My Web

Emmanuel

CONTACT

Wednesday, August 29, 2012

Valeri Amos kuzuru Syria na Lebanon leo

Naibu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusiana na Maswala ya Kibinadamu, Valerie Amos, anatarajiwa kutembelea Syria na Lebanon, katika juhudi za kuimarisha misaada kwa waathiriwa wote wa mapigano kati ya Serikali na makundi ya waasi nchini Syria
Kulingana na ratiba ya Umoja wa Mataifa, Bi Valerie Amos, atatembelea Syria na Lebanon kuanzia leo tarehe 14 hadi 16, Agosti, mwaka huu.
Ziara hiyo ya siku tatu inatazamia kumulika hali ya kibinadamu inayozorota nchini Syria na jinsi inavyoathiri wale walio nchini humo au wale wanaotorokea mataifa jirani, kukiwemo Lebanon.
Hali nchini Syria imezorota majuma machache yaliyopita kufuatia kusambaa kwa mapitano katika mji mkuu wa Damascus na Aleppo na katika miji mingine pia. Inadaiwa kuwa zaidi ya watu milioni mbili wameathiriwa na mapigano hayo na zaidi ya milioni moja wametimuliwa kutoka makaazi yao nchini Lebanon.
Zaidi ya watu 140,000 wametoroka na kuingia katika mataifa jirani ya Lebanon, Jordan, Uturuki na Iraq.
Katika ziara yake nchini Syria, Bi Amos anatarajiwa kujadiliana na maafisa wa Serikali jinsi jamii ya kutoa misaada inavyopaswa kuimarisha ugawaji wa misaada kwa waathirika wa mapigano hayo. Wale watakaoshirikishwa katika mashauriano ya kuimarisha misaada nchini humo watakuwa maafisa wa Serikali, tawi la Syria la Mwezi Mwekundu na mashirika mengine ya kutoa misaada.
Nchini Lebanon, Bi Amos atakutana na familia za waliotoroka Syria na kujadiliana na Serikali na makundi ya kutoa misaada ya kibinadamu nchini humo jinsi wanavyopaswa kusaidia wakimbizi.
Ziara hii ya Bi Amos imefanywa wakati ambapo wapiganaji nchini Syria wameonyesha kwenye vidio walioisambaza kwenye mtandao wakionyesha jinsi walivyoangusha ndege ya kijeshi ya Serikali ya aina ya Mig 23. Picha hizo zinaonyesha rangi na alama zinazothibitisha kama ndege za jeshi la Syria.

No comments:

Post a Comment

New