My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, December 10, 2012

JK:Wenye hila na chuki wanabeza maendeleo yetu

  

 Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Rais Jakaya Mrisho Kikwete (wa pili kushoto) Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohammed Shein (kushoto), Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange,Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal, Wakiwa makini wakati wimbo wa Taifa ulipokuwa ukiimbwa kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam katika maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru jana.Picha na Salhim Shao

 “Utaratibu uliopo ni kuzungumza kila baada ya miaka mitano, lakini mwaka huu ninazungumza na wananchi kutokana na kuwapo kwa viongozi wa mataifa ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc). Nataka wasikie mafanikio yetu ya miaka 51 ya Uhuru,” alisema Rais Kikwete.

RAIS Jakaya Kikwete amesema wenye hila na chuki pekee ndiyo wanaosema kuwa Tanzania hakuna maendeleo.
Alisema hayo jana alipolihutubia Taifa kwenye maadhimisho ya miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
“Utaratibu uliopo ni kuzungumza kila baada ya miaka mitano, lakini mwaka huu ninazungumza na wananchi kutokana na kuwapo kwa viongozi wa mataifa ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc). Nataka wasikie mafanikio yetu ya miaka 51 ya Uhuru,” alisema Rais Kikwete.
Viongozi walioshiriki maadhimisho hayo ni marais Armando Guebuza wa Msumbiji, Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) na Hifikepunye Pohamba wa Namibia.
Nchi zilizotuma wawakilishi katika sherehe hizo zilizohudhuriwa na umati wa watu ni Lesotho, Zambia, Angola, Swaziland, Shelisheli, Rwanda, Zimbabwe, Mauritius na Malawi.
Rais Kikwete alisema mwenye macho hawezi kusema lolote, lakini kwa mwenye hila hakosi maneno na kutoa dosari kwa maendeleo yaliyofikiwa.
“Watu waliobahatika kuiona Tanzania ya mwaka 1961 wakija sasa hivi, wataona mabadiliko makubwa. Kuna mabadiliko makubwa na hii inatokana na kuboresha nyanja mbalimbali za kiuchumi, ulinzi na usalama na miundombinu... kwa wenye hila hawakosi la kusema ila mwenye macho haambiwi tazama,” alisema.
Aliwashukuru viongozi walioshiriki mkutano SADC… “Tumepata bahati ya uwepo wa viongozi waandamizi wa SADC baada ya kukubali ombi langu la kuhudhuria sherehe hizi japo wengine wametoa udhuru na kutuma wawakilishi,” alisema.
Viongozi mashuhuri wakosekana
Baadhi ya viongozi wa kitaifa wakiwamo wastaafu, hawakuwamo katika sherehe hizo.
Miongoni mwa viongozi hao ni pamoja na mtangulizi wa Kikwete, Benjamin Mkapa ambaye yuko Lushoto mkoani Tanga.
Wengine ni Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Idd ambao hata hivyo, haikuelezwa sababu za kukosekana kwa

No comments:

Post a Comment

New