My Web

Emmanuel

CONTACT

Saturday, October 13, 2012

UN yataka kuona mpango kuhusu Mali

Mataifa ya Afrika Magharibi yanajitayarisha kukamilisha mipango yao ya kuingilia kijeshi nchini Mali, kuwaondoa wapiganaji wa Kiislamu walioteka zaidi ya nusu ya nchi hiyo kufuatia jaribio la kupindua serikali mwezi Machi.
Wapiganaji wa Mali
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetaka kupewa maelezo kamili ya mpango huo katika siku 45 zijazo, ili kuamua kama itatoa idhini au la.
Lakini hadi sasa ni mataifa machache tu ya Afrika Magharibi ambayo yamejitolea kutoa wanajeshi kwa kikosi hicho.
Baadae juma hili, Umoja wa Mataiafa, wakuu wa Ulaya na Umoja wa Afrika watajumuika na wawaikilishi wa Mali mjini Bamako, kujaribu kutafuta mkakati imara wa kuingia Mali kijeshi.

No comments:

Post a Comment

New