My Web

Emmanuel

CONTACT

Thursday, October 24, 2013

JINSI YA KUONDOA MAKOVU YA CHUNUSI

MARA nyingi chunusi zikitumbuliwa mbichi husababisha makovu yanayoleta weusi mbaya kwenye ngozi.
Ukiachana na njia za gharama za kuondoa makovu hayo, kuna njia rahisi za kuondoa tatizo hilo:
1. Paka ‘bleach cream’ kwenye sehemu zenye makovu, cream hii husaidia kuondoa makovu.
2. Tumia ‘scrub’ ambayo huondoa ngozi ya juu (exfoliate) kwa kupaka kwenye sehemu zenye makovu kama usoni na kwingineko ambako ni rahisi kupaka. Unaweza kufanya zoezi hilo angalau mara mbili kwa wiki.
3. Tumia bidhaa ambazo zina ‘hydroxyl acids`, hutibu ngozi yako na itaonekana nyororo. Unaweza kupata hydroxyl acids tofautitofauti za ngozi (skin care products) kama vile cleansers na lotion.
4. Pia unaweza kuyafanyia masaji makovu ya chunusi ili kuvunja mafuta yaliyoganda ambayo huleta chunusi.
5. Fanya ‘diet’, unatakiwa kula vyakula vyenye vitamin na nutrition, vinasaidia kutengeneza ngozi yako kuwa na afya.

No comments:

Post a Comment

New