My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, January 23, 2012

MMAREKANI AKWAMISHA MSUMARI KWENYE UBONGO WAKE BILA KUJUA

Msumari ukiwa katika ubongo wa Autullo kama ulivyoonyeshwa na mashine ya X-ray.

Dante Autullo anaelezea jinsi msumari ulivyopenya kwenye ubongo wake.

Mchumba wa Autullo aitwaye Gail Glaenzer akifurahia mafanikio ya tiba ya mpenzi wake. PICHA ZOTE NA SHIRIKA LA AP

MWANAMME mmoja wa Marekani, Dante Autullo, aliandikwa sana na vyombo vya habari hivi karibuni nchini humo baada ya kujidunga msumari wa sentimita tisa kwa bunduki ya kuchomeka misumari ambapo chuma hicho kilikaa katika ubongo wake kwa karibu siku mbili na yeye akiwa hajagundua hali hiyo.

Autullo, anayeishi Orland Park, Illinois, ambaye baadaye alionyesha picha zake za X-ray katika mtandao wa Facebook, alikwenda hospitali yakiwa yamepita masaa 36 baada ya kujipiga na msumari huo.

Hata hivyo, hakugundua madhara ya hali hiyo kwani msumari huo ulikuwa umeacha mkwaruzo mdogo tu wakati ulipoingia kwenye ubongo wake – jambo ambao lilimfanya afikiri kwamba msumari ulikuwa umemkosa.

Autullo alilazimika kwenda kutibiwa baada ya kulalamika alikuwa anasikia kichefuchefu na kuumwa kichwa.

Madaktari walimshangaa kwa kuendelea kutembea na kuzungumza bila wasiwasi na baadaye walimwambia kwamba msumari huo ulikuwa umepita milimita kadhaa pembeni mwa sehemu muhimu ya ubongo wake.

Hata hivyo, jamaa huyo alipewa tiba iliyofanikiwa katika hospitali ya Christ Medical Center, hukohuko Illinois, ambako msumari huo ulitolewa na akawekewa kisahani cha madini ya ‘titanium’ kwenye fuvu lake ambako msumari huo ulipenya.

No comments:

Post a Comment

New