My Web

Emmanuel

CONTACT

Saturday, July 25, 2015

Marekani yakosoa ushindi wa Nkurunziza

Waziri wa masuala ya Nje wa Marekani John Kerry amekashifu matokeo ya uchaguzi ya Burundi yaliyotolewa hapo jana ambapo rais Pierre Nkurunziza alitangazwa kusajili ushindi mkubwa.
Kerry ametaja uchaguzi huo kuwa ukiukaji mkubwa wa katiba na kejeli kwa mfumo wa haki huku akimlaumu rais Pierre Nkurunziza kwa ghasia zilizotokea nchini humo wiki chache kabla ya kufanyika uchaguzi.
 
Rais Nkurunziza alitangazwa mshindi na asilimia 70 ya kura
Katika taarifa kwa vyombo vya habari saa chache zilizopita, waziri huyo wa mambo ya nje wa Marekani amesema kuwa amesikitishwa kwa namna rais Nkurunziza ameiponda katiba ya nchi na kupuuza mkataba waliosaini mjini Arusha miaka kumi na tano iliyopita.
Amesema kuwa rais huyo ametumia mbinu ghushi kung'ang'ania madarakani katika uchaguzi ambao sio huru wala wa haki.
 
 
Kerry anasisitiza kuwa mazungumzo ya amani yafanyike
Kerry amesisitiza kuwa ni lazima pande zote husika nchini humo zirudi katika majadiliano ya dhati na kuhusisha pia mashirika ya kijamii.
Amesema kuwa hii ndio njia ya pekee ya kurejesha imani sio tu ya raia wa Burundi bali jamii ya kimataifa pia, na kuzuia ghasia zaidi nchini humo zilizosababisha watu kuikimbia nchi.
Hapo jana tume huru ya uchaguzi nchini Burundi ilitangaza kuwa rais Nkurunziza amepata asilimia karibu sabini ya kura zilizopigwa katika uchaguzi huo uliofanyika siku ya Jumanne wiki hii.
 
 
Kerry amesisitiza kuwa ni lazima pande zote husika nchini humo zirudi katika majadiliano
Kura katika majimbo zinatarajiwa kutangazwa katika kipindi cha wiki moja ijayo.
Viongozi wakuu wa upande wa upinzani nchini Burundi walisusia uchaguzi huo,lakini majina yao yalisalia katika karatasi za kupigia kura.
Kiongozi wa upinzani Agathon Rwasa alimaliza katika nafasi ya pili akizoa asilimia kumi na tisa ya kura zilizopigwa.

Obama: Uchumi wa Afrika umeimarika sana






Rais wa Marekani Barrack Obama amesifu uwezo wa biashara na uchumi wa bara Afrika kwenye hotuba yake ya kwanza tangu aingie nchini Kenya siku ya Ijumaa.
"Africa inasonga mbele,.. watu wanainuliwa kutoka kwa umasikini.


'' mapato yanapanda na idadi ya matajiri inaongezeka’’
Obama alisema hayo kwenye hotuba ya uzinduzi wa Kongamano la wajasiria mali.
Rais Obama alizuru kumbukumbu ya ubalozi wa Marekani uliolipuliwa na bomu mwaka wa 1998, kabla ya majadiliano ya usalama na rais wa Kenya katika ikulu ya Nairobi.
Obama ni rais wa kwanza wa Marekani kuzuru nchi ya Kenya.



Ziara hii imetajwa kama kurejea nyumbani na vyombo vya habari vya Kenya, huku mamia ya watu wakijitokeza kumshangilia rais huyo ambaye baba yake ni mzaliwa wa Kenya.
Shughuli ya kwanza ya Obama ilikuwa ni kuhutubia Kongamano la wajasiria mali kutoka mataifa 120 kote duniani.
Alisema Afrika yapasa kuwa chemchemi ya maendeleo ya siku za usoni, na kuongeza kuwa serikali zinafaa kuhakikisha kuwa ufisadi haukiti kambi.



Aidha Obama alinena kuwa Kenya imeendelea sana tangu awe nchini humo mara ya mwisho. ‘nilipokuwa hapa Nairobi miaka kumi iliyopita, ilikuwa tofauti sana na ilivyo sasa’.
Rais Obama hivi sasa yuko katika ikulu ya Nairobi anakotarajiwa kutia sahihi makubaliano ya kiuchumi baina ya taifa lake na Kenya.
 

Tuesday, July 21, 2015

Burundi wamiminika uchaguzi wa rais

Bujumbura, Burundi
Kumetokea ufyatulianaji wa risasi na milipuko usiku kucha nchini Burundi, usiku wa kuamkia uchaguzi wa rais uliozua utata. Kiongozi wa sasa wa nchi hiyo anawania muhula wa 3 kama rais licha ya madai kuwa anakwenda kinyume na katiba ya nchi.
Viongozi wengi wa upande wa upinzani wameapa kususia uchaguzi huo.

NI KWELI MAYAI HUSABABISHA UGONJWA WA MOYO?

UTAFITI uliofanywa nchini Marekani hivi karibuni unaonesha kuwa katika miaka ya 1950, wastani wa ulaji wa mayai ya kuku ulikuwa mayai 375 kwa mtu mmoja, lakini hadi kufikia mwaka 2007, kiwango hicho kimepungua hadi kufikia mayai 250 tu kwa mtu mmoja, ikiwa ni punguzo la asilimia 33.

MADHARA YA WANAFUNZI KUTOKUPENDA SHULE


Wanafunzi wengi wamekuwa na tabia ya kutokupenda shule. Wengi wao ukiwaliza kwa nini hutoroka masomo na kwenda kwenye makundi yasiyofaa hawajui msingi wake; pengine watakujibu kwa Kiswahili cha kisasa: “Shuleni kunaboa.” Yaani hakufurahishi.
Lakini ukweli ni kwamba mwanafuzni yo yote ambaye hapendi shule moja kwa moja anakuwa amejiingiza kwenye kundi la watu ambao hawawezi kufaulu mitihani na hivyo kujikuta akiwa mtu wa kukabiliana na changamoto wanazokutana nazo watu ambao hawajasomo; moja kati ya hizo ni kutoheshimiwa, kushindwa kumudu maisha ya kisasa na kutopata nafasi ya kuajiriwa.
Hii ina maana kwamba; kabla mwanafunzi hajaanza safari ya kutafuta ufaulu katika masomo yake, ni lazima ajenge au ajengewe mazingira ya kupenda shule. Kazi hii ifanywe na mwanafunzi mwenyewe, wazazi au waalimu wake ambapo dokezo za kufanikisha jambo hili ni :

TATIZO LA KUTOKWA NA HARUFU MBAYA MWILINI

Harufu mbaya ni kitu kisichompendeza mtu yeyote. Unapotoa harufu mbaya toka mwilini mwako, haikupendezi wewe mwenyewe wala mtu wa jirani. Kama kitu hukipendi wewe na ukakiona hakifai basi usimlazimishe mwenzio akipende au akione cha kawaida.

Harufu mbaya mwilini inatoka maeneo yote ya mwili kuanzia kichwani hadi miguuni.
Zipo sababu nyingi zinazomfanya mtu atokwe na harufu mbaya, inaweza kuwa uchafu, maradhi au maumbile.
Hali ya uchafu ipo wazi endapo mtu haogi, hafui au hanawi. Uchafu wa kichwani inaweza kuwa nywele au wigi au kitu chochote kinachowekwa kichwani.Uchafu unaweza kuwa maeneo mbalimbali ya mwili.
Maradhi ya ngozi, kansa au vidonda vyenye maambukizi vinaweza kusababisha kutoa harufu mbaya au vitambaa vilivyofungiwa vidonda.
Kwa hiyo kundi la maradhi ni pana kwa kuwa tatizo la ngozi pekee linaweza kuathiri kwa kiasi kikubwa.
Sababu za kimaumbile linawahusu zaidi watu wanene ingawa hata wembamba pia wanaweza kupatwa na tatizo hili kutegemea na harufu inatoka eneo gani la mwili.
Watu wanene hupatwa na matatizo ya kutoa harufu mbaya kama hawatazidisha usafi na kuhakikisha miili yao sehemu za mikunjo inakuwa mikavu. Sehemu hizo ni chini ya kifua au matiti, nyama za tumboni, chini ya tumbo, mbavuni, sehemu za siri na mapajani.
Unene pamoja na matatizo mengi yanayoweza kujitokeza pia huweza kusababisha magonjwa ya ngozi na kutokwa na jasho lenye harufu kali.
MAENEO YANAYOTOA HARUFU MBAYA
Sehemu yoyote ya mwili inaweza kutoa harufu mbaya kama tulivyoona hapo mwanzoni kuanzia kichwani hadi miguuni. Lakini yapo maeneo kama masikioni na puani pia harufu mbaya hutoka. Harufu za maeneo hayo mara nyingi haziwi kali.

KUTOKWA HARUFU MBAYA KINYWANI
Tatizo la kutokwa na harufu mbaya mdomoni au kinywani hutokana na matatizo mbalimbali kama kuwa na meno mabovu, magonjwa ya fizi, ulimi, fangasi za kinywani na uchafu kutokana na kutosafisha kinywa vizuri.
Wapo watu ambao kwa asili hutoa harufu mbaya kinywani pasipo kuwa na magonjwa ya kinywa na huwa makini kusafisha kinywa, lakini harufu haiishi.
Tatizo hili hutibika baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kina katika tabaka linalotandika ndani ya kinywa.
Wakati mwingine harufu mbaya ya kinywa husababishwa na ulaji wa vyakula, unywaji pombe, uvutaji wa sigara, bangi na ugoro.
KUTOKWA NA HARUFU MBAYA KWAPANI
Kutokwa na harufu mbaya kwapani au kunuka kikwapa inatokana na mambo mbalimbali hata kama unajisafisha mara kwa mara na kutoa vinyweleo vya kwapani.
Harufu ya kikwapa husababishwa na njia ambazo ngozi ya kwapani hupumua zinaziba, hivyo kusababisha njia za kutolea jasho kuwa chache na jasho kutoka kidogo kidogo na kujaa kwapani.
Hivyo kujaa na kulowesha nguo sehemu hizo, hali hii ikiendelea kwa muda mrefu husababisha bakteria aina ya ‘staphylloccocus’ kuanza kuishi hapo na jasho linalojirundika kukauka na kuganda, hivyo kutoa harufu mbaya.
Tatizo la kikwapa likiendelea kwa muda mrefu baadhi ya njia za jasho huziba kabisa na bakteria kujipenyeza. Hapo ndipo unaweza kusumbuliwa na majipu ya mara kwa mara kwapani, kutokwa na vipele vikubwa kwapani na muwasho mkali baada ya kunyoa kwapani na hata vidonda vidogovidogo.
Matumizi ya baadhi ya pafyumu husababisha mzio ambapo kwapa litawasha sana kila wakati au utatokwa na vipele vingi au ngozi ya kwapani inabadilika na kuwa nyeusi sana huku ikitoka harufu mbaya. Tatizo hili linaweza kutibika hospitali.
HARUFU MBAYA SEHEMU ZA SIRI
Harufu mbaya sehemu za siri inaweza kuwa kwa wanaume na wanawake. Zipo sababu mbalimbali kwa wanaume ambazo zinahitaji uchunguzi wa kina na tiba.
Kwa wanawake harufu inaweza kutoka ukeni ikiambatana na uchafu au la. Harufu ya ukeni huwa mbaya inayofanana na shombo la samaki hutokana na kutokuwa makini kiusafi.
Maambukizi ya fangasi na bakteria, magonjwa ya zinaa, kisonono na kaswende ni sababu mojawapo.
Wapo wanawake ambao hutokwa na harufu sehemu za siri kutokana na mikunjo ya kwenye mapaja yao, hasa kwa wale wanene. Harufu pia inaweza kutoka katika sehemu ya haja kubwa na hii ni ya kinyesi endapo hutanawa vizuri au kuwa na maradhi sehemu hiyo.
NINI CHA KUFANYA?
Endapo utakuwa na tatizo hili la kutoa harufu mbaya maeneo tofauti ya mwili au unahisi mwenzio ana tatizo hili na anakukwaza, inashauriwa uwaone madaktari katika hospitali za wilaya kwa uchunguzi wa kina.
Tatizo hili linatibika na hupotea kabisa na kukuacha huru. Tatizo la kutokwa na majipu, vipele, kubadilika rangi ya ngozi kwapani, chini ya matiti na sehemu za siri, pia linatibika kabisa endapo utawaona wataalamu. Wahi mapema hospitali.

JAJI MARK BOMANI MGENI RASMI UTOAJI TUZO KWA WATANZANIA WALIOTOA MCHANGO MKUBWA KUTETEA HAKI NA JAMII NCHINI DAR ES SALAAM JANA‏

Jaji mstaafu Mark Bomani (kulia) akimkabidhi Tuzo ya maono mapevu, Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila.

Jaji mstaafu Mark Bomani akimvisha skafu yenye Neno Tanzania Mkurugenzi wa Under the Same Sun,Vicky Ntetema.
Jaji mstaafu Mark Bomani akimkabidhi Tuzo ya  uwazi na ukweli  Mkurugenzi wa Under the Same Sun,Vicky Ntetema tuzo ya ubunifu, tuzo ambazo zimetolewa na taasisi ya Dream Success Enterprises.

Tuesday, July 14, 2015

HIV goal to treat 15 million is met


Drawing blood

The goal to get HIV treatment to 15 million people by the end of 2015 has already been met, says the United Nations Aids agency.

The landmark figure was reached in March - nine months ahead of schedule.

It follows decades of global efforts and investment to get antiretroviral drugs to those in need - such as people living in sub-Saharan Africa.

In 2000, when the UN first set goals to combat HIV, fewer than 700,000 people were receiving these vital medicines.

According to UN Aids, which has a report out today, the global response to HIV has averted 30 million new HIV infections and nearly eight million Aids-related deaths since the millennium.

Over the same time frame, new HIV infections have fallen from 2.6 million per year to 1.8 million, and Aids-related deaths have gone down from 1.6 million to 1.2 million.

Meanwhile, global investment in HIV has gone up from £3.1bn ($4.8bn) in 2000 to more than £13bn ($20bn) in 2014.

And concerted action over the next five years could end the Aids epidemic by 2030, says UN Aids.

But progress has been slower in some areas.

Ending Aids

A major gap seems to be in awareness of HIV status, which is the biggest barrier to treatment access, says the report.

And treatment access for children has lagged behind adults - although this is now improving.

The proportion of children living with HIV who receive antiretroviral therapy almost doubled between 2010 and 2014 (from 14% to 32%), but coverage "remains notably lower than it does for adults", says the report.

Even though new HIV infections have gone down, there is still an unacceptable number of new HIV infections each year, contributing to the burden of the epidemic.

In 2014, sub-Saharan Africa accounted for 66% of all new HIV infections. And at the last headcount, there were an estimated 25.8 million people in this region living with HIV. The estimated count for the whole world was 36.9 million.

This year sees the switch from Millennium Development Goals to broader Sustainable Development Goals.

Ban Ki-moon, Secretary General of the United Nations said: "The world has delivered on halting and reversing the Aids epidemic.

"Now we must commit to ending the Aids epidemic as part of the Sustainable Development Goals."

The report says the next five years will be critical and recommends front-loading investment to "sprint" towards an ambition of ending the Aids epidemic by 2030.

Saturday, July 11, 2015

Chama tawala nchini Tanzania Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaendelea na mikutano yake ya mwaka.


Moto wawaka chama tawala CCM Tanzania 

Alasiri hii halmashauri kuu ya chama hicho inafanya kikao chake kupata majina matatu, halafu baadae leo jioni mkutano mkuu wa chama hicho unatarajiwa kukaa kupigia kura jina moja kati ya hayo matatu.

Yule atakayeibuka mshindi kati ya watatu hao ndiye atakaye kuwa mgombea urais wa chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu

Hata hivyo kutangazwa kwa majina matano na kamati kuu ya halmashauri kuu ya taifa (CC-NEC) ya chama hicho jana usiku, kuliibua mgawanyiko miongoni mwa wajumbe wa kamati hiyo, ambapo watatu wa wajumbe 32 wa kamati hiyo waliibuka wazi na kupinga uteuzi wa majina hayo mbele ya vyombo vya habari

null
Watanzania kumjua ni nani atakayekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao 

Wajumbe waliopinga uteuzi huo ni Dk. Emmanuel Nchimbi, Sophia Simba na Adam Kimbisa

Wajumbe hao walidai kuwa kanuni za utendaji katika vikao vilivyotangulia kamati kuu zimekiukwa na kufafanua kwamba kamati hiyo ilipokea majina matano kutoka kamati ya maadili na usala, badala ya kupewa majina yote ya walioomba kuteuliwa, halafu yenyewe ndiyo ichambue majina matano.

“Kanuni zinasema Kamati Kuu itapokea majina ya waombaji wote na ikishafanya uchambuzi wa kila muombaji, yakiwemo maoni ya kamati ya usalama na maadili, ndiyo huchagua majina matano yanayofikishwa mbele ya Halmashauri Kuu,” alihoji Dk. Nchimbi

null
Mpasuko huu unaonekana kuwa mwanzo wa kutimia kwa utabiri wa wachambuzi mbalimbali

Mpasuko huu unaonekana kuwa mwanzo wa kutimia kwa utabiri wa wachambuzi mbalimbali ambao walionya mchakato huu unahatarisha uhai wa chama kikongwe nchini Tanzania

Majina matano yaliyopitishwa na Kamati Kuu ni Bernard Membe (Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. John Magufuli (Waziri wa Ujenzi) Dk. Asha-Rose Migiro (Waziri wa Katiba na Sheria) January Makamba (Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia) na Balozi Amina Salum Ali (Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Tume ya Umoja wa Afrika kwenye Umoja wa Mataifa, Marekani)

Kufikia Jumapili, tarehe 12. Julai, Watanzania watakuwa wamejua ni nani atakayekuwa mgombea wa urais kwa tiketi ya CCM kwa uchaguzi mkuu ujao

Mchakato wa uchaguzi ccm

https://www.facebook.com/simutv.tz/videos/716680491792398/

Monday, July 6, 2015

Hutoagi wa Leseni kumi (10) wa Redio zilizotolewa na TCRA


Mr. Emmanuel Mallewo Director Storm fm Geita akiwa anapokea Leseni ya Radio 
Akikabidhiwa na Mh. Elizabeth Nzagi wakati wa utoagi wa Leseni hizo.


Mr. Santa chacha akipokea Leseni ya Redio iliyotolewa wakati huo anaempatia
Ni Mh. Elizabeth Nzagi


Hii ndio Leseni iliyotolewa wakati huo huu Ni upande wa nje wa Leseni hiyo


Upande wa ndani wa Leseni hiyo


Mr. Santa chacha akipokea Leseni Kutoka kwa mkurugezi mkuu wa 
TCRA wakati wa utoagi wa leseni hizo


Hawa Ni baadhi ya wachukuaji Leseni za Redio zao kulikuwa na Leseni 
Kumi zilizotolewa wakati huo


Miss Modesta Olga mmoja wa wakurugezi Storm Fm Geita nae akipokea Leseni 
Toka kwa Mh. Elizabeth Nzagi


Mr. Santa Chacha na Miss Modesta Olga wakiwa kwenye picha ya pamoja
Baada ya kutoka nje ya jengo la TCRA.



Baadhi ya mmoja wa Redio kutoka mbeya akisalimiana na Mkurugezi 
Mkuu wa TCRA.




Mr. Emmanuel Mallewo akipiga picha baada ya kutoka kwenye jengo la 
TCRA Mara baada ya kupata Leseni.



Mr. Santa Chacha akipiga picha baada ya kutoka kwenye jengo la 
TCRA Mara baada ya kupata Leseni.



Miss Modesta Olga nae akipiga picha Mara baada ya kutoka kwenye jengo la 
TCRA baada ya kupata Leseni.



Miss Modesta Olga akipiga picha kwenye bango la 
TCRA Mara baada ya kupata Leseni.



Mr. Emmanuel Mallewo akipiga picha baada ya kutoka kwenye jengo la 
TCRA baada ya kupata Leseni.


Mr. Emmanuel Mallewo akipiga picha baada ya kutoka kwenye jengo la 
TCRA Mara baada ya kupata Leseni.






New