My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, March 6, 2016

Hizi Hapa Sababu Zitakazokufanya Wewe Binti Usiolewe Mapema



★1. Kuvaa nguo za ajabu ajabu kama changudoa. Sijui ni nani aliyewaambia kuwa mkivaa hivyo mnapendeza!

★2. Kujipaka marangi ya ajabu ajabu usoni kama mwali wa kimakonde au kizaramo kwanza mnatutisha tu.

★3. Kupenda kujirahisisha au kujipendekeza pendekeza kwa wanaume, yani ukiguswa kidogo tu twende.

★4. Kuwa na picha karibia 500 Facebook, Twitter nk halafu picha zenyewe hazieleweki yani zimepigwa katika mavazi au mapozi ya ajabu ajabu, mara umebinua makalio, mara tumbo, mara mdomo, Haaaaa!

★5. Kila unachofanya basi unakimbilia kupost mfano kwenye Facebook account
yako au Instagram na nyinginezo hata ukienda haja basi lazima upost.

★6. Ni mtu wa maneno maneno yani we kila unachokiona unaongea na kuropoka ropoka tu hauna break! mwanamke gani?

★7. Huna mawazo ya malengo endelevu yani we kwenye bichwa lako kumejaa umbea tu sijui leo Wema Sepetu amefanya nini? Sijui Kim, Lupita amefanya vile na upuuzi mwingine.

★8. Mizinga. Yani siku ya pili tu baada ya kukutongoza unaanza " honey nataka galaxy" Htc" Huawei" mara baby nimeona nguo nzuri mara ooh baby yaani njaa inauma'' kwani huyo mwanaume ni babaako, utasindikiza harusi za wenzio hadi upigwe alama..


No comments:

Post a Comment

New