My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, January 23, 2012

Mwaka 2012, badilisha fikra chakavu kuhusu mapenzi-2

Na Luqman Maloto
Wiki iliyopita tulianza kuijadili mada hii ya kubadilisha fikra chakavu kuhusu mapenzi na kuishia kwenye mfano wa wapenzi wawili, Justin na Jamie. Justin anamlalamikia mpenzi wake kuwa kuna mambo ambayo huwa hamtekelezei na huwa hamuonei wivu kabisa. Wiki hii tunaendelea na mfano huo ambapo Justin anazidi kumlalamikia mpenzi wake huyo.
Justin anasema...

“Nikiwaona marafiki zangu jinsi wao na wapenzi wao wanavyoishi, nashangaa kwangu mbona haiwi hivyo? Naweza kuwa mbali naye hata kwa siku mbili lakini wala hashtuki, haniulizi.
“Tukikutana haoneshi shauku ya kuwa na mimi mpaka nahisi thamani yangu kwake ni ndogo. Hajawahi hata kunikumbatia na hasemi kama alikuwa amenimisi. Nyumbani kwangu naishi peke yangu lakini hutamsikia akisema anataka kuja mpaka nimuombe, tena kwa kumbembeleza, wakati mwingine anasema yupo bize.
“Tukiwa katika ulingo wa mapenzi haoneshi msisimko. Nijuavyo mimi wanawake wengine hutoa hamasa kwa kuangusha kilio fulani cha mahaba na kusifia jinsi kazi inavyofanyika, Jamie yeye habari hiyo hana. Hata nyonga yake anaibania. Ukimuuliza kama anatosheka anadai anafika bila wasiwasi. Hapa ndipo anaponifanya nijiulize maswali mengi.

“Mara mbili nimejikuta nikitoka na rafiki zake wawili. Wa kwanza alionesha ananijali kuliko hata Jamie mwenyewe. Nilipotoka naye nilijiona mwanaume kamili hasa. Ananiuliza maswali ya mahaba, ananikumbatia kwa bashasha kila tunapokutana. Tukiwa kwenye shughuli ananionesha jinsi anavyoridhika na mimi.
“Mwingine hivyohivyo, tunapomaliza mchezo ananimwagia sifa kemkemu, ananiambia hajapata mwanaume aliyemsafirisha kule ambako nimempeleka. Katikati ya mahaba ananililia kwa sauti fulani ya kutoka puani. Kusema ukweli, hao marafiki wamenikosha kiasi ambacho naona thamani yao ni kubwa kuliko Jamie.
“Vile vilio vya kimahaba, sauti za kubembeleza na pongezi baada ya kazi ni kitu kikubwa kwangu. Hata kama ni sifa za uongo lakini mimi zinanipeleka pale ninapotaka. Sijisikii kwenda faragha na mtu ambaye mimi najitahidi kumfurahisha na kumridhisha lakini yeye ananitolea macho utadhani hana hisia. Najisikia kumchoka!”
Kauli ya Justin kama nilivyomnukuu kwenye makala haya, inaweza kuwa fundisho kwako kwa sababu wengi wamejikuta wakipoteza mvuto wao, kisa ni vitu vidogo.
Hii ndiyo sababu ya kumtaka kila mmoja kuzingatia yale ambayo mwenzi wake atakuwa anapenda na kutekeleza kwa kiwango bora ili kumridhisha. Sanaa ya mapenzi kama ambavyo nimekuwa nikipigania kuisambaza siku zote, inamtaka mtu kuishi ndani ya mwenzake. Kuugua kwa maumivu, kuhuzunika katika majonzi na kufurahia palipo na sherehe.

Ni kituko mwenzi wako anaumia wewe unacheka. Yupo kwenye maumivu makali, wakati huo kwa upande wako ni chereko kwa kwenda mbele. Aina hii ya maisha haiwezi kuwa sawa na haikubaliki. Unapaswa kumjali mpenzi wako hata kama haikugusi lakini machoni muoneshe kuwa upo pamoja naye, vinginevyo ni mateso kwako.
Zingatia: Inawezekana mwenzi wako hakwambii lakini ukweli usimame kwenye kipimo chake kwamba anahitaji manjonjo yako ili afurahie penzi. Kama humtekelezei, tambua anaumia kwa sababu unabana.

No comments:

Post a Comment

New