My Web

Emmanuel

CONTACT

Thursday, December 17, 2015

Wananchi wa Kenya watamani kuwa na Rais kama Magufuli


Akamatwa Akitorosha Madini Ya Tanzaninte


Hela za Elimu Bure zapatikana Bilioni 131/- zatengwa elimu bure




RAIS John Magufuli amewahakikishia Watanzania kuwa fedha kwa ajili ya kutimiza ahadi ya kutoa elimu bure kwa shule za msingi na sekondari, zimetengwa Sh bilioni 131 mwezi huu na kupelekwa moja kwa moja katika shule husika.

Amesema Wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Mikoa, watapatiwa nakala za taarifa za ugawaji wa fedha hizo na kuonya kuwa hatua kali zitachukuliwa kwa yeyote atakayethubutu kuzitumia vibaya.

Rais Magufuli alisema hayo Ikulu Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe aliyemtumia salamu za pongezi kwa kuchaguliwa kuiongoza Tanzania.

Dk Magufuli aliongeza kuwa fedha hizo ambazo ni pamoja na fedha za maendeleo, fedha za mitihani na fedha vifaa vya ku fundishia zitaanza kutumwa kila mwezi kuanzia mwezi huu.

Katika kipindi cha kampeni, Rais Magufuli aliahidi kutoa elimu bure kuanzia shule za msingi hadi sekondari kidato cha nne na hivi karibuni kupitia Wizara ya Elimu ilitoa waraka maalumu wa kusisitiza agizo hilo la elimu bure.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli amempongeza Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Dk Philip Mpango kwa kazi nzuri ya ukusanyaji wa mapato inayofanywa na mamlaka hiyo.

“Kwa mara ya kwanza mwezi huu ukusanyaji wa mapato hayo unatarajiwa kuwa zaidi ya shilingi trilioni moja na bilioni mia tatu,” alisema Rais Magufuli katika taarifa hiyo iliyotolewa jana na Ikulu.

Rais Magufuli pamoja na mambo mengine, jana alipokea ujumbe maalumu wa maandishi kutoka kwa Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe uliowasilishwa na Waziri wa Nchi anayeshughu likia Mambo ya Nje ya Japan, Seiji Kihara.

Ujumbe huo umemueleza Rais Magufuli kuwa Japan imeridhishwa na hatua ambazo Serikali ya Tanzania inazichukua katika kuharakisha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kuahidi kuongeza msukumo kwa upande wa Japan katika kuharakisha utekelezaji wa miradi inayofadhiliwa na Japan nchini.

Mjumbe huyo juzi alishuhudia utiaji saini wa makubaliano ya ujenzi wa njia ya umeme yenye urefu wa kilometa 441.5 kutoka Singida - Manyara - Namanga na kuunganisha hadi Kenya, ambapo Japan imetoa mkopo wa Dola za Marekani milioni 96 ili kufanikisha mradi huo.

WALIOJENGA PEMBEZONI YA BONDE LA MTO MSIMBAZI WAPITIWA NA BOMOA BOMOA

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na Manispaa za jiji la Dar es salaam zitafanya zoezi la kuondoa wavamizi maeneo yote ya Mabondeni, kingo za mito  na za Bahari, maeneo ya wazi, maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi zaidi ya 150 katika  jiji la Dar es salaam. Bomoa bomoa ya leo inaendelea katika Bonde la mto msimbazi.Mkuu wa Kitengo cha Sheria Balaza la Taifa la usimamizi wa mazingira Tanzania (NEMC), Manchale Heche akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juu ya zoezi la Bomoabomoa maeneo ya miundombinu na maeneo yote hatarishi nakuwataka wananchi waliojenga katika fukwe za bahari Kingo za mito na mikondo ya bahari kuhamisha mali zao mapema.
Wananchi wakitoa samani pamoja na vitu mbalimbali ndani ya nyumba zao ili kupisha ubomoaji wa nyumba zilizo maeneo hatarishi. 

WAZIRI KITWANGA AWAPA POLISI SIKU MOJA YA KUJIELEZA NI KWA NINI HAWALINDI BANDARI YA DAR ES SALAAM


Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga ametoa siku moja kwa Jeshi la Polisi kueleza ni kwa nini askari hawalindi Bandari ya Dar es Salaam badala yake kazi hiyo inafanywa na kampuni binafsi za ulinzi.
Kitwanga amepanga kukutana na viongozi waandamizi wa Polisi kesho ili kujadili mipango na mikakati mbalimbali ya kuongeza ufanisi wa kazi ya kuwahudumia wananchi.
Akizungumza na maofisa waandamizi wa polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam baada ya kufanya ziara katika Chuo cha Taaluma ya Polisi na kuangalia makazi ya askari, Kurasini, Kitwanga alieleza kusikitishwa na hatua ya polisi kuacha kutoa ulinzi bandarini na kuita kitendo hicho kuwa ni udhaifu wa jeshi hilo.
Alisema kitendo hicho kimetoa mwanya kwa baadhi ya wafanyabiashara kukwepa kodi wakati wa kushusha bidhaa zao akisema Bandari ni eneo la mpaka ambalo linahitaji ulinzi wa polisi kama mipaka mingine ya nchi.
Akionekana kukerwa, Waziri Kitwanga alimkatisha Kamishna wa Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alipojaribu kutoa sababu akimtaka kutumia siku nzima ya leo kuandaa majibu ili kesho wayazungumze kwenye kikao rasmi.
Waziri Kitwanga amelitaka pia jeshi la polisi kumweleza mipango ya kukabiliana na dawa za kulevya kwa sababu ndiyo zimekuwa chanzo cha matukio mengi ya uhalifu ikiwamo tishio la ugaidi.
Alisema haiwezekani kitengo cha kupambana na dawa za kulevya kikaachiwa jukumu hilo wakati jeshi la polisi liko kwenye operesheni zake kila siku.
Kuhusu msongamano wa magari katika jiji la Dar es Salaam, waziri huyo alisema ni uzembe wa askari wa usalama barabarani kwa sababu wameshindwa kusimamia sheria na kuwachukulia hatua madereva wazembe.
Alisema zipo nchi za Afrika ambazo hazina askari wa barabarani kwa sababu kiwango cha nidhamu ya madereva wake ni kikubwa na wamekuwa wakifanya vizuri kuhakikisha kwamba suala la msongamano usio wa lazima unadhibitiwa kwa kufuata sheria.
Baadhi ya askari walimweleza Kitwanga kero zao. Mmoja wao, Alphonce Malowa alisema nyumba za askari ni chache na nyingi zimechakaa kiasi cha kuwafanya kudharaulika mbele ya wananchi.
Inspekta Novatus Makondowa alieleza juu ya umuhimu wa Serikali kuwasomesha walimu wa chuo cha taaluma za polisi ili kuwajengea uwezo zaidi wa kufundisha maofisa wengine chuoni hapo. 

New