My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, September 1, 2015

BARUA PEPE ZA HILLARY CLINTON KUKAGULIWA

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Bi. Hillary Clinton.
New York, Marekani
Maelfu ya kurasa za barua pepe (emails) binafsi za aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Bi. Hillary Clinton zilizotumwa kwa anuani binafsi ya Waziri huyo, zimewekwa wazi hii leo na idara za Usalama nchini humo.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imesema kuwa, kati ya barua pepe hizo, 150 kati yake ni zile zinazodaiwa kuwa na taarifa muhimu na za siri za serikali ya Marekani. Hata hivyo, Bi. Clinton mwenyewe amesema kuwa barua pepe hizo alizituma kimakosa, kwa kutumia anuani binafsi kwa shughuli rasmi za kiserikali.
Shirika la Ujasusi la Marekani FBI linachunguza ili kubaini kama ni kweli barua pepe hizo zilitumwa kimakosa au la.
Tukio hili limekuwa gumzo nchini Marekani hasa wakati huu ambapo Hillary Clinton anatafuta ridhaa ya chama chake kuwania urais wa taifa hilo kubwa katika uchaguzi wa mwaka 2016.

NA BBC SWAHILI

No comments:

Post a Comment

New