My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, November 8, 2011

sherehe za siku ya kuzaliwa mwanzilishi wa dini ya Sikh Guru Singh Sabha,

Wafuasi wa dini ya Sikh wakiwa katika sherehe hiyo.

salam,

MAELFU ya wafuasi wa dini ya Sikh walijitokeza siku ya Jumapili tarehe 6 Novemba 2011 katika mji wa Southall, Middlesex UK ili kusherehekea siku ya kuzaliwa kwa mwanzilishi wa dini yao Guru Nanak aliyezaliwa mwaka 1469 nchini Pakistan.

Muasisi wa Dini ya Sikh

Wakati akiwa na umri wa miaka 30 alipotea kwa hali ya miujiza kwa muda wa siku tatu. Alipo rejea alianza kuhubiri, kufundisha na kuandika dini ya Sikh wakati wa maisha yake yote. Pia Guru Nanak alisafiri dunia nzima kuitangaza na kujadili dini hii kwa waumini wengine kama waislamu pamoja na Wahindu.

Kwa miaka zaidi ya 550 wafuasi wa dini hii wamekuwa na desturi hii ya kusherehekea siku moja kabla ya kuzaliwa kwake Guru Nanak kwa kuandaa maandamano haya makubwa ya Sherehe hii ambayo hufanyika India pamoja na baadhi ya sehemu za nchi ya Uingereza.

Kwa kawaida sherehe hizi huongozwa na wafuasi wakuu watano wanaojulikana kama "Panj Piare" wakiambatana na waimbaji, wanamuziki na timu ya wacheza Upanga (Martial Arts) kuelekea hekaluni kwao "Gurdwara" Sri Guru Singh Sabha, hapa Southall hekalu lao ndio kubwa kuliko yote katika bara la ulaya.

Sherehe hizi huanza mapema asubuhi kwa kuimba, kuomba kwa pamoja. Baadae chakula cha kitamaduni kinachojulikana kama "Langar" hutolewa bure kwa kila mtu.

Maandamano ya Southall yanaitwa Nagar Kirtan,

Asanteni,

No comments:

Post a Comment

New