiro kitakuwa kikali ingawa zilimpa ushindi wa kura chache tu Rais Obama katika majimbo kadhaa muhimu.
Vituo vya kupigia kura vilianza kufungwa mapema katika maeneo ya Mashariki mwa nchi , huku majimbo ya Virginia na Ohio nayo yakifunga mapema.
Kwa sasa kura za Electoral College zinaonyesha Obama yuko nyuma ya Romney kwa kura sita

Thursday, November 1, 2012

RAIS KIKWETE AFUNGUA RASMI BARABARA YA MKUU ROMBO-TARAKEA

 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifurahia jambo na Mbunge wa Rombo Mhe Joseph Selasin katika hafla ya ufunguzi rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea leo Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea kabla ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea leo Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaidiwa na Mbunge wa Rombo Mhe. Joseph Selasini kukunjua pazia kama ishara ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea leo Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na Mbunge wa Rombo, Mhe. Joseph Selasini kukunjua pazia kama ishara ya kufungua rasmi  wa barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea leo Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na washika dau wa miundombinu wakikata utepe ishara ya kufungua rasmi barabara ya KM32 kutoka Mkuu Rombo hadi Tarakea leo Oktoba 30, 2012 kijijini Tarakea, wilaya ya Rombo mkoa wa Kilimanjaro ambako Rais Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku nne.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea katika moja ya maongezi yake na wananchi wakati alipokuwa akisimamishwa karibu kila kijiji wakati wa ziara yake Wilaya ya Same.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea katika moja ya maongezi yake na wananchi wakati alipokuwa akisimamishwa karibu kila kijiji wakati wa ziara yake Wilaya ya Same.
(PICHA NA IKULU)

RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA BARABARA YA KWA SADALA-MASAMA, WILAYANI HAI

 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Hai Mhe Novatus Makunga katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongezza  Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe  kwa hotuba nzuri ya kumkaribisha na kumsifia kwa kazi anayofanya katika maendeleo ya miundombinu nchini katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe L:eonidas Gama na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisaidiwa kuzindua jiwe la msingi  na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na kupewa shukurani  na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Miundombinu Mhe John Pombe Magufuli Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe L:eonidas Gama na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe wakikata utepe mojawapo ya magreda katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Miundombinu Mhe John Pombe Magufuli Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe Leonidas Gama na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe Freeman Mbowe katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Kilimanjaro  baada ya  uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisindikizwa  na Mbunge wa Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mwenyekiti wa CHADEMA, Mhe Freeman Mbowe kutoka katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani hai leo.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipongezwa na wananchi  katika eneo la sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Kwa Sadala-Masama wilayani Hai leo.
(PICHA NA IKULU)

WAKAZI WA DAR WAFURAHIA USAFIRI WA GARI MOSHI

 
Bi. Rose Ngauga akizungumza  na mwandishi wetu aliyemtembea ofisini 
kwake kujua mawili matatu kuhusiana na usafiri huo.
WAKAZI wa Jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake, wamefurahia kuanza kwa usafiri wa treni waliousubiri kwa muda mrefu ulioanza juzi.
 
Abiria wakigombea kupanda treni kutoka katikati ya jiji kueleke Ubungo.
Kamera yetu leo ilitua katika ofisi ya mkuu wa kituo kinachodili na usafiri huo, Bi. Rose Ngauga na kuzungumza mambo kadhaa kuhusiana na usafiri huo.
Ngauga alisema kuwa usafiri huo siyo nguvu ya soda kama inavyodaiwa na baadhi ya watu na kwamba utakuwa endelevu.
 
Wanafunzi wakipanda katika behewa lao maalumu tayari kwa safari.
 
Bi. Rose akimuonyesha mwandishi wetu (hayupo pichani) tiketi zinazotumika kwa abiria wa kawaida na wanafunzi.
 
Abiria wakiwa katika dirisha la kukatia tiketi.
 
Wanafunzi wakikata tiketi katika dirisha maalumu kwa ajili yao.
 
Kichwa cha treni kikiunganishwa na mabehewa kabla ya kuanza safari.
 
Abiria wakiwa wameketi ndani ya behewa wakisubiri kuanza safari.
 
Mkuu wa Kituo cha Reli, Bi. Rose Ngauga akikagua mabehewa kabla ya 
gari moshi kuanza safari leo saa 9.40 alasiri.
akikabidhiwa ripoti.
 
Gari moshi likiwa katika mwendo na baadhi ya abiria wakionekana wakichati na simu.
 
Mwandishi mwanadamizi wa Global Publisher, Haruni Sanchawa  akishuka kutoka katika treni hiyo  maeneo ya Ubungo Maziwa ambako treni hiyo umalizia safari yake.
 
Abiria wakishuka kwenye treni.

Pamoja na usafiri huo kuanza, mafundi wa shirika la reli bado wanaendelea na ukarabati  wa reli kama wanavyoonekana pichani.

New