My Web

Emmanuel

CONTACT

Tuesday, October 23, 2012

Watoto wauawa kwenye mapigano Sudan



Eneo la milimani Kordofan Kusini

Jeshi la Sudan limesema watato wawili wameuawa kufuatia mashambulio mapya ya mabomu yaliyotekelezwa na waasi katika mji mkuu wa jimbo la Kordofan ya Kusini.
Msemaji wa jeshi la nchini hiyo amesema kuwa raia wanane walijeruhiwa wakati wa shambulio hilo mjini Kadugli.
Kundi la waasi wa SPLM-North nchini Sudan limesema lilikuwa likijibu mashambulio ya siku kadhaa yaliyotekelezwa dhidi yao na wanajeshi wa serikali
Umoja wa mataifa unakadiria kuwa maelfu ya watu wamehama makwao na wengine wengi kuathirika kutokana na mapigano hayo katika eneo la Kordofan ya Kusini, tangu uasi huo ulipoanza mwaka uliopita wakati Sudan Kusini ilijapatia uhuru wake.

No comments:

Post a Comment

New