My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, December 20, 2011

WEMA ana kidole Gundu

Na Mwandishi Wetu

Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ametajwa kuwa na kidole chenye gundu.

Kidole cha Wema kinachotajwa kuwa na gundu ni kile cha pete kwa maelezo kuwa kila akivalishwa pete ya uchumba hufarakana ndani ya muda mfupi.

Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Wema huwa na bahati ya kung’ara kwenye uhusiano wa kawaida lakini uchumba ni mzito.

Ripoti ya uchunguzi huo inanyevua kuwa wanaume watatu ambao Wema amewahi kuvaa pete zao za uchumba, wote alitibuana nao muda mfupi baada kumvalisha madini kwenye kidole.

Katika safari ya mapenzi, Wema ameshavaa pete za wanaume watatu, mjasiriamali, Jumbe Yusuf, mwanamuziki wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Charlz Baba’ na mwana-Bongo Fleva, Naseeb…

Na Mwandishi Wetu

Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ametajwa kuwa na kidole chenye gundu.

Kidole cha Wema kinachotajwa kuwa na gundu ni kile cha pete kwa maelezo kuwa kila akivalishwa pete ya uchumba hufarakana ndani ya muda mfupi.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kuwa Wema huwa na bahati ya kung’ara kwenye uhusiano wa kawaida lakini uchumba ni mzito.

Ripoti ya uchunguzi huo inanyevua kuwa wanaume watatu ambao Wema amewahi kuvaa pete zao za uchumba, wote alitibuana nao muda mfupi baada kumvalisha madini kwenye kidole.

Katika safari ya mapenzi, Wema ameshavaa pete za wanaume watatu, mjasiriamali, Jumbe Yusuf, mwanamuziki wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Charles Gabriel Mbwana ‘Charlz Baba’ na mwana-Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond’.

JUMBE
Wema alipoanza mahaba na Jumbe, ikawa patashika. Nchi nzima ikatambua kwamba mtoto huyo wa Balozi Isaac Abraham Sepetu, yupo kwenye uhusiano wa kimapenzi na kijana wa Kingazija, Jumbe.

Kumbukumbu zinafunua kuwa kutokana na kukolea kimapenzi, wakaishi pamoja Tabata, Dar es Salaam.

Data zinaonesha kuwa baada ya kuishi kwa muda mrefu kidogo, huku wakiitana mke na mume, waliamua kuvuka hatua moja kwa Jumbe kumvisha pete ya uchumba Wema.

Hata hivyo, pete hiyo haikuwa na matunda, kwani baada ya mwezi mmoja, waliachana.

CHARLZ BABA
Wema alipoachana na Jumbe, alijirusha kwa muda na Mkurugenzi wa Hartmann Production, Hartmann Mbilinyi kabla ya kutua kwa Charlz ambaye aling’ara naye kiasi kwamba zikaibuka taarifa kuwa watafunga ndoa.

Kuthibitisha upendo wake, Charlz alimvalisha pete ya uchumba ambayo iliibua matokeo mabaya pia, kwani muda mfupi baadaye Wema alikwenda Marekani na akiwa huko alivunja uhusiano na mwana Twanga Pepeta huyo, aliporudi nchini alitua moja kwa moja kwenye mikono ya Diamond.

DIAMOND
Walikuwa kama watoto, wakijifungia ndani wanapiga mapicha ya denda na mapozi mbalimbali ya kimahaba.

Dhahiri, ilionekana wanaendana, kwa hiyo kilichosubiriwa ikawa ndoa. Kukaribisha hatua hiyo, Diamond aliitumia siku yake ya kuzaliwa kumvalisha pete Wema ndani ya New Maisha Club.

Kama kawaida, balaa likafuata baada ya pete, kwani wiki moja na nusu baadaye, Diamond alitangaza kuachana na Wema kwa madai kwamba ni mvivu kwenye kazi za nyumbani, vile vile hampendi mama yake.

Pamoja na Wema kuomba msamaha na kurudiana kwa shinikizo la mama wa Diamond, imeonekana ‘bwa mdogo’ huyo alishaamua kuangalia mbele, kwani hivi karibuni yameibuka madai kwamba yupo katika uhusiano wa kimapenzi na Miss Tanzania namba mbili mwaka 2006-07, Jokate Mwegelo.

WEMA
Katika maelezo yake kuhusu kuachana na wanaume wake, alisema kuwa jamii humuona ni malaya lakini ukweli ni kwamba hujitahidi kuvumilia na anapoinua mikono maana yake ameshindwa kwa njia zote.

Hii inamaanisha kuwa Wema anaamini matatizo yapo kwa wanaume wake ambao huwavumilia mno lakini mwisho hushindikana.


No comments:

Post a Comment

New