My Web

Emmanuel

CONTACT

Saturday, December 31, 2011

wolper ala Kristmasi kitandani

Na Erick Evarist

Sura ya mauzo kunako Bongo Movie, Jacqueline Wolper amejikuta akila Sikukuu ya Krismasi kitandani baada ya kushindwa kujikinga na ‘anopheles’ mdudu anayeambukiza ugonjwa wa Malaria.

Habari kutoka kwa mtu wa karibu na nyota huyo zinasema Wolper alibanwa na homa hiyo kiasi cha kushindwa kutoka nje hivyo kuisikia sikukuu kwenye redio tu.

“Duh! Jamani shosti ‘angu ameshindwa ku-enjoy sikukuu na hivi ninavyomjua anapenda kujiachia, lo!” alisema rafiki wa karibu wa Wolper.

Akizungumza kwa tabu kwa njia ya simu na paparazi wetu, Wolper alikiri ‘kupigwa’ na malaria siku hiyo na kudai kwa sasa hajambo, anaendelea vizuri baada ya kutumia dozi.

“Kwa sasa naendelea vizuri kwa kweli, namshukuru Mungu, lakini nilikuwa hoi sikukuu yote hii,” alisema Wolper.

No comments:

Post a Comment

New