My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, September 30, 2012

Shule ya kanisa yashambuliwa Nairobi

Shambulio la guruneti la mkononi dhidi ya shule ya Jumapili ya watoto wa Kikristo mjini Nairobi limeuwa mtoto mmoja na kujeruhi wengine kadha.


Polisi wa Kenya

Taarifa zinazohusianaKenya, GhasiaMkuu wa polisi wa Nairobi, Moses Ombati, ameliambia gazeti la Daily Nation kwamba watu watatu wamekamatwa, na kwamba watu hao walionekana wakipiga picha za kanisa la Saint Polycarp lilolengwa.

Msikiti ulio karibu na hapo ulishambuliwa na vijana waliokuwa na hasira.

Afisa wa polisi wa Nairobi aliwasihi watu wawe watulivu.

Shambulio lilitokea katika mtaa wa Juja Road, unaopakana na mtaa wa Eastleaigh.

Inaaminiwa kuwa guruneti lilirushiwa kanisa la Saint Polycap kama saa tano punde baada ya misa ya asubuhi.

No comments:

Post a Comment

New