My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, July 2, 2013

dinner in Pretoria



  • The president meet briefly earlier on Saturday with members of Mandela's family and spoke on the phone to the ailing leader's wife
  • He is not now planning to see the man he has called a personal hero
  • The First Lady also spoke to young South Africans and shared her own story of growing up without wealth and facing doubts

The President and First Lady ended a busy first full day in South Africa by attending an official dinner along with South African president Jacob Zuma and first lady Thobeka Madiba-Zuma in Pretoria on Saturday evening.
Michele Obama looked stunning in a pleated one-shoulder evening dress which looked to incorporate all the colors of a South African sunset.
The Obamas are staying in nearby Johannesburg overnight before stopping in Cape Town on Sunday and visiting Robben Island, the prison where Mandela spent 18 of his 27 years in jail.
Scroll down for video
President Obama and First lady Michelle Obama are greeted by South Africa's President Jacob Zuma and South African First lady Thobeka Madiba-Zuma at an official dinner in Pretoria on Saturday
President Obama and First Lady Michelle Obama are greeted by South Africa's President Jacob Zuma and South African First Lady Thobeka Madiba-Zuma at an official dinner in Pretoria on Saturday evening
First Lady Michelle Obama looked stunning in a pleated one-shoulder evening dress which looked to incorporate all the colors of a South African sunset
First Lady Michelle Obama looked stunning in a pleated one-shoulder evening dress which seemed to incorporate all the colors of a South African sunset
Obama's stop in South Africa marks the midway point of a week-long trip to Africa, his most significant engagement with the continent since taking office in 2009. The trip will close with a visit to Tanzania.
Earlier in the day Michelle Obama challenged young adults in South Africa to channel the hope that former President Nelson Mandela held while imprisoned for 27 years during racist white rule.

JINSI MAANDALIZI YA UJIO WA OBAMA IKULU YALIVYOKUWA








OBAMA KUKANYAGA ARDHI YA TANZANIA LEO


Rais wa Marekani, Barack Obama anatua nchini kwa ziara ya siku mbili ikiwa ni hatua yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.
Dar es Salaam. Yametimia! Baada ya siku kadhaa za kusubiri kwa hamu, vitabu vya historia ya Tanzania vinaongezewa kumbukumbu wakati Rais wa Marekani, Barack Obama atakapowasili nchini leo mchana kwa ziara ya siku mbili. Ndege ya Air Force One itakayombeba  Obama na msafara wake itakanyaga ardhi ya Tanzania saa 8.40 mchana kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ambako atapokelewa na mwenyeji wake, Rais Jakaya Kikwete.
 Obama ambaye anafuatana na mkewe Michelle na binti zake, Malia na Sasha, anatua Tanzania ikiwa ni sehemu yake ya mwisho ya ziara yake barani Afrika.


Anawasili Tanzania akitokea Afrika Kusini ambako alikwenda Ijumaa baada ya ziara yake ya Senegal.
Historia imetimia
Imepita miaka 50, tangu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere alipotembelea Marekani, Julai 13, 1963 na kukutana rais wa nchi hiyo wakati huo, John F Kennedy na ziara hiyo inaaminika kuanzisha urafiki wa viongozi hao ambao umedumu hadi sasa. 
Ujio wa Rais Obama una maana na faida kubwa kwa Tanzania katika maeneo ukiangalia kihistoria, kisiasa, kidiplomasia na kiuchumi pia.
Ziara ya  Obama ni heshima kubwa kwa Tanzania na itaingia katika vitabu vya kihistoria kwani ana rekodi ya kuwa mtu mweusi wa kwanza kuchaguliwa kuongoza taifa la Marekani. Kuchaguliwa kwake (Obama), ambaye baba yake mzazi alikuwa na asili ya Kenya kuliashiria nuru mpya kwa siasa za Marekani kwani watu weusi wa taifa hilo kwa miaka mingi walikuwa wakipigania haki za kufaidika na fursa za kiuchumi na kisiasa katika taifa la Marekani.
Tanzania, kwa miaka mingi ilikuwa inaunga mkono harakati za watu weusi na ndiyo 


iliikuwa karibu na viongozi wa harakati za kupigania haki za watu weusi.
Mwalimu Julius Nyerere alikuwa karibu na Martin Luther King na mkewe Correta , ambao waliongoza harakati za mtu mweusi kujikomboa.Pia, viongozi wengine wa harakati hizo za mtu mweusi kutambuliwa kule Marekani, Jesse Jackson, Andrew Young na Malcolm X waliitembelea Tanzania mara nyingi.    Obama alipochaguliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2008 alifurahiwa na wapenda amani kote duniani na hasa Waafrika kwani walimhesabu kuwa ni sehemu yao.
Kuja kwake leo ni heshima kubwa kwani Tanzania inakuwa nchi ya nne  Afrika kutembelewa na Obama baada ya Ghana mwaka 2009 na ziara yake ya hivi karibuni ya nchi za Senegal na Afrika Kusini.
Ukizingatia kuwa  Obama  ana miaka mitatu na nusu kabla ya kumaliza kipindi chake cha pili cha uongozi wake huenda ziara hii ndiyo ikawa ya mwisho kwake barani Afrika akiwa na wadhifa wa rais.

Mapokezi ya obama Ikulu jijini Dar es salaam

ob1 36bee

ob2 cfb21

ob3 0d344


ob4 1ef66




ob5 49977

ob6 40198
Rais Barack Obama wa Marekani na mkewe Michelle Obama akipokewa kwa Shangwe Ikulu, Dar es salaam
na baadaye akaongea na wanahabari

Monday, July 1, 2013

HISTORIA YA MAISHA YA MAPENZI YA MZEE MADIBA!



BABA wa Taifa la Afrika Kusini na kipenzi cha wengi, Nelson Rolihlahla Madiba Mandela ‘Mzee Madiba’ (94), anabaki kuwa mmoja wa mashujaa walioongoza vita dhidi ya ubaguzi wa mtu mweusi hapa duniani ukiwaacha akina Martin Luther King aliyekuwa uhamishoni Marekani, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wa Tanzania, Patrick Lumumba wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, zamani Zaire, Nkwame Nkuruma wa Ghana na wengineo.

Kwenye makala haya sitazungumza ‘profaili’ ya Mzee Madiba isipokuwa nimenyofoa kipengele kimoja tukijadili.
Tunajua katika maisha kuna wakati mtu unakutana na vipingamizi vya kufikia malengo kutoka ndani ya familia au jamii inayokuzunguka.

MCHANGO WA KIFAMILIA
Baba yake alifariki dunia wakati Mzee Madiba akiwa na umri wa miaka tisa tu kwa hiyo hakuna mchango wa mzazi huyo kwenye harakati zake.
Alipoanza mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi na kutafuta usawa kwa wote, ilitegemewa kuwa mkewe ndiye angekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mafanikio yanapatikana.

Mzee Madiba alioa mara tatu. Mke wa mwisho alimuoa alipokuwa akiadhimisha miaka 80 ya kuzaliwa.
Mzee Madiba katika kipindi chote cha historia ya maisha yake amekuwa mtetezi wa watoto kupitia Mfuko wa Nelson Mandela wa kusaidia watoto.
Mzee Madiba ni baba wa watoto sita. Wanne aliwazaa na mkewe wa kwanza, Evelyn Mase na wawili alizaa na mke wake wa pili, Winnie Madikizela Mandela.
Baadhi ya watoto wake hawakwenda kumuona wakati akiwa gerezani.
Maajabu! Watoto wake wote wawili wa kike aliowazaa na mke wa kwanza walikuwa wakitumia jina la Makazawie!

Mtoto wake wa kwanza alifariki dunia akiwa na umri wa miezi tisa na mtoto wa pili aliyejulikana kwa jina la Madiba Thembikile (Thembi) alifariki dunia katika ajali ya gari mwaka 1969 akiwa na umri wa miaka 25.
Masikini! Mzee Mdiba wakati huo alikuwa gerezani na hakuruhusiwa kwenda kuhudhuria mazishi ya mwanaye.

Mwanaye Makgatho alifariki dunia kwa Ugonjwa wa Ukimwi mwaka 2005. Watu walipotaka kuficha kilichomuua, Mzee Madiba aliingilia kati na kusema hadharani kuwa Ukimwi ndiyo umemuua! Kuanzia hapo Mzee Madiba amekuwa mstari wa mbele kupiga vita Virusi vya HIV na Ukimwi akitumia namba 46664 ambayo ni namba aliyopewa alipokuwa gerezani.

Mzee Madiba na Evelyn walidumu katika ndoa yao kwa miaka 13 kabla ya kuvunjika mwaka 1957.
Evelyn alikuwa muumini wa Dhehebu la Mashahidi wa Yehova ambalo lilikuwa haliruhusu waumini wake kushiriki kwenye siasa, akashindwa kumsapoti mumewe, Alifariki dunia mwaka 2004.
Mwaka mmoja baadaye,1958 Mzee Madiba alimuoa Winnie Madikizela. Winnie Madikizela Mandela aliyezaliwa Sauzi Septemba 26, 1936. Ni mwanasiasa aliyewahi kushika nafasi kadhaa serikalini, kama vile African National Congress Women’s League. Kwa sasa ni mwanachama katika Chama cha National Executive Committee. Japokuwa aliolewa na Mzee Madiba, wakati mzee huyo anapata urais hakuwa ‘first lady’ kwani wawili hao, waliachana miaka miwili baadaye kwa madai ya kuwa Winnie, alikuwa siyo mwaminifu baada ya Mzee Madiba kutoka gerezani ambapo alimpa talaka rasmi Machi 19,1996.

Pamoja na kuwa mpiganiaji haki na maarufu kwa wanachama wake ambao humwiita ‘Mama wa Taifa’ lakini alishindwa kuzuia tamaa ya mwili na kujikuta akimsaliti Mzee Madiba.
Muda mwingi hawakuishi pamoja kwa sababu Mzee Madiba alikuwa akitumikia kifungo huku Winnie akijijengea umaarufu katika majukwaa ya siasa.

Mwaka 1998, Mzee Madiba alimuoa Graca Machel ambaye alikuwa mke wa kwanza wa Rais wa Msumbiji, Hayati Samora Machel. Wameishi wote katika siku zao za uzeeni huku wakipeana sapoti ya hali ya juu bila mtoto

KATIKA UFUNGUZI WA MKUTANO WA SMART PARTNERSHIP DIALOGUE 2013

 


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na viongozi mbalimbali pamoja na vijana 
wa umri wa CPTM 29ers waliohudhuria mkutano wa Smart Partneship Dialogue 2013 
wakati wa ufunguzi rasmi wa mkuatno huo unaoshirikisha watu zaidi ya 800 katika 
Ukumbi wa Mwalimu Nyerere Convention Centre jijini Dar es salaam Ijumaa Juni 28, 2013
Rais Kikwete na viongozi mbalimbali wa nchi za Afrika wakishiriki katika 
mijadala na vijana wa CPTM 29ers
Viongozi mbalimbali wa nchi za Afrika wakishiriki katika mijadala na vijana 
wa CPTM 29ers
Mjadala ukiendelea
Rais wa Sri Lanka akishiriki mjadala na vijana wa CPTM 29ers

Wengi wamtakia Mandela afya njema

Mamia ya watu wanaendelea kukusanyika nje ya hospitali alikolazwa Nelson Mandela mjini Pretoria Afrika Kusini. Inaarifiwa Mandela bado yuko hali mahututi.
Wamekuwa wakimuimbia nyimbo na kumuombea nje ya hospitali. Wengine wamekusanyika katika iliyokuwa makaazi ya Mandela mtaani Soweto.
Watu wana wasiwasi kuhusu hali y mandela lakini pia wanataka kuonyesha wanavyojivunia kiongozi wao ambaye wanamuona kama baba wa taifa lao.
Mandela , rais wa kwanza mweusi Afrika Kusini, anaugua maradhi ya Mapafu.
Mamia ya wananchi walikesha kwa maombi maombi nje ya makaazi ya zamani ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Nelson mtaani Soweto.
Rais Jacob Zuma amesema kuwa afya ya shujaa huyo aliyepigana dhidi ya ubaguzi wa rangi nchini humo inaendelea kuimarika.
Mandela aliye na umri wa miaka 94 amekuwa hospitalini akiuguwa ugonjwa wa maambukizi ya mapafu.
Awali mwanawe wa kike, Makaziwe alisema afya ya babake inaendelea kuwa njema.
Aidha Makaziwe amevikashifu vyombo vya habari kwa kukita kambi nje ya hospitali alikolazwa shujaa huyo akisema wanahabari wanapaswa kumheshimu babaake.
Rais Jacob Zuma alisema Alhamisi kuwa hali ya Mandela iliimarika lakini bado yuko hali mahututi.
"leo angalau yuko sawa kidogo kuliko nilivyomwacha jana usiku,'' alisema Rais Zuma baada ya kuongea na madakatari wanaomtibu Mandela.
Bwana Zuma alifutilia mbali safari yake ya Msumbiji ili kumtembelea Mandela hospitalini.
Wakati huohuo mwanawe Mandela Makaziwe alisema Mzee 'bado yupo' na kuwa anaweza kuhisi mtu akimgusa.

Obama akutana na rais Zuma



Rais Obama na rais Jacob Zuma wakiwahutubia waandishi wa habari

Rais wa Marekani Barack Obama, amesema uvumilivu na ujasiri wa Nelson Mandela ni mfano mwema kwa dunia na upendo wa dhati wa rais huyo wa zamani wa taifa la Afrika Kusini inaonyesha ni kwa namna gani alivyo na utu wa kibinadamu.
Bwana Obama ameongeza kuwa Mandela, alionyesha ukweli na ukakamavu ambao una maana kubwa katika utu wa kibinadamu ambao uliondoa tabaka la ubaguzi, udini na utaifa.
Rais huyo wa marekani ameyazungumza hayo mjini Pretoria baada ya mazungumzo na rais wa sasa wa Afrika kusini, Jacob Zuma.
Ziara hiyo ya bwana Obama ina lengo la kuongeza mauhusiano ya kibiashara lakini imetekwa na hisia za ugonjwa wa bwana Mandela ambaye amelazwa hospitalini kwa muda wiki tatu sasa kutokana na maradhi ya mapafu yanayosumbua mfumo wake wa kupumulia.

Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela

Katika kikao hicho wawili hao walizungumza na vyombo vya habari kuhusu ushirikiano wa mataifa yao kibiashara mbali na kutafuta suluhu ya kudumu katika mataifa yaliokumbwa na ghasia mashariki ya kati.
Ikulu ya White House imesema kuwa Obama pia atakutana na familia ya Mandela anayeugua maambukizi ya mapafu ili kuifariji.
Awali Rais Obama, aliye ziarani barani afrika alitoa shukran za dhati kwa uongozi ulioonyeshwa na Mandela.
Wakati wa ziara hiyo Obama pia atakutana na wanafunzi huko Soweto kabla ya kuelekea katika jela la Robben Island ambayo Mandela alihudumia kifungo chake cha miaka 27 wakati wa utawala wa ubaguzi wa rangi..

WATANZANIA WAONDOLEWA HOFU JUU YA ZIARA YA RAIS OBAMA LEO, BARABARA ATAKAZOTUMIA ZATANGAZWA

Rais Jakaya Kikwete kushoto akiwa na Rais Barack Obama
....................................................................................
 
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, SAID MECK SADICK, amesema serikali imechukua tahadhari zote katika kuhakikisha shughuli zote za wananchi za kibiashara zinaendelea kama kawaida wakati wa ziara ya rais wa Marekani Barack Obama.
 
Aidha mkuu huyo wa mkoa amesema katika kipindi hicho wafanyabiashara kutoka mikoani na ndani ya jiji wataendelea kuingiza bidhaa zao katika masoko kama kawaida bila kuzuiliwa, na kwamba si barabara zote zitakazofungwa na kutolea mfano wa barabara itakayofungwa kuwa ni barabara ya Nyerere ambayo wageni wengi hutumia na kwamba ziara hiyo haitaathiri maonesho ya 37 biashara maarufu kama sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. JULIUS NYERERE.
 
Rais wa Marekani Barack Obama anatarajia kuzuru Tanzania siku ya jumatatu ambapo miongoni mwa masuala atakayoangazia ni pamoja na kuhamasisha demokrasia na kukuza fursa za kiuchumi.
 
Maandalizi ya mapokezi ya Rais Obama yamezidi kupamba moto hasa katika jiji la Dar-es salaam ambapo ndipo kituo chake cha kwanza kwa rais huyo nchini Tanzania huku suala la usafi na matengenezo katika barabara nyingi Jijini likionekana kupewa kipaumbele tofauti na siku zote.
 
Pia abiria wa ndege na wale wa mabasi ya mikoani wametakiwa kuripoti mapema katika vituo vyao ili kuepuka kukosa usafiri siku hiyo ,huku akitaka mabasi ya mikoani ambayo yanaondoka baada ya saa 3 kuzingatia muda kwani baada ya saa 3 barabara zitafungwa hivyo kukosa kusafiri hadi ugeni utakapoondoka
 
Pia  jeshi la  polisi nchini na lile  ya Marekani likakuwa linaweka  rekodi ya matukio yote kwa maeneo yote ambayo Rais Obama atapita  hivyo kwa wale  watakaofanya vurugu  watafuatiliwa popote duniani

New