My Web

Emmanuel

CONTACT

Monday, January 23, 2012

Mwaka 2012, badilisha fikra chakavu kuhusu mapenzi

Ni mwaka mpya wa 2012, inakubidi na wewe uwe na fikra mpya. Uondokane na vitu ambavyo vinaweza kukuondolea mvuto au kukuingiza kwenye migogoro. Jiepushe na kila kilichokugombanisha na mwenzi wako.

Ni vizuri uwe na hisia hizo ili somo hili likuingie sawia. Mapenzi hayahitaji ugumu. Huwezi kusifiwa kwa kushindwa kumnyenyekea mwenzi wako. Jeuri dhidi ya mwenzako, maana yake una alama ‘F’ kwenye mapenzi.

Kila mtu anapenda kuonewa wivu ili awe na uthibitisho kuhusu mvuto wake. Anahitaji kujua kama anapendwa na kwamba yupo anayemjali, kwa hiyo asipokuwa karibu yake, atamsumbua kwa maswali,
“Upo wapi? Unafanya nini? Na nani?”

Asije kukudanganya mtu kuwa hapendi kuonewa wivu. Mara kwa mara huwa nalazimika kutoa neno hili kwa sababu kumekuwa na tabia ya watu kuongopeana kuwa hawapendi usumbufu. Wengine wanajaza hekima dhaifu za mapokeo ya kizamani: “Mimi mpenzi wangu Mzungu, hanibani wala nini!”
Je, ni kweli kuwa Wazungu hawaoni wivu? Huko nyuma nimewahi kuuliza swali hili: Ni kwa nini Chris Brown alimpa kipigo Robyn Rihanna Fenty? Uhusiano wa kimapenzi una nguzo zake, na moja kuu ni jinsi wewe unavyomjali mwenzi wako na kumfanya ajione mwenye thamani.

Hujui kuwa mpenzi ni mali yenye thamani? Kama unatambua hilo ni vizuri kuilinda kwa gharama yoyote. Abiria anahimizwa achunge mzigo wake, iweje wewe usidhamirie kumhifadhi mwandani wako? Akili itulie kichwani kwako, wapo wanaolia kwa kuzidiwa kete na marafiki zao.
Hawajui kuwa walicheza ‘faulo’ ndiyo maana wakajikuta wanawekwa pembeni. Hutaki kumuonesha unamjali kwa kipimo kinachostahili, matokeo yake rafiki yako anachukua nafasi. Hujui kumuuliza kulikoni anapokuwa mnyonge, mwenzako anatimiza hilo.

Mapenzi ni sanaa ambayo inamtaka mtu aishi ndani ya mwenzi wake. Uwe rahisi kujua yaliyomo kwenye fikra zake. Katika ‘malavidavi’ epuka u-sistaduu, u-brazameni wala ugumu. Unahitaji kuwa rahisi kwa mwenzi wako na umfanye ajione hajakamilika bila uwepo wako.

Unaweza kufanya kitu ambacho wewe utakiona ni kidogo lakini kwa mwenzako ukawa umemmaliza kabisa. Fikiria unaamka asubuhi mapema unamuamsha kuwahi kazini. Anakuta umemuandalia kila kitu, mnakwenda kuoga pamoja, mnapata kifungua kinywa mezani halafu mnatengana kwa muda kwa sababu mnawajibika ofisi tofauti.

Si kwa kuangalia jinsia. Fikiria pia wewe ni mwanaume ambaye unafanya kitu kumfurahisha mwenzi wako. Unaamka mapema na kunyoosha nguo za mkeo. Unamuamsha na kukuta kila kitu tayari, anajiona mwepesi. Anakukumbatia na kukushukuru kwa sababu anakuona ni mtu wa kipekee. Wengi wamelemazwa na mfumo dume!
Kufanya hivyo, haina maana ni ‘ubushoke’ kama inavyoweza kutafsiriwa, isipokuwa ni njia ya kumpa sababu ya kukupenda. Atakuona ni mwanaume bora uliyekamilika, na usipokuwa naye ataona kuna upungufu mkubwa. Usisome kama mapitio ya vitu rahisi, ila unatakiwa kutunza kichwani na kuhamishia katika vitendo kile ambacho unakipata hapa.


Asilimia kubwa ya watu waliosalitiwa kimapenzi na marafiki zao, ilisababishwa na watu kutoheshimu hisia za wenzi wao. Kiasili, kuna mambo ambayo mtu anakuwa anahitaji kutoka moyoni afanyiwe na mwenzi wake lakini anakuwa hapati, hivyo kusababisha aone pengine jirani anaweza kumtekelezea.

CHUKUA MFANO HUU
Justin na Jamie wapo kwenye uhusiano wa kimapenzi kwa miaka mitatu sasa. Tatizo kubwa linalowakabili ni kwamba mara kwa mara huwa wanagombana na kusalitiana. Hata hivyo, wao hawajui.
Justin anasema: “Nampenda sana Jamie lakini kuna mambo huwa hanitekelezei, na zaidi huwa nashangaa hata hanionei wivu.

No comments:

Post a Comment

New