My Web

Emmanuel

CONTACT

Wednesday, December 18, 2013

Kuna mfano wa Mandela duniani

Nelson Mandela daima alitajwa kama 'kiongozi mkongwe wa dunia' ambaye alikuwa na ujuzi wa kutatua matatizo ya kidunia. Sifa yake ya madili mema ilimfanya kuonekama kama mrithi wa Mahatma Gandhi. Nani sasa anaweza kuchukua majuku ya Mandela?
Maswala ya Lockerbie, Burundi, DR Congo, Lesotho, Indonesia, Israel-Palestine, Kashmir, Mauaji ya Stephen Lawrence, uhamasisho wa Ukiwmi na kombe la dunia.
Orodha ya mambo aliyoyaweka karibu naye Mandela ni ndefu.
Katika baadhi ya mizozo kama mgogoro wa muda mrefu nchini Burundi alikuwa mpatanishi.
Maswala kama Ukimwi, alikuwa mwanaharakati na baba aliyepoteza mwanawe kwa maradhi hayo.
Mchango wake ulikubalika na ukakaribishwa sana.
Alipinga kuingiliwa kati mzozo wa Kosovo mwaka 1999 na kukosoa sera ya kigeni ya Marekani, wakati huo uhusiano wake na Kanali Gadaffi na aliyekuwa Rais Suharto haukuchukuliwa kwa wema.
Wengi walihisi kuwa alichelewa katika harakati zake dhidi ya ukimwi nchini Afrika Kusini.
Lakini wakosoaji wake wanakubali kuwa alikuwa kiongozi asiyekuwa na mfano wake duniani.
Alikuwa kiongozi ambaye watu walikuwa na matumaini naye, mtu ambaye alitoa mfano wa kuigwa duniani.
Mandela alionekana kama mtu aaliyweza kukabidhiwa majukumu na kuyafanya kwa kuzingatia ukweli kwani safari yake Jakarta ambako mwanasiasa wa Timor Mashariki alikuwa amezuiliwa mwaka 1997 ilipelekea kufanyika kwa kura ya maoni na kuachiliwa kwa mfungwa huyo Gusmao miaka miwili iliyofuata.

Viongozi walioachiwa jukumu la Mandela

  • Martti Ahtisaari
  • Kofi Annan (Mwenyekiti)
  • Ela Bhatt
  • Lakhdar Brahimi
  • Gro Harlem Brundtland
  • Fernando H Cardoso
  • Jimmy Carter
  • Hina Jilani
  • Graca Machel
  • Mary Robinson
  • Ernesto Zedillo
  • Desmond Tutu

Alikuwa na maadili ya hali ya juu sana ambayo yanaweza kuwa funzo kwa wanasiasa wote duniani wasiokuwa na mwelekeo mwema na yote yalitokana na vita vyake dhidi ya utawala wa kibaguzi miaka ya themanini.
Kumekuwa na marais wengine wakongwe lakini wao walikuwa watu ambao siasa zao zilihusu maswala ya ndani ya nchi zao.
Mfano Jimmy Carter alitumwa Korea Kaskazini kuzungumzia maswala muhimu na pia amekuwa akijihusisha na maswala ya demokrasia barani Afrika lakini hana hisia alizokuwa nazo Mandela kuhusiana na maswala kadhaa kama Mandela alivyokuwa.
Tony Blair alijaribu kujihusisha na juhudi za upatanisho Mashariki ya kati lakini wengi waliona kama alikuwa anajaribu kujifutia historia mbaya aliyo nayo kuhusu vita vya Iraq.
Lakini jambo ambalo litasalia vichwani mwa wengi ni Mandela alipoamua kutangaza kuwa mwanawe amefariki kutokana na Ukimwi mwaka 2005. Hii ilikuwa mapema wakati ambapo Ukimwi ulikuwa umekuwa donda sugu Afrika Kusini. Mandela aliwataka wananchi wa taifa hilo kuweka wazi maswala ya Ukimwi.
Unaweza kwenda popote duniani na picha yake na hakuna asiyemfahamu . Hakuna mfano wa Mandela. Aung San Suu Kyi labda kidogo anaonekana kuwa kama Mandela lakini sio rahisi kwake kutambulika kama alivyotambulika Mandela.
Gandhi, Mandela na Suu Kyi walikuwa wafungwa wa kisiasa na kujitolea kwao kwa jamii ilikuwa sehemu kubwa ya maisha yao.
Wakati wa sherehe za kuzaliwa kwake alipokuwa na umri wa miaka 89, Mandela alibuni kikundi cha viongozi wakongwe aliowataka kuendeleza amani duniani.
Dunia inahitaji mtu mpole, mkarimu na wa kujitolea. Bila ya watu kama Mandela kuna uwezekano wa dunia kutumbukia katika migogoro ambayo haitapata wasuluhishi na kwa mtizamo wa wengi ni vigumu kupata mfano wa Mandela duniani.

AIR TANZANIA YARUDISHA SAFARI ZA NDEGE ZA KWENDA BURUNDI

 
Meneja Rasilimali watu kutoka Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), Eliezer Mwasele, akishuka kutoka ndani ya ndege mara baada ya ndege ya Air Tanzania kutua wakati wa uzinduzi wa safari za kwenda Bujumbura- Burundi. Nyuma yake ni aliekuwa Balozi wa Tanzania Burundi, Francis Mndolwa.
 
Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dk. James Nzagi (kushoto) akiwa na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Francis Mndolwa (wa pili kushoto) mara baada ya kupokea ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania, Air Tanzania, iliyoanza sarai za kwenda Bujumbura mwishoni mwa wiki. Wengine mbele ni baadhi ya mawaziri wa serikali ya Burundi.
 Baadhi ya abiria wakipanda ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania –Air Tanzania- kabla ya kuanza safari ya kuelekea Bujumbura –Burundi, wakati wa uzinduzi wa safari hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki.
 Baadhi ya viongozi wakisindikiza abiria walioshuka kwenye ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania –Air Tanzania- mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Bujumbura- Burundi kama ishara ya uzinduzi rasmi wa safari hizo. Kutoka kushoto ni Waziri wa Burundi wa Afrika Mashariki, Bi Nziyemana Leontine akifuatiwa na Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dk. James Nzagi na aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Francis Mndolwa.
Air Tanzania yarudisha safari za ndege za kwenda Burundi
·       Waanza safari za kwenda Mbeya
·       Warejesha safari za Mwanza

SHIRIKA la Ndege la Tanzania (ATCL) limezindua rasmi huduma za usafiri wa anga kutoka Dar es Salaam kuelekea Bujumbura, Burundi kwa kupitia mkoani Kigoma, safari hizo zitafanyika mara tatu kwa wiki yaani Jumatano, Ijumaa na Jumapili.
Hatua hiyo imekuja baada ya hali ya amani kutengamaa katika nchi hiyo ya Burundi ambayo ilikumbwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuilazimu Tanzania kusitisha huduma hizo kwa muda wa miaka 20.
Wakati huo huo, ATCL pia imeanza safari za Dar es Salaam kwenda Mbeya, safari hizo zitafanyika mara nne kwa wiki yaani Jumatatu, Jumatano, Ijumaa na Jumapili. imerejesha safari za Dar es Salaam – Mwanza kila siku, safari  zilizoanza rasmi Jumapili iliyopita.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Bujumbura Burundi katika uzinduzi wa huduma hizo juzi, Meneja Rasilimali watu wa Shirika hilo la ndege, Ndugu Eliezer Mwasele, alisema uzinduzi wa safari hizo utakuwa ni njia mojawapo ya kuchochea maendeleo ya uchumi kwa nchi zote mbili.
Alisema kutokana na hali hiyo Watanzania wanatakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika nchi hiyo ya Burundi, kwani asilimia kubwa ya wafanyabiashara wa nchi za Kongo na Burundi wanatarajiwa kuanza kutumia usafiri huo kwa wingi.
Akizungumzia hatua hiyo, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Dk. James Nzagi, alisema kuanza kwa safari hizo ilikuwa ni ndoto ya siku nyingi ambayo aliipigania na kutamani kuona wananchi wa pande zote mbili wananufaika kwa pamoja.
“Tumefurahi sana kwa kutimiza ndoto hii leo (juzi), kwa sababu sasa uhusiano kati ya nchi hizi mbili unazidi kuimarika hasa ukizingatia tunategemena kibiashara kulingana na fursa zilizopo.
Kwa upande wake, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Francis Mndolwa, alisema kwa kuwa ATCL imefunga mkanda na kuanzisha tena safari hizo, ni vyema ikazingatia muda na kuhakikisha huduma stahiki zinatolewa ili kukuza shirika hilo.
Naye Waziri wa Burundi katika Bunge la Afrika Mashariki, Nziyemana Leontine alisema, “kuanzishwa kwa Air Tanzania kuja Burundi, kutasaidia wananchi wa Burundi, hususani wafanyabiashara kwani walikuwa wanaunganisha ndege kupitia nchi nyingine, lakini sasa hivi wananchi watakuja moja kwa moja. Tunashukuru sana,” alisema.
Naye mmoja wa abiria kutoka Burundi waliopanda ndege hiyo, Dk. Owera Kodime, alisema, kuanzishwa kwa safari hizo kutawapunguzia sana gharama za usafiri wananchi wa Burundi, kwa sababu Tanzania imepunguza gharama kuliko mashirika mengine.
“Tulikuwa tukitumia muda mrefu sana kuzunguka lakini sasa tutaweza kuja moja kwa moja Dar es Salaam, ni hatua nzuri ambayo imetuletea faraja sana Warundi,” alisema.
Kwa upande wa abiria kutoka Tanzania, Joseph Kisaro, alisema, “ Muda mrefu sana kulikuwa hakuna huduma, tangu mwaka 1993 huduma zilikatatika, lakini uongozi wa Tanzania umefanya juhudi baada ya mapigano kuisha. “Tunashukuru ubalozi ulioteuliwa mwaka 2003 kwani ulianza harakati haraka za kurudisha huduma hizi ambazo sasa tumefanikiwa.
“Tunaomba uongozi wa ATCL uangalie pia kuwa na safari za kuelekea Kongo mashariki kwa sababu kuna abiria wengi sana ambao ni wafanyabiashara wanaokuja Tanzania,” alisema

Mama Vicky Nsilo Swai Alipomrudishia Viatu Alivyoviacha Tanzania Rais wa kwanza Mzalendo na Mpigania Uhuru wa Afrika Kusini, Nelson Mandela ‘Madiba’

 Rais wa kwanza Mzalendo na Mpigania Uhuru wa Afrika Kusini, Nelson Mandela ‘Madiba’ akiwa ameshikilia viatu vyake ambavyo aliviacha nyumbani kwa Mzee Nsilo Swai alipoingia Tanzania kwa mara ya kwanza mwaka 1962 akitokea Afrika Kusini.



Mandela aliahidi kuvichukua viatu hivyo pindi atakaporejea Tanzania lakini katika safari hiyo ndipo alipoishia mikoni mwa makaburu wa Afrika Kusini na kumfunga kwa miaka 27.



Viatu hivyo aina ya Buti vilihifadhiwa hadi alipotoka na kukabidhiwa kwa Mandela na mjane wa Mzee Nsilo Swai, Bi Vicky Nsilo Swai (pichani kulia) mwaka 1995 Mandela alipotoka gerzani na hatim,aye kuwa Rais wa kwanza Mweusi wa Afrika Kusini.

New