My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, March 6, 2016

MWANAMKE wa daraja la Pili

Kipindi utakapokubali kutoka kimapenzi na mme wa mtu, utakuwa umekubaliana kuwa mwanamke wa daraja la pili. Na siku zote mtu wa daraja la pili ni mtu wa daraja la chini ukilinganisha na daraja la kwanza.

Angalia sasa...kama yupo na wewe na mke wake akapiga simu atamdanganya mkewe kwamba yupo ofisini au katika kikao na hautakuwa na ujasiri wa kuingilia mawasiliano yake. Pia anapokua nyumbani kwake kwa mkewe huwezi kumpigia au hata kumtumia text.

Dada yangu wewe ni mdoli? Anakuchukua kwenu na gari yake anakupeleka katika vyumba vya hotel lakini mke wake amemkabidhi nyumba nzima. Dada yangu shtuka!! Anakutembelea nyumbani kwako na unamtambulisha kwa rafiki zako na majirani kwamba ni boyfriend wako bila kujua unajizibia nafasi za kupata mtu sahihi wa kuweza kujenga nae maisha. Na mbaya zaidi hupajui hata yeye anapoishi.

Dada yangu mpaka lini utaendelea kujiharibia future yako? Anatoka na wewe out na anakununulia kila aina ya pombe na wakati huo huo hawezi kumruhusu mkewe kunywa pombe ya aina yoyote ile. Akili ya kawaida ikwambie kwamba anafanya hivyo ili ulewe vilivyo na apate wasaa wa kukukandamiza vizuri kitandani.

Dada yangu Je mwili wako ni wa majaribio? Anakupa mimba na anakupa pesa uende ukaitoe lakini mke wake akipata mimba nyumbani ni sherehe na anampa pesa za kuandaa martenity dress na vitu vya mtoto.

Dada yangu kumbuka tayari anayo familia yake, kama ulikua hujui Jamaa huwaelezea marafiki zake yote mnayofanya hotelini, lakini hata siku moja hawezi kuwalezea yale anayofanya na mkewe. Hii inafanya marafiki zake wakuone kama mwanamke wa hadhi ya chini kabisa.

Unazo picha zake katika simu yako na ume save namba yake kwa majina mazuri kama Sweetheart, My love, etc... Lakini picha zako haziwezi kupatikana ktk simu yake na namba yako amei Save kama Fundi Genereta, Fundi gari, Mzibua Chemba.

Unatakiwa ukumbuke kwamba mwanamke asie na akili sehemu zake za siri ndizo zitakazoumia zaidi.


No comments:

Post a Comment

New