My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, October 1, 2013

MISS WORLD 2013

Miss World 2013, Megan Young wa Ufilipino.
MASHINDANO ya kumsaka Miss World 2013, mwishoni mwa wiki iliyopita (Septemba 28, 2013) yalitimua vumbi katika Ukumbi wa Bali Nusa Dua Convention Centre kisiwani hapa na kuwashindanisha warembo 127 ambapo Megan Young wa Ufilipino alitawazwa kuwa mshindi, akifuatiwa na Marine Lorphelin wa Ufaransa na Carranzar Naa Okailey wa Ghana.
WASHINDI WA MATAJI MBALIMBALI
Katika mashindano ya kuwania mataji mbalimbali, wafuatao ndiyo walioibuka kidedea na majina ya vipengele walivyoshinda kwenye mabano: Vania Larissa, Indonesia (Miss Talent),  Ishani Shrestha, Nepal (Beauty with Purpose), Megan, Ufilipino (Top Model), Jacqueline Steenbeek, Uholanzi (Sports), Sancler Frantz, Brazil (Beach Fashion) na Navneet Dhillon, India (Multimedia).
WALIOINGIA TOP TEN
Washiriki waliobahatika kuingia kumi bora ni Carranzar (Ghana), Gina Hargitay (Jamaica), Elena Ibarbia JimĂ©nez (Hispania), Vania Larissa (Indonesia), Kirsty Heslewood (England), Ishani Shrestha (Nepal), Marine (Ufaransa), Erin Holland  (Australia), Sancler Frantz Konzen (Brazil) na Megan Young ( Ufilipino).
MSHIRIKI WA TANZANIA
Katika mashindano hayo ambayo ma- MC walikuwa ni Jennifer Reoch na Kamal Ibrahim, Tanzania iliwakilishwa na mrembo Brigitte Alfred Lyimo ambaye alijitahidi kwenye taji la Beauty with Purpose na kuambulia nafasi ya tatu katika kipengele hicho

No comments:

Post a Comment

New