My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, January 23, 2012

Siri nzito bifu la Johari, Nora

Nuru Nassor Masoud ‘Nora’.

Blandina William Chagula ‘Johari’.

Brighton Masalu na Erick Evarist
KUFUATIA tangazo lake la kurejea katika ulingo wa filamu Bongo, msanii Nuru Nassor Masoud ‘Nora’, ametonesha kidonda cha bifu lake la kitambo na muigizaji mwenzake, Blandina William Chagula ‘Johari’ akieleza kuwa nyuma yake kulikuwa na siri nzito.
Akizungumza ishu hiyo alipopewa nafasi na Ijumaa Wikienda mwishoni mwa wiki iliyopita, Nora alifunguka kuwa kisa cha yeye kutofautiana na Johari kilikuwa ni mwanaume.
Alipotakiwa kumwanika mwanaume huyo, Nora alishikilia msimamo wake kuwa hayupo tayari mtu huyo aandikwe gazetini. Akaongeza kuwa wakati akiwa na uhusiano na mwanaume huyo, akageuziwa kibao kwamba alikuwa ni mali ya Johari.
“Sikuwa na mpango na huyo mwanaume lakini Johari alidhani namchukua hivyo nikaundiwa kundi la kunifanyia kitu mbaya,” alisema Nora.
Johari alipotafutwa kwa njia ya simu ili kusema anachokijua juu ya bifu hilo, alisema yuko mbali na Jiji la Dar es Salaam hivyo atalizungumzia suala hilo kiundani atakaporejea.
Hivi karibuni, wawili hao walikutana kwenye msiba wa mwigizaji mkongwe, marehemu Fundi Said ‘Mzee Kipara’ ambapo walilizika rasmi bifu hilo kwa kuwa hakuna aliyefanikiwa kuolewa na mwanaume huyo katika vita hiyo.

No comments:

Post a Comment

New