My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, January 23, 2012

LULU SKENDO NO 1 2012

Na Shakoor Jongo
ELIZABETH Michael ‘Lulu’ amesahau waraka alioandika Mwaka Mpya 2012 kuwa amejirekebisha na hataki tena skendo kwani kabla ya mwezi Januari kumalizika, tayari amekwaa skendo namba moja ya kujihusisha na vitendo vya kisagaji.
Picha ya Lulu anayefanya poa kwenye filamu za Kibongo imenaswa mtandaoni akilishana keki kwa staili ya ‘kudendeka’ na msanii anayeuza nyago kwenye video za wanamuziki wa Bongo Fleva, Halima Mohamed ‘Baby Candy’.
Picha hiyo ilionesha ilipigwa ndani Club Bilicanas, Dar es Salaam, Jumapili ya Januari 15, mwaka huu.
Tukio hilo limesababisha mjadala mzito kwa watu walioiona picha hiyo kwenye mtandao wa BBM kufuatia kuwepo kwa tuhuma zinazoenea kwamba baadhi ya mastaa wa filamu kwa sasa wamejikita zaidi kwenye ‘kamchezo hako’.
“Inawezekana ni mtindo wa kisasa kulishana keki kwa mdomo, lakini hawa wamezidisha hasa katika kipindi hiki ambacho wasanii wengi wanatuhumiwa kujihusisha na usagaji,” ilisomeka sehemu ya maoni ya picha hiyo.
Baada ya kuona mjadala unazidi kushika kasi, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Lulu ili kupata undani wa picha hiyo ambapo hakuonesha kushtushwa na chochote kwa kudai ni jambo la kawaida.
“Ni kweli ilikuwa Bilicanas, siku hiyo shosti wangu Baby Candy alikuwa na sherehe ya kuzaliwa, kwangu mimi hakuna ubaya wowote,” alifunguka Lulu nusunusu kwa kukataa maswali zaidi.

No comments:

Post a Comment

New