My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, November 28, 2011

Jk akutana na Chadema

Rais JK akiagana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Ikulu mara baada ya mazunguzo jana.

Leo wanakutana tena kuendelea na mazungumzo yao

...akiagana na Mhe. Tundu Lissu

....akiagana na Mhe. John Mnyika

...akiagana na Prof. Adabballah Safari

..Mhe. Lissu akisepa taratibu kutoka Ikulu

...mambo yalivyokuwa ndani wakati wakipata chai na juisi...ilikuwa kirafiki zaidi.

PICHA: Hisani ya Ikulu

************************************************************************

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,

Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ujumbe

wa Serikali yake leo, Jumapili, Novemba 27,

2011, amekutana na kufanya mazungumzo

na ujumbe wa Chama cha Demokrasia na

Maendeleo (CHADEMA).



Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika

Ikulu, Dar Es Salaam, yamefanyika katika

mazingira ya urafiki na ujumbe wa CHADEMA

umewasilisha mapendekezo yake kuhusu

mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya

Tanzania. Serikali imepokea mapendekezo

Hata hivyo, pande zote mbili zimekubaliana

kukutana tena asubuhi ya kesho, Jumatatu,

Novemba 28, 2011, ili kuipa nafasi Serikali

iweze kutafakari mapendekezo hayo.

Lakini pande hizo mbili zimekubaliana kuwa

Katiba ya sasa ni Katiba nzuri iliyolilea Taifa

kwa miaka 50 iliyopita kwa sababu ni Katiba ya

sasa iliyoliwezesha Taifa la Tanzania kuwa na

amani, utulivu na kupata maendeleo makubwa

ambayo nchi yetu imepata mpaka sasa.



Pia pande zote mbili zimekubaliana kuhusu

umuhimu wa kutunga Katibu Mpya kama

Mheshimiwa Rais Kikwete alivyoliahidi taifa

wakati wa salamu zake za mwaka mpya

Desemba 31, mwaka jana, 2010, Katiba

ambayo italiongoza Taifa la Tanzania kwa

miaka mingine 50 ijayo.



Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Rais

aliwahakikishia wajumbe hao wa CHADEMA

wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho,

Mheshimiwa Freeman Mbowe kuwa ni dhamira

yake na ya Serikali yake kuhakikisha kuwa

Tanzania inapata Katiba mpya.



Katika mkutano huo, pande zote mbili

zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu sana

kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba

Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na

kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na

umoja wa kitaifa.



Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa

mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia

misingi ya mambo mengine muhimu kwa taifa

la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo

vya uvunjifu wa amani, kuligawa Taifa kwa

misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa

misingi ya maeneo.



IMETOLEWA NA:

KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

NOVEMBA 27, 2011

DAR ES SALAAM

No comments:

Post a Comment

New