My Web

Emmanuel

CONTACT

Saturday, December 31, 2011

Dhana hizi zinawaharibia wanawake kimapenzi 4

Wiki hii tunaendelea na sehemu nyingine ya mada yetu ya dhana zinazowaharibia wanawake kimapenzi ikiwa ni mwendelezo wa pale tulipoishia wiki iliyopita.

Ukiacha mateso ya Janette baada ya kutoswa na Mully aliporudi mara ya pili, Jambo la kuzingatia ni jinsi alivyomtenda boyfriend wake aliyekuwa anamhudumia na kwenda kuangukia kwa mwanaume ambaye ni mume wa mtu. Hakutafakari mwenye faida kwake ni nani, leo anahangaika.

Aina ya wanawake kama Janette ndiyo wanaosababisha wanaume watambe mitaani wakitoa maneno ya kebehi kwamba wanawake wote mwalimu wao ni kipofu. Hakutambua jema wala hakujua kwenye maisha haya anahitaji nini.

Mtu anayejihusisha kimapenzi na mume au mke wa mtu, maana yake hajui kesho yake ni nini.

Mully ni mmoja wa waathirika, wapo wanaume wengi waliotendwa na wapenzi wao ambao waliwalea na kutumia fedha nyingi kuwasomesha. Mambo yao yalipokaa sawa na kupata kazi, wakasahau walipotoka na kuanzisha uhusiano na wengine. Kipya kinyemi, mume aliyemsomesha akatupwa mbali.

Janette na wengine wenye tabia za namna hiyo ni mwendelezo wa dhana zinazowaharibia wanawake kimapenzi. Wanatakiwa wajirekebishe ili mambo yakae sawa. Wasiwaponze wengine wenye tabia safi, wenye akili hai za kulea familia yenye mafanikio tele.

Ipo dhana nyingine kuwa mwanamke akipendwa sana, hujenga kiburi na matokeo yake humdharau mwanaume anayeonesha mahaba ya ndani kabisa. Kwamba anaweza kumgeuza mwanaume punda kwa sababu tu anajua anampenda.

Hachukulii upendo ni tunu, yeye anaubeba kama fimbo ya kuchapia.

Nimeshakutana na watu kadhaa, wananieleza matatizo yao na jinsi walivyoshauriwa na watu mbalimbali. Mathalan, mtu mke wake anamsumbua, anamueleza mshauri kila kitu kinachozunguka mgogoro ndani ya familia yake. Mwisho katika kushauriwa anaambiwa: “Tatizo, umemuonesha mkeo unampenda sana.”

Je, kumuonesha mtu kuwa unampenda ndiyo igeuke adhabu kwako? Ni wazi kuwa mapenzi ya siku hizi, yanatawaliwa na nguvu kubwa ya shetani ndiyo maana tafsiri yake inakosewa. Ukweli wa mapenzi ni kuwa wawili wanaoamua kupendana ni lazima upendo wao uwe wa ndani ya nyoyo zao na waudhihirishe kwa vitendo.

Ni mateso kujilazimisha kuficha mapenzi, eti unahofia ukimuonesha atajua na atakufanyia vitimbi. Kufanya hivyo ni mateso, bora kutopenda kabisa. Inatupasa kupendana bila kuwa na shaka yoyote ndani. Kila mtu ausikilize moyo wake namna unavyomuongoza na atende pasipo kuhofia kuitwa Bushoke.

Wakati nashauri kwa watu kuruhusu nyoyo zao ziwaongoze katika kudhihirisha mapenzi yao bila kuogopa jinsi watakavyochukuliwa na jamii, ni vema nikatoa angalizo kwa wale wanaooneshwa mapenzi, kuheshimu hisia za wenzao. Maisha ya sasa, kupata mtu anayekupenda, anayekujali na kukuheshimu kwa dhati, ni bahati.

Ukigundua ni bahati, basi ni vizuri kuitunza kwelikweli, vinginevyo unaweza kuichezea, ukaipoteza, matokeo yake ni kujuta baadaye. Usimfanye mwenzi wako ashindwe kukuonesha penzi la dhati. Mpe uhuru na amani juu yako. Mpokee vizuri, zungumza naye kwa lugha tamu ili ajisikie kuwa nawe.
Ni vipi mwenzio kwa mapenzi aamue kukununulia zawadi aliyoona inafaa, wewe kwa sababu unamdharau kutokana na jinsi anavyokupenda kupitiliza, unaitazama kwa nyodo kisha unapotezea. Husemi hata asante. Inawezekana inakuvutia lakini hutaki tu kumuonesha kwa sababu unamuona katuni, kisa anakupenda kupitiliza.
Mwenzio ametulia, anaona akutoe ‘auti’, mwende sehemu mkapate chakula cha jioni. Hisia zako za dharau juu yake, iliyotokana na mtazamo kuwa anakupenda mpaka kero, unaamua kukataa bila sababu: “Sitaki tu kwenda, acha nipumzike nyumbani.”

Dar LIve

Na Luqman Maloto
Baada ya tafsiri iliyotawala muda mrefu kuwa Wilaya ya Temeke, ipo nyuma katika mambo ya burudani ndani ya Jiji la Dar es Salaam, sasa hivi imekuwa tofauti kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa ukumbi mkubwa wa kisasa wenye hadhi ya kimataifa unaoitwa Dar Live.
Ukumbi huo ambao ni wa kwanza kuwahi kutokea ndani ya Dar es Salaam na Tanzania kwa jumla, umejengwa eneo la Mbagala, Zakhem, wilayani Temeke.
Dar Live, umejengwa na Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd ambayo imejipatia umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi katika sekta ya habari na uandaaji wa matamasha makubwa kama vile, Mfalme wa Rhymes, Champions Day na mengineyo, bila kusahau lile la kuhamasisha uzalendo kwa Watanzania lililofanyika hivi karibuni.
Akiutambulisha ukumbi huo kwa waandishi wa habari juzi, Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdallah Mrisho, alisema kuwa Dar Live ni ukumbi wa aina yake, utakaojishughulisha na utoaji wa huduma za matamasha ya muziki, disko, sherehe za harusi, michezo ya watoto, mikutano na vinywaji.
Alisema, ukumbi huo ni fahari ya Mbagala na Temeke yote, hivyo aliwataka wakazi wa eneo hilo kuanza kujivunia, kwani sasa watakuwa wanapata burudani ya uhakika nyumbani, tofauti na mwanzo walipokuwa wanalazimika kufunga safari hadi Wilaya za Kinondoni na Ilala.
“Pamoja na uwepo wa vifaa vya huduma za michezo ya watoto, kingine ni kwamba Dar Live tumefunga jukwaa kubwa la kisasa la kudumu. Jukwaa ambalo linakidhi mahitaji ya shoo yoyote ya kimataifa.
“Jukwaa limekamilika, lina taa za kutosha, sound (muziki) yenye ujazo mkubwa. Siyo kama kumbi nyingine ambazo hulazimika kukodi majukwaa na muziki. Dar Live imekamilika kila idara. Pamoja na yote hayo, pia kuna bwawa la kuogelea,” alisema Mrisho.

WANAMUZIKI WAKUBWA KUPAMBA UZINDUZI
Mrisho alisema kuwa Dar Live utazinduliwa Januari Mosi, 2012, kuanzia saa 4:00 asubuhi na sherehe za uzinduzi zitakamilika saa 6:00 usiku.
Alisema, kufanikisha uzinduzi huo, wanamuziki wakubwa nchini, watafanya shoo kubwa, itakayoendana na hadhi ya ukumbi wenyewe.
Aliwataja wanamuziki watakaotumbuiza siku hiyo kuwa ni Juma Kassim Kiroboto ‘Sir Nature’ na Kundi lake la Wanaume Halisi, mkongwe Joseph Haule ‘Prof. Jay’, Kundi la Gangwe Mob likiongozwa na Haroun Kahena ‘Inspector’ pamoja na vijana chipukizi wakali wa Kundi la JNY Unit.
Aliongeza, kwa upande wa dansi, Bendi ya Extra Bongo ‘Wazee wa Kizigo’, ikiongozwa na Ali Choki ‘Mzee wa Farasi’ itafanya kazi nzuri ikiwatumia rapa Saulo John ‘Ferguson’, wanenguaji Aisha Mbegu ‘Madinda’, Hassan Musa ‘Nyamwela’ na wengine wengi.
Kwa upande wa burudani ya Taarab, Mrisho alisema kuwa Kundi la Jahazi Modern Taaarab, likiongozwa na Mfalme Mzee Yusuf, litasababisha mirindimo ya Pwani.
Mrisho alitaja viingilio vya siku hiyo kuwa ni shilingi 10,000 kwa VIP, kawaida ni shilingi 5,000 na shilingi 1,000 kwa watoto.
“Watoto wao watafurahia uzinduzi kuanzia asubuhi mpaka saa 12:00 jioni, watu wazima wao kazi kwao kusherehekea matunda ya Dar Live mwanzo mwisho,” alisema Mrisho.
Kuna la ziada? Mbagala wapewe nini wakati wao kesho ndiyo Alfa na Omega?

wolper ala Kristmasi kitandani

Na Erick Evarist

Sura ya mauzo kunako Bongo Movie, Jacqueline Wolper amejikuta akila Sikukuu ya Krismasi kitandani baada ya kushindwa kujikinga na ‘anopheles’ mdudu anayeambukiza ugonjwa wa Malaria.

Habari kutoka kwa mtu wa karibu na nyota huyo zinasema Wolper alibanwa na homa hiyo kiasi cha kushindwa kutoka nje hivyo kuisikia sikukuu kwenye redio tu.

“Duh! Jamani shosti ‘angu ameshindwa ku-enjoy sikukuu na hivi ninavyomjua anapenda kujiachia, lo!” alisema rafiki wa karibu wa Wolper.

Akizungumza kwa tabu kwa njia ya simu na paparazi wetu, Wolper alikiri ‘kupigwa’ na malaria siku hiyo na kudai kwa sasa hajambo, anaendelea vizuri baada ya kutumia dozi.

“Kwa sasa naendelea vizuri kwa kweli, namshukuru Mungu, lakini nilikuwa hoi sikukuu yote hii,” alisema Wolper.

Diamondi

Na Luqman Maloto

Ushamba wa mapenzi alionao dogo ‘mgonjwa’ wa warembo, Naseeb Abdul ‘Diamond’ (pichani), umekwenda hatua mbaya zaidi, alichokifanya Uingereza hivi karibuni, kimeshusha thamani yake kutoka geji hafifu hadi sifuri.

Akiwa Uingereza, Diamond alibwabwaja maneno ‘mbofumbofu’ ambayo siyo tu kwamba yalimfanya azomewe jukwaani, bali pia yaliwadhalilisha warembo wenye majina makubwa Bongo, Wema Sepetu na Jokate Mwegelo.

Inadaiwa kuwa Diamond akiwa katikati ya shoo kwenye ukumbi mmoja jijini London, alisimamisha muziki halafu akawaambia mashabiki waliohudhuria, wamchagulie mpenzi wa maisha yake, kati ya Wema na Jokate.

Madai yanaanikwa kwamba kitendo hicho, kiliwakera mashabiki ambao walilipuka na kumzomea, huku wengi wakimponda kwa kumwita limbukeni wa mapenzi, anayetumia umaarufu wake vibaya kuwachezea warembo.

Mashabiki mbalimbali wametoa maoni kwamba kauli ya Diamond kuwa hamjui mpenzi wake kati ya Wema na Jokate, inatosha kuchangamsha ubongo wa warembo hao ili wajivue gamba mapema na endapo wataendelea naye, basi nao wataonekana ni sifuri.

Dongo hilo la mashabiki, linanogesha kama siyo kusherehesha msemo kuwa mia halali kitanda kimoja na nunge, siku zote ziro huchangia shuka na sifuri kwa sababu ndiyo wanaofanana kuanzia thamani mpaka umbile.

Kwa upande mwingine, kauli ya Diamond imeibua mjadala mkubwa kwenye mitandao mbalimbali, huku kipande cha video, kinachomuonesha ‘dogo huyo mpenda sifa’ akibwabwaja jukwaani kikisambazwa kwa fujo kupitia intaneti na kuchangiwa maoni ya kufuru.

Kuweka pamoja maelfu ya maoni yaliyotumwa, wachangiaji wamemwita Diamond ni mchafuzi wa watoto wa kike, hana mapenzi ya kweli, gusa unate, mkuki popote na mengineyo ambayo hayana tafsiri nzuri kwa ‘dogo huyo’ aliyekulia Tandale, Dar.
Promota mmoja wa Uingereza (jina tunalo), aliliambia gazeti hili kuwa alipanga kumpa shoo tatu Diamond katika majiji ya Leads, Swansea na Leiceste lakini aliahirisha baada ya kuona amewachafua mashabiki na hakubaliki tena.

NI TUSI KUBWA KWA WEMA
Oktoba 2, 2011, Diamond kwa utashi wake, bila kulazimishwa, alijishaua kumvisha pete ya uchumba, Wema ambaye ni staa wa filamu mwenye taji la Miss Tanzania 2006-07.

Diamond, alimvalisha pete Wema na kuahidi kufunga naye ndoa katika tukio kubwa la shoo ya siku yake ya kuzaliwa, iliyochukua nafasi ndani ya New Maisha Club, Masaki, Dar es Salaam.

Wakati Diamond anautangazia ulimwengu kuwa Wema ndiye mke wake mtarajiwa, Jokate ambaye ni Miss Tanzania namba mbili 2006-07, alikuwepo.

Kwa mujibu wa watoa maoni, tusi kwa Wema ni kuwa kumbe alivishwa pete kanyaboya isiyo na mapenzi ya moyoni, kama ni mpira, basi alipangwa kikosi cha kwanza kwa ajili ya kumshikia nafasi mchezaji mwenye namba yake.

UKWELI NI UPI?
Jokate anaendelea kusisitiza kwamba hajawahi kukwea kitandani na Diamond, isipokuwa yupo karibu na ‘bwa mdogo’ huyo mpenda wa’mama kwa ajili ya kazi tu.

Wema anadai anao ushahidi kuwa Jokate kaanguka dhambini, wakati huo huo Diamond naye anajichetua ili aonekane kidume cha mbegu kwa kuomba mashabiki wamchagulie anayefaa.

HESHIMA YA JOKATE
Kabla ya tukio hilo, Jokate ni mrembo maarufu ambaye heshima yake kwenye jamii ilikuwa juu kutokana na jinsi alivyoendesha mtindo wa maisha yake.

Tathmini inaonesha kuwa tangu alivyoanza kuhusishwa kutoka kimapenzi na Diamond, heshima yake imepungua, huku watu wengi wanaompenda wakisema kwamba mrembo huyo ameingia ‘chaka’.

Kitendo cha Diamond kumuweka mezani na Wema, kisha kumchezesha bahati nasibu kama atashinda au la, kimezidi kuporomosha heshima ya Jokate.

Mrembo huyo ambaye amekuwa akifanya kazi nyingi za harakati, ameshauriwa kuwa hadhi yake ni kubwa, hivyo haipendezi kugombania sadakalawe na Wema ili kumpata Diamond.

KUTOKA RISASI
Wema na Jokate, kama kuna makosa ambayo mmefanya ni wakati wenu kujisahihisha. Mungu amewajaalia vipaji na nyota za umaarufu, haivutii mkatumiwa bila heshima mithili ya vitanda vya nyumba za kulala wageni.

Maisha yenu ni mazuri endapo mtaamua kushika yenye faida. Kwa Diamond, vema akajikosoa, umri wake ni mdogo, kwa hiyo anatakiwa kuzingatia kwamba anaweza kuzunguka mabucha nyama ni ileile. Akidanganywa na ujana, fainali uzeeni.

Kasheshe BBM

Na Mwandishi Wetu

Ujio wa mtandao mpya wa kijamii kupitia simu za mkononi aina ya BlackBerry almaarufu BBM, sasa umezua kasheshe miongoni mwa mastaa wa Bongo waliojisajili kwenye huduma hiyo.

Kasha la upekuzi wa gazeti hili limesheheni habari mbichi za hivi karibuni kuwa, chokochoko, ugomvi na kumalizana kistaa, shetani wake ni meseji za umbeya zinazotundikwa na wadau wa mtandao huo.

UNATAKA KUJUA ZAIDI?
Habari zisizokuwa na chenga kutoka kwa baadhi ya wanachama wa BBM zinafafanua hivi: “Mtandao huu unawachonganisha sana mastaa na hasa akina dada, utakuta mtu anakutungia jambo na kuliweka kwenye ukurasa wake, lengo likiwa ni kukuharibia.

“Wanaosoma posti hiyo ya umbeya wanaamini, wanaanza kukutukana au kukudhalilisha, matokeo yake ni kuwekeana bifu zisozokuwa na msingi,” alisema Jane Abbas, mtumiaji wa BBM ambaye pia ni mwigizaji chipukizi.

VIONJO VYA MESEJI ZA BBM
Hakuna ubishi kwa sababu, timu ya Gazeti la Risasi mchanganyiko imeshuhudia baadhi ya meseji za vijembe vya baadhi ya mastaa zikisomeka: “Msanii maarufu hawezi kuishi Manzese (eneo moja jijini Dar). Usipende kuiga tembo we mwanamke. Mzuri atakuwa yeye?”

Inaelezwa kuwa maneno yenye sura hiyo huwa ni sawa na dongo gizani, atakayelia na kujibu kwa jazba ujue ujumbe umemgusa na kutoka hapo mtafutano wa kitemi huanza safari zake.

HITIMISHO
Mbali na matumizi hayo mabaya ya mtandao huo, wapo baadhi ya watu ambao hutumia BBM kuhabarishana ishu za kijamii na hivyo ‘kuwakipu bize’ muda mwingi. Mfano ni picha za ukurasa wa mbele ambazo mastaa walipigwa siku moja wakati Irene Uwoya akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa yaani birthday.

Tuesday, December 20, 2011

Babu miaka 7 jela

Na Makongoro Oging’

Mchungaji Ambilikile Masapile ‘Babu Ambi’ wa Samunge, Loliondo, Arusha, atapanda kizimbani kukabili kesi za madai na jinai, hii ni kwa mujibu wa wakili maarufu, Mabere Nyaucho Marando.

Wakili huyo alisema, endapo mahakama itamkuta na hatia ya kutenda jinai, Babu Ambi, anaweza kuhukumiwa kifungo kisichopungua miaka saba jela.

Marando alisema, kesi ya jinai ambayo Babu Ambi anafunguliwa ni ile ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kwamba aliwahadaa watu kuwa dawa yake inatibu, wakati hakuna mtumiaji aliyepona.

Aliongeza kuwa kesi ya madai, inafunguliwa kwa sababu anatakiwa alipe fidia za watu waliopoteza maisha na wote waliosafiri kutokana sehemu mbalimbali wakitumia gharama kubwa kwa dawa isiyotibu.

Marando alifafanua, Babu Ambi, anaweza kukumbana na kifungo hicho endapo atakutwa na hatia kutokana na sheria ya jinai namba 302.

“Nipo makini na suala hili, hawezi kupona, nitasimamia kesi na tutamfunga,” alisema Marando na kuongeza:

“Nina taarifa nyingi kuhusu watu waliokufa, hakuna aliyepona.

Mazingira ya kisheria, yanatoa picha rahisi kuwa Babu atakutwa na hatia.”

Kutokana na msimamo huo, Marando aliwataka wale wote waliotibiwa na Babu Ambi lakini hawakupona, waende kwake kwa sababu amedhamiria kuisimamia kesi hiyo.

“Kiukweli babu aliwadanganya watu kuwa anatibu magonjwa sugu, lakini watu walipokwenda na kupata kikombe, hawakupona, na hawezi kuthibitisha mahakamani kuwa dawa yake imethibitishwa na serikali kuwa inatibu magonjwa aliyoyasema,” alisema Marando.

Aliongeza kuwa yupo tayari kuandaa kesi hizo na ndugu wote waliokunywa dawa na hawakupona, wanaweza kwenda kwake ili wakusanye ushahidi wa kutosha.

“Ni jambo linaloumiza, nitasimamia kesi hiyo na nitahakikisha anafungwa si chini ya miaka saba kama sheria inavyosema...ama zake ama zetu, alisababisha wagonjwa wa Ukimwi kuacha kutumia ARV, wengine wakatoroka hospitalini kwenda kwake na wengi wamepoteza maisha,” alisema Marando.

Wakili huyo aliigeukia serikali na kuilaumu kwa kumruhusu Babu kuwapa dawa watu wakati ikijua kuwa ilikuwa haijafanyiwa majaribio ya kitaalamu kujua kuwa kama inatibu au la.

Alisema anaweza kumfungulia kesi ya madai mchungaji huyo kwa kuwa wagonjwa wengi waliuza mali au kuchukua akiba zao na kusafiri hadi Samunge wakijua kuwa watapona baada ya kunywa dawa yake.

“Badala ya kupona wengi walifariki dunia huku wengine wakibaki masikini na hawajapona kutokana na udanganyifu mkubwa uliofanywa na Babu huyo na sasa hawawezi tena kupata mali nyingine,” alisema Marando.

Mwanasheria mwingine, Dk. Ngali Maita alipohojiwa kwa simu alisema atakuwa tayari kumsaidia mawazo ya kisheria Marando ikiwa atahitajika kwa kile alichodai, Babu alidanganya watu kuhusu tiba ya kikombe.

“Ni kitu kibaya sana alifanya Babu wa Loliondo, amesababisha maafa makubwa kwa jamii na mbaya zaidi hadi sasa uchunguzi wa dawa yake upo gizani, serikali haisemi chochote licha ya kuahidi wananchi kuwa watataarifiwa… hii ni mbaya na ni hatari,” alisema Dk. Ngali.

WAGANGA WA DAR
Kwa upande wa Mwenyekiti wa Chama cha Waganga wa Tiba Asilia jijini Dar es Salaam, Maneno Tamba alisema alishangazwa sana na serikali kumruhusu Babu kufanya tiba bila kufuata sheria ya tiba asili ya mwaka 2002.

“Sifa za kutibu kiasili zimebainishwa na sheria, kwamba pamoja na sheria nyingine mtoa dawa ni lazima awe chini ya mganga wa jadi kwa miaka mitatu ndipo anaweza kusajiliwa.

Je, Babu alisajiliwa? Inafaa ashitakiwe,” alisema Tamba.

TAMOPHA
Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi Tanzania (Tamopha), Julius Kaaya alilithibitishia gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita alipohojiwa kwa njia ya simu kuwa, wanachama wake 14 waliopelekwa kwa Babu kutibiwa kwa majaribio, hakuna hata mmoja aliyepona.

ALICHOSEMA BABU
Babu wa Loliondo alijipatia umaarufu mapema mwaka huu baada ya kutangaza kwamba amezungumza na Mungu kwenye ndoto na kumuonesha dawa inayoitwa Mugariga inayotibu Ukimwi, Kisukari, Moyo, Kifafa na magonjwa mengine sugu.

Mchungaji Masapila alisema dawa yake ambayo ni dozi ya kikombe kimoja ilikuwa na gharama ya shilingi 500, hali iliyofanya maelfu ya watu wakiwemo mawaziri, wabunge na wafanyabiashara kwenda kwake huku wakitumia magari na wengine kukodi helikopta.

Hivi sasa idadi ya wagonjwa wanaokwenda kutibiwa huko ni ndogo sana na Babu anadai hali hiyo imetokana na kupigwa vita na baadhi ya viongozi wa dini na waganga wa jadi.


SAkata la ukosefu wa Mafuta Dar

Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwa kwenye foleni ya mafuta katika Kituo cha Mafuta cha Bamaga, Mwenge jijini.

Jamaa huyu anaonekana akilalamika akiwa kwenye foleni hiyo.

Baadhi ya madumu ya kuchukulia mafuta yakiwa yamepangwa kwenye foleni na wateja, tayari kwa kutiwa mafuta iwapo yatapati.…

Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam wakiwa kwenye foleni ya mafuta katika Kituo cha Mafuta cha Bamaga, Mwenge jijini.
Jamaa huyu anaonekana akilalamika akiwa kwenye foleni hiyo.
Baadhi ya madumu ya kuchukulia mafuta yakiwa yamepangwa kwenye foleni na wateja, tayari kwa kutiwa mafuta iwapo yatapati.
Magari yakiwa kwenye msululu wa kugoja kujaziwa mafuta.

SAKATA la kuadimika kwa nishati ya mafuta nchini limeibuka tena leo, ambapo wakazi wa jiji la Dar es Salaam wameendelea kuhangaika kutafuta nishati hiyo bila mafanikio.

Tatizo hilo linazidi kuipaka matope Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), kufuatia kutoweka wazi tatizo linalosababisha upatikanaji wa mafuta katika vituo mbalimbali.

Baadhi ya wateja wa nishati ya mafuta ya petroli na dizeli leo wamelalamikia utaratibu wa vituo vya mafuta kuendelea kugoma kuwauzima nishati hiyo kwa madai ya kwisha katika vituo vyao.

“Inanikela sana hali ni mbaya maana nimetafuta mafuta tangu asubuhi sijapata, na nikiangalia sababu hata sielewi, nini kinachowafanya Ewura kutosema tatizo kwetu wateja wao ili tusisumbuke?” alihoji mkazi mmoja huku mwingine naye akilalamika kuwa:

“ Hawa Ewura hawafai kabisa, yaani leo wamenifanya kutoenda kazini kwa ajili ya kuhangaika huku na kule kutafuta mafuta, huwezi kuamini, gari limenizimikia Sinza Mugabe na sasa niko hapa kituo cha mafuta Bamaga tangu saa tatu asubuhi na mafuta sijapata, wauzaji wanatuyeyusha tu.” Alisema mkazi huyo.


WEMA ana kidole Gundu

Na Mwandishi Wetu

Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ametajwa kuwa na kidole chenye gundu.

Kidole cha Wema kinachotajwa kuwa na gundu ni kile cha pete kwa maelezo kuwa kila akivalishwa pete ya uchumba hufarakana ndani ya muda mfupi.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Wema huwa na bahati ya kung’ara kwenye uhusiano wa kawaida lakini uchumba ni mzito.

Ripoti ya uchunguzi huo inanyevua kuwa wanaume watatu ambao Wema amewahi kuvaa pete zao za uchumba, wote alitibuana nao muda mfupi baada kumvalisha madini kwenye kidole.

Katika safari ya mapenzi, Wema ameshavaa pete za wanaume watatu, mjasiriamali, Jumbe Yusuf, mwanamuziki wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Charlz Baba’ na mwana-Bongo Fleva, Naseeb…

Na Mwandishi Wetu

Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ametajwa kuwa na kidole chenye gundu.

Kidole cha Wema kinachotajwa kuwa na gundu ni kile cha pete kwa maelezo kuwa kila akivalishwa pete ya uchumba hufarakana ndani ya muda mfupi.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Wema huwa na bahati ya kung’ara kwenye uhusiano wa kawaida lakini uchumba ni mzito.

Ripoti ya uchunguzi huo inanyevua kuwa wanaume watatu ambao Wema amewahi kuvaa pete zao za uchumba, wote alitibuana nao muda mfupi baada kumvalisha madini kwenye kidole.

Katika safari ya mapenzi, Wema ameshavaa pete za wanaume watatu, mjasiriamali, Jumbe Yusuf, mwanamuziki wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Charlz Baba’ na mwana-Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.

JUMBE
Wema alipoanza mahaba na Jumbe, ikawa patashika. Nchi nzima ikatambua kwamba mtoto huyo wa Balozi Isaac Abraham Sepetu, yupo kwenye uhusiano wa kimapenzi na kijana wa Kingazija, Jumbe.

Kumbukumbu zinafunua kuwa kutokana na kukolea kimapenzi, wakaishi pamoja Tabata, Dar es Salaam.

Data zinaonesha kuwa baada ya kuishi kwa muda mrefu kidogo, huku wakiitana mke na mume, waliamua kuvuka hatua moja kwa Jumbe kumvisha pete ya uchumba Wema.

Hata hivyo, pete hiyo haikuwa na matunda, kwani baada ya mwezi mmoja, waliachana.

CHARLZ BABA
Wema alipoachana na Jumbe, alijirusha kwa muda na Mkurugenzi wa Hartmann Production, Hartmann Mbilinyi kabla ya kutua kwa Charlz ambaye aling’ara naye kiasi kwamba zikaibuka taarifa kuwa watafunga ndoa.

Kuthibitisha upendo wake, Charlz alimvalisha pete ya uchumba ambayo iliibua matokeo mabaya pia, kwani muda mfupi baadaye Wema alikwenda Marekani na akiwa huko alivunja uhusiano na mwana Twanga Pepeta huyo, aliporudi nchini alitua moja kwa moja kwenye mikono ya Diamond.

DIAMOND
Walikuwa kama watoto, wakijifungia ndani wanapiga mapicha ya denda na mapozi mbalimbali ya kimahaba.

Dhahiri, ilionekana wanaendana, kwa hiyo kilichosubiriwa ikawa ndoa. Kukaribisha hatua hiyo, Diamond aliitumia siku yake ya kuzaliwa kumvalisha pete Wema ndani ya New Maisha Club.

Kama kawaida, balaa likafuata baada ya pete, kwani wiki moja na nusu baadaye, Diamond alitangaza kuachana na Wema kwa madai kwamba ni mvivu kwenye kazi za nyumbani, vile vile hampendi mama yake.

Pamoja na Wema kuomba msamaha na kurudiana kwa shinikizo la mama wa Diamond, imeonekana ‘bwa mdogo’ huyo alishaamua kuangalia mbele, kwani hivi karibuni yameibuka madai kwamba yupo katika uhusiano wa kimapenzi na Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006-07, Jokate Mwegelo.

WEMA
Katika maelezo yake kuhusu kuachana na wanaume wake, alisema kuwa jamii humuona ni malaya lakini ukweli ni kwamba hujitahidi kuvumilia na anapoinua mikono maana yake ameshindwa kwa njia zote.

Hii inamaanisha kuwa Wema anaamini matatizo yapo kwa wanaume wake ambao huwavumilia mno lakini mwisho hushindikana.


Monday, November 28, 2011

kupandisha posho za wabunge ni ukuchaa

Nimeshtushwa sana na taarifa za kupandishwa kwa posho za vikao kwa Wabunge. Nimeshtushwa zaidi kwamba Posho hizi zimeanza kulipwa katika mkutano wa Bunge uliopita kabla hata Rais hajaamua maana maslahi yote ya Wabunge huamuliwa na Rais Baada ya kupokea mapendekezo ya Bunge kupitia Tume ya Bunge.

Wabunge wote watambue kwamba kuamua kujipandishia posho zao bila kuzingatia Hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida ni usaliti usio na mfano. Mbunge yeyote ambaye anabariki Jambo hili au anaishi hewani haoni tabunza wananchi au ni mwizi tu na anaona Ubunge ni Kama nafasi ya kujitajirisha binafsi.

Kwa Wabunge wa Chadema, wajue uamuzi kuhusu posho ni uamuzi wa chama na ni uamuzi wa kisera. Mbunge yeyote wa Chadema anayepokea posho za vikao anakwenda kinyume na maamuzi ya sera za chama tulizoahidi wananchi wakati wa uchaguzi. Nimemwomba Katibu Mkuu wa chama kuitisha kikao maalumu cha Kamati Kuu ya chama kujadili suala hili.

Toka tarehe 8 juni mwaka 2011 nilikataa kupokea posho za vikao. Popote ninapohudhuria vikao huomba Risiti ya fedha ninazokataa. Baadhi ya Wabunge Kama Januari Makamba wamekataa posho na hata kwenye semina ya kamati ya nishati alikataa na tumeona kwenye vyombo vya habari jina lake likiwa limekatwa ilhali viongozi wakubwa kabisa wamechukua posho. Nampongeza kijana mwenzangu kwa uzalendo huu. Nawataka wabunge wengine wenye Moyo wa dhati kukataa sio tu ongezeko hili la posho Bali posho yote ya vikao. Kwa nini mbunge akubali kulipwa kwa kukaa?

Tazama nchi hii, juzi serikali ilipokea Msaada wa tshs 20bn kwa ajili ya Sensa ya mwakani wakati wabunge wanalipwa 28bn Kama posho za kukaa tu.

Tanzania inaagiza gesi ya matumizi ya nyumbani kutoka nje kwa kutumia mamilioni ya dola za kimarekani. Kuwanda cha kutengeneza LPG kinagharimu tshs 35bn tu, Wabunge peek Yao kwa mwaka wanatumia 28bn kwa posho za kukaa tu achilia mbali mishahara na marupurupu mengine.

Ipo siku Watanzania watatupiga mawe kwa usaliti huu dhidi yao.

http://zittokabwe.wordpress.com/

Kilichotokea Dodoma kwenye vikao vya CCM - Tafsiri yangu

Ndugu zangu
Waafrika sisi tu mahodari sana wa kufunga safari, lakini, huwa hatupangi safari. Kuna tofauti ya kufunga safari na kupanga safari. Kuna tofauti pia ya kuwa na mipango na mikakati na kuwa na mipango na mikakati sahihi.
Mara nyingi wenye kupanga safari zao, na hata kuwa na mipango na mikakati sahihi hufanikiwa zaidi. Na ndivyo ilivyo kwenye siasa.

Kule Dodoma tumeshuhudia ’ Vita vya wenyewe kwa wenyewe’ ndani ya CCM. Inahusu safari ya kuelekea 2015, na si kitu kingine. Kule Dodoma CCM hawakutoka WaMOJA . Wametoka kwenye mapande makubwa mawili na mafungu mengine madogo madogo.

Na CCM ya sasa ina makundi, walau hili wamekiri rasmi CCM wenyewe. Na kwenye kuelekea 2015 tunayaona makundi makubwa mawili; lile linaloongozwa na Edward Lowassa na la akina Samwel Sitta. Kule Dodoma tumeushudia mnyukano wa wazi wa makundi haya yakiwahusisha pia vijana wa chama hicho.

Yote haya yanatoa fursa kwa upinzani kufanya vizuri kama itatumia vema fursa hii ya Wana- CCM wanaonyukana wenyewe kwa wenyewe. Huu ni wakati kwa Wapinzani kuwaonyesha Watanzania kuwa CCM ni chama cha kawaida tu na unaweza kuwepo mbadala wa chama hicho. Ni wakati pia kwa wapinzani kuongeza nguvu ya kusukuma hoja ya kuandikwa Katiba Mpya itakayowashirikisha wananchi katika hatua zote.

Na mpambano ule wa Dodoma, katika hali inayoweza hata kumstajabisha Lowassa mwenyewe, umempa sio tu ushindi Lowassa na kundi lake, bali pia, Lowassa ametoka kwenye vikao vile akiwa, walau kwa wakati huu, na nguvu nyingi zaidi za kisiasa ndani ya chama hicho . Inaonekana ’ jeshi la Lowassa’ ni kubwa, limesambaa na lina nguvu za kimikakati. Ndio, Edward Lowassa amenufaika sana kisiasa na vikao vya chama chake kule Dodoma.

Na mwananchi wa kawaida anasemaje?

Namwuliza , Andrew, kijana dereva wa teksi hapa Iringa; “ Unasemaje kuhusu yaliyotokea Dodoma CCM?”
”Lowassa hayumo!” Ananijibu.
”Una maana gani?” Namwuliza.
”Tuliambiwa Lowassa ni fisadi kumbe hayumo.”

Dereva wa teksi anaonyesha kufurahi kuujua ukweli. Swali ni hili; Je, aliousikia dereva wa teksi ni ukweli kamili? Hivyo basi, waliomwaminisha dereva wa teksi kuwa Lowassa ni fisadi wana mtihani wa kuja na ushahidi wa kumtia hatiani mtuhumiwa ili nao waaminike.

Na katika hili nayakumbuka maandiko ya mwanafasihi Kezilahabi: “ Siku hiyo ikifika utaona ishara itakayokuongoza. Utakapofika pale ambapo kila binadamu lazima afike utajua hukukosea; kwani njia ya kwenda huko inajulikana kwa wote na inakwenda moja kwa moja bila kupinda.

Huna haja ya kusoma kitabu chochote kupata maelezo ya kwenda huko wala hakuna haja ya kusikiliza mahubiri. Hakuna utalaamu unaohitajika maana utajikuta umefika. Utakapofika utamkuta amekaa peke yake akiwatazama wale wengine . Hao wengine utawatambua maana ni ndugu zako wote.

Wengi kati yao ndio wale waliokuwa askari wa mwanga. Wale ambao hutaweza kuwatambua atakumbulisha kwao na wewe utachukua nafasi yako. Usistuke utakaposikia majina yao; maana, wengi kati yao wana majina makubwa. Utawakuta wanafanya jambo fulani. Wewe pia fanya kama wao bila kuuliza bila manung’uniko na usikate tamaa. Kwa sasa hivi subiri ishara” ( E. Kezilahabi, Nagona)

Ni kina nani wamejeruhiwa Dodoma?

Nape Nnauye hawezi kuwa mwana- CCM mwenye furaha kwa wakati huu. Nahofia kuna hesabu za kisiasa alizozichanganya vibaya sana. Kama mwenezi wa chama alijichanganya sana kwenye kuilezea kwa umma dhana ya ’ Kujivua Gamba’ . Badala ya kuonekan kuwa ni mkakati wa mabadiliko ya jumla kwa CCM Nape aliitumia dhana hiyo kuwahukumu WanaCCM wenzake . Hivyo basi, kuonekana zaidi kuwa ni mbinu ya kutaka kuondokana nao ili kupisha njia kwa watu wa kundi lake. Na hapo ndio kwenye tatizo la msingi kwa Nape. Kwamba anaonekana kuwa na kundi lake kuelekea 2015.

Kujichanganya kwa Nape kimsingi kumewapa fursa akina Lowassa na wenzake kupanga mashambulizi na kuyatekeleza kwa mafanikio makubwa. Na kama kuna mtu aliyejeruhiwa vibaya kwenye vikao vya Dodoma ni Nape Moses Nnauye. Ana lazima ya kujipanga na kurudisha mashambulizi ili kulinda heshima yake na hata taswira yake kwa jamii. Hivyo hivyo kwa Samwel Sitta na wenzake. Dakika 45 za kuongea peke yake kwenye ITV hazikumwongezea nguvu Samwel Sitta na kundi lake na labda kinyume chake.

Je, ina maana vita ndani ya CCM ndio imekoma?
Hapana, huu ni mwanzo tu, vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya CCM vitaendelea na moto wake kuongezeka. Mwakani kuna uchaguzi wa ndani ya chama hicho. Tulichokiona Dodoma ni ’ rasha-rasha’ tu. Kutoka Dodoma makundi yanayohasiamiana ndani ya CCM yatazidi kupambana mikoani, wilayani na hata kwenye kata. Watazidi kupambana pia kupitia vyombo vya habari. Yote ni katika kuhakikisha wanajipanga kushika nafasi muhimu kwenye uchaguzi ujao wa chama chao, nafasi zitakazohakikisha wagombea wao wanapata tiketi za kuwania urais na hatimaye kushika dola.

Na Lowassa na wenzake wana kibarua kigumu cha kuwabadilisha WaTanzania kutoka kile walichoaminishwa kabla . Ni kibarua kigumu kama vile kumwambia mtu kuwa rangi nyekundu si nyekundu tena bali ni nyeupe. Kwamba alichokuwa akiamini mtu huyo siku zote kuwa ndicho, sicho. Ni watu hawa hawa ambao hawakupata tabu jana kujibu swali la je, fisadi mkuu ni nani? Na anayefuatia….?

Je, uchaguzi wa ndani ya CCM ukimalizika mwakani ndio mwisho wa vita?

Hapana, kundi litakaloibuka na ushindi wa jumla litahamishia mapambano yake kwa wapinzani wa chama na mgombea wao Urais walio nje ya chama chao. Kwa ilivyo sasa mashambuzi yanaweza kuelekea kwa Chadema. Hiki ni chama chenye nguvu na ushawishi mkubwa kwa wananchi kwa sasa.

Hivi ni Lowassa tu aliyeibuka mshindi kule Dodoma?
Hapana, kuna MwanaCCM mwingine aliyetoka Dodoma kimya kimya huku kikapu chake kikiwa kimejaa mavuno. Ni Fredrick Tluway Sumaye. Msomaji lishike jina hili. Huyu bwana hadi wakati huu anazicheza karata zake vizuri sana. Yaelekea mafunzo yake ya Uongozi aliyoyapata kule Havard Marekani yanamsaidia.
Si tulimsikia Sumaye kule Dodoma akisimama na kumtetea ’ majeruhi’ mwenzake Lowassa bila kutamka kuwa naye, Sumaye ni ’ majeruhi’ wa ’ Siasa uchwara’ kama anavyoziita Rostam Aziz. Sumaye ana mitaji ya kisiasa anayowekeza.

Je, ni kweli Lowassa ana nguvu na ushawishi mkubwa kisiasa?

Nikijibu hapana nitaongopa. Edward Lowassa ni mwanasiasa mahiri na mwenye ushawishi mkubwa ndani na hata nje ya chama chake. Wanaomjua Lowassa wanasema ana vitu viwili vikubwa; authority na humbleness. Kwamba ana uwezo wa kushawishi na kufanya vitu vifanyike na pia ni mnyenyekevu. Hilo la mwisho kuna wanaosema Lowassa anaweza kuongea na mtu mdogo sana, lakini atahakikisha hajibu simu ya mtu mwingine mpaka amalize mazungumzo na anayeongea nae.

Nikiwa Bagamoyo kwenye mkutano wa masuala ya elimu juma la jana kuna hoja ilizuka juu ya shule za sekondari za kata. Kikundi cha majadiliano nilichokuwamo kiliwajumuisha watendaji wa elimu kutoka Wilaya mbali mbali za Tanzania.
Swali likaulizwa; ” Ilikuaje sekondari za kata zikajengwa kwa kasi vile?”
”Ni Lowassa!” Alijibu mmoja wa washiriki.

Alifanyaje? Akauliza mwingine.
”Waliokuwa wakiratibu michango ya elfu kumi kumi kutoka kwa Watumishi walitwambia; Lowassa anataka tumpelekee orodha ya ambao hawakulipa michango hiyo, si orodha ya waliyolipa. Ni kwa njia hiyo kila mmoja wetu akachangia na shule zikajengwa. Ni nani anayetaka jina lake lifikishwe kwa Lowassa?” Alimalizia kwa kuuliza mmoja wa wanakikundi cha majadiliano.

Na kwa yaliyotokea Dodoma kuna watakaoshika tama na kusema, kumbe, Edward Lowassa hajamalizwa kisiasa! Je, akina Mwakyembe hawakufahamu, kuwa simba humwui kwa risasi ya kumpapasa masikioni?
Kama ni mchezo wa ngumi, basi, kwa mpinzani wa Lowassa, akubali, kuwa kummaliza Lowassa , awe tayari kucheza raundi zote 12.

Naam, tutayaona mengi mengine huko twendako, tuombe uhai.

Rais Kikwete akutana na Viongozi wa Chadema Ikulu

HUJAFA hujaumbika! Ni habari mbaya inayogusa ‘kapo’ ya Wema Isaac Sepetu na Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’ baada ya mnyange huyo kupoteza uzao wao kufuatia mimba yake ya takribani miezi miwili kuchoropoka, Ijumaa Wikienda linairusha hewani ‘laivu’ bila chenga.

TUJIKUMBUSHE SIKU YA FURAHA
Wiki kadhaa zilizopita, huku akiwa na furaha, Wema ambaye ni staa mkubwa wa filamu za Kibongo, alisimama mbele ya kamera za video za gazeti ndugu la hili, Risasi Mchanganyiko na kuthibitisha kuwa ana ujauzito wa mwezi mmoja na nusu baada ya kutoka kwenye vipimo (pregnancy test).

“Ni jambo la furaha sana, ni muda muafaka kwangu kupata mtoto,” alinukuliwa Wema akiwa hachezi mbali na ubuyu, ndimu na maembe mabichi.

CHANZO
Wiki mbili baadaye, The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda lilipokea simu kutoka kwa chanzo chake na mazungumzo yalikuwa hivi;
Chanzo: Ijumaa Wikienda mna habari?

Wikienda: Habari tunazo nyingi tu, soma magazeti ya Global Publishers, lakini kama una ya kwako, nayo ni muhimu ukitupatia tutairusha hewani.

Chanzo: Kwa taarifa yenu, mimba ya Wema imechoropoka na hapa tunapozungumza yupo hoi kitandani, anaumwa.
Wikienda: Una uhakika? Amelazwa hospitali gani?

Chanzo: Kwani nilishawahi kuwadanganya? Yupo nyumbani anakoishi na Diamond, Sinza-Madukani, Dar. Sitaki mahojiano zaidi, fuatilieni mtajua ukweli na tafadhali naomba msinitaje.

IJUMAA WIKIENDA MZIGONI
Baada ya maelezo hayo, Ijumaa Wikienda lilizama mzigoni na kujikusanyia data zilizokaribia kwenye ukweli kutoka kwa watu wa karibu na wapenzi hao.

Hata hivyo, timu ya Ijumaa Wikienda ilipotaka kumuweka Wema kwenye ‘tageti’, alisafiri na Diamond kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya shoo na mapumziko mafupi.

AREJEA BONGO, AWEKWA ‘MTUKATI’ Aliporejea Bongo mwishoni mwa wiki iliyopita, Ijumaa Wikienda lilimuweka ‘mtukati’ na kumtaka kuonesha kibendi kilipoyeyukia. Alifunguka huku akijua kuwa akibisha, aibu itamfika kwani hana tena kile kitumbo kilichogeuka kero kwa mastaa wenzake kufuatia kutema mate ovyo.

Alisema: “Ilikuwa Jumatatu ileee (wiki mbili zilizopita), nilikuwa katika hali mbaya na baadaye niligundua kuwa mimba yangu inachoropoka. Nilikimbilia ‘famasi’ ya Primar na kumweleza mtaalamu hali yangu.
“Aliniambia mimba yangu imechoropoka hivyo nilipatiwa dawa kwa ajili ya kusafisha kizazi.

MUNGU HAKUPANGA AZAE?
“Ukweli niliumia sana, lakini nilijua Mungu hakupanga nizae wakati huu, najua amenipangia muda muafaka.
“Nahisi chanzo ni vipigo vya ‘toto yangu’ (Diamond Platinum Baby), lakini pia nahisi ni kwa sababu ya matumizi ya pombe kali.

DIAMOND ALIA KAMA MTOTO MDOGO
“Nilipomjulisha Diamond juu ya kupoteza kiumbe chake tumboni, alijisikia vibaya sana, alilia kwa uchungu kama mtoto mdogo.
“Kwa sasa niko fiti kabisa na namuomba Mungu nishike ujauzito mwingine kwani natamani kupata mtoto kuliko kitu kingine chochote.”

DIAMOND VIPI?
Diamond alikiri kumtandika Wema kutokana na kushindwa kuzuia hasira hasa mwanadada huyo anapomkosea, lakini hakuweza kuzungumzia kuchoropoka kwa ujauzito huo.
“Hata makofi muda mwingine yanafunza,” alisema Diamond.

ATHARI YA VIPIGO NA
POMBE KALI KWA MJAMZITO
Diamond na wanaume wengine wanapaswa kujua kuwa kasumba ya mwanaume kumpiga mwanamke ni ya kizamani na mke hapigwi makofi bali kwa upande wa khanga.

Pia Wema na wanawake wengine wanatakiwa kujua kuwa kunywa pombe wakati wa ujauzito ni sawa na kumpiga mwanao nyundo akiwa hai na kumuua.

NENO LA WIKIENDA
Kwetu sisi Wema na Diamond anayefanya vizuri kimuziki ni vijana watafutaji ambao ni mfano wa kuigwa kwani hawapendi kubweteka hivyo tunawapa pole kwa kupoteza uzao wao wa kwanza.

Mimba ya wema yachoropoka

HUJAFA hujaumbika! Ni habari mbaya inayogusa ‘kapo’ ya Wema Isaac Sepetu na Naseeb Abdul Jumaa ‘Diamond’ baada ya mnyange huyo kupoteza uzao wao kufuatia mimba yake ya takribani miezi miwili kuchoropoka, Ijumaa Wikienda linairusha hewani ‘laivu’ bila chenga.

TUJIKUMBUSHE SIKU YA FURAHA
Wiki kadhaa zilizopita, huku akiwa na furaha, Wema ambaye ni staa mkubwa wa filamu za Kibongo, alisimama mbele ya kamera za video za gazeti ndugu la hili, Risasi Mchanganyiko na kuthibitisha kuwa ana ujauzito wa mwezi mmoja na nusu baada ya kutoka kwenye vipimo (pregnancy test).

“Ni jambo la furaha sana, ni muda muafaka kwangu kupata mtoto,” alinukuliwa Wema akiwa hachezi mbali na ubuyu, ndimu na maembe mabichi.

CHANZO
Wiki mbili baadaye, The Biggest IQ Paper, Ijumaa Wikienda lilipokea simu kutoka kwa chanzo chake na mazungumzo yalikuwa hivi;
Chanzo: Ijumaa Wikienda mna habari?

Wikienda: Habari tunazo nyingi tu, soma magazeti ya Global Publishers, lakini kama una ya kwako, nayo ni muhimu ukitupatia tutairusha hewani.

Chanzo: Kwa taarifa yenu, mimba ya Wema imechoropoka na hapa tunapozungumza yupo hoi kitandani, anaumwa.
Wikienda: Una uhakika? Amelazwa hospitali gani?

Chanzo: Kwani nilishawahi kuwadanganya? Yupo nyumbani anakoishi na Diamond, Sinza-Madukani, Dar. Sitaki mahojiano zaidi, fuatilieni mtajua ukweli na tafadhali naomba msinitaje.

IJUMAA WIKIENDA MZIGONI
Baada ya maelezo hayo, Ijumaa Wikienda lilizama mzigoni na kujikusanyia data zilizokaribia kwenye ukweli kutoka kwa watu wa karibu na wapenzi hao.

Hata hivyo, timu ya Ijumaa Wikienda ilipotaka kumuweka Wema kwenye ‘tageti’, alisafiri na Diamond kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya shoo na mapumziko mafupi.

AREJEA BONGO, AWEKWA ‘MTUKATI’ Aliporejea Bongo mwishoni mwa wiki iliyopita, Ijumaa Wikienda lilimuweka ‘mtukati’ na kumtaka kuonesha kibendi kilipoyeyukia. Alifunguka huku akijua kuwa akibisha, aibu itamfika kwani hana tena kile kitumbo kilichogeuka kero kwa mastaa wenzake kufuatia kutema mate ovyo.

Alisema: “Ilikuwa Jumatatu ileee (wiki mbili zilizopita), nilikuwa katika hali mbaya na baadaye niligundua kuwa mimba yangu inachoropoka. Nilikimbilia ‘famasi’ ya Primar na kumweleza mtaalamu hali yangu.
“Aliniambia mimba yangu imechoropoka hivyo nilipatiwa dawa kwa ajili ya kusafisha kizazi.

MUNGU HAKUPANGA AZAE?
“Ukweli niliumia sana, lakini nilijua Mungu hakupanga nizae wakati huu, najua amenipangia muda muafaka.
“Nahisi chanzo ni vipigo vya ‘toto yangu’ (Diamond Platinum Baby), lakini pia nahisi ni kwa sababu ya matumizi ya pombe kali.

DIAMOND ALIA KAMA MTOTO MDOGO
“Nilipomjulisha Diamond juu ya kupoteza kiumbe chake tumboni, alijisikia vibaya sana, alilia kwa uchungu kama mtoto mdogo.
“Kwa sasa niko fiti kabisa na namuomba Mungu nishike ujauzito mwingine kwani natamani kupata mtoto kuliko kitu kingine chochote.”

DIAMOND VIPI?
Diamond alikiri kumtandika Wema kutokana na kushindwa kuzuia hasira hasa mwanadada huyo anapomkosea, lakini hakuweza kuzungumzia kuchoropoka kwa ujauzito huo.
“Hata makofi muda mwingine yanafunza,” alisema Diamond.

ATHARI YA VIPIGO NA
POMBE KALI KWA MJAMZITO
Diamond na wanaume wengine wanapaswa kujua kuwa kasumba ya mwanaume kumpiga mwanamke ni ya kizamani na mke hapigwi makofi bali kwa upande wa khanga.

Pia Wema na wanawake wengine wanatakiwa kujua kuwa kunywa pombe wakati wa ujauzito ni sawa na kumpiga mwanao nyundo akiwa hai na kumuua.

NENO LA WIKIENDA
Kwetu sisi Wema na Diamond anayefanya vizuri kimuziki ni vijana watafutaji ambao ni mfano wa kuigwa kwani hawapendi kubweteka hivyo tunawapa pole kwa kupoteza uzao wao wa kwanza.

Jk akutana na Chadema

Rais JK akiagana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Ikulu mara baada ya mazunguzo jana.

Leo wanakutana tena kuendelea na mazungumzo yao

...akiagana na Mhe. Tundu Lissu

....akiagana na Mhe. John Mnyika

...akiagana na Prof. Adabballah Safari

..Mhe. Lissu akisepa taratibu kutoka Ikulu

...mambo yalivyokuwa ndani wakati wakipata chai na juisi...ilikuwa kirafiki zaidi.

PICHA: Hisani ya Ikulu

************************************************************************

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe

wa Serikali yake leo, Jumapili, Novemba 27,

2011, amekutana na kufanya mazungumzo

na ujumbe wa Chama cha Demokrasia na

Maendeleo (CHADEMA).



Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika

Ikulu, Dar Es Salaam, yamefanyika katika

mazingira ya urafiki na ujumbe wa CHADEMA

umewasilisha mapendekezo yake kuhusu

mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya

Tanzania. Serikali imepokea mapendekezo

Hata hivyo, pande zote mbili zimekubaliana

kukutana tena asubuhi ya kesho, Jumatatu,

Novemba 28, 2011, ili kuipa nafasi Serikali

iweze kutafakari mapendekezo hayo.

Lakini pande hizo mbili zimekubaliana kuwa

Katiba ya sasa ni Katiba nzuri iliyolilea Taifa

kwa miaka 50 iliyopita kwa sababu ni Katiba ya

sasa iliyoliwezesha Taifa la Tanzania kuwa na

amani, utulivu na kupata maendeleo makubwa

ambayo nchi yetu imepata mpaka sasa.



Pia pande zote mbili zimekubaliana kuhusu

umuhimu wa kutunga Katibu Mpya kama

Mheshimiwa Rais Kikwete alivyoliahidi taifa

wakati wa salamu zake za mwaka mpya

Desemba 31, mwaka jana, 2010, Katiba

ambayo italiongoza Taifa la Tanzania kwa

miaka mingine 50 ijayo.



Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Rais

aliwahakikishia wajumbe hao wa CHADEMA

wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho,

Mheshimiwa Freeman Mbowe kuwa ni dhamira

yake na ya Serikali yake kuhakikisha kuwa

Tanzania inapata Katiba mpya.



Katika mkutano huo, pande zote mbili

zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu sana

kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba

Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na

kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na

umoja wa kitaifa.



Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa

mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia

misingi ya mambo mengine muhimu kwa taifa

la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo

vya uvunjifu wa amani, kuligawa Taifa kwa

misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa

misingi ya maeneo.



IMETOLEWA NA:

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

NOVEMBA 27, 2011

DAR ES SALAAM

Tuesday, November 8, 2011

Mkurugenzi wa mawasiliano Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto), akiwa ameshikilia na kuelezea moja ya kipeperushi kinachoonyesha namna ya kuupigia kura mlima Kilimanjaro ili uweze kuingia kwenye maajabu saba ya Dunia. Kulia ni Ofisa Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bw. Geofrey Tengeneza. Ili kupiga Kura Bure mteja wa Airtel Tuma neno KILI kwenda namba 15771.
Mkurugenzi wa mawasiliano Airtel Tanzania, Beatrice Singano, akiwa ameshikilia simu huku akitoa maelekezo namna ya kuupigia kura mlima Kilimanjaro kura BURE kupitia Airtel ili uweze kuingia kwenye maajabu saba ya Dunia hadi tarehe 11 novemba…

Mkurugenzi wa mawasiliano Airtel Tanzania, Beatrice Singano (kushoto), akiwa ameshikilia na kuelezea moja ya kipeperushi kinachoonyesha namna ya kuupigia kura mlima Kilimanjaro ili uweze kuingia kwenye maajabu saba ya Dunia. Kulia ni Ofisa Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bw. Geofrey Tengeneza. Ili kupiga Kura Bure mteja wa Airtel Tuma neno KILI kwenda namba 15771.
Mkurugenzi wa mawasiliano Airtel Tanzania, Beatrice Singano, akiwa ameshikilia simu huku akitoa maelekezo namna ya kuupigia kura mlima Kilimanjaro kura BURE kupitia Airtel ili uweze kuingia kwenye maajabu saba ya Dunia hadi tarehe 11 novemba 2011.

Ofisa Uhusiano wa Bodi ya Utalii Tanzania, Geofrey Tengeneza, akifafanua jambo mbele ya waandishi wa habari. Kushoto ni Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice Singano wakati wa hafla fupi ya kutangaza Ofa kwa wateja wa Airtel kupigia kura mlima Kilimanjaro bure. Tuma KILI kwenda 15771 sasa.


Lulu Basi


Na Waandishi Wetu
MATUKIO yenye sura za aibu kwa kinda anayewika katika Tasnia ya Filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ yamezidi na sasa baadhi ya wasanii wenzake wamemshukia na kusema basi, imetosha, Risasi Mchanganyiko pekee limeshikilia mkoba wenye mafaili yote.

Baadhi ya wasanii wa kike waliozungumza na gazeti hili kwa sharti la majina yao kutochorwa gazetini, Ijumaa iliyopita katika Viwanja vya Gymkhana, jijini Dar es Saalam, walisema wamechoshwa na vituko vya msanii huyo na lazima wamkomeshe.

Wasanii wa filamu walikuwa viwanjani hapo katika mechi ya mpira wa miguu iliyochezwa kati ya Timu ya Bongo Movie na wafanyabiashara maarufu, ambapo kama kawaida Lulu alifanya vibweka.


Awali, waandishi wetu walimshuhudia msanii huyo akiwa kimya kama amemwagiwa maji ya baridi wakati akifuatilia mechi hiyo lakini kama vile asingeinuka na kucheza ngoma zilizokuwa zikipigwa katika viwanja hivyo.

Baadaye, ghafla Lulu alisimama na kuanza kucheza katika mitindo mbalimbali ambayo ilionekana dhahiri kuwa na nia ya kuwatega wanaume, baada ya Bongo Movie kupachika bao kwa wafanyabiashara hao.

“Huyu mtoto tumemvumilia tumechoka, kila siku anatutia aibu. Hebu ona anavyocheza...ngoma za namna gani zinachezwa vile? Ona anavyoonesha makalio, yaani huyu Lulu huyu! Dawa yake inachemka,” alisema staa mmoja wa sinema mwenye jina kubwa.

Matukio ya Lulu kulewa na kufanya vituko katika shughuli mbalimbali hayajaanza leo, lakini hata yanaporipotiwa ni kama anaambiwa aendelee kufanya vibweka, hapa chini ni baadhi ya matukio yaliyopo katika makabrasha ya Risasi Mchanganyiko;

SEPTEMBA, 2010 BILICANAS
Kamera za mapaparazi wa Risasi Mchanganyiko, zilimnasa msanii huyu laivu bila chenga ndani ya Ukumbi wa Bilicanas, Posta, Dar akiwa amelewa chakari huku akijiachia hovyo na hivyo mwili wake kubaki nje.

Habari hii iliandikwa na moja ya magazeti ya Global lakini Lulu hakukoma, aliendelea kama kawa na tabia yake hiyo.

AGOSTI 2011, MOSHI
Katika msafara wa wasanii wa Klabu ya Bongo Movie, Moshi, Kilimanjaro kulipokuwa na Tamasha la Kuelekea Miaka 50 ya Uhuru, lililochukua nafasi katika Viwanja vya Hugo mjini humo paparazi wetu alikuwemo.

Kama kawaida, msanii huyo alitia kinyaa baada ya kucheza katika mtindo usiokubalika hadi kujiangusha chini, aidha alikuwa amelewa tilalila kama kawaida yake (angalia picha ukurasa wa mbele).

SEPTEMBA 2011, LAMADA
Mafaili yetu yanaonesha kwamba tarehe hiyo Lulu alifanya kihoja kama hicho katika Viwanja vya Hoteli ya Lamada, Ilala, Dar, lakini safari hii alikwenda mbali zaidi na kula denda na msanii mwenzake Soud Ally ‘Akhui’.

Ilikuwa ni hafla fupi ya ‘birthday’ ya msanii anayekuja juu kwenye soko la filamu Bongo, Zuwena Mohammed ‘Shilole’, ambapo Lulu alitakiwa kutoa fedha au kumchagua mwanaume na kula naye denda hadharani, akachangua denda!

OKTOBA 2011, GYMKHANA
Maktaba ya Risasi Mchanganyiko inafunga ripoti yake kwa tukio lililotokea Ijumaa iliyopita, Oktoba 28, mwaka huu ambapo kila timu ya Bongo Movie ilipopachika bao, alianza kucheza katika mitindo ya aibu (kama picha zinavyoonekana ukurasa wa mbele).

AUNDIWA ZENGWE
Uamuzi uliofikiwa na baadhi ya wasanii wa kike waliozungumza na waandishi wetu Gymkhana, umeamua kumuundia zengwe ili kukomesha tabia yake hiyo mbaya.

“Kwa sababu tumeshagundua kwamba kila anapokwenda kwenye shughuli za kisanii anaharibu, tutazungumza na uongozi ili kuona kama wanaweza kumfungia kuhudhuria kwenye hafla yoyote ya msanii au inayohusu Bongo Movie.

“Hilo likishindikana, basi bado kuna sababu ya kuongea na uongozi na kuwaambia kwamba kama Lulu akiingia kwenye sherehe zetu basi asinywe pombe kabisa, maana haziwezi. Acha tukazungumze na viongozi wetu halafu tutawajulisha,” alisema mmoja wa wasanii hao.

Lulu ni msichana mdogo ambaye bado ana nafasi ya kubadilika. Ni vyema akatambua thamani yake kama msanii na kuchukua hatua za makusudi haraka.

Ukosefu usingizi una athiri afya yako

UNAWEZA kuwa makini sana na kila kitu unachochokula au unachokunywa kwa lengo la kulinda afya yako, lakini kama wakati wa kulala hupati usingizi, hali hiyo inaweza kuathiri afya yako.

Halikadhalika, kama mahali unapolala (kitandani au jamvini) na mazingira yake hayaendani na mahitaji ya mwili wako, huwezi kuwa na afya njema pia.

Mahali tunapolala pamoja na suala la kupata usingizi ni kitu muhimu sana kama kilivyo chakula. Utakumbuka kwamba karibu nusu ya maisha yetu tunayamalizia kitandani. Kama mtu ukijaaliwa kuishi duniani kwa muda wa miaka 60, kwa mfano, miaka 20 au 25 utakuwa umeitumia kwa kulala.

Unapolala, usingizi hufanyakazi ya kurejesha nguvu ya ubongo na mwili iliyopotea wakati wa mchana. Usingizi hurejesha upya nishati ya mwili na ubongo inayokuwezesha kupata akili ya kuainisha matatizo na kuyapatia ufumbuzi. Vile vile hukuwezesha kuamka asubuhi ukiwa na nguvu mpya ya kupambana na masuala mengine ya siku hiyo.

KWA NINI USIPATE USINGIZI?
Kama usingizi ndiyo muhimu kiasi hicho, kwa nini mtu usilale na kupata usingizi? Kuna sababu kadhaa zinazoweza kukufanya usipate usingizi, kuanzia chakula unachokula hadi mahali unapolala. Lakini habari njema ni kwamba kasoro zote unaweza kuzirekebisha na kupata usingizi mnono.

Kama una matatizo wakati wa kulala, kama vile kukosa usingizi, kuamka usiku mara kwa mara, kujisikia mchovu unapoamka asubuhi, au unahitaji kuboresha usingizi wako, kuna mambo mengi ya kufanya, yakiwemo haya yafuatayo:
HAKIKISHA unalala muda ule ule kila siku na muda mzuri ni saa 4:00 usiku.

JIEPUSHE kula vyakula muda mfupi kabla ya kupanda kitandani, hususan vitafunwa (snacks) vitokanavyo na nafaka na vyenye sukari. Badala yake kula vyakula vyepesi vya kuongeza protini mwilini, kama vile maziwa, n.k.

HAKIKISHA chumba unacholala kisiwe na baridi au joto sana. Wastani mzuri wa kiwango cha joto kinachokubalika kiafya ni nyuzi joto kati ya 18 na 21.

EPUKA kunywa kahawa au chai muda mfupi kabla ya kulala, vinywaji hivi huathiri usingizi kwa kiasi kikubwa.
HAKIKISHA unafanya mazoezi mara kwa mara, lakini siyo muda mfupi kabla ya kulala. Fanya mazoezi mapema na upate muda mrefu wa kupumzika kabla ya kupanda kitandani.

MWISHO kitanda, shuka na mto unaolalilia, hakikisha una ubora unaotakiwa. Shuka ya kujifunika na mto uliotengenezwa kutokana na pamba halisi (cotton wool) ni bora zaidi kuliko zilizotengenezwa kwa malighafi zingine, kama ‘polyester’, ‘synthetics’ n.k., ambazo zinadaiwa kuwa na kemikali zenye madhara kiafya.


Kafara Nzito


Na Luqman Maloto
VIONGOZI wakuu wa Dini ya Shetani, Freemasons, wamefanya kafara nzito kuadhimisha kukamatwa, kuteswa kisha kuuawa kwa aliyekuwa Kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi.

Vyanzo vimesema kuwa ni kawaida kwa Freemasons kufanya sherehe yenye mrengo wa kafara kila mara, mpango wao unapofanikiwa sehemu yoyote ile.

Kwa mujibu wa mitandao kadhaa inayojihusisha na utoaji wa habari za jamii ya Freemasons, kafara ambayo hufanywa ni ile ya mnyama hususan mbuzi mwenye pembe zinazofanana na zile za jini anayeitwa Lucifer (jini mkuu) ambaye huabudiwa na wafuasi wa Dini ya…

Na Luqman Maloto
VIONGOZI wakuu wa Dini ya Shetani, Freemasons, wamefanya kafara nzito kuadhimisha kukamatwa, kuteswa kisha kuuawa kwa aliyekuwa Kiongozi wa Libya, Muammar Gaddafi.

Vyanzo vimesema kuwa ni kawaida kwa Freemasons kufanya sherehe yenye mrengo wa kafara kila mara, mpango wao unapofanikiwa sehemu yoyote ile.

Kwa mujibu wa mitandao kadhaa inayojihusisha na utoaji wa habari za jamii ya Freemasons, kafara ambayo hufanywa ni ile ya mnyama hususan mbuzi mwenye pembe zinazofanana na zile za jini anayeitwa Lucifer (jini mkuu) ambaye huabudiwa na wafuasi wa Dini ya Shetani.

Mnyama huyo huchinjwa kisha damu na kichwa chake huhifadhiwa kwenye chombo chochote chenye muundo wa ndoo ili pembe zitokeze kwa juu na kutengeneza alama maarufu ya Freemasons ambayo wafuasi wake huitumia kwa njia ya vidole kutoa salamu.

Habari zinasema Freemasons walifanya kafara hiyo usiku wa manane kwenye hekalu moja kubwa lililojengwa kwenye eneo la jangwa lililopo ndani ya Jiji la Misrata, Libya.

Inabainishwa kuwa viongozi mbalimbali wakubwa kwenye nchi zilizoendelea kiuchumi ambao wana vyeo vikubwa ndani ya jamii ya Freemasons, walihudhuria kafara hiyo.

MKAKATI HATARI
Habari zinabainisha kuwa Freemasons ipo kwenye mkakati thabiti wa kuitawala dunia kabla ya Desemba 2012.
Kutokana na mkakati huo, imebainishwa kuwa Freemasons wamekuwa wakiratibu sera zao kwa kuangusha utawala wa nchi mbalimbali ambao viongozi wake wameshindwa kuendana na matakwa yake.

Inaelezwa kuwa Gaddafi alikuwa kiongozi mwenye mrengo wa Kiislam japo alikuwa haweki wazi kwenye utawala wake na kwamba alikuwa anapingana vikali na Freemasons.

Kwa mujibu wa mnajimu msomi, Maalim Hassan Yahya Hussein, Jeshi la Kujihami la Umoja wa Nchi za Magharibi (Nato), hutekeleza mipango ya Freemasons kama lilivyofanya Libya kumng’oa Gaddafi.

Maalim Hassan ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mnajimu maarufu barani Afrika, marehemu Sheikh Yahya Hussein, alisema kuwa dhumuni kuu la Freemasons ni kuzipiga vita dini za Kiislam na Kikristo.

“Ipo wazi kuwa wao lengo lao ni kuitawala dunia, kwa hiyo wanahakikisha hilo linawezekana kwa kudhoofisha Uislam na Ukristo ili ufe kisha Shetani ashinde hapa duniani,” alisema Maalim Hassan ambaye ni mrithi wa kazi za unajimu za marehemu Sheikh Yahya.

Aliongeza: “Mkakati mkubwa zaidi ni kuhakikisha dunia inaabudu Dini ya Shetani, wanataka kila mtu awe chini ya mamlaka ya jini mkuu (Lucifer). Dunia nzima itawaliwe na serikali moja na iwe na sarafu moja.”

Kauli ya Maalim Hassan inashabihiana na ile iliyopo kwenye maandiko kwamba zama za Dini ya Shetani kuishika dunia, kutakuwa na mfumo ambao utazuia mtu yeyote kupata huduma za kijamii mpaka awe mwanachama na atatambulika kwa chapa 666.

Habari zaidi zinaeleza kuwa Freemasons wanatumia njia mbalimbali kuhakikisha ulimwengu mzima hakuna anayeamini dini za Mungu na wanapambana kuhakikisha hata Yesu (Nabii Isa) atakaporejea akute hakuna aliye tayari kukombolewa.

Katika kuhakikisha wanapambana na nguvu ya Yesu, Freemasons wamekuwa wakitumia damu ndiyo maana hutoa kafara kwa kuchinja mnyama hasa mbuzi au kondoo wenye pembe kwa imani kwamba huwaongezea nguvu ya kuishika dunia.

Kutokana na tishio la Freemasons, viongozi wa kidini hususan wale wa Mashariki ya Kati, wamekuwa wakiwataka Waislam na Wakristo kwa imani zao, kufunga na kusali ili Dini ya Shetani isipate mafanikio inayoyataka.

SAKATA LA USHOGA
Habari zinasema kuwa Serikali ya Uingereza imekuwa ya kwanza kutumiwa na Freemasons katika kuhakikisha nchi zote zinazounda Jumuiya ya Madola zinapitisha sheria zinazokinzana na maandiko matakatifu yanayoaminiwa na waumini wa Dini za Kiislam na Kikristo.

Ushoga na usagaji ni vitendo ambavyo vinakemewa na dini hizo lakini hivi sasa, Freemasons wanadaiwa kuchochea mabadiliko ili watu wanaojihusisha na hulka hizo wawe huru kikatiba duniani.

Hivi karibuni, Waziri Mkuu wa Uingereza, David Cameron, alitangaza kuwa mwanachama wa Jumuiya ya Madola ili apate misaada inabidi kwanza aruhusu ndoa za jinsi moja (ushoga na usagaji) kwenye katiba ya nchi yake.

Tanzania ikiwa moja ya wanachama wa Jumuiya ya Madola, inapitiwa kwenye rungu hili, ingawa Balozi wa Uingereza nchini, Diana Corner alisema nchi yetu haihusiki.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe alishatoa tamko kwamba Tanzania haipo tayari kuruhusu ndoa za mashoga na wasagaji kisha akaonya kuwa kauli ya Cameron inaweza kuivunja Jumuiya ya Madola.

SIYO FREEMASONS PEKE YAKE
Mbali na Freemasons, dini nyingine zenye mrengo wa Shetani ni Illuminati na Skull & Bones ambazo zinavuma zaidi Marekani.

VIGOGO WA FREEMASONS
Viongozi wanaotajwa kuwa vigogo wa jamii hiyo ni marais wa 43 na 44 wa Marekani, Barack Obama na George Bush, Rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy ambao wanaonesha alama za vidole ukurasa wa kwanza. Yupo pia Cameron na wengine wengi.


Mbio za Mwenge zaingia Mbeya

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stellah Manyanya (kulia), akimkabidhi mwenge wa uhuru Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro,baada ya mwenge huo kumaliza mbio zake mkoani Rukwa, katika hafla iliyofanyika jana, kijiji cha Mkutano wilayani Mbozi.
Mkuu wa Wilaya ya Mbozi Gabriel Kimolo (kulia), akimkabidhi mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Mbeya mjini,Evance Balama, baada ya mwenge huo kumaliza mbio zake wil;ayani Mbozi.Makabidhiano hayo yalifanyika Songwe Viwandani mkoani Mbeya.Mwenge huo mkaoni Mbeya utafungua miradi yenye thamani ya sh.bilioni 2.6 na Wilayani Mbozi umefungua miradi mitatu ya sh.milioni 156.
Askari wa kutuliza ghasia na skauti wakiulinda mwenge wa uhuru baada ya kuwasili viwanja vya Bomani wilayani Mbozi.
Mkimbiza Mwenge Kitaifa,Mtumwa Rashid Halfan, kutoka kaskazini Unguja,akivuta pazia kuashiria uzinduzi wa Bweni la wanafunzi wa Kiume wa Sekondari ya Mwalimu Jk.Nyerere iliyopo Tunduma wilayani Mbozi mkoani Mbeya.

sherehe za siku ya kuzaliwa mwanzilishi wa dini ya Sikh Guru Singh Sabha,

Wafuasi wa dini ya Sikh wakiwa katika sherehe hiyo.

salam,

MAELFU ya wafuasi wa dini ya Sikh walijitokeza siku ya Jumapili tarehe 6 Novemba 2011 katika mji wa Southall, Middlesex UK ili kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa dini yao Guru Nanak aliyezaliwa mwaka 1469 nchini Pakistan.

Muasisi wa Dini ya Sikh

Wakati akiwa na umri wa miaka 30 alipotea kwa hali ya miujiza kwa muda wa siku tatu. Alipo rejea alianza kuhubiri, kufundisha na kuandika dini ya Sikh wakati wa maisha yake yote. Pia Guru Nanak alisafiri dunia nzima kuitangaza na kujadili dini hii kwa waumini wengine kama waislamu pamoja na Wahindu.

Kwa miaka zaidi ya 550 wafuasi wa dini hii wamekuwa na desturi hii ya kusherehekea siku moja kabla ya kuzaliwa kwake Guru Nanak kwa kuandaa maandamano haya makubwa ya Sherehe hii ambayo hufanyika India pamoja na baadhi ya sehemu za nchi ya Uingereza.

Kwa kawaida sherehe hizi huongozwa na wafuasi wakuu watano wanaojulikana kama "Panj Piare" wakiambatana na waimbaji, wanamuziki na timu ya wacheza Upanga (Martial Arts) kuelekea hekaluni kwao "Gurdwara" Sri Guru Singh Sabha, hapa Southall hekalu lao ndio kubwa kuliko yote katika bara la ulaya.

Sherehe hizi huanza mapema asubuhi kwa kuimba, kuomba kwa pamoja. Baadae chakula cha kitamaduni kinachojulikana kama "Langar" hutolewa bure kwa kila mtu.

Maandamano ya Southall yanaitwa Nagar Kirtan,

Asanteni,

New