My Web

Emmanuel

CONTACT

Sunday, August 12, 2012

TAMASHA LA DINI "LOVE TANZANIA" LILIVYOTIA FORA VIWANJA VYA JANGWANI JIJI DAR.



Pichani Juu na Chini ni Umati wa Watanzania uliofurika kwenye 
Tamasha la Dini lililopewa jina la LOVE TANZANIA linaloendelea 
katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam likiongozwa na Askofu 
Andrew Palau kutoka Marekani.
Vijana walioongoza na Askofu Andrew Palau wakitoa burudani na 
mafundisho ya dini kwa njia muziki.
Wana Dar es Salaam wakiendelea kumiminika katika
 viwanja vya Jangwani.
Mmoja wa Wahudumu katika Tamasha hilo akipata chakula cha 
mchana na familia yake Uwanjani hapo.
Umati wa watu ukiwa kwenye foleni ya kupata 
huduma ya chakula uwanja hapo.
Moja ya Magari na wafanyakazi wa Kampuni ya Usafi iliyopewa 
Zabuni ya kusafisha Manispaa ya Ilala Green Waste Pro Ltd likiwa 
limepaki katika Viwanja vya Jangwani kuhakikisha Usafi unazingatiwa 
Uwanjani hapo wakati tamasha la Dini lililopewa jina la 
LOVE TANZANIA likiendelea.
Pichani Juu na Chini ni moja ya michezo iliyofanyika kama sehemu ya 
burudani uwanjani hapo ambapo ilionekana kuvutia Umati wa Watanzania
 waliohudhuria tamasha hilo.
Vijana, Watoto kwa Wazee wakitazama mchezo wa mapikipiki.
Mmoja wa wafanyakazi wa Kampuni ya Green Waste Pro Ltd 
akihakikisha swala usafi linazingitiwa uwanjani hapo 
kama inavyoonekana.
Wananchi waliohudhuria tamasha hilo wakishuhudia 
mchezo wa Baiskeli.
Palikuwa hapatoshi Jangwani.
Ulinzi na Usalama kwa raia ulikuwepo.
Familia zikiendelea kula, kunywa na kufurahi uwanjani hapo.
Hili ni Jukwaa la kimataifa kutoka nchini Uganda maalum kwa ajili ya 
Tamasha lililopewa jina la LOVE TANZANIA likiongozwa na 
Askofu Andrew Palau kutoka nchini Marekani, haijawahi kutokea 
kusikia Sound na Mziki wa Ukweli nchini kwa mliohudhuria 
tamasha hili mtasema.

No comments:

Post a Comment

New